Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Prof. Kitila Mkumbo, ang'atuka uanachama ACT-Wazalendo

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,931
mkumbo.jpg


Katika Barua ambayo imetolewa leo ambayo Kitila Mkumbo amekiri ni ya kwake, amesema kwamba ameona kuna mgongano wa kimaslahi anaoupata kwa kutumikia Ukatibu Mkuu wa wizara, huku akiwa amevaa uanachama cha ACT- Wazalendo.

"Katika maelezo niliyoyaandika hapo juu na ili kuepuka mgongano wa wazi wa maslahi, nimeamua kung'atuka uanachama wangu wa ACT- Wazalendo, kuanzia terehe iliyoonyeshwa chini ya barua hii", ilisomeka sehemu ya barua hiyo.

Kitila Mkumbo amesema uamuzi zaidi anauachia uongozi wa chama cha ACT- Wazalendo, na huku akiwashukuru kwa ushirikiano kwa muda wote ambao walikuwa kwenye chama.

kitila.jpeg


Maneno ya Kitila Mkumbo kuthibitisha kuwa barua hiyo ni ya kwake



CHANZO: EATV
 
Mwigulu Nchemba mwenye jimbo lake anakuja,
Faru J lazima akutwishe zigo na hiyo wizara ya wasiojulikana

Ukiboronga hapo sababu tosha ya kukata jina lako

M4C kitengo cha ujasusi wako vizuri rangi halisi ya prof imeonekana
 
Nadhani hakuwa mwanachama tena Baada tu ya kuteuliwa na raisi kuwa Katibu mkuu wa wizara ya maji.Ilikuwa kiini macho tu.
 
Ni sahihi alichokifanya Prof. Maana haileti maana Prof. Ni Mtendaji mwandamizi wa serikali ya Magufuli na alikuwa mshauri Mkuu wa ACT, wakati huo huo Zitto anaipinga serikali hiyo hiyo kwenye media. It is a contradictions. Na Zitto usipojitathmini na kubadili aina ya siasa unazofanya nature itaamua
 
Back
Top Bottom