Capt Tamar
JF-Expert Member
- Dec 15, 2011
- 11,741
- 14,639
Katika kipindi hiki ambacho tunapambana na changamoto kubwa kisiasa,tunahitaji kuwa na watu makini wenye ushawishi na uwezo wa kujenga hoja, na zaidi ni kuwa na uwezo wa kutumia kila fursa inayojitokeza ili kujenga chama bora, chenye ushindani na utayari wa kuongoza dola.
Nimesikitishwa sana na katibu mwenezi wetu wa kata ya Themi kujipa likizo binafsi, nimejitahidi kuwahamasisha wafanyakazi wenzangu ili kutuunga mkono kwenye harakati za kuleta mabadiliko, hatimaye bila shaka yoyote wamekubali kuungana nasi, ila nilipowapeleka kwa katibu wetu huyu ili akamilishe utaratibu wa kuwaelimisha zaidi,na kuwakabidhi kadi,yeye alidai kuwa huu ni wakati wake wa kupumzika kwani kazi za uenezi hufanyika kipindi cha uchaguzi na si sasa!
Kwa kweli kauli hii imenivunja nguvu na kufikiri upya uwepo wetu ndani ya jamii, hapana! Ni wakati sasa wa kutafuta watu sahihi kwa kazi sahihi! Kumbuka kuwa kata yetu haina mbunge, diwani wala mwenyekiti, nafikiri huu ndio wakati sahihi wa kusambaza elimu ya uraia kwa wengi walioikosa, kujenga misingi imara ya chama kwenye ngazi hizi za chini nk, ila kwa mwendo huu wa katibu wetu huyu mwendo utakuwa mrefu.
Naomba sana tumtazame ndugu yetu huyu ili tujiridhishe kama kweli anafaa kuwepo kwenye nafasi hiyo, niliwahi kumuuliza kuhusu utata wa uanachama wa mwenyekiti aliyevua gamba na kuvaa gwanda ndugu Subira mwanga, alinijibu kuwa kweli haelewi kama subira ni mwanachama halali wa CDM ila atajua mwenyewe (Subira) kama yupo kwetu au CCM, hii siyo kauli njema kutoka kwa mwenezi wetu, hakika anastahili kutazamwa.
Nimesikitishwa sana na katibu mwenezi wetu wa kata ya Themi kujipa likizo binafsi, nimejitahidi kuwahamasisha wafanyakazi wenzangu ili kutuunga mkono kwenye harakati za kuleta mabadiliko, hatimaye bila shaka yoyote wamekubali kuungana nasi, ila nilipowapeleka kwa katibu wetu huyu ili akamilishe utaratibu wa kuwaelimisha zaidi,na kuwakabidhi kadi,yeye alidai kuwa huu ni wakati wake wa kupumzika kwani kazi za uenezi hufanyika kipindi cha uchaguzi na si sasa!
Kwa kweli kauli hii imenivunja nguvu na kufikiri upya uwepo wetu ndani ya jamii, hapana! Ni wakati sasa wa kutafuta watu sahihi kwa kazi sahihi! Kumbuka kuwa kata yetu haina mbunge, diwani wala mwenyekiti, nafikiri huu ndio wakati sahihi wa kusambaza elimu ya uraia kwa wengi walioikosa, kujenga misingi imara ya chama kwenye ngazi hizi za chini nk, ila kwa mwendo huu wa katibu wetu huyu mwendo utakuwa mrefu.
Naomba sana tumtazame ndugu yetu huyu ili tujiridhishe kama kweli anafaa kuwepo kwenye nafasi hiyo, niliwahi kumuuliza kuhusu utata wa uanachama wa mwenyekiti aliyevua gamba na kuvaa gwanda ndugu Subira mwanga, alinijibu kuwa kweli haelewi kama subira ni mwanachama halali wa CDM ila atajua mwenyewe (Subira) kama yupo kwetu au CCM, hii siyo kauli njema kutoka kwa mwenezi wetu, hakika anastahili kutazamwa.