Filosofia ya Rorya
JF-Expert Member
- Sep 20, 2021
- 3,214
- 3,587
Taifa la Kenya linawaka moto kufuatia Mhimili wa Utendaji kuingia kwenye mgogoro wa kikatiba na Mhimili wa Mahakama (ambayo ndiyo inastahili kutafsiri sheria ikiwemo Katiba).
Mataifa ya Magharibi yaliyoingilia uchaguzi hata ulipokuwa Mahakamani yametumia Mhimili huo wa Mahakama kuhalalisha Ushoga na Usagaji LGBTQIA+ Kenya.
Jill Biden mke wa rais wa US ameizuru Kenya kwa siku moja na nyuma yake punde tu Shirika la Marekani la Misaada ya Kimataifa la USAID limeikabidhi Kenya msaada wa USD 120ml (KSH.16bl) kuokoa watu 1.3ml wanaokabiliwa na njaa kali kufuatia ukame wa miaka 3 mfululizo uliovunja rekodi ya miaka 40.
Mgogoro huo sasa umefika kwenye taasisi za Kiroho/Imani ambazo zimeungana na Mhimili wa Utendaji kuupinga Mhimili wa Mahakama.
Inapotokea kuwa rais hawezi kumuondoa Jaji kazini na Jaji akaamua kutumia Mahakama kuiuza nchi, taifa linasalimikaje hapa?
Rais Ruto alikuwa swahiba mkubwa wa Mahakama kupitia Jaji Mkuu Martha Koome wakati wa kesi ya uchaguzi.
Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Upeo chini ya Jaji Mkuu Martha Koome kutoa hukumu tata ya kuitaka nchi kutambua kwa sheria haki za Mashoga na Wasagaji umeiweka serikali ya rais Ruto kwenye mashaka makubwa ya uhalali wake kwa wapigakura kiasi kwamba uswahiba wa rais na Jaji Mkuu una muelekeo wa kuporomoka kama siyo hila imetengenezwa.
Uamuzi wa Jaji Mkuu juu ya jambo hili ni mtego na janja ya Ruto kutaka kuonyesha kwamba Katiba ina mapungufu hivyo ifanyiwe marekebisho ILI SASA ATUMIE MWANYA HUO KUIFANYIA MAREKEBISHO MAKUBWA KUINGIZA MAMBO ANAYOTAKA KWA MASLAHI YA SERIKALI YAKE. Ruto na Koome lao moja.
Nyumba ya jirani inapoungua moto jiandalie ndoo za maji.
Ela ya Mzungu tamu lakini chungu, ukiila tu lazima ikukwame kooni.
Napendekeza Afrika ifanye chaguzi kwa ela za ndani ili kulinda uhuru wake.
NB.
Hiyo note book hapo chini nayo ni ya LGBTQIA+?
Bendera za nchi nyingi zina rangi za LGBTQIA+, nazo zibadilishwe?
Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Mataifa ya Magharibi yaliyoingilia uchaguzi hata ulipokuwa Mahakamani yametumia Mhimili huo wa Mahakama kuhalalisha Ushoga na Usagaji LGBTQIA+ Kenya.
Jill Biden mke wa rais wa US ameizuru Kenya kwa siku moja na nyuma yake punde tu Shirika la Marekani la Misaada ya Kimataifa la USAID limeikabidhi Kenya msaada wa USD 120ml (KSH.16bl) kuokoa watu 1.3ml wanaokabiliwa na njaa kali kufuatia ukame wa miaka 3 mfululizo uliovunja rekodi ya miaka 40.
Mgogoro huo sasa umefika kwenye taasisi za Kiroho/Imani ambazo zimeungana na Mhimili wa Utendaji kuupinga Mhimili wa Mahakama.
Inapotokea kuwa rais hawezi kumuondoa Jaji kazini na Jaji akaamua kutumia Mahakama kuiuza nchi, taifa linasalimikaje hapa?
Rais Ruto alikuwa swahiba mkubwa wa Mahakama kupitia Jaji Mkuu Martha Koome wakati wa kesi ya uchaguzi.
Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Upeo chini ya Jaji Mkuu Martha Koome kutoa hukumu tata ya kuitaka nchi kutambua kwa sheria haki za Mashoga na Wasagaji umeiweka serikali ya rais Ruto kwenye mashaka makubwa ya uhalali wake kwa wapigakura kiasi kwamba uswahiba wa rais na Jaji Mkuu una muelekeo wa kuporomoka kama siyo hila imetengenezwa.
Uamuzi wa Jaji Mkuu juu ya jambo hili ni mtego na janja ya Ruto kutaka kuonyesha kwamba Katiba ina mapungufu hivyo ifanyiwe marekebisho ILI SASA ATUMIE MWANYA HUO KUIFANYIA MAREKEBISHO MAKUBWA KUINGIZA MAMBO ANAYOTAKA KWA MASLAHI YA SERIKALI YAKE. Ruto na Koome lao moja.
Nyumba ya jirani inapoungua moto jiandalie ndoo za maji.
Ela ya Mzungu tamu lakini chungu, ukiila tu lazima ikukwame kooni.
Napendekeza Afrika ifanye chaguzi kwa ela za ndani ili kulinda uhuru wake.
NB.
Hiyo note book hapo chini nayo ni ya LGBTQIA+?
Bendera za nchi nyingi zina rangi za LGBTQIA+, nazo zibadilishwe?
Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app