Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,818
- 4,569
Salaam Wakuu,
Leo tarehe 11/11/2021 yanatolewa maamuzi ya kesi ndogo Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe.
Kujua jana kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri Mahakama Kuu kesi ndogo ya Mbowe, Superitendent Jumanne Malangahe atoa Ushahidi
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
Picha: Watu mbalimbali waliohudhuria Mahakama kuu leo 11/11/2021
UPDATES;
Jaji ameingia Mahakamani Sasa Saa 5 Na Dakika 15 Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa.
Wakili wa Serikali Robert Kidando anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula
3. Jenitreza Kitali
4. Nassoro Katuga
4. Esther Martin
5. Tulimanywa Majige
6. Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anawatambulisha jopo la Mawakili wa Utetezi:
1. Jeremiah Mtobesya
2. Paul Kaunda
3. Fredrick Kihwelo
4. Dickson Matata
5. Iddi Msawanga
6. John Mallya
7. Alex Massaba
8. Khadija Aaron
9. Evaresta Kisanga
10. Maria Mushi
- Jaji anawaita washtakiwa wote wanne, na wanaitika kwamba wapo.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri linakuja Kwa ajili ya kusikiliza Uamuzi wa Mahakama, sisi tupo tayari Wakili Peter Kibatala: Nasi pia kwa Ruhusa yako tupo tayari Kupokea Uamuzi na Kuendelea na Kesi.
- Jaji anaandika Kidogo
Jaji: Jana nilisikikiza Pingamizi la Upande wa Utetezi, Na baada ya Kusikiliza Pande zote Mbili, Maamuzi yapo tayari Jana wakati Shahidi akitoa Ushahidi alieleza Kwamba Baada ya Kupewa Maelekezo ya Kumwandika Maelezo Mshtakiwa namba tatu
Jaji: Na baada ya kupitia Nyaraka hiyo Shahidi alisema anaitambua na baada ya hapo aliomba Mahakama Ipokee Nyaraka hiyo kwa ajili ya Utambuzi, Kitu ambacho Mawakili Wa Washtakiwa wote wanne walipinga Vikali
Jaji: Inapaswa Shahidi ajenge Misingi Kwamba Kwa namna Gani Kielelezo Kimemfikiaje Mahakamani, Na Mawakili Wakasema Kinachotolewa Mahakamani ni Register siyo Entry Kwa Mfano Ingekuwa na Features ambazo zinaonyesha Register hiyo Inatumika Central tu na siyo Mahala Pengine popote
Na Pale ambapo Shahidi ametoa Ushahidi wake anaweza Kufafanua, Wakaomba Mahakama Ione Kielelezo Kilichopo Mahakamani shahidi anaweza Kutoa Ushahidi Wake, Wakaeleza tarehe 07 August 2020 namba alivyo fika Saa 11 Alfajiri na Jinsi ambavyo Shahidi aliweka Entry na aliweza Kukitambua
Jaji: na hicho ndicho kimezua shaka. Na Upande wa Mashtaka Walipata nafasi Ya Kujibu kwa Kuwakilishwa na Abdallah Chavula na Pius Hilla Walisema Kwamba Mapingamizi hayana Mashiko, Wakaja na Kesi ya DPP VS SHARIF Authentication ya Mahakama Inapaswa Kufanywa na Ushahidi Wa Shahidi.
Wakaomba Mahakama itofautishe Kesi ya DPP VS SHARIF ATHUMAN kwamba kesi ile Kielelezo Kilikuwa Gari na Kwenye Kesi hii Kielelezo ni Nyaraka, Wakarejea Kesi ya CHARLES GAZILABO dhidi Ya Jamhuri Kwamba Kesi hiyo iliweka Mambo Matatu ya Relevance, Competence na Shahidi Husika
Wakasema Kwamba Kwa namna ambavyo Shahidi alikuwa anatoa Ushahidi Wake ni Competent. Wakasema Kwenye Kesi Ya CHARLES GAZILABO Kwamba Mtu anaye weza Kuelezea Kielelezo NA kukitambua, Kitu ambacho Shahidi alifanya.
Shahidi alieleza Kwamba alifika kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam, Hiyo inathibitisha kwamba Shahidi anaweza Kufanya Utambuzi na wakaomba Mahakama Itupilie mbali, Upande wa Utetezi Walipata tena nafasi ya Kujibu na Kuona Bado Mapingamizi yao yanayo Sababu
Jaji: Na wakaendelea Kusema Kwamba Suala Zima la Chain of Custody, Mahakama Imeshatolea Maamuzi Kwamba Chain of Custody Inaweza Kujadiliwa Mwishoni, Wakasema Shahidi alijitahidi Kueleza Kwamba aliweka Entry na hilo pekee ndiyo lina fanya Shahidi aonekane anaweza Kukitambua.
Jaji: Kwenye kesi Ya SHARIF ni kwamba wanaona Kanuni inaweza Kutumika Kwenye kesi yoyote, Na Kwamba Shahidi ameeleza Entry na a siyo Kielelezo Chenyewe na Kwamba Suala la Authentication halijaweza Kukidhiwa, Na swala Zima la Kuamua Chain of Custody Wali endelea Kusema Swala La Kupinga Kielelezo ni Jukumu lao Kupinga Wakati Wa Uchukuliwaji, Upande wa Mashtaka wamekosa Hoja za Msingi kuhusiana na Mapingamizi yao.
Na Kwamba Hakuna Features Mahususi Kuhusiana na Kielelezo hicho ili Kutofautisha Detention Register na Detention Register zingine zinazotumika katika Vituo Vingine.. Na suala la Chain Of Custody haijaelezwa Vizuri ni wapi Walipo toa Kielelezo hicho, Kwamba kwa Kumbukumbu zilizopo bado Kielelezo Kipo Chini ya Mahakama. Huo ndiyo ulikuwa Mwisho wa Muhtasari. Sasa twende kwenye maamuzi.
Jaji: Identification of EXHIBIT, Establishing Chain Of Custody, Identification of Objects. Haya siyo Maneno yangu ni Maneno ya Maamuzi ambayo nimeyanukuu hapo juu. Lengo la Chain Of Custody wanapaswa Kueleza Kielelezo Wamekitoa wapi.
Na Kuhusiana na Competence ya Shahidi imeelezwa Kwenye kesi ya CHARLES GAZILABO, KHAMIS ADAM Kwamba Mtu ambaye amekifanyia kazi Kielelezo siyo tu anaweza Kukitolea Ushahidi Bali anaweza za Pia Kukitolea Maelezo
Jaji anasoma maamuzi ya kesi hiyo aliyonukuu
MAAMUZI
JAJI: Tunakubaliana kwa pamoja Kwamba Pingamizi linapinga ipokelewaji wa Vielelezo na Siyo Jambo geni Mahakamani, Na Maamuzi Yamefanywa na Mahakama zetu katika Upokeaji wa Vielelezo Mahakamani. Maamuzi yameonyesha Taratibu, Kanuni na Muongozo.
Kufuatia Maamuzi ya SHARIF MOHAMMED na wenzake Mahakama ya Rufani Ilitoa Maamuzi Kwamba tunao Ushahidi Wa Namna Nne Uhalisi, Testimonial, Documentary Evidence, Na Kwamba Mahakama inaweza Kupokea Ushahidi Mahakamani Wakati wowote.
Mahakama Ijiridhe Kama Ushahidi ni Relevance, Material na Competence, Na Katika Maamuzi yake wamejadili kwa kina kuhusu Ushahidi Halisi. Nimesema Mpaka Mwisho Sijaona Kwamba Vigezo ambavyo vinatumika Katika Real Evidence haitakiwi Kutumika katika Kupokea Documentary Evidence.
- Jaji amemaliza kusoma Maamuzi ya Shauri hilo kama Rejea yake,
Jaji: Kimsingi hayo ndiyo maamuzi ya mahakama ya Rufaa.. Kwa sababu hiyo sasa ilikupima Competence ya Shahidi, Na Kwa Kesi hii Shahidi ameeleza Vizuri kuhusu Kielelezo hicho ambacho alikotumia Kuweka ENTRY ili Kumtoa.
Shahidi Kwenda Kumchukua Mtuhumiwa Maelezo yake. Kwa Maana hiyo anayo Competence. Kuhusiana na Relevance ni Ukweli kwamba Kipo Relevance sababu inadaiwa ndiyo walitumia Kielelezo hicho Kumtoa Mtuhumiwa
Kuhusiana na Materiality ni kweli kabisa kwamba kitasaidia Mahakama Kufanya Maamuzi, ikiwemo Katika Pingamizi Kwamba Mshitakiwa hakuwa hi Kuwepo Katika Kituo hicho cha Polisi. Mahakama hii inaona kwamba ni sahihi kabisa kuendelea kutumika.
Jaji: Imebakia suaala la Chain Of Custody, Ni kweli Shahidi namba Moja ameeleza Kwamba anaweza Kutambua Kielelezo hicho Kwa Majina yake na Sahihi Yake na Majina ya Mtuhumiwa, Ukweli ni kwamba ameweza Kukitambua, Ingawa Mr. MTOBESYA amepinga Kwamba Features zilizoelezwa ni za Entry na siyo Register Yenyewe.. Lakini Mahakama yenyewe inaweza Kutambua kuwa Kielelezo hicho huwezi Kutenganisha Entry na Register. Na Kuhusiana na Chain Of Custody Shahidi hajeleza Chain of Custody Kwamba ni Kwa namna gani Kielelezo hicho Kimemfikia.
Jaji: Ni kweli Kwamba hajaeleza ametoa wapi, Ni kweli Kwamba Kielelezo Kipo Kwenye Kumbukumbu ya Shauri Lingine, Ili Mahakama ione kama kilifuata Utaratibu kilipaswa kionekane kwamba ni kweli Kilifuata Utaratibu wa kiutawala kutoka Mahakamani.
Na Kwa namna hiyo Kielelezo kinajifuta Chenyewe kwa sababu Shahidi hakuonyesha namna gani kilimfikia, Assumption ni kwamba Kielelezo Kipo Kwenye Chumba cha Mtunza Kielelezo Cha a Mahakama, Hakuna Ushahidi Kwamba Shahidi alikipataje kuja Mahakamani.
Jaji: Kwa sababu hiyo mahakama inakikataaaaa kielelezo hiki natoa amri.
- Mawakili wa pande zote wanasimama na kuinama kuonyesha kukubaliana na uamuzi wa Jaji.
Jaji: Shahidi wenu yupo wapi tuendelee
Jaji: Shahidi nakukumbusha Upo chini ya Kiapo ambacho Ulikiapa wakati Unatoa Ushahidi Wako
Shahidi: Wakati na chukua Mohammed Abdilah Ling'wenya alikuwa Mwenye Afya Njema na Hakuwa na Tatizo lolote
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumchukua Ulimpeleka wapi
Shahidi: Nilimpeleka Pembeni Kidogo Kwenye Chumba Kwa ajili ya Mahijiano na Mtuhumiwa huyo
Wakili wa Serikali: Elezea Baada ya Kukaa Pamoja nini Kiliendelea
Shahidi: Nikijambulisha Kwa Majina Kwamba Mimi ni ASP JUMANNE MALANGAHE, Na Mtuhumiwa akajitambulisha kwa Majina yake Kwamba anaitwa Mohammed Abdilah Ling'wenya alimaarufu kama DOYI
Wakili wa Serikali: Elezea Ni kitu gani sasa Ulifanya Baada ya Kujitambulisha
Shahidi: Nilimuonya Kwamba anatuhumiwa kwa Makosa ya Kula Njama za Kutenda Matendo Ya Ugaidi, Nilimueleza kwamba Katika tuhuma hizo alazimiki kueleza Chochote isipokuwa kwa hiari yake Mwenyewe chochote atakachokieleza kinaweza Kutumika kama Ushahidi Mahakamani, Vilevile anayo Haki ya Kuwepo Mwanasheria Wake, Ndugu yake, Jamaa yake, Rafiki ili ashuhudie Wakati Maelezo hayo yakiandikwa, Baada ya Hatua hiyo, Mimi Nilisaini na Mtuhumiwa alisaini ilikuonyesha nilimuonya.
Shahidi: Baada ya kumaliza Hatua hiyo Mtuhumiwa Mohammed Abdilah Ling'wenya alimaarufu DOYI alijibu Onyo hilo.. Kwamba yeye Mohamed Abdilah Ling'wenya Alimaarufu DOYI ameonywa na Mimi ASP JUMANNE MALANGAHE anatuhumiwa kwa Kosa la Kula Njama kutenda Vitendo Vya Ugaidi Chini ya Sheria namba 24 ya Sheria ya Kupambama na Ugaidi, Kwamba alazimishwi Kusema Lote isipokuwa kwa hiari Yake Mwenyewe. Chocolate atakachoandika Linaweza Kutumika aka Ushahidi Mahakamani.
Na pia anaweza Kuwepo Mwanasheria Wake, Ndugu yake, Jamaa yake, au Rafiki ili ashuhudie Wakati Maelezo yake yakiandikwa. Baada ya Mtuhumiwa kuulizwa Onyo hilo kama Yupo Tayari Kutoa Maelezo yake, Mtuhumiwa akajibu Ndiyo Nipo tayari, Nilimuuliza nani awepo Wakati anatoa Maelezo yake, Mtuhumiwa alijibu yeye Mwenyewe anatosha Wakati wa Kutoa Maelezo yake, alisaini na Mimi nikasaini, baada ya hapo akawa tayari Kutoa Maelezo Yake, Saa 2 na Dakika 20 nilianza kuandika Maelezo Ya Mtuhumiwa,
Wakili wa Serikali: Wewe Ulifanya nini baada ya yeye Kusema yupo tayari Kutoa Maelezo
Shahidi: Nilimuuliza Mtuhumiwa Ushiriki wake Kuhusu tuhuma nilizomueleza
Shahidi: Nilimueleza kila anapohusika na ambapo yeye alikiri
Wakili wa Serikali: Wewe baada Kueleza ulifanya nini
Shahidi: Nilikuwa na andika Kwenye Karatasi, Fomu kile alichokuwa ananieleza
Wakili wa Serikali: Kilikuchukua amuda gani?
Shahidi: Muda wa Masaa 2 na Dakika 42
Wakili wa Serikali: baada ya Kumalizia Kuandika Ulifanya nini?
Shahidi: Nilimpatia Maelezo ayasome, ilikuweza Kuongeza, Kupunguza au Kufanya Marekebisho kwa yake aliyiyasema
Wakili wa Serikali: Baada ya Mtuhumiwa Kusoma Maelezo hayo akasemaje
Shahidi: Ameridhika na hana cha Kupunguza wala Kuongeza
Wakili wa Serikali: Ulifanya nini baada ya kuandika
- Kibatala: OBJECTION anachofanya Wakili anajua Hakiruhusiwi
Wakili wa Serikali: Baada ya kumaliza Kuandika Ulifanya nini?
Shahidi: Alisaini na Mimi nikasaini, na baada ya hapo nikaandika Uthibitisho wangu mimi Mwenyewe.
Wakili wa Serikali: Baada ya akumaliza Kuandika Uthibitisho huo Ulifanya nini
Shahidi: Niliandika Muda wa Kuandika Maelezo
Wakili wa Serikali: baada ya Kumalizia Kuandika Maelezo Ulifanya nini na Mtuhumiwa
Shahidi: Nilimchukua na Kumrejeaha Chumba cha Mashtaka
Wakili wa Serikali: Maelezo ya Mshitakiwa Mohammed Abdilah Ling'wenya uliyapeleka wapi
Shahidi: Kwa Assistant Inspector Swila
Wakili wa Serikali: Ilikuwa ni Lini?
Shahidi: Ilikuwa ni Siku hiyo hiyo
Wakili wa Serikali: Elezea Baada ya Shughuli hiyo Ulikutana wapi tena na Mtuhumiwa
Shahidi: Niliondoka Kwenda Kufanya Majukumu Mengine kwa Kadri nilivyokuwa naelekezwa na ACP kingai, Siku ya tarehe 08 August 2020 Majira ya Saa 5 Asubuhi Tukiwepo na Inspector Mahita, Tulielekezwa na Afande Kingai Kumuhamisha Mtuhumiwa na Kumpeleka Kituo cha Polisi Mbweni.
Wakili wa Serikali: Wakati Mlielekea Mbweni Ni kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Hakuna Kilichoendelea, Tulipofika Tukiwakabidhi watuhumiwa, Na Kwenda Kuonana na Kiongozi wetu ACP KINGAI kwa Upelelezi wa watuhumiwa Wengine
Wakili wa Serikali: Elezea Baada ya hapo Ulionana naye wapi?
Shahidi: Sikuwahi Kuonana tena na Mtuhumiwa huyo..
Wakili wa Serikali: Kwa Ufahamu Wako Vituo ambavyo Mohammed Abdilah Ling'wenya aliweza Kufikishwa ni Vingapi?
Wakili wa Serikali: Unasema Siku Mnampeleka Kituo Cha Polisi Mbweni hakuna Kilichofanyika zaidi ya kumkabidhi pale, Sababu hasa ni nini?
Shahidi: Sababu zilikuwa za Kiupelelezi, Sababu Kuna Mwingiliano Wa watuhumiwa wengi wanaingia na Kutoka ni wengi.. Tulihofia Taarifa zinaweza Kufika Kwa Watuhumiwa ambao bado tunawatafuta Kwa urahisi.
Wakili wa Serikali: Siku unaandika maelezo ya Mtuhumiwa pale, unasema ulimpa Inspector Swila, Je Inspector Swila alipeleka wapi? -
- Mtobesya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji huyo siyo Swila na hawezi Kujibu kwa niaba ya Swila
Wakili wa Serikali: Ngoja Nirudie Swali
Wakili wa Serikali: Ulipompa Swila hizi Karatasi, alifanya nini na Hizo Karatasi
Shahidi: Ndiyo tulikuwa tunampa Nyaraka zetu, Kwa hiyo alizochukua akaenda Kuweka kwenye Jalada
- Mtobesya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hizo ni hearsay
Jaji: Jiande uje kumuuliza labda walikuwa naye.
Shahidi: Swila amuda Mwingi tulikuwa naye, alienda Kuweka kwenye Jalada la Upelelezi
- Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Wakili anahama Eneo, Je ulichokiandika Siyo HearSay
Wakili wa Serikali: Sisi Bado hatuoni tatizo, huyu Mohamed Abdilah Ling'wenya amepinga Maelezo ya Onyo kwamba hakuwahi Kufika Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam na ajawahi Kuandika Maelezo hayo..
Shahidi: Siyo Kweli, Mimi Mwenyewe ndiyo Niliyempeleka Pale, Nikaenda Kumchukua Mimi Mwenyewe Kutoka Kwenye Chumba Cha Mashtaka Nikiwa Pekee yangu bila Uwepo wa Askari Mwingine yoyote akiwa na hali Nzuri, na Mimi Niliondoka nikiwa nje ya Kituo na yale maelezo, Nikampigia Assistant Inspector Swila yale achukue yale maelezo ili aweke kwenye Jalada la Kesi.
Wakili wa Serikali: Wewe una utbitisho gani kwamba uliandika Hayo Maelezo siku ya tarehe 07 August 2020
Shahidi: Alikuwepo Askari aliyekuwepo pale Chumba cha Mashtaka. Na baada ya kumaliza Kuandika Maelezo Askari huyo huyo alimpokea na Kumrudisha Lockup.
Wakili wa Serikali: anachosema ni kwamba ulimtishia kwa Bastola ilikutoa Maelezo
Shahidi: Siyo Kweli, Sikuwahi Kumtishia Mtuhumiwa huyo Kwani alikuwa na Ushirikiano, Sikuwa na Sababu hiyo
- Kibatala: OBJECTION, huyu labda hajasikia Vizuri Mapingamizi, nayasoma tena kwa sauti ayasikie
Wakili wa Serikali: Sawa Ngoja Nirudie, Ulimtishia Kwamba Asipo Saini Ile Karatasi ya Maelezo basi yale Mateso Mliyompatia Moshi Mtayarudia
Shahidi: Si kweli Sikumtishia kwa sababu sikuwa na sababu hiyo.
Wakili wa Serikali: Maelezo ya Mohammed Abdilah Ling'wenya ukiyaona unaweza Kuyatambuaje
Shahidi: Naweza Kuyatambua Kwa Majina Yangu, Sahihi yangu, Uwepo wa Majina ya Mtuhumiwa na Sahihi zak na Yote aliyo I eleza Nikaandika kwenye Karatasi ya Maelezo.
Wakili wa Serikali: Samahani Mheshimiwa Jaji tunaomba tumpatie Nyaraka Kwa sababu ya Utambuzi
- Shahidi anamkabidhiwa Nyaraka
Wakili wa Serikali: Angalia Nyaraka hiyo Kama Umeitambua na Useme ni Kitu gani?
Shahidi: Ndiyo nimeitambua Nyaraka hii Kama Maelezo Niliyoaandika kutoka kwa Mohamed Abdilah Ling'wenya Maarufu Kama DOYI,
Wakili wa Serikali: Umeitambuaje?
Shahidi: Kwa Majina Yangu, Sahihi Yangu Pamoja na Saini zake pamoja na aliyoyaeleza
- Kibatala: OBJECTION kwa Stage ya Utambuzi anatakiwa asifike kwenye aliyoyaandika Sababu ni Content
Wakili wa Serikali: Sisi hatuoni tatizo
Kibatala: Kwa Stage ya Utambuzi, aliyoyaandika ni Content
Jaji: content yake hatuingii, anaishia Kusema ameyaona
Wakili wa Serikali: Ungependa Mahakama ifanye nini katika Hayo Maelezo uliyoandika kutoka Kwa Mohammed Abdilah Ling'wenya alimaarufu kama DOYI
Shahidi: Ningependa Mahakama Iyapokee kwa Utambuzi
Mtobesya: Hatupingi Upokelewaji wa Maelezo haya Kwa niaba ya Mshtakiwa wa Kwanza Sababu ni Zifuatazo Naomba Iwe on record Kwamba Mahakama inayajua hayo Maelezo lakini Mshtakiwa wa tatu Amekataa hayo Maelezo Kutokupinga huku Hakumaanishi Kwamba Mshtakiwa anakubaliana na Content.
Wakili wa Serikali S Pius Hilla: OBJECTION Mheshimiwa Jaji natafakari kwamba hupingi lakini kwa conditions kwamba lazima sababu zieleweke, Kama hupingi, Lakini unapoongezea Vitu Vingine inamaana hukubaliani, Tunatengeneza Record gani kwa Mahakama. Kama kuna Jambo it's better akapinga tu hadharani..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: kwa Kuongezea tu, hili zoezi la Trial Within Trial na Hii Conditions alizo +toa hapa hairuhusiwi.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Sijui Kwanini Wenzangu Wamesimama, Wenzangu Waniambie Kwamba Ni Sheria gani inakataza Ninaposema sipingi siruhusiwi Kuongeza Maneno.. Sijui Wenzangu Wanahofu gani labda.. Wakasome Kesi ya Martha Weja sisi Kama Utetezi tunaruhusiwa Kuhoji content.
Jaji: katika Kesi yoyote Mahakama haijui chochote, Bila nyinyi Kueleza Mahakama, Mahakama Imeelekezwa Kwamba Isiyapolee yanayo Vunja Sheria yoyote, Sioni Tatizo Kwa Mtobesya Kuzungumza alichozungumza na huwezi kujua atakitumia wapi.
Mtobesya: naomba nikumbushwe niliishia wapi
Jaji: uliishia Mheshimiwa Jaji
Mahakama: Kicheko
Jaji: Unakubaliana na Mahakama Kupokea Lakini Hukubaliani na Content..
Mtobesya: naomba niishie hapo
- Anasimama Wakili Paul Kaunda...
PAUL KAUNDA: kwa niaba ya Mshtakiwa wa Pili tunaomba kufunga Mkono kilichozungumzwa na Wakili wa Mshtakiwa Wa Kwanza Fredrick Kihwelo: Tunakubaliana na Uwepo wa Nyaraka hii lakini hatukubaliani na Kilichopo Ndani
Kibatala: Kwa niaba ya Mshtakiwa wa Nne na sisi Hatupingi, Tunategemea Kuitumia Nyaraka hii katika Kuhoji Dodoso katika kesi hii Ndogo
Jaji: Yaliyosemwa na Mtobesya Mnalolote la Kujibu (Mashtaka) WS Wanateta Kidogo napokea kama ID namba 1
- Wote wanakubali.
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Naomba Dakika Mbili Nishauriane na Wenzangu Kuhusu Hoja ya Mtobesya kama Kuna la Kumjibu..
Wakili wa Serikali: Off Record Kwanza, Kuna Jambo la Mtobesya Kwamba Kwenye kesi ya Martha Weja, Tukasema tunaomba tujiridhishe kwanza.
Mtobesya: Kwa haki tuwaache wajiridhishe tu, Ni Kesi ambayo Imeripotiwa Kwenye TANZANIA LAW REPORT ya Mwaka 1982 Ukurasa wa 35..
Kibatala: nawakumbusha kwamba wenzetu wazingatie na muda kwa sababu leo tumeamza Saa tano na shahidi ana siku mbili kizimbani.
Jaji: Siku 3 labda kwenye kesi Ndogo ndiyo Siku 2..
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa tupewe tu Muda wa Kutosha kwa sababu hatuna hapa na hatuwezi Kupata ipo Ofisini
Jaji: Mtobesya ametaja Mpaka Kurasa labda anayo hapo.
Mtobesya: Hapana sina hapa ni kesi ya siku nyingi lakini tunatumia sana, Naweza kuiomba na Mimi ofisini Wakascan wakanitumia
Jaji: Natoa Hairisho la Dakika 45, tutarudi Saa 8 Jaji anatoka.
Zinapigwa kelele za kooooooortiiiiiii
Jaji ameingia.. Kesi inatajwa... Quorum zipo vile vile.
Mtobesya: Shahidi Wakati Mnamkamata Ling'wenya ni taarifa zipi Mlikuwa nazo tayari?
Shahidi: Taarifa tulizokuwa nazo alikuwa ni Miongoni Mwa Kundi ambalo lina fanya Njama Kwa Kufanya Vitendo Vya Kigaidi ambavyo ni Kushiriki katika Kulipua Vituo Vya kuuzia Mafuta Kukata Miti na Kuweka Barabarani, Kulipua maeneo yenye Mkusanyiko wa watu na Kuhamasisha Maaandamano ya siyo na Kikomo.
Mtobesya: Ni hizo Taarifa tu au Mlikuwa na Zingine?
Shahidi: Kimyaaa
Mtobesya: Ni nani aliwasaidia Kuwapa Taarifa Mpaka Mkajua Eneo alilokuwa Ling'wenya?
Shahidi: Nilikuwa na Mkuu wangu Afande Kingai yeye Ndiye alikuwa anajua aliyekuwa nampa taarifa nilikuwa naenda Field Kuthibitisha tuhuma kama Mtuhumiwa huyo anahusika
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji ilichukua muda gani, tangu unatengeneza Dhana hiyo Mpaka Mnamkamata Ling'wenya
Kimyaaaaaaaaaa kinatawala kwa sekunde kadhaa
Mtobesya: Nitakuwa sahihi Kwamba Mpelelezi yoyote kabla hajafanya Upelelezi anakuwa na dhana Kichwani unapoenda Field Unaenda kuthibitisha Kama ni Chanya au Hasi ni sahihi?
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji Kwenye Shauri hili Dhana yako ilikuwa ni nini?
Jaji: anamuuliza Shahidi kama ameelewa Swali
- Shahidi anapata kigugumizi kidogo anashindwa kuongea hapa.. Lakini anafanikiwa kuendelea..
Shahidi: Ni palepale nilipopata Taarifa na Kuanza Kutafakari na haikuchukua Muda Mrefu
Mtobesya: Mueleze Jaji Taarifa hizo ulizipata lini
Shahidi: Siku ya Tarehe 04 August 2020
Mtobesya: na Ling'wenya Mlimkamata tarehe ngapi?
Shahidi: Naomba nirejee Nyuma ya Swali Lako ulilokuwa Umeniuliza
MTOBESYA: enheeeeeeee!
Shahidi: UMENIULIZA Iinachukua Muda gani Kuniwezesha Kwenda Field
Mtobesya: Sijakuuliza Swali hilo Shahidi: Dhana ni Kama Kitu ambacho huna a Uhakika nacho
Mtobesya: Hapa namaanisha HYPOTHESIS, Mpelelezi Yoyote lazima awe na Hypothesis
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mtobesya: Nakurudisha Kwenye Swali Sasa, Je Mlimkamata lini Ling'wenya
Shahidi: Tarehe 05 August 2020
Mtobesya: Maelezo Ya Ling'wenya uliyaandika lini
Shahidi: Tarehe 07 August 2020
Mtobesya: Kwa hiyo nitakuwa Sasa Kwamba Wakati Unamuhoji ulikuwa na Taarifa
Shahidi: Hapana Sikuwa na Taarifa
Mtobesya: Siwezi Kukunyonga kwa Majibu yako. Haya Umesema Ling'wenya alikiri Kujihusisha Kufanya Vitendo hivyo ni Vipi
Shahidi: Kwamba kweli alijihusisha na Vitendo Vya kupanga Njama
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema Mpelelezi asiandike Maelezo ya Mtuhumiwa, Kwa sababu Mpelelezi anataarifa Nyingi Wakati anampeleleza?
Shahidi: Hapana Siyo Sahihi
Mtobesya: Kwa hiyo pale ambapo Kuna Askari Mwingine na Mpelelezi Yupo Hairuhusiwi Askari Mwingine Kuchukua Maelezo
Shahidi: Hapana Inaruhusiwa
Mtobesya: Zoezi la Kuchukua Maelezo lilianzishwa na nani
Shahidi: Mimi Ndiyo Wajibu wangu
Mtobesya: Kwa hiyo iingie kwenye Record Kwamba ni wewe Ndiyo Uliomba Kuchukua Maelezo?
Shahidi: ni Wajibu wangu
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi kuna aina 2 Uchukuaji wa Maelezo, pale ambapo Mshtakiwa anaomba au Askari anataka Kufanya hivyo
Shahidi: Hapana Mtuhumiwa hawezi Kuomba
Mtobesya: Kwa hiyo Hakuna Sehemu Mtuhumiwa anaweza Kuomba Kuandikwa Maelezo?
Shahidi: inategemea na Mazingira
Mtobesya: Kwa hiyo tunakubaliana kwamba mtuhumiwa mwenyewe anaweza kuomba kuandikwa Maelezo?
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Jaji: Kama hujamuelewa uliza wakueleweshe...
Shahidi: Natafakari kidogo
Jaji: Ujibu kwa speed sasa
Mtobesya: Kwa hiyo Kuna namna Mbili au Moja
Shahidi: Hakuna Namna mbili
Mtobesya: Maelezo uliyachukua kwa namna ipi Shahidi Kwa namna Mbili Baada Ya Kumuuliza na Yeye Kuwa anajibu
Mtobesya: Kwa hiyo Maelezo Yake yanatokana na Majibu yako
Shahidi: Kulikuwa na Maswali na Sehemu zingine pana Maelezo
Mtobesya: Nilikusikia wakati hujaanza Kuchukua Maelezo Kwamba Ulimpatia Haki zake za Kuwa na Wakili na Ndugu halafu akasema ataandika Mwenyewe, Lakini Hukusema Kwamba Wakati Wote Mnamkamata Mpaka Mnamchukua Maelezo kwamba Hamkuwezesha Kukutana na Ndugu.
Shahidi: Sahihi Sikusema
Shahidi: Ni yale yanayo chukuliwa Kuhusu Mtuhumiwa anahusishwa na Kutenda aina fulani ya Kosa
Mtobesya: Ni hivyo tu?
Shahidi: INATOSHA
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi nikisema Maelezo ya Onyo Yanatakiwa Kuonyesha Mtuhumiwa Kosa analo tuhumiwa nalo
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi Kwamba Kosa Unalomuonya Nalo ni lazima liwe limetamwaka Kwenye Sheria
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi Kwamba Maelezo ya Onyo Yanatakiwa kuwa Sheria na inatakiwa Kuonyesha Kifungu Unachomuonya nacho
Shahidi: Siyo Kweli, unaweza Kumwambia kwa Maneno tu
Mtobesya: Kwa hiyo siyo Muhimu Kumtajia Kifungu unacho Muonya nacho?
Shahidi: Ni Muhimu kwa Minajiri ya Kumuonya mshtakiwa Mwenyewe
Mtobesya: Kwa hiyo kwako wewe Siyo Muhimu?
Shahidi: Nilisahau lakini nilikuwa nishamwambia
Mtobesya: Nitakuwa sahihi Kwamba ni Matakwa ya Kisheria, Baada ya zoezi la Kuonya Kuisha Tarehe, Mwaka na Muda lazima viwe katika fomu unayotumia Kumuonya
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: na wewe Uliweka hivyo
Shahidi: Ndiyo Niliweka
Mtobesya: Tutaona baadae kama Uliweka
Mtobesya: na nitakuwa Sahihi Muda wa Kuonya Siyo Muda wa Kuchukua Maelezo, Unamuonya kwanza kisha Unamchukua Maelezo
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Kwa hiyo ni sahihi Kwamba muda wa Kuonya ni Tofauti na muda wa Kuchukua Maelezo
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Twende kwenye Hitimisho la Kuandika Maelezo pale unapotakiwa Kuthibitisha, nitakuwa Sahihi nikisema Ufungaji wa Maelezo ya onyo una namna Mbili au Tatu kwanza wa Mtu anaye Jua Kusoma na Kuandika na ameridhia Kwa anaye andika, ambaye ajui Kusoma na Kuandika au amekataa na Mwisho Mtu ambaye amekataa
Shahidi: Siyo Sahihi
Mtobesya: Haya tueleze Wewe Wa kwanza anathibitisha vipi
Shahidi: Yeye Mwenyewe anaandika Kwamba nimeyasoma na Kuyaelewa
Mtobesya: na hiyo inaonekana katika Statement uliyoiandika
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mtobesya: na wewe Mwenyewe Unaandikaje Mwishoni?
Shahidi: Unathibitisha Kuandika Maelezo ya Mtuhumiwa huyo
Mtobesya: huyo ambaye amesoma na kuandika, anathibitisha Vipi? KWA signature na Dole Gumba Maana havitumiki kwa Pamoja.
Shahidi: Vyote Vinatumika
Mtobesya: na huo ndiyo Ushahidi wako
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Unafahamu PGO ni Nini
Shahidi: Nafahamu Ndiyo
Mtobesya: Nitakuwa sahihi Kwamba Ndiyo Kitendea Kazi chenu cha Kila Siku
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Haya Mwambie Mheshimiwa Jaji PGO inasemaje
Shahidi: Kwa yule ambaye anajua Kusoma na Kuandika ataweka Sahihi na Kuweka Dole Gumba na Yule ambaye hajui Kusoma na kuandika atashindwa Kuweka Dole Gumba,
Mtobesya: Huyo Ling'wenya alifanya nini kama ulivyo tueleza
Shahidi: Alisaini Pamoja na Dole Gumba
Mtobesya: Kule Chini Mnapoweka Ithibati Kuna Vifungu Mnaviandika
Shahidi: sahihi Mtobesya: Mueleze Jaji kwenye Maelezo yenu Mlitumia Vifungu gani
Shahidi: Ilikuwa Imeshaandikwa Kwenye Karatasi, niliona hakuna haja ya Kuweka hiko Kifungu
Mtobesya: Kitaje Kifungu
Shahidi: Kilikuwa Kifungu Cha 57(3)
Mtobesya: Umekitaja Maana Yake unakifahamu Mueleze Mheshimiwa Jaji kama hicho Kifungu aya zake
Shahidi: Sikumbuki Kama Zipo hizo aya
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba nipatiwe ID 1
- Mahakama inampatia Mtobesya ID1
Mtobesya: Na Kuonyesha Kielelezo Cha Mahakama Nikuulize Maswali Machache, Iambie Mahakama Kama Baada Onyo Uliweka Muda
- Shahidi anakuwa mbishiiiii hapa, Mbishi, lakini Mwishoni anasema HAKUNA MUDA..
Mtobesya: tuonyeshe uthibitisho amesoma na Kuyaelewa Sehemu gani
Shahidi: Mtuhumiwa amesaini na Kuweka Dole Gumba
Mtobesya: na Kifungu cha Sheria
Shahidi: Ndiyo nimesema Kwamba Karatasi ilikuwa Tight sikupata nafasi ya kuweka
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji Pale ambapo Maelezo ya Mtuhumiwa anathibitisha Kuna Kifungu cha Sheria au Hakipo
Shahidi: Hakipo Kifungu cha Sheria
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji Ulipoishia wewe Kuthibitisha, Kama Kipengele cha Mwisho Kifungu kimelezwa ni Kifungu 57(3) na aya zake au Hapana
Shahidi: Tunaona Kifungu Cha 57(3)
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kurudisha Kielelezo
Mtobesya: Ni kwanini Hamkuweza Kuchukua Maelezo ya Mtuhumiwa Mkiwa Moshi?
Shahidi: Tulikuwa tunawatafuta watuhumiwa wengine na Watuhumiwa walikuwa ni sehemu ya Kusaidia na Pia Shauri Lenyewe lilikuwa DSM na Pia Nature ya Tukio ilikuwa inaenda Kutokea Mikoa ya Dar es Salaam Arusha Kilimanjaro, MBEYA, Mwanza na Morogoro
Mtobesya: Mweleze Mheshimiwa Jaji Kama Unatambua Utaratibu wa Kuchukua Maelezo halafu baadae unaweza za Kuandika Maelezo ya Ziada (Additional Statement)
Shahidi: Sitambui
Mtobesya: Mtajie mheshimiwa Jaji Kama ni Kanuni au sheria gani inayo kulazimisha kwenda kuchukua maelezo sehemu uliyofungulia shauri
Shahidi: Siyo sheria wala Kanuni lakiniiiiiiiiiiii
Mtobesya: hakuna cha lakini hapa, Mheshimiwa Jaji naomba kuishia hapo...
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kwa Muda gani Shahidi: Kwa Miaka 7
Mallya: Ni sahihi Ulikuwa katika Ofisi ya DCI
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Nitakuwa Sahihi nikisema Uinajua Dar es Salaam
Shahidi: Siyo Sahihi
Mallya: Ramadhan Kingai kabla hajawa RCO alikuwa Msaidizi wa ZCO Dar es Salaam
Shahidi: Ni Sahihi
Mallya: Kwenye Timu yenu nikisema kwenye timu yenu angalau Kuna watu Wawili Wa naijua Vizuri Dar es Salaam nitakuwa Sahihi
Shahidi: Siwezi Kusemea Wote
Mallya: Ofisi ya DCI ipo Katikati ya Jiji la Dar es Salaam au Sema Ipo wapi
Shahidi: Mtaa wa OHIO
Mallya: Makao Makuu ya Polisi Mpaka Dar es Salaam ni Umbali gani Kwa Kukadiria
Shahidi: Siwezi Kukadiria
Mallya: lakini Unajua Kuwa Makao Makuu ya Polisi na Polisi Mjini Kati Dar es Salaam Vipo Wilaya Moja
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kituo cha Polisi Mbweni Unakifahamu
Shahidi: Nakifahamu
Mallya: Kituo cha Polisi cha Mbweni ni Kituo cha Wilaya ya Kipolisi Kawe
Shahidi: Sina Uhakika
Mallya: Kwamba Wakati Unapeleka Watuhumiwa Mbweni ulikuwa ujui Kuna Kituo cha Polisi Cha Wapi
Shahidi: Nilikuwa najua ni Kituo cha Polisi tuh
Mallya: Je Kuna Kesi yoyote Umeshawahi Kusikia kwamba Kuna Mtu alienda Kutoa Taarifa Kwamba watuhumiwa wamekamatwa Ututajie
Shahidi: Ni Mambo ya siri
Mallya: nimesikia una Mwambia Mtobesya Wakati Mnawakamata Kipaumbele Kilikuwa Matukio yasitokee
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Ni sahihi Kwamba Wakati Wote Polisi mnapaswa Kutenda kazi Kwa Mujibu wa Sheria
Shahidi: kimyaaa
Mallya: Kwamba Wakati Unapeleka Watuhumiwa Mbweni ulikuwa ujui Kuna Kituo cha Polisi Cha Wapi
Shahidi: Nilikuwa najua ni Kituo cha Polisi tuh
Mallya: Je, Kuna Kesi yoyote Umeshawahi Kusikia kwamba Kuna Mtu alienda Kutoa Taarifa Kwamba watuhumiwa wamekamatwa Ututajie
Mallya: Wakati mnapokea Simu ya Boaz Kwamba Mrudi Dar es Salaam ilikuwa Mkoa gani
Shahidi: Kilimanjaro Moshi
Mallya: kilichoWafanya Msiwaandike maelezo Muda huo ni nini baada ya Kuambiwa zoezi la Kuacha Kumtafuta Lijenje
Shahidi: Tulikuwa tunawahi Kuja Kuendelea Kuwatafuta Watuhumiwa Wengine Dar es Salaam na Kuendelea na Upelelezi
Mallya: Je Mohammed Ling'wenya alitishiwa au alitoa kwa hiari
Shahidi: Alitoa kwa Hiari
Mallya: Ulipata Kufahamu Kuwa Mohammed Ling'wenya alishawahi Kuwa Moshi
Shahidi: Nakumbuka alikwenda Mara Mbili
Mallya: alikaa kwa muda gani
Shahidi: alilala Siku Moja
Mallya: Wapi
Shahidi: Hotel ya Aishi
Mallya: Mlangoni au Bar?
Shahidi: alilala Ndani
Mallya: alikaa wapi
Shahidi: mara ya Pili alifika Aishi Hotel na Baadae katoka akawa anakaa Moshi Mpaka tunamkamata
Mallya: Usiku huo alikuwa ametokea Kulala wapi
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Kwa Kumbukumbu zako Mohammed Ling'wenya ni Mwenyeji wa wapi
Shahidi: Mtwara
Mallya: Wewe Umekaa Moshi kwa Muda gani
Shahidi: Nyakati mbalimbali na Mafunzo mbalimbali
Mallya: Ulielezea Mahakama Utafutaji wenu ulikuwa wa Namna gani
Shahidi: Tulikuwa tunafika Maeneo Mbalimbali
Mallya: Kwa Siku Ya Kwanza Pasua Mlienda Saa ngapi
Shahidi: Majira ya alasiri
Mallya: ambapo Exactly Mlipoanzia ni Wapi
Shahidi: Rau Madukani
Mallya: Kutoka Rau kwenda Moshi police Central ni Umbali wa Kilometers ngapi
Shahidi: Siwezi Kukadiria
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba Jibu lake Lirekodiwe
Mallya: Kutoka Rau Kwenda KCMC Mlitumia Muda gani
Shahidi: Dakika 15
Mallya: Baada ya KCMC Mlienda wapi..?
Shahidi: Tulirudi Mpaka Majengo
Mallya: Unaweza Kukadiria Kama Muda gani
Shahidi: Kwa sababu Hatukuwa na Mwendo Sana tuliitumia Walau Dakika 45
Mallya: Moja ya Tunachojivunia Wachaga Moshi haina Foleni, ila endelea tu kujibu , Baada ya Majengo Mlienda wapi
Shahidi: Tukaenda Pasua,
Mallya: Mie napajua Kote, Mlitumia Muda gani Kutoka Majengo kwenda Pasua
Shahidi: Sikumbuki Muda Exactly nilikuwa siangalii Muda
Mallya: Ulikuwa ni Muda gani
Shahidi: Ulikuwa Muda wa Jioni
Mallya: Baada ya Kutoka Pasua Mkaenda wapi
Shahidi: Machame, Aishi Hotel
Mallya: Aishi ni Kitu gani Kijiji, Kata au Wapi
Shahidi: ni Hotel
Mallya: Ulipofika Aishi Mkafika Maeneo gani
Shahidi: Kingai aliingia Ka anaingia Ndani,
Mallya: Kwa hiyo ni Ushahidi Wako Kingai aliingia Ndani
Shahidi: hakuingia Ndani alielekea Sehemu ya Majengo
Mallya: Unaweza Kutuchorea Picha ya eneo la Aishi Hotel
Shahidi: Siwezi kuchora sababu Sikushuka Kwenye gari
Mallya: Baada ya Aishi Hotel Mkaenda wapi
Shahidi: Maeneo ya Boma Ng'ombe
Mallya: Mlitumia Muda gani Kufika BomaNg'ombe
Shahidi: Siwezi Kujua Muda nilitumia, Kikubwa tulichokiwa tunakifanya ni Kufanikisha Kazi yetu
Shahidi: Palikuwa peshaanza Giza
Mallya: Kwa Makadirio yako a kutoka Boma Mpaka Moshi ni Kilometer ngapi hivi
Shahidi: Inaweza Ikawa Kilometer 50 au Zaidi
Mallya: Nilikusikia unasema mlifika Moshi Sa 5 za Usiku
Shahidi: Saa 4 kwenda Saa 5
Mallya: Ulipata Kueleza Kwamba Kilichokufanya Usiandike Maelezo Muda huo ni nini
Shahidi: Nilishaeleza Mallya: hivi Mbowe Ukifika Kumuhoji saa ngapi Za Usiku Vile..?
Jaji: Suala la Maelezo ya Mbowe havipo Katika Kesi Ndogo
Mallya: Baada Ya Boma Ng'ombe Mlienda wapi
Shahidi: Mbele ya Boma Ng'ombe Kama Unaenda Arusha, Tulifika Maeneo ambayo tulihisi kwamba tungeweza Kuwakuta
Mallya: Kwa hiyo Wewe Ulikuwa unajiongeza Kwenda Sehemu zingine ambazo watuhumiwa awajakutajia
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Kwa hiyo Siyo lazima uende na Watuhumiwa Kwa sababu Ulikuwa aukitajiwa Sehemu A Unaweza Kwemda sehemu B
Shahidi: Watuhumiwa walikuwa wanatusaidia na pia Tulikuwa hatumjui
Mallya: Baada ya Boma Mlienda wapi
Shahidi: Tulirudi Moshi
Mallya: Palikuwa na Mwanga au giza
Mallya: naomba Nimuachie Mwenzangu amallizie Kuuliza Machache
KAUNDA: ulisema Ulipomkamata Mshitakiwa Wa 3 Ulimpeleka Central Police
Shahidi: Nili fikisha Kituoni
KAUNDA: Wakati huo Mlishafungua Kesi ya Madawa ya Kulevya
Shahidi: Ndiyo Unga Unaozaniwa kuwa madawa ya kulevya
KAUNDA: Wakati huo uliwaacha kwenye gari Muda wao wote wakiwa na Pingu Mikononi
Shahidi: Ndiyo
KAUNDA: haukuiambia Mahakama Kwamba ulipowarudisha ukiwafungulia Pingu
Shahidi: Ndiyo Sikusema
PAUL KAUNDA: na Hukusema Mahakamani Kwamba Uliwakabidhi Askari gani wa Chumba Cha Mashitaka kwa Majina yao na Force Namba zao
Shahidi: Sikuongozwa Kusema hivyo
PAUL KAUNDA: na Wala hujui Kilichotokea Kuanzia Muda unawakabidhi Watuhumiwa Muda Ule Usiku Mpaka Asubuhi
Shahidi: Sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Sahihi kwamba wewe Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Arumeru
Shahidi: ni sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba wewe Kazi yako Kuwasimamia Kazi Askari wa Chini yako
Shahidi: sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba Jeshi la Polisi limewafukuza Askari Wanne na Wasaidizi wa Polisi wawili, Wamesimamishwa
Shahidi: sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Wewe ni Mmoja wa Polisi wasaidizi waliosimamishwa Kazi Arumeru
Shahidi: Ni Masuala ya kiutawala Siyo Kesi hii
KIHWELO: ni sahihi Mohammed Ling'wenya Mlimtafuta Kupitia Mitandao ya simu
Shahidi: Siyo Sahihi KIHWELO: akitokea Mtu akasema Boazi aliitoa Malekezo Ya Watuhumiwa Kuletwa Dar es Salaam Siku ileile, Je Kati yake na wewe Nani atakuwa Muongo
Shahidi: Siwezi Kumsemea Mtu Mwingine
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba Watuhumiwa hawaKupokelewa Kituoni Moshi
Shahidi: Hakuna Utaratibu wa Kupokelewa Bali Kuna Sehemu ya kuandika Kuwakabidhi Watuhumiwa
KIHWELO: ni sahihi hapa Mahakamani hapa Kuna Nyaraka ya Kukabidhi watuhumiwa
Shahidi: Siwezi kulisemea
FREDRICK KIHWELO: nitakuwa Sahihi Nikisema Watuhumiwa waliingizwa Kituo cha Polisi Moshi Kwa Dhumuni la Kuwatesa
Shahidi: Utakuwa Haupo Sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Hukusaini Detention Register Wakati Unawakabidhi Watuhumiwa Kituo cha Polisi Moshi
Shahidi: NI SAHIHI
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba Watuhumiwa mliowakamata hawakuwa Wenyeji wa Moshi
Shahidi: Hautokuwa Sahihi
FREDRICK KIHWELO: una nyaraka Yoyote inayoonyesha Kwamba Mlipata BREAK DOWN Njia Panda Himo
Shahidi: Sina Kwa sababu Magari ya Serikali yana Utaratibu wake
FREDRICK KIHWELO: Akitokea Mtu akasema kwamba Central Police Dar es Salaam Siyo sehemu ya Kuhifadhi Watuhumiwa WA Ugaidi atakuwa sahihi
Shahidi: Sijui hilo
KIHWELO: Akitokea Mtu akasema Walipotoka Moshi Walifikia Polisi Tazara ambapo watuhumiwa wa ugaidi uhifadhiwa
Shahidi: Mimi Ndiyo nilikuwa na Watuhumiwa, Sikwenda Huko
KIHWELO: ni hayo tu
JAJI: Ingekuwa inaruhusiwa Ningekupigia makofi ila Upo Mahakamani, Umetumia muda Vizuri Kibatala Muda Utakutosha
Kibatala: Nitajitahidi Kibatala: Shahidi Unafahamu Kwamba UGAIDI ni Kesi Kubwa Sana
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Ulichukua Maelezo Kwa kifungu cha 57(3)
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kifungu Hicho Kinakuruhusu Kuchukua Record ya %Video au Sauti Wakati anakiri
Shahidi: Siyo lazima kutumia Hiyo
Kibatala: Sasa Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Palikuwa na fursa hiyo ya Kisheria lakini hukutumia kwa sababu fulani
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Mtu anapokiri Makosa yake Kuna hitaji la Kumpeleka Kwa Mlinzi wa Amani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kwa Mujibu wa Maelekezo ya Jaji Mkuu kwamba Mtu anapopelekwa kwa Mlinzi wa Amani kwanza anatakiwa Kumkagua Mtuhumiwa Kama ana majeraha
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Mohammed Ling'wenya alipelekwa Kwa Mlinzi wa Amani
Shahidi: Hapana
Kibatala: na Unafahamu Kwamba Kukiri Kwa Mohammed Ling'wenya Kulipaswa Kupelekwa Kwa Mlinzi Wa Amani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu na Hukumpeleka
Shahidi: Kimyaaaaa
Kibatala: Ulimpeleka Mohammed Ling'wenya Kwa Daktati Kuona Alikuwa na Majeraha
Shahidi: Hilo sina Jibu
Kibatala: Uliwaza Kumpeleka Mtuhumiwa Kwa Daktari Kuthibitisha Kwamba hana majeraha
Shahidi: Siyo Taratibu zangu za Kazi
Kibatala: Kuna sehemu kwenye CPA au PGO inakataza Wewe Kumpeleka Mtuhumiwa Kwa Daktari Kwa ajili ya kujiridhisha
Shahidi: Hapana
Kibatala: ili tuone kama Kweli Hamkuwa Mmetumia Muda huo Kuwatesa, je Dada wa Moses Lijenje Unamfahamu Jina lake
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Maelezo Yako ya Kuharibikiwa Gari Himo Kwenye Maelezo Yako Uliandika au Hukuandika
Shahidi: Sikuandika
Kibatala: Watuhumiwa Wanasema Mlipowatoa Moshi Mliwapeleka Tazara kisha Mbweni, Je Sababu za Kuwahamisha ni za Kiupelelezi au Kiusalama
Shahidi: Zote zote
Kibatala: Tuanze na suala la Upelelezi, Kama Mohammed Ling'wenya ameshakiri tayari uliogopa nini
Shahidi: Taarifa Kutoka Nje, Kuna wengine tulikuwa tunawatafuta
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Walipokuwa Central walikuwa in ISOLATION na Watuhumiwa wengine?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Ulipowapeleka Mbweni waliwekwa IN ISOLATION na Watuhumiwa Wengine
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je Kupima Ukweli Wenu, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulimwambia Mkuu wa Kituo au OCD kwamba Watuhumiwa Watengwe
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Nimesikia Umesema Kwamba Sababu ya Kuwahamisha Watuhumiwa Kutoka Central Dar es Salaam kwenda Mbweni ni kwamba Watuhumiwa Walipo Dar es Salaam wasijue Kinacho endelea, Je Mbweni ni Mkoa gani
Shahidi: Ni Dar es Salaam
Kibatala: Unamfahamu Afisa wa Jeshi anaitwa Chuma Chugulu
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Kule Arusha Kuna washitakiwa wa Ugaidi au hawapo
Shahidi: Wapo wapi K
Kibatala: Gereza la Kisongo, Masheikh,
Shahidi: Wapo
Kibatala: Maelezo yao yalichukuliwa Dar es Salaam
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Kuna Kifungu chochote Cha Sheria ya Mwenendo Wa Makosa ya Jinai na PGO inayolazimisha Mtuhumiwa achukuliwe Maelezo Sehemu tu ambapo faili lilifunguliwa
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Na ulijua Kwamba Shauri hili litafika Mahakamani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na wewe Kama Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Arumeru(OC-CID), Jukumu lako ni Kufunga Mianya yote ya kuharibu kesi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Kuna sehemu yoyote Ambayo Umeonyesha Kwamba kama angekuwa Tayari ningempa Simu yake au Simu yangu awasiliane na Ndugu, Jamaa na Marafiki zake...
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Kule Moshi, Nakuuliza Kuhusu Ufahamu wa Kuingia Na Kutoka Polisi Central Police.
Shahidi: Nafahamu kwa sababu nilisaini
Kibatala: Wewe Ndiye Uliyemuingiza Mohammed Ling'wenya na Kumtoa Mahabusu Moshi
Shahidi: nilikuwa na Afande Mahita
Jaji: liweke Vizuri hilo swali
Kibatala: Unataarifa sahihi Kuhusu Detention Register, Je Ulisaini Out Saa Ngapi,
Shahidi: Tarehe 06 Aug 2010 Saa 11 alfajiri
Kibatala: Kati yako wewe na Mahita nani alikuwa Custodian Officer wa Mohammed Ling'wenya
Shahidi: Mimi Mwenyewe
Kibatala: Aliyekimkabidhi Mohammed Ling'wenya pale CRO central.?
Shahidi: Mimi
Kibatala: Kingai alikwepo wakati mnawakabidhi polisi Central Dar es Salaam?
Shahidi: Ndiyo alikuwepo.... Lakiniiiiiiiiiiii
Kibatala: Hakuna cha lakiniiiiiiiiiiii hapa...
Kibatala: Wakati Unahojiwa na Wenzangu Kwamba Ulisema DCI BOAZI aliwambia kwamba Watuhumiwa Tuwapeleke Moshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Una' personal Knowledge ya Malekezo Ya DCI au Kingai Ndiye anayejua
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Naomba niishie hapo Mheshimiwa Jaji
Jaji: Serikali
Wakili wa Serikali: Shahidi Umeulizwa swali Kuhusiana na kutosema kwenye Ushahidi wako kama Hukusema kama ulimpa simu, kwa nini Hukusema
- Kibatala: OBJECTION kwanini.., Siyo swali nililouliza..
Jaji: Swali haliingi kwenye Record za Mahakama
Shahidi: Kama angeomba Mtu aje, Utaratibu Ungefanyika, Simu ingepatikana
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu Watuhumiwa Kutenganishwa Central na Kule Mbweni, Ukasema Hukusema Kwenye Ushahidi Wako Shahidi Mahabusu Wanatenganishwa...
- MTOBESYA: OBJECTION Kwenye Ufafanuzi, It's not an Open Check
Wakili wa serikali: Elezea kwa nini Hukusema Kama Mliwatenga
Shahidi: Kwa sababu anaye weza Kujua Watuhumiwa wamekaa Je huko Lock up ni Mtu wa Chumba Cha Lock Up
Wakili wa Serikali: Ukaulizwa Swali Ulikiri kwamba Mtuhumiwa anayekiri anatakiwa Kupelekwa Kwa Mlinzi Wa Amani, Ukaulizwa Ulimpeleka kwa Mlinzi wa Amani Ukasema Hapana, Ni kwanini
Shahidi: Hatukumpeleka kwa Mlinzi wa Amani, kwa sababu Tulikuwa tunawahi Kuhakikisha Hivyo Vitendo Vya Kigaidi havifanyiki
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali na Mtobesya Kwamba Kama Ulikuwa na Taarifa za Awali Ukasema Hukuwa na Taarifa
Shahidi: Nilikuwa na Taarifa za Awali, Siyo Za kina wakati namkamata Mtuhumiwa,
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Tukomee hapa
Jaji: Shahidi tunakushukuru Kwa Ushahidi wako Kwenye Kesi Ndogo
Wakili wa Serikali: Robert Kidando Mheshimiwa Jaji tunaomba Hairisho Mpaka Kesho tarehe 12 Mwezi wa 11 2021, Ilituendelee na Shahidi Mwingine Na Ilituweze Kujiandaa Tunaomba Kesi ianze Saa 4 Asubuhi
Jaji: Utetezi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: Shahidi tunakushukuru Kwa Ushahidi wako Kwenye Kesi Ndogo
- Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na Jaji
Jaji: Maombi ya hairisho yamekubaliwa, nahairisha Mpaka Tarehe 12.11.2021. Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi Saa 4 Asubuhi
- Jaji anatoka
Leo tarehe 11/11/2021 yanatolewa maamuzi ya kesi ndogo Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe.
Kujua jana kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri Mahakama Kuu kesi ndogo ya Mbowe, Superitendent Jumanne Malangahe atoa Ushahidi
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
Picha: Watu mbalimbali waliohudhuria Mahakama kuu leo 11/11/2021
UPDATES;
Jaji ameingia Mahakamani Sasa Saa 5 Na Dakika 15 Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa.
Wakili wa Serikali Robert Kidando anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula
3. Jenitreza Kitali
4. Nassoro Katuga
4. Esther Martin
5. Tulimanywa Majige
6. Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anawatambulisha jopo la Mawakili wa Utetezi:
1. Jeremiah Mtobesya
2. Paul Kaunda
3. Fredrick Kihwelo
4. Dickson Matata
5. Iddi Msawanga
6. John Mallya
7. Alex Massaba
8. Khadija Aaron
9. Evaresta Kisanga
10. Maria Mushi
- Jaji anawaita washtakiwa wote wanne, na wanaitika kwamba wapo.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri linakuja Kwa ajili ya kusikiliza Uamuzi wa Mahakama, sisi tupo tayari Wakili Peter Kibatala: Nasi pia kwa Ruhusa yako tupo tayari Kupokea Uamuzi na Kuendelea na Kesi.
- Jaji anaandika Kidogo
Jaji: Jana nilisikikiza Pingamizi la Upande wa Utetezi, Na baada ya Kusikiliza Pande zote Mbili, Maamuzi yapo tayari Jana wakati Shahidi akitoa Ushahidi alieleza Kwamba Baada ya Kupewa Maelekezo ya Kumwandika Maelezo Mshtakiwa namba tatu
Jaji: Na baada ya kupitia Nyaraka hiyo Shahidi alisema anaitambua na baada ya hapo aliomba Mahakama Ipokee Nyaraka hiyo kwa ajili ya Utambuzi, Kitu ambacho Mawakili Wa Washtakiwa wote wanne walipinga Vikali
Jaji: Inapaswa Shahidi ajenge Misingi Kwamba Kwa namna Gani Kielelezo Kimemfikiaje Mahakamani, Na Mawakili Wakasema Kinachotolewa Mahakamani ni Register siyo Entry Kwa Mfano Ingekuwa na Features ambazo zinaonyesha Register hiyo Inatumika Central tu na siyo Mahala Pengine popote
Na Pale ambapo Shahidi ametoa Ushahidi wake anaweza Kufafanua, Wakaomba Mahakama Ione Kielelezo Kilichopo Mahakamani shahidi anaweza Kutoa Ushahidi Wake, Wakaeleza tarehe 07 August 2020 namba alivyo fika Saa 11 Alfajiri na Jinsi ambavyo Shahidi aliweka Entry na aliweza Kukitambua
Jaji: na hicho ndicho kimezua shaka. Na Upande wa Mashtaka Walipata nafasi Ya Kujibu kwa Kuwakilishwa na Abdallah Chavula na Pius Hilla Walisema Kwamba Mapingamizi hayana Mashiko, Wakaja na Kesi ya DPP VS SHARIF Authentication ya Mahakama Inapaswa Kufanywa na Ushahidi Wa Shahidi.
Wakaomba Mahakama itofautishe Kesi ya DPP VS SHARIF ATHUMAN kwamba kesi ile Kielelezo Kilikuwa Gari na Kwenye Kesi hii Kielelezo ni Nyaraka, Wakarejea Kesi ya CHARLES GAZILABO dhidi Ya Jamhuri Kwamba Kesi hiyo iliweka Mambo Matatu ya Relevance, Competence na Shahidi Husika
Wakasema Kwamba Kwa namna ambavyo Shahidi alikuwa anatoa Ushahidi Wake ni Competent. Wakasema Kwenye Kesi Ya CHARLES GAZILABO Kwamba Mtu anaye weza Kuelezea Kielelezo NA kukitambua, Kitu ambacho Shahidi alifanya.
Shahidi alieleza Kwamba alifika kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam, Hiyo inathibitisha kwamba Shahidi anaweza Kufanya Utambuzi na wakaomba Mahakama Itupilie mbali, Upande wa Utetezi Walipata tena nafasi ya Kujibu na Kuona Bado Mapingamizi yao yanayo Sababu
Jaji: Na wakaendelea Kusema Kwamba Suala Zima la Chain of Custody, Mahakama Imeshatolea Maamuzi Kwamba Chain of Custody Inaweza Kujadiliwa Mwishoni, Wakasema Shahidi alijitahidi Kueleza Kwamba aliweka Entry na hilo pekee ndiyo lina fanya Shahidi aonekane anaweza Kukitambua.
Jaji: Kwenye kesi Ya SHARIF ni kwamba wanaona Kanuni inaweza Kutumika Kwenye kesi yoyote, Na Kwamba Shahidi ameeleza Entry na a siyo Kielelezo Chenyewe na Kwamba Suala la Authentication halijaweza Kukidhiwa, Na swala Zima la Kuamua Chain of Custody Wali endelea Kusema Swala La Kupinga Kielelezo ni Jukumu lao Kupinga Wakati Wa Uchukuliwaji, Upande wa Mashtaka wamekosa Hoja za Msingi kuhusiana na Mapingamizi yao.
Na Kwamba Hakuna Features Mahususi Kuhusiana na Kielelezo hicho ili Kutofautisha Detention Register na Detention Register zingine zinazotumika katika Vituo Vingine.. Na suala la Chain Of Custody haijaelezwa Vizuri ni wapi Walipo toa Kielelezo hicho, Kwamba kwa Kumbukumbu zilizopo bado Kielelezo Kipo Chini ya Mahakama. Huo ndiyo ulikuwa Mwisho wa Muhtasari. Sasa twende kwenye maamuzi.
Jaji: Identification of EXHIBIT, Establishing Chain Of Custody, Identification of Objects. Haya siyo Maneno yangu ni Maneno ya Maamuzi ambayo nimeyanukuu hapo juu. Lengo la Chain Of Custody wanapaswa Kueleza Kielelezo Wamekitoa wapi.
Na Kuhusiana na Competence ya Shahidi imeelezwa Kwenye kesi ya CHARLES GAZILABO, KHAMIS ADAM Kwamba Mtu ambaye amekifanyia kazi Kielelezo siyo tu anaweza Kukitolea Ushahidi Bali anaweza za Pia Kukitolea Maelezo
Jaji anasoma maamuzi ya kesi hiyo aliyonukuu
MAAMUZI
JAJI: Tunakubaliana kwa pamoja Kwamba Pingamizi linapinga ipokelewaji wa Vielelezo na Siyo Jambo geni Mahakamani, Na Maamuzi Yamefanywa na Mahakama zetu katika Upokeaji wa Vielelezo Mahakamani. Maamuzi yameonyesha Taratibu, Kanuni na Muongozo.
Kufuatia Maamuzi ya SHARIF MOHAMMED na wenzake Mahakama ya Rufani Ilitoa Maamuzi Kwamba tunao Ushahidi Wa Namna Nne Uhalisi, Testimonial, Documentary Evidence, Na Kwamba Mahakama inaweza Kupokea Ushahidi Mahakamani Wakati wowote.
Mahakama Ijiridhe Kama Ushahidi ni Relevance, Material na Competence, Na Katika Maamuzi yake wamejadili kwa kina kuhusu Ushahidi Halisi. Nimesema Mpaka Mwisho Sijaona Kwamba Vigezo ambavyo vinatumika Katika Real Evidence haitakiwi Kutumika katika Kupokea Documentary Evidence.
- Jaji amemaliza kusoma Maamuzi ya Shauri hilo kama Rejea yake,
Jaji: Kimsingi hayo ndiyo maamuzi ya mahakama ya Rufaa.. Kwa sababu hiyo sasa ilikupima Competence ya Shahidi, Na Kwa Kesi hii Shahidi ameeleza Vizuri kuhusu Kielelezo hicho ambacho alikotumia Kuweka ENTRY ili Kumtoa.
Shahidi Kwenda Kumchukua Mtuhumiwa Maelezo yake. Kwa Maana hiyo anayo Competence. Kuhusiana na Relevance ni Ukweli kwamba Kipo Relevance sababu inadaiwa ndiyo walitumia Kielelezo hicho Kumtoa Mtuhumiwa
Kuhusiana na Materiality ni kweli kabisa kwamba kitasaidia Mahakama Kufanya Maamuzi, ikiwemo Katika Pingamizi Kwamba Mshitakiwa hakuwa hi Kuwepo Katika Kituo hicho cha Polisi. Mahakama hii inaona kwamba ni sahihi kabisa kuendelea kutumika.
Jaji: Imebakia suaala la Chain Of Custody, Ni kweli Shahidi namba Moja ameeleza Kwamba anaweza Kutambua Kielelezo hicho Kwa Majina yake na Sahihi Yake na Majina ya Mtuhumiwa, Ukweli ni kwamba ameweza Kukitambua, Ingawa Mr. MTOBESYA amepinga Kwamba Features zilizoelezwa ni za Entry na siyo Register Yenyewe.. Lakini Mahakama yenyewe inaweza Kutambua kuwa Kielelezo hicho huwezi Kutenganisha Entry na Register. Na Kuhusiana na Chain Of Custody Shahidi hajeleza Chain of Custody Kwamba ni Kwa namna gani Kielelezo hicho Kimemfikia.
Jaji: Ni kweli Kwamba hajaeleza ametoa wapi, Ni kweli Kwamba Kielelezo Kipo Kwenye Kumbukumbu ya Shauri Lingine, Ili Mahakama ione kama kilifuata Utaratibu kilipaswa kionekane kwamba ni kweli Kilifuata Utaratibu wa kiutawala kutoka Mahakamani.
Na Kwa namna hiyo Kielelezo kinajifuta Chenyewe kwa sababu Shahidi hakuonyesha namna gani kilimfikia, Assumption ni kwamba Kielelezo Kipo Kwenye Chumba cha Mtunza Kielelezo Cha a Mahakama, Hakuna Ushahidi Kwamba Shahidi alikipataje kuja Mahakamani.
Jaji: Kwa sababu hiyo mahakama inakikataaaaa kielelezo hiki natoa amri.
- Mawakili wa pande zote wanasimama na kuinama kuonyesha kukubaliana na uamuzi wa Jaji.
Jaji: Shahidi wenu yupo wapi tuendelee
Jaji: Shahidi nakukumbusha Upo chini ya Kiapo ambacho Ulikiapa wakati Unatoa Ushahidi Wako
Wakili wa Serikali Robert Kidando ameanza kuuliza maswali
Wakili wa Serikali: Shahidi Ulisema Kwamba Siku ya Tarehe 07 August 2020 ulimchukua Mohammed Ling'wenya Kwenda Kumchukua Maelezo, Eleza Siku hiyo alikuwa na hali ganiShahidi: Wakati na chukua Mohammed Abdilah Ling'wenya alikuwa Mwenye Afya Njema na Hakuwa na Tatizo lolote
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumchukua Ulimpeleka wapi
Shahidi: Nilimpeleka Pembeni Kidogo Kwenye Chumba Kwa ajili ya Mahijiano na Mtuhumiwa huyo
Wakili wa Serikali: Elezea Baada ya Kukaa Pamoja nini Kiliendelea
Shahidi: Nikijambulisha Kwa Majina Kwamba Mimi ni ASP JUMANNE MALANGAHE, Na Mtuhumiwa akajitambulisha kwa Majina yake Kwamba anaitwa Mohammed Abdilah Ling'wenya alimaarufu kama DOYI
Wakili wa Serikali: Elezea Ni kitu gani sasa Ulifanya Baada ya Kujitambulisha
Shahidi: Nilimuonya Kwamba anatuhumiwa kwa Makosa ya Kula Njama za Kutenda Matendo Ya Ugaidi, Nilimueleza kwamba Katika tuhuma hizo alazimiki kueleza Chochote isipokuwa kwa hiari yake Mwenyewe chochote atakachokieleza kinaweza Kutumika kama Ushahidi Mahakamani, Vilevile anayo Haki ya Kuwepo Mwanasheria Wake, Ndugu yake, Jamaa yake, Rafiki ili ashuhudie Wakati Maelezo hayo yakiandikwa, Baada ya Hatua hiyo, Mimi Nilisaini na Mtuhumiwa alisaini ilikuonyesha nilimuonya.
Shahidi: Baada ya kumaliza Hatua hiyo Mtuhumiwa Mohammed Abdilah Ling'wenya alimaarufu DOYI alijibu Onyo hilo.. Kwamba yeye Mohamed Abdilah Ling'wenya Alimaarufu DOYI ameonywa na Mimi ASP JUMANNE MALANGAHE anatuhumiwa kwa Kosa la Kula Njama kutenda Vitendo Vya Ugaidi Chini ya Sheria namba 24 ya Sheria ya Kupambama na Ugaidi, Kwamba alazimishwi Kusema Lote isipokuwa kwa hiari Yake Mwenyewe. Chocolate atakachoandika Linaweza Kutumika aka Ushahidi Mahakamani.
Na pia anaweza Kuwepo Mwanasheria Wake, Ndugu yake, Jamaa yake, au Rafiki ili ashuhudie Wakati Maelezo yake yakiandikwa. Baada ya Mtuhumiwa kuulizwa Onyo hilo kama Yupo Tayari Kutoa Maelezo yake, Mtuhumiwa akajibu Ndiyo Nipo tayari, Nilimuuliza nani awepo Wakati anatoa Maelezo yake, Mtuhumiwa alijibu yeye Mwenyewe anatosha Wakati wa Kutoa Maelezo yake, alisaini na Mimi nikasaini, baada ya hapo akawa tayari Kutoa Maelezo Yake, Saa 2 na Dakika 20 nilianza kuandika Maelezo Ya Mtuhumiwa,
Wakili wa Serikali: Wewe Ulifanya nini baada ya yeye Kusema yupo tayari Kutoa Maelezo
Shahidi: Nilimuuliza Mtuhumiwa Ushiriki wake Kuhusu tuhuma nilizomueleza
Shahidi: Nilimueleza kila anapohusika na ambapo yeye alikiri
Wakili wa Serikali: Wewe baada Kueleza ulifanya nini
Shahidi: Nilikuwa na andika Kwenye Karatasi, Fomu kile alichokuwa ananieleza
Wakili wa Serikali: Kilikuchukua amuda gani?
Shahidi: Muda wa Masaa 2 na Dakika 42
Wakili wa Serikali: baada ya Kumalizia Kuandika Ulifanya nini?
Shahidi: Nilimpatia Maelezo ayasome, ilikuweza Kuongeza, Kupunguza au Kufanya Marekebisho kwa yake aliyiyasema
Wakili wa Serikali: Baada ya Mtuhumiwa Kusoma Maelezo hayo akasemaje
Shahidi: Ameridhika na hana cha Kupunguza wala Kuongeza
Wakili wa Serikali: Ulifanya nini baada ya kuandika
- Kibatala: OBJECTION anachofanya Wakili anajua Hakiruhusiwi
Wakili wa Serikali: Baada ya kumaliza Kuandika Ulifanya nini?
Shahidi: Alisaini na Mimi nikasaini, na baada ya hapo nikaandika Uthibitisho wangu mimi Mwenyewe.
Wakili wa Serikali: Baada ya akumaliza Kuandika Uthibitisho huo Ulifanya nini
Shahidi: Niliandika Muda wa Kuandika Maelezo
Wakili wa Serikali: baada ya Kumalizia Kuandika Maelezo Ulifanya nini na Mtuhumiwa
Shahidi: Nilimchukua na Kumrejeaha Chumba cha Mashtaka
Wakili wa Serikali: Maelezo ya Mshitakiwa Mohammed Abdilah Ling'wenya uliyapeleka wapi
Shahidi: Kwa Assistant Inspector Swila
Wakili wa Serikali: Ilikuwa ni Lini?
Shahidi: Ilikuwa ni Siku hiyo hiyo
Wakili wa Serikali: Elezea Baada ya Shughuli hiyo Ulikutana wapi tena na Mtuhumiwa
Shahidi: Niliondoka Kwenda Kufanya Majukumu Mengine kwa Kadri nilivyokuwa naelekezwa na ACP kingai, Siku ya tarehe 08 August 2020 Majira ya Saa 5 Asubuhi Tukiwepo na Inspector Mahita, Tulielekezwa na Afande Kingai Kumuhamisha Mtuhumiwa na Kumpeleka Kituo cha Polisi Mbweni.
Wakili wa Serikali: Wakati Mlielekea Mbweni Ni kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Hakuna Kilichoendelea, Tulipofika Tukiwakabidhi watuhumiwa, Na Kwenda Kuonana na Kiongozi wetu ACP KINGAI kwa Upelelezi wa watuhumiwa Wengine
Wakili wa Serikali: Elezea Baada ya hapo Ulionana naye wapi?
Shahidi: Sikuwahi Kuonana tena na Mtuhumiwa huyo..
Wakili wa Serikali: Kwa Ufahamu Wako Vituo ambavyo Mohammed Abdilah Ling'wenya aliweza Kufikishwa ni Vingapi?
Wakili wa Serikali: Unasema Siku Mnampeleka Kituo Cha Polisi Mbweni hakuna Kilichofanyika zaidi ya kumkabidhi pale, Sababu hasa ni nini?
Shahidi: Sababu zilikuwa za Kiupelelezi, Sababu Kuna Mwingiliano Wa watuhumiwa wengi wanaingia na Kutoka ni wengi.. Tulihofia Taarifa zinaweza Kufika Kwa Watuhumiwa ambao bado tunawatafuta Kwa urahisi.
Wakili wa Serikali: Siku unaandika maelezo ya Mtuhumiwa pale, unasema ulimpa Inspector Swila, Je Inspector Swila alipeleka wapi? -
- Mtobesya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji huyo siyo Swila na hawezi Kujibu kwa niaba ya Swila
Wakili wa Serikali: Ngoja Nirudie Swali
Wakili wa Serikali: Ulipompa Swila hizi Karatasi, alifanya nini na Hizo Karatasi
Shahidi: Ndiyo tulikuwa tunampa Nyaraka zetu, Kwa hiyo alizochukua akaenda Kuweka kwenye Jalada
- Mtobesya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hizo ni hearsay
Jaji: Jiande uje kumuuliza labda walikuwa naye.
Shahidi: Swila amuda Mwingi tulikuwa naye, alienda Kuweka kwenye Jalada la Upelelezi
- Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Wakili anahama Eneo, Je ulichokiandika Siyo HearSay
Wakili wa Serikali: Sisi Bado hatuoni tatizo, huyu Mohamed Abdilah Ling'wenya amepinga Maelezo ya Onyo kwamba hakuwahi Kufika Kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam na ajawahi Kuandika Maelezo hayo..
Shahidi: Siyo Kweli, Mimi Mwenyewe ndiyo Niliyempeleka Pale, Nikaenda Kumchukua Mimi Mwenyewe Kutoka Kwenye Chumba Cha Mashtaka Nikiwa Pekee yangu bila Uwepo wa Askari Mwingine yoyote akiwa na hali Nzuri, na Mimi Niliondoka nikiwa nje ya Kituo na yale maelezo, Nikampigia Assistant Inspector Swila yale achukue yale maelezo ili aweke kwenye Jalada la Kesi.
Wakili wa Serikali: Wewe una utbitisho gani kwamba uliandika Hayo Maelezo siku ya tarehe 07 August 2020
Shahidi: Alikuwepo Askari aliyekuwepo pale Chumba cha Mashtaka. Na baada ya kumaliza Kuandika Maelezo Askari huyo huyo alimpokea na Kumrudisha Lockup.
Wakili wa Serikali: anachosema ni kwamba ulimtishia kwa Bastola ilikutoa Maelezo
Shahidi: Siyo Kweli, Sikuwahi Kumtishia Mtuhumiwa huyo Kwani alikuwa na Ushirikiano, Sikuwa na Sababu hiyo
- Kibatala: OBJECTION, huyu labda hajasikia Vizuri Mapingamizi, nayasoma tena kwa sauti ayasikie
Wakili wa Serikali: Sawa Ngoja Nirudie, Ulimtishia Kwamba Asipo Saini Ile Karatasi ya Maelezo basi yale Mateso Mliyompatia Moshi Mtayarudia
Shahidi: Si kweli Sikumtishia kwa sababu sikuwa na sababu hiyo.
Wakili wa Serikali: Maelezo ya Mohammed Abdilah Ling'wenya ukiyaona unaweza Kuyatambuaje
Shahidi: Naweza Kuyatambua Kwa Majina Yangu, Sahihi yangu, Uwepo wa Majina ya Mtuhumiwa na Sahihi zak na Yote aliyo I eleza Nikaandika kwenye Karatasi ya Maelezo.
Wakili wa Serikali: Samahani Mheshimiwa Jaji tunaomba tumpatie Nyaraka Kwa sababu ya Utambuzi
- Shahidi anamkabidhiwa Nyaraka
Wakili wa Serikali: Angalia Nyaraka hiyo Kama Umeitambua na Useme ni Kitu gani?
Shahidi: Ndiyo nimeitambua Nyaraka hii Kama Maelezo Niliyoaandika kutoka kwa Mohamed Abdilah Ling'wenya Maarufu Kama DOYI,
Wakili wa Serikali: Umeitambuaje?
Shahidi: Kwa Majina Yangu, Sahihi Yangu Pamoja na Saini zake pamoja na aliyoyaeleza
- Kibatala: OBJECTION kwa Stage ya Utambuzi anatakiwa asifike kwenye aliyoyaandika Sababu ni Content
Wakili wa Serikali: Sisi hatuoni tatizo
Kibatala: Kwa Stage ya Utambuzi, aliyoyaandika ni Content
Jaji: content yake hatuingii, anaishia Kusema ameyaona
Wakili wa Serikali: Ungependa Mahakama ifanye nini katika Hayo Maelezo uliyoandika kutoka Kwa Mohammed Abdilah Ling'wenya alimaarufu kama DOYI
Shahidi: Ningependa Mahakama Iyapokee kwa Utambuzi
Mtobesya: Hatupingi Upokelewaji wa Maelezo haya Kwa niaba ya Mshtakiwa wa Kwanza Sababu ni Zifuatazo Naomba Iwe on record Kwamba Mahakama inayajua hayo Maelezo lakini Mshtakiwa wa tatu Amekataa hayo Maelezo Kutokupinga huku Hakumaanishi Kwamba Mshtakiwa anakubaliana na Content.
Wakili wa Serikali S Pius Hilla: OBJECTION Mheshimiwa Jaji natafakari kwamba hupingi lakini kwa conditions kwamba lazima sababu zieleweke, Kama hupingi, Lakini unapoongezea Vitu Vingine inamaana hukubaliani, Tunatengeneza Record gani kwa Mahakama. Kama kuna Jambo it's better akapinga tu hadharani..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: kwa Kuongezea tu, hili zoezi la Trial Within Trial na Hii Conditions alizo +toa hapa hairuhusiwi.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Sijui Kwanini Wenzangu Wamesimama, Wenzangu Waniambie Kwamba Ni Sheria gani inakataza Ninaposema sipingi siruhusiwi Kuongeza Maneno.. Sijui Wenzangu Wanahofu gani labda.. Wakasome Kesi ya Martha Weja sisi Kama Utetezi tunaruhusiwa Kuhoji content.
Jaji: katika Kesi yoyote Mahakama haijui chochote, Bila nyinyi Kueleza Mahakama, Mahakama Imeelekezwa Kwamba Isiyapolee yanayo Vunja Sheria yoyote, Sioni Tatizo Kwa Mtobesya Kuzungumza alichozungumza na huwezi kujua atakitumia wapi.
Mtobesya: naomba nikumbushwe niliishia wapi
Jaji: uliishia Mheshimiwa Jaji
Mahakama: Kicheko
Jaji: Unakubaliana na Mahakama Kupokea Lakini Hukubaliani na Content..
Mtobesya: naomba niishie hapo
- Anasimama Wakili Paul Kaunda...
PAUL KAUNDA: kwa niaba ya Mshtakiwa wa Pili tunaomba kufunga Mkono kilichozungumzwa na Wakili wa Mshtakiwa Wa Kwanza Fredrick Kihwelo: Tunakubaliana na Uwepo wa Nyaraka hii lakini hatukubaliani na Kilichopo Ndani
Kibatala: Kwa niaba ya Mshtakiwa wa Nne na sisi Hatupingi, Tunategemea Kuitumia Nyaraka hii katika Kuhoji Dodoso katika kesi hii Ndogo
Jaji: Yaliyosemwa na Mtobesya Mnalolote la Kujibu (Mashtaka) WS Wanateta Kidogo napokea kama ID namba 1
- Wote wanakubali.
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Naomba Dakika Mbili Nishauriane na Wenzangu Kuhusu Hoja ya Mtobesya kama Kuna la Kumjibu..
Wakili wa Serikali: Off Record Kwanza, Kuna Jambo la Mtobesya Kwamba Kwenye kesi ya Martha Weja, Tukasema tunaomba tujiridhishe kwanza.
Mtobesya: Kwa haki tuwaache wajiridhishe tu, Ni Kesi ambayo Imeripotiwa Kwenye TANZANIA LAW REPORT ya Mwaka 1982 Ukurasa wa 35..
Kibatala: nawakumbusha kwamba wenzetu wazingatie na muda kwa sababu leo tumeamza Saa tano na shahidi ana siku mbili kizimbani.
Jaji: Siku 3 labda kwenye kesi Ndogo ndiyo Siku 2..
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa tupewe tu Muda wa Kutosha kwa sababu hatuna hapa na hatuwezi Kupata ipo Ofisini
Jaji: Mtobesya ametaja Mpaka Kurasa labda anayo hapo.
Mtobesya: Hapana sina hapa ni kesi ya siku nyingi lakini tunatumia sana, Naweza kuiomba na Mimi ofisini Wakascan wakanitumia
Jaji: Natoa Hairisho la Dakika 45, tutarudi Saa 8 Jaji anatoka.
Zinapigwa kelele za kooooooortiiiiiii
Jaji ameingia.. Kesi inatajwa... Quorum zipo vile vile.
Mtobesya: Shahidi Wakati Mnamkamata Ling'wenya ni taarifa zipi Mlikuwa nazo tayari?
Shahidi: Taarifa tulizokuwa nazo alikuwa ni Miongoni Mwa Kundi ambalo lina fanya Njama Kwa Kufanya Vitendo Vya Kigaidi ambavyo ni Kushiriki katika Kulipua Vituo Vya kuuzia Mafuta Kukata Miti na Kuweka Barabarani, Kulipua maeneo yenye Mkusanyiko wa watu na Kuhamasisha Maaandamano ya siyo na Kikomo.
Mtobesya: Ni hizo Taarifa tu au Mlikuwa na Zingine?
Shahidi: Kimyaaa
Mtobesya: Ni nani aliwasaidia Kuwapa Taarifa Mpaka Mkajua Eneo alilokuwa Ling'wenya?
Shahidi: Nilikuwa na Mkuu wangu Afande Kingai yeye Ndiye alikuwa anajua aliyekuwa nampa taarifa nilikuwa naenda Field Kuthibitisha tuhuma kama Mtuhumiwa huyo anahusika
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji ilichukua muda gani, tangu unatengeneza Dhana hiyo Mpaka Mnamkamata Ling'wenya
Kimyaaaaaaaaaa kinatawala kwa sekunde kadhaa
Mtobesya: Nitakuwa sahihi Kwamba Mpelelezi yoyote kabla hajafanya Upelelezi anakuwa na dhana Kichwani unapoenda Field Unaenda kuthibitisha Kama ni Chanya au Hasi ni sahihi?
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji Kwenye Shauri hili Dhana yako ilikuwa ni nini?
Jaji: anamuuliza Shahidi kama ameelewa Swali
- Shahidi anapata kigugumizi kidogo anashindwa kuongea hapa.. Lakini anafanikiwa kuendelea..
Shahidi: Ni palepale nilipopata Taarifa na Kuanza Kutafakari na haikuchukua Muda Mrefu
Mtobesya: Mueleze Jaji Taarifa hizo ulizipata lini
Shahidi: Siku ya Tarehe 04 August 2020
Mtobesya: na Ling'wenya Mlimkamata tarehe ngapi?
Shahidi: Naomba nirejee Nyuma ya Swali Lako ulilokuwa Umeniuliza
MTOBESYA: enheeeeeeee!
Shahidi: UMENIULIZA Iinachukua Muda gani Kuniwezesha Kwenda Field
Mtobesya: Sijakuuliza Swali hilo Shahidi: Dhana ni Kama Kitu ambacho huna a Uhakika nacho
Mtobesya: Hapa namaanisha HYPOTHESIS, Mpelelezi Yoyote lazima awe na Hypothesis
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mtobesya: Nakurudisha Kwenye Swali Sasa, Je Mlimkamata lini Ling'wenya
Shahidi: Tarehe 05 August 2020
Mtobesya: Maelezo Ya Ling'wenya uliyaandika lini
Shahidi: Tarehe 07 August 2020
Mtobesya: Kwa hiyo nitakuwa Sasa Kwamba Wakati Unamuhoji ulikuwa na Taarifa
Shahidi: Hapana Sikuwa na Taarifa
Mtobesya: Siwezi Kukunyonga kwa Majibu yako. Haya Umesema Ling'wenya alikiri Kujihusisha Kufanya Vitendo hivyo ni Vipi
Shahidi: Kwamba kweli alijihusisha na Vitendo Vya kupanga Njama
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema Mpelelezi asiandike Maelezo ya Mtuhumiwa, Kwa sababu Mpelelezi anataarifa Nyingi Wakati anampeleleza?
Shahidi: Hapana Siyo Sahihi
Mtobesya: Kwa hiyo pale ambapo Kuna Askari Mwingine na Mpelelezi Yupo Hairuhusiwi Askari Mwingine Kuchukua Maelezo
Shahidi: Hapana Inaruhusiwa
Mtobesya: Zoezi la Kuchukua Maelezo lilianzishwa na nani
Shahidi: Mimi Ndiyo Wajibu wangu
Mtobesya: Kwa hiyo iingie kwenye Record Kwamba ni wewe Ndiyo Uliomba Kuchukua Maelezo?
Shahidi: ni Wajibu wangu
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi kuna aina 2 Uchukuaji wa Maelezo, pale ambapo Mshtakiwa anaomba au Askari anataka Kufanya hivyo
Shahidi: Hapana Mtuhumiwa hawezi Kuomba
Mtobesya: Kwa hiyo Hakuna Sehemu Mtuhumiwa anaweza Kuomba Kuandikwa Maelezo?
Shahidi: inategemea na Mazingira
Mtobesya: Kwa hiyo tunakubaliana kwamba mtuhumiwa mwenyewe anaweza kuomba kuandikwa Maelezo?
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Jaji: Kama hujamuelewa uliza wakueleweshe...
Shahidi: Natafakari kidogo
Jaji: Ujibu kwa speed sasa
Mtobesya: Kwa hiyo Kuna namna Mbili au Moja
Shahidi: Hakuna Namna mbili
Mtobesya: Maelezo uliyachukua kwa namna ipi Shahidi Kwa namna Mbili Baada Ya Kumuuliza na Yeye Kuwa anajibu
Mtobesya: Kwa hiyo Maelezo Yake yanatokana na Majibu yako
Shahidi: Kulikuwa na Maswali na Sehemu zingine pana Maelezo
Mtobesya: Nilikusikia wakati hujaanza Kuchukua Maelezo Kwamba Ulimpatia Haki zake za Kuwa na Wakili na Ndugu halafu akasema ataandika Mwenyewe, Lakini Hukusema Kwamba Wakati Wote Mnamkamata Mpaka Mnamchukua Maelezo kwamba Hamkuwezesha Kukutana na Ndugu.
Shahidi: Sahihi Sikusema
Shahidi: Ni yale yanayo chukuliwa Kuhusu Mtuhumiwa anahusishwa na Kutenda aina fulani ya Kosa
Mtobesya: Ni hivyo tu?
Shahidi: INATOSHA
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi nikisema Maelezo ya Onyo Yanatakiwa Kuonyesha Mtuhumiwa Kosa analo tuhumiwa nalo
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi Kwamba Kosa Unalomuonya Nalo ni lazima liwe limetamwaka Kwenye Sheria
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi Kwamba Maelezo ya Onyo Yanatakiwa kuwa Sheria na inatakiwa Kuonyesha Kifungu Unachomuonya nacho
Shahidi: Siyo Kweli, unaweza Kumwambia kwa Maneno tu
Mtobesya: Kwa hiyo siyo Muhimu Kumtajia Kifungu unacho Muonya nacho?
Shahidi: Ni Muhimu kwa Minajiri ya Kumuonya mshtakiwa Mwenyewe
Mtobesya: Kwa hiyo kwako wewe Siyo Muhimu?
Shahidi: Nilisahau lakini nilikuwa nishamwambia
Mtobesya: Nitakuwa sahihi Kwamba ni Matakwa ya Kisheria, Baada ya zoezi la Kuonya Kuisha Tarehe, Mwaka na Muda lazima viwe katika fomu unayotumia Kumuonya
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: na wewe Uliweka hivyo
Shahidi: Ndiyo Niliweka
Mtobesya: Tutaona baadae kama Uliweka
Mtobesya: na nitakuwa Sahihi Muda wa Kuonya Siyo Muda wa Kuchukua Maelezo, Unamuonya kwanza kisha Unamchukua Maelezo
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Kwa hiyo ni sahihi Kwamba muda wa Kuonya ni Tofauti na muda wa Kuchukua Maelezo
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Twende kwenye Hitimisho la Kuandika Maelezo pale unapotakiwa Kuthibitisha, nitakuwa Sahihi nikisema Ufungaji wa Maelezo ya onyo una namna Mbili au Tatu kwanza wa Mtu anaye Jua Kusoma na Kuandika na ameridhia Kwa anaye andika, ambaye ajui Kusoma na Kuandika au amekataa na Mwisho Mtu ambaye amekataa
Shahidi: Siyo Sahihi
Mtobesya: Haya tueleze Wewe Wa kwanza anathibitisha vipi
Shahidi: Yeye Mwenyewe anaandika Kwamba nimeyasoma na Kuyaelewa
Mtobesya: na hiyo inaonekana katika Statement uliyoiandika
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mtobesya: na wewe Mwenyewe Unaandikaje Mwishoni?
Shahidi: Unathibitisha Kuandika Maelezo ya Mtuhumiwa huyo
Mtobesya: huyo ambaye amesoma na kuandika, anathibitisha Vipi? KWA signature na Dole Gumba Maana havitumiki kwa Pamoja.
Shahidi: Vyote Vinatumika
Mtobesya: na huo ndiyo Ushahidi wako
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Unafahamu PGO ni Nini
Shahidi: Nafahamu Ndiyo
Mtobesya: Nitakuwa sahihi Kwamba Ndiyo Kitendea Kazi chenu cha Kila Siku
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Haya Mwambie Mheshimiwa Jaji PGO inasemaje
Shahidi: Kwa yule ambaye anajua Kusoma na Kuandika ataweka Sahihi na Kuweka Dole Gumba na Yule ambaye hajui Kusoma na kuandika atashindwa Kuweka Dole Gumba,
Mtobesya: Huyo Ling'wenya alifanya nini kama ulivyo tueleza
Shahidi: Alisaini Pamoja na Dole Gumba
Mtobesya: Kule Chini Mnapoweka Ithibati Kuna Vifungu Mnaviandika
Shahidi: sahihi Mtobesya: Mueleze Jaji kwenye Maelezo yenu Mlitumia Vifungu gani
Shahidi: Ilikuwa Imeshaandikwa Kwenye Karatasi, niliona hakuna haja ya Kuweka hiko Kifungu
Mtobesya: Kitaje Kifungu
Shahidi: Kilikuwa Kifungu Cha 57(3)
Mtobesya: Umekitaja Maana Yake unakifahamu Mueleze Mheshimiwa Jaji kama hicho Kifungu aya zake
Shahidi: Sikumbuki Kama Zipo hizo aya
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba nipatiwe ID 1
- Mahakama inampatia Mtobesya ID1
Mtobesya: Na Kuonyesha Kielelezo Cha Mahakama Nikuulize Maswali Machache, Iambie Mahakama Kama Baada Onyo Uliweka Muda
- Shahidi anakuwa mbishiiiii hapa, Mbishi, lakini Mwishoni anasema HAKUNA MUDA..
Mtobesya: tuonyeshe uthibitisho amesoma na Kuyaelewa Sehemu gani
Shahidi: Mtuhumiwa amesaini na Kuweka Dole Gumba
Mtobesya: na Kifungu cha Sheria
Shahidi: Ndiyo nimesema Kwamba Karatasi ilikuwa Tight sikupata nafasi ya kuweka
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji Pale ambapo Maelezo ya Mtuhumiwa anathibitisha Kuna Kifungu cha Sheria au Hakipo
Shahidi: Hakipo Kifungu cha Sheria
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji Ulipoishia wewe Kuthibitisha, Kama Kipengele cha Mwisho Kifungu kimelezwa ni Kifungu 57(3) na aya zake au Hapana
Shahidi: Tunaona Kifungu Cha 57(3)
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kurudisha Kielelezo
Mtobesya: Ni kwanini Hamkuweza Kuchukua Maelezo ya Mtuhumiwa Mkiwa Moshi?
Shahidi: Tulikuwa tunawatafuta watuhumiwa wengine na Watuhumiwa walikuwa ni sehemu ya Kusaidia na Pia Shauri Lenyewe lilikuwa DSM na Pia Nature ya Tukio ilikuwa inaenda Kutokea Mikoa ya Dar es Salaam Arusha Kilimanjaro, MBEYA, Mwanza na Morogoro
Mtobesya: Mweleze Mheshimiwa Jaji Kama Unatambua Utaratibu wa Kuchukua Maelezo halafu baadae unaweza za Kuandika Maelezo ya Ziada (Additional Statement)
Shahidi: Sitambui
Mtobesya: Mtajie mheshimiwa Jaji Kama ni Kanuni au sheria gani inayo kulazimisha kwenda kuchukua maelezo sehemu uliyofungulia shauri
Shahidi: Siyo sheria wala Kanuni lakiniiiiiiiiiiii
Mtobesya: hakuna cha lakini hapa, Mheshimiwa Jaji naomba kuishia hapo...
MALLYA ANAANZA KUULIZA MASWALI
Mallya: Kabla hujahamia Arusha ulikuwa Ofisi ya Upelelezi Dar es SalaamShahidi: Sahihi
Mallya: Kwa Muda gani Shahidi: Kwa Miaka 7
Mallya: Ni sahihi Ulikuwa katika Ofisi ya DCI
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Nitakuwa Sahihi nikisema Uinajua Dar es Salaam
Shahidi: Siyo Sahihi
Mallya: Ramadhan Kingai kabla hajawa RCO alikuwa Msaidizi wa ZCO Dar es Salaam
Shahidi: Ni Sahihi
Mallya: Kwenye Timu yenu nikisema kwenye timu yenu angalau Kuna watu Wawili Wa naijua Vizuri Dar es Salaam nitakuwa Sahihi
Shahidi: Siwezi Kusemea Wote
Mallya: Ofisi ya DCI ipo Katikati ya Jiji la Dar es Salaam au Sema Ipo wapi
Shahidi: Mtaa wa OHIO
Mallya: Makao Makuu ya Polisi Mpaka Dar es Salaam ni Umbali gani Kwa Kukadiria
Shahidi: Siwezi Kukadiria
Mallya: lakini Unajua Kuwa Makao Makuu ya Polisi na Polisi Mjini Kati Dar es Salaam Vipo Wilaya Moja
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kituo cha Polisi Mbweni Unakifahamu
Shahidi: Nakifahamu
Mallya: Kituo cha Polisi cha Mbweni ni Kituo cha Wilaya ya Kipolisi Kawe
Shahidi: Sina Uhakika
Mallya: Kwamba Wakati Unapeleka Watuhumiwa Mbweni ulikuwa ujui Kuna Kituo cha Polisi Cha Wapi
Shahidi: Nilikuwa najua ni Kituo cha Polisi tuh
Mallya: Je Kuna Kesi yoyote Umeshawahi Kusikia kwamba Kuna Mtu alienda Kutoa Taarifa Kwamba watuhumiwa wamekamatwa Ututajie
Shahidi: Ni Mambo ya siri
Mallya: nimesikia una Mwambia Mtobesya Wakati Mnawakamata Kipaumbele Kilikuwa Matukio yasitokee
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Ni sahihi Kwamba Wakati Wote Polisi mnapaswa Kutenda kazi Kwa Mujibu wa Sheria
Shahidi: kimyaaa
Mallya: Kwamba Wakati Unapeleka Watuhumiwa Mbweni ulikuwa ujui Kuna Kituo cha Polisi Cha Wapi
Shahidi: Nilikuwa najua ni Kituo cha Polisi tuh
Mallya: Je, Kuna Kesi yoyote Umeshawahi Kusikia kwamba Kuna Mtu alienda Kutoa Taarifa Kwamba watuhumiwa wamekamatwa Ututajie
Mallya: Wakati mnapokea Simu ya Boaz Kwamba Mrudi Dar es Salaam ilikuwa Mkoa gani
Shahidi: Kilimanjaro Moshi
Mallya: kilichoWafanya Msiwaandike maelezo Muda huo ni nini baada ya Kuambiwa zoezi la Kuacha Kumtafuta Lijenje
Shahidi: Tulikuwa tunawahi Kuja Kuendelea Kuwatafuta Watuhumiwa Wengine Dar es Salaam na Kuendelea na Upelelezi
Mallya: Je Mohammed Ling'wenya alitishiwa au alitoa kwa hiari
Shahidi: Alitoa kwa Hiari
Mallya: Ulipata Kufahamu Kuwa Mohammed Ling'wenya alishawahi Kuwa Moshi
Shahidi: Nakumbuka alikwenda Mara Mbili
Mallya: alikaa kwa muda gani
Shahidi: alilala Siku Moja
Mallya: Wapi
Shahidi: Hotel ya Aishi
Mallya: Mlangoni au Bar?
Shahidi: alilala Ndani
Mallya: alikaa wapi
Shahidi: mara ya Pili alifika Aishi Hotel na Baadae katoka akawa anakaa Moshi Mpaka tunamkamata
Mallya: Usiku huo alikuwa ametokea Kulala wapi
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Kwa Kumbukumbu zako Mohammed Ling'wenya ni Mwenyeji wa wapi
Shahidi: Mtwara
Mallya: Wewe Umekaa Moshi kwa Muda gani
Shahidi: Nyakati mbalimbali na Mafunzo mbalimbali
Mallya: Ulielezea Mahakama Utafutaji wenu ulikuwa wa Namna gani
Shahidi: Tulikuwa tunafika Maeneo Mbalimbali
Mallya: Kwa Siku Ya Kwanza Pasua Mlienda Saa ngapi
Shahidi: Majira ya alasiri
Mallya: ambapo Exactly Mlipoanzia ni Wapi
Shahidi: Rau Madukani
Mallya: Kutoka Rau kwenda Moshi police Central ni Umbali wa Kilometers ngapi
Shahidi: Siwezi Kukadiria
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba Jibu lake Lirekodiwe
Mallya: Kutoka Rau Kwenda KCMC Mlitumia Muda gani
Shahidi: Dakika 15
Mallya: Baada ya KCMC Mlienda wapi..?
Shahidi: Tulirudi Mpaka Majengo
Mallya: Unaweza Kukadiria Kama Muda gani
Shahidi: Kwa sababu Hatukuwa na Mwendo Sana tuliitumia Walau Dakika 45
Mallya: Moja ya Tunachojivunia Wachaga Moshi haina Foleni, ila endelea tu kujibu , Baada ya Majengo Mlienda wapi
Shahidi: Tukaenda Pasua,
Mallya: Mie napajua Kote, Mlitumia Muda gani Kutoka Majengo kwenda Pasua
Shahidi: Sikumbuki Muda Exactly nilikuwa siangalii Muda
Mallya: Ulikuwa ni Muda gani
Shahidi: Ulikuwa Muda wa Jioni
Mallya: Baada ya Kutoka Pasua Mkaenda wapi
Shahidi: Machame, Aishi Hotel
Mallya: Aishi ni Kitu gani Kijiji, Kata au Wapi
Shahidi: ni Hotel
Mallya: Ulipofika Aishi Mkafika Maeneo gani
Shahidi: Kingai aliingia Ka anaingia Ndani,
Mallya: Kwa hiyo ni Ushahidi Wako Kingai aliingia Ndani
Shahidi: hakuingia Ndani alielekea Sehemu ya Majengo
Mallya: Unaweza Kutuchorea Picha ya eneo la Aishi Hotel
Shahidi: Siwezi kuchora sababu Sikushuka Kwenye gari
Mallya: Baada ya Aishi Hotel Mkaenda wapi
Shahidi: Maeneo ya Boma Ng'ombe
Mallya: Mlitumia Muda gani Kufika BomaNg'ombe
Shahidi: Siwezi Kujua Muda nilitumia, Kikubwa tulichokiwa tunakifanya ni Kufanikisha Kazi yetu
Shahidi: Palikuwa peshaanza Giza
Mallya: Kwa Makadirio yako a kutoka Boma Mpaka Moshi ni Kilometer ngapi hivi
Shahidi: Inaweza Ikawa Kilometer 50 au Zaidi
Mallya: Nilikusikia unasema mlifika Moshi Sa 5 za Usiku
Shahidi: Saa 4 kwenda Saa 5
Mallya: Ulipata Kueleza Kwamba Kilichokufanya Usiandike Maelezo Muda huo ni nini
Shahidi: Nilishaeleza Mallya: hivi Mbowe Ukifika Kumuhoji saa ngapi Za Usiku Vile..?
Jaji: Suala la Maelezo ya Mbowe havipo Katika Kesi Ndogo
Mallya: Baada Ya Boma Ng'ombe Mlienda wapi
Shahidi: Mbele ya Boma Ng'ombe Kama Unaenda Arusha, Tulifika Maeneo ambayo tulihisi kwamba tungeweza Kuwakuta
Mallya: Kwa hiyo Wewe Ulikuwa unajiongeza Kwenda Sehemu zingine ambazo watuhumiwa awajakutajia
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Kwa hiyo Siyo lazima uende na Watuhumiwa Kwa sababu Ulikuwa aukitajiwa Sehemu A Unaweza Kwemda sehemu B
Shahidi: Watuhumiwa walikuwa wanatusaidia na pia Tulikuwa hatumjui
Mallya: Baada ya Boma Mlienda wapi
Shahidi: Tulirudi Moshi
Mallya: Palikuwa na Mwanga au giza
Mallya: naomba Nimuachie Mwenzangu amallizie Kuuliza Machache
KAUNDA: ulisema Ulipomkamata Mshitakiwa Wa 3 Ulimpeleka Central Police
Shahidi: Nili fikisha Kituoni
KAUNDA: Wakati huo Mlishafungua Kesi ya Madawa ya Kulevya
Shahidi: Ndiyo Unga Unaozaniwa kuwa madawa ya kulevya
KAUNDA: Wakati huo uliwaacha kwenye gari Muda wao wote wakiwa na Pingu Mikononi
Shahidi: Ndiyo
KAUNDA: haukuiambia Mahakama Kwamba ulipowarudisha ukiwafungulia Pingu
Shahidi: Ndiyo Sikusema
PAUL KAUNDA: na Hukusema Mahakamani Kwamba Uliwakabidhi Askari gani wa Chumba Cha Mashitaka kwa Majina yao na Force Namba zao
Shahidi: Sikuongozwa Kusema hivyo
PAUL KAUNDA: na Wala hujui Kilichotokea Kuanzia Muda unawakabidhi Watuhumiwa Muda Ule Usiku Mpaka Asubuhi
Shahidi: Sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Sahihi kwamba wewe Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Arumeru
Shahidi: ni sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba wewe Kazi yako Kuwasimamia Kazi Askari wa Chini yako
Shahidi: sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba Jeshi la Polisi limewafukuza Askari Wanne na Wasaidizi wa Polisi wawili, Wamesimamishwa
Shahidi: sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Wewe ni Mmoja wa Polisi wasaidizi waliosimamishwa Kazi Arumeru
Shahidi: Ni Masuala ya kiutawala Siyo Kesi hii
KIHWELO: ni sahihi Mohammed Ling'wenya Mlimtafuta Kupitia Mitandao ya simu
Shahidi: Siyo Sahihi KIHWELO: akitokea Mtu akasema Boazi aliitoa Malekezo Ya Watuhumiwa Kuletwa Dar es Salaam Siku ileile, Je Kati yake na wewe Nani atakuwa Muongo
Shahidi: Siwezi Kumsemea Mtu Mwingine
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba Watuhumiwa hawaKupokelewa Kituoni Moshi
Shahidi: Hakuna Utaratibu wa Kupokelewa Bali Kuna Sehemu ya kuandika Kuwakabidhi Watuhumiwa
KIHWELO: ni sahihi hapa Mahakamani hapa Kuna Nyaraka ya Kukabidhi watuhumiwa
Shahidi: Siwezi kulisemea
FREDRICK KIHWELO: nitakuwa Sahihi Nikisema Watuhumiwa waliingizwa Kituo cha Polisi Moshi Kwa Dhumuni la Kuwatesa
Shahidi: Utakuwa Haupo Sahihi
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Hukusaini Detention Register Wakati Unawakabidhi Watuhumiwa Kituo cha Polisi Moshi
Shahidi: NI SAHIHI
FREDRICK KIHWELO: ni sahihi Kwamba Watuhumiwa mliowakamata hawakuwa Wenyeji wa Moshi
Shahidi: Hautokuwa Sahihi
FREDRICK KIHWELO: una nyaraka Yoyote inayoonyesha Kwamba Mlipata BREAK DOWN Njia Panda Himo
Shahidi: Sina Kwa sababu Magari ya Serikali yana Utaratibu wake
FREDRICK KIHWELO: Akitokea Mtu akasema kwamba Central Police Dar es Salaam Siyo sehemu ya Kuhifadhi Watuhumiwa WA Ugaidi atakuwa sahihi
Shahidi: Sijui hilo
KIHWELO: Akitokea Mtu akasema Walipotoka Moshi Walifikia Polisi Tazara ambapo watuhumiwa wa ugaidi uhifadhiwa
Shahidi: Mimi Ndiyo nilikuwa na Watuhumiwa, Sikwenda Huko
KIHWELO: ni hayo tu
JAJI: Ingekuwa inaruhusiwa Ningekupigia makofi ila Upo Mahakamani, Umetumia muda Vizuri Kibatala Muda Utakutosha
Kibatala: Nitajitahidi Kibatala: Shahidi Unafahamu Kwamba UGAIDI ni Kesi Kubwa Sana
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Ulichukua Maelezo Kwa kifungu cha 57(3)
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Kifungu Hicho Kinakuruhusu Kuchukua Record ya %Video au Sauti Wakati anakiri
Shahidi: Siyo lazima kutumia Hiyo
Kibatala: Sasa Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Palikuwa na fursa hiyo ya Kisheria lakini hukutumia kwa sababu fulani
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Mtu anapokiri Makosa yake Kuna hitaji la Kumpeleka Kwa Mlinzi wa Amani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kwa Mujibu wa Maelekezo ya Jaji Mkuu kwamba Mtu anapopelekwa kwa Mlinzi wa Amani kwanza anatakiwa Kumkagua Mtuhumiwa Kama ana majeraha
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Mohammed Ling'wenya alipelekwa Kwa Mlinzi wa Amani
Shahidi: Hapana
Kibatala: na Unafahamu Kwamba Kukiri Kwa Mohammed Ling'wenya Kulipaswa Kupelekwa Kwa Mlinzi Wa Amani
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu na Hukumpeleka
Shahidi: Kimyaaaaa
Kibatala: Ulimpeleka Mohammed Ling'wenya Kwa Daktati Kuona Alikuwa na Majeraha
Shahidi: Hilo sina Jibu
Kibatala: Uliwaza Kumpeleka Mtuhumiwa Kwa Daktari Kuthibitisha Kwamba hana majeraha
Shahidi: Siyo Taratibu zangu za Kazi
Kibatala: Kuna sehemu kwenye CPA au PGO inakataza Wewe Kumpeleka Mtuhumiwa Kwa Daktari Kwa ajili ya kujiridhisha
Shahidi: Hapana
Kibatala: ili tuone kama Kweli Hamkuwa Mmetumia Muda huo Kuwatesa, je Dada wa Moses Lijenje Unamfahamu Jina lake
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Maelezo Yako ya Kuharibikiwa Gari Himo Kwenye Maelezo Yako Uliandika au Hukuandika
Shahidi: Sikuandika
Kibatala: Watuhumiwa Wanasema Mlipowatoa Moshi Mliwapeleka Tazara kisha Mbweni, Je Sababu za Kuwahamisha ni za Kiupelelezi au Kiusalama
Shahidi: Zote zote
Kibatala: Tuanze na suala la Upelelezi, Kama Mohammed Ling'wenya ameshakiri tayari uliogopa nini
Shahidi: Taarifa Kutoka Nje, Kuna wengine tulikuwa tunawatafuta
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Walipokuwa Central walikuwa in ISOLATION na Watuhumiwa wengine?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Ulipowapeleka Mbweni waliwekwa IN ISOLATION na Watuhumiwa Wengine
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je Kupima Ukweli Wenu, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulimwambia Mkuu wa Kituo au OCD kwamba Watuhumiwa Watengwe
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Nimesikia Umesema Kwamba Sababu ya Kuwahamisha Watuhumiwa Kutoka Central Dar es Salaam kwenda Mbweni ni kwamba Watuhumiwa Walipo Dar es Salaam wasijue Kinacho endelea, Je Mbweni ni Mkoa gani
Shahidi: Ni Dar es Salaam
Kibatala: Unamfahamu Afisa wa Jeshi anaitwa Chuma Chugulu
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Kule Arusha Kuna washitakiwa wa Ugaidi au hawapo
Shahidi: Wapo wapi K
Kibatala: Gereza la Kisongo, Masheikh,
Shahidi: Wapo
Kibatala: Maelezo yao yalichukuliwa Dar es Salaam
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Kuna Kifungu chochote Cha Sheria ya Mwenendo Wa Makosa ya Jinai na PGO inayolazimisha Mtuhumiwa achukuliwe Maelezo Sehemu tu ambapo faili lilifunguliwa
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Na ulijua Kwamba Shauri hili litafika Mahakamani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na wewe Kama Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Arumeru(OC-CID), Jukumu lako ni Kufunga Mianya yote ya kuharibu kesi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Kuna sehemu yoyote Ambayo Umeonyesha Kwamba kama angekuwa Tayari ningempa Simu yake au Simu yangu awasiliane na Ndugu, Jamaa na Marafiki zake...
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Kule Moshi, Nakuuliza Kuhusu Ufahamu wa Kuingia Na Kutoka Polisi Central Police.
Shahidi: Nafahamu kwa sababu nilisaini
Kibatala: Wewe Ndiye Uliyemuingiza Mohammed Ling'wenya na Kumtoa Mahabusu Moshi
Shahidi: nilikuwa na Afande Mahita
Jaji: liweke Vizuri hilo swali
Kibatala: Unataarifa sahihi Kuhusu Detention Register, Je Ulisaini Out Saa Ngapi,
Shahidi: Tarehe 06 Aug 2010 Saa 11 alfajiri
Kibatala: Kati yako wewe na Mahita nani alikuwa Custodian Officer wa Mohammed Ling'wenya
Shahidi: Mimi Mwenyewe
Kibatala: Aliyekimkabidhi Mohammed Ling'wenya pale CRO central.?
Shahidi: Mimi
Kibatala: Kingai alikwepo wakati mnawakabidhi polisi Central Dar es Salaam?
Shahidi: Ndiyo alikuwepo.... Lakiniiiiiiiiiiii
Kibatala: Hakuna cha lakiniiiiiiiiiiii hapa...
Kibatala: Wakati Unahojiwa na Wenzangu Kwamba Ulisema DCI BOAZI aliwambia kwamba Watuhumiwa Tuwapeleke Moshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Una' personal Knowledge ya Malekezo Ya DCI au Kingai Ndiye anayejua
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Naomba niishie hapo Mheshimiwa Jaji
Jaji: Serikali
Wakili wa Serikali: Shahidi Umeulizwa swali Kuhusiana na kutosema kwenye Ushahidi wako kama Hukusema kama ulimpa simu, kwa nini Hukusema
- Kibatala: OBJECTION kwanini.., Siyo swali nililouliza..
Jaji: Swali haliingi kwenye Record za Mahakama
Shahidi: Kama angeomba Mtu aje, Utaratibu Ungefanyika, Simu ingepatikana
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu Watuhumiwa Kutenganishwa Central na Kule Mbweni, Ukasema Hukusema Kwenye Ushahidi Wako Shahidi Mahabusu Wanatenganishwa...
- MTOBESYA: OBJECTION Kwenye Ufafanuzi, It's not an Open Check
Wakili wa serikali: Elezea kwa nini Hukusema Kama Mliwatenga
Shahidi: Kwa sababu anaye weza Kujua Watuhumiwa wamekaa Je huko Lock up ni Mtu wa Chumba Cha Lock Up
Wakili wa Serikali: Ukaulizwa Swali Ulikiri kwamba Mtuhumiwa anayekiri anatakiwa Kupelekwa Kwa Mlinzi Wa Amani, Ukaulizwa Ulimpeleka kwa Mlinzi wa Amani Ukasema Hapana, Ni kwanini
Shahidi: Hatukumpeleka kwa Mlinzi wa Amani, kwa sababu Tulikuwa tunawahi Kuhakikisha Hivyo Vitendo Vya Kigaidi havifanyiki
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali na Mtobesya Kwamba Kama Ulikuwa na Taarifa za Awali Ukasema Hukuwa na Taarifa
Shahidi: Nilikuwa na Taarifa za Awali, Siyo Za kina wakati namkamata Mtuhumiwa,
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Tukomee hapa
Jaji: Shahidi tunakushukuru Kwa Ushahidi wako Kwenye Kesi Ndogo
Wakili wa Serikali: Robert Kidando Mheshimiwa Jaji tunaomba Hairisho Mpaka Kesho tarehe 12 Mwezi wa 11 2021, Ilituendelee na Shahidi Mwingine Na Ilituweze Kujiandaa Tunaomba Kesi ianze Saa 4 Asubuhi
Jaji: Utetezi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: Shahidi tunakushukuru Kwa Ushahidi wako Kwenye Kesi Ndogo
- Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na Jaji
Jaji: Maombi ya hairisho yamekubaliwa, nahairisha Mpaka Tarehe 12.11.2021. Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi Saa 4 Asubuhi
- Jaji anatoka