Ketoka
JF-Expert Member
- Sep 23, 2015
- 1,087
- 1,913
KATIBU Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhandisi Mussa Iyombe, ametaja sababu za wakuu wa wilaya na wakurugenzi ambao uteuzi wao ulitenguliwa hivi karibuni.
KATIBU Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhandisi Mussa Iyombe akizungumza na wakuu wa wailya katika kikoa hicho.
Akizungumza jana katika kikao kazi cha wakuu wa wilaya 26 walioteuliwa na Rais John Magufuli hivi karibuni, Iyombe alisema miongoni mwa sababu za kutenguliwa huko ni kutojiheshimu.
Alisema wakuu wa wilaya wengi waliondolewa ni kutokana na kugombana na wabunge au wakurugenzi wa halmashauri.
"Unamnyang'anya gari dereva unaendesha wewe au wewe kazi yako ni kugombana tu na wabunge, wakati wewe una kazi zako na mbunge ana kazi zake. Niwaambie tu ukweli wengi walioondoka ni kwa sababu hiyo. Sasa wewe kila siku unagombana na mbunge, serikali gani hiyo ambayo inagombana tu na wawakilishi wa wananchi,"alisema.
Katibu mkuu huyo alisema wakuu hao wa wilaya wanatakiwa kutengeneza mazingira ya haki ni haki na sheria ni sheria na si kuwaweka ndani ovyo watu.
"Umepewa mamlaka hayo lazima uyatumie vizuri maana ukimweka ndani inapaswa kesho umfungulie mashtaka ya kijinai na ni lipi sasa? Unaweza kukuta labda tulikutana huko. Tuligombana enzi hizo, sasa kwa kuwa umepata ukuu wa wilaya unasema ndio atanikoma," alisema.
Iyombe aliwataka kujiepusha na vitendo hivyo na kutunza heshima ya Rais kwa kuwa ana imani sana na wao na anakasirishwa na hali hiyo.
"(Rais) ana vyombo vingi vya kukuangalia wewe. Kwa hiyo mnatakiwa kuwa waangalifu kwenye hizi nafasi zenu. Niwaombe sana nyie muwe ‘model’ (mfano). Kama kuna mtumishi amekosea kuna mamlaka ya nidhamu, iagize tu. Usiende pale ukamweka ndani kwani kuna sheria zinazomlinda huyo si mwanasiasa," alisema.
Alibainisha kuwa kama hajawajibika kuna mamlaka ya nidhamu ya kushughulikia ni lazima kufuata sheria na taratibu zilizopo.
"Serikali ina taratibu zake usiziruke na kujiamulia. Angalia imekulinda kisheria, taratibu zimefuatwa hata kama wewe ni mkono wa Rais," alisema na kuongeza kuwa mengi aliyoyaona kwa wakuu wa wilaya waliokuwa wameteuliwa yalikuwa yanatia aibu.
"Wewe mkuu wa wilaya unaitisha kikao vizuri, unaenda saa saba wakati kikao ni saa nne sasa unajenga heshima gani hapo? Unataka uwafundishe nini uliowaita? Nimewatahadharisha haya mambo ya kiutendaji tendaji," alisema huku akiwataka kutunza heshima ya Rais na wanatakiwa kuwa mfano.
Akifungua kikao hicho, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi, Selemani, Jafo alisema akienda wilayani anakuta mkuu wa wilaya ki vyake, mkurugenzi, mwenyekiti wa halmashauri, mbunge wilaya nzima inafanya kazi kivyake.
"Ukiacha wilaya ambazo nafasi zilizokuwa wazi, hizi zingine zote ukifika uliza utaambiwa kulikuwa na hali gani na maeneo mengi pale utakuta yule aliyeondoka aliyestaafishwa au kuondolewa kuna suala kubwa la uhusiano,"alisema.
Jafo alitaka wakajenge uhusiano na kufanya kazi na kuwatii viongozi wao kwa kuwa maeneo mengine mkuu wa mkoa hataki mkuu wa wilaya aonekane anafanya kazi na analijua hilo.
KATIBU Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhandisi Mussa Iyombe akizungumza na wakuu wa wailya katika kikoa hicho.
Akizungumza jana katika kikao kazi cha wakuu wa wilaya 26 walioteuliwa na Rais John Magufuli hivi karibuni, Iyombe alisema miongoni mwa sababu za kutenguliwa huko ni kutojiheshimu.
Alisema wakuu wa wilaya wengi waliondolewa ni kutokana na kugombana na wabunge au wakurugenzi wa halmashauri.
"Unamnyang'anya gari dereva unaendesha wewe au wewe kazi yako ni kugombana tu na wabunge, wakati wewe una kazi zako na mbunge ana kazi zake. Niwaambie tu ukweli wengi walioondoka ni kwa sababu hiyo. Sasa wewe kila siku unagombana na mbunge, serikali gani hiyo ambayo inagombana tu na wawakilishi wa wananchi,"alisema.
Katibu mkuu huyo alisema wakuu hao wa wilaya wanatakiwa kutengeneza mazingira ya haki ni haki na sheria ni sheria na si kuwaweka ndani ovyo watu.
"Umepewa mamlaka hayo lazima uyatumie vizuri maana ukimweka ndani inapaswa kesho umfungulie mashtaka ya kijinai na ni lipi sasa? Unaweza kukuta labda tulikutana huko. Tuligombana enzi hizo, sasa kwa kuwa umepata ukuu wa wilaya unasema ndio atanikoma," alisema.
Iyombe aliwataka kujiepusha na vitendo hivyo na kutunza heshima ya Rais kwa kuwa ana imani sana na wao na anakasirishwa na hali hiyo.
"(Rais) ana vyombo vingi vya kukuangalia wewe. Kwa hiyo mnatakiwa kuwa waangalifu kwenye hizi nafasi zenu. Niwaombe sana nyie muwe ‘model’ (mfano). Kama kuna mtumishi amekosea kuna mamlaka ya nidhamu, iagize tu. Usiende pale ukamweka ndani kwani kuna sheria zinazomlinda huyo si mwanasiasa," alisema.
Alibainisha kuwa kama hajawajibika kuna mamlaka ya nidhamu ya kushughulikia ni lazima kufuata sheria na taratibu zilizopo.
"Serikali ina taratibu zake usiziruke na kujiamulia. Angalia imekulinda kisheria, taratibu zimefuatwa hata kama wewe ni mkono wa Rais," alisema na kuongeza kuwa mengi aliyoyaona kwa wakuu wa wilaya waliokuwa wameteuliwa yalikuwa yanatia aibu.
"Wewe mkuu wa wilaya unaitisha kikao vizuri, unaenda saa saba wakati kikao ni saa nne sasa unajenga heshima gani hapo? Unataka uwafundishe nini uliowaita? Nimewatahadharisha haya mambo ya kiutendaji tendaji," alisema huku akiwataka kutunza heshima ya Rais na wanatakiwa kuwa mfano.
Akifungua kikao hicho, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi, Selemani, Jafo alisema akienda wilayani anakuta mkuu wa wilaya ki vyake, mkurugenzi, mwenyekiti wa halmashauri, mbunge wilaya nzima inafanya kazi kivyake.
"Ukiacha wilaya ambazo nafasi zilizokuwa wazi, hizi zingine zote ukifika uliza utaambiwa kulikuwa na hali gani na maeneo mengi pale utakuta yule aliyeondoka aliyestaafishwa au kuondolewa kuna suala kubwa la uhusiano,"alisema.
Jafo alitaka wakajenge uhusiano na kufanya kazi na kuwatii viongozi wao kwa kuwa maeneo mengine mkuu wa mkoa hataki mkuu wa wilaya aonekane anafanya kazi na analijua hilo.