Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Hili ni jambo la muhimu sana. Kuna mawazo tuliwahi kuyatapanya huko nyuma kuhusu jambo la aina hii hii. Nitaorodhesha yale yaliyomo kichwani mwangu kwa wakati huu:

(a) Jambo la kwanza kubwa sana tunalotakiwa kufanya ni kupunguza madaraka ya rais; kwa sasa rais wetu ana madaraka makubwa mno. Ikiwa ni pamoja na kuteua baadhi ya wabunge, kuteua majaji, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya. Tumeshaona kuwa Rais anaweza kutumia madaraka hayo kuteua watu wa kumstarehesha binafsi bila kujali utendaji wao wa kazi.

(b) Wateule wote wa Rais wawe wanapitishwa na bunge. Waitwe bungeni wahojiwe kuhusu uwezo wao na ikionekana kuwa mteule hana ubavu wa jukumu analopewa asipistishwe, badala yake rais ashauriwe kuteua mtu mwingine.

(c) Rais asiteua mawaziri wake kutokana na wabunge. Kwa vile uchaguzi wa rais hautegemei wingi wa wabunge wa chama chake, inawezekana rais akatoka kwenye chama ambacho hakina mbunge hata mmoja. Vilevile kuwa na waziri ambao ni wabunge kunapunguza ukali wa bunge katika kufanya kazi yake ya kuisimami serikali.

(d) Kama nyongeza ya (c), Rais asiteue mbunge yeyote.

(e) Wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wasiteuliwe na raisi bali wagombee kama wabunge.

(f) Iundwe tume huru ya utumishi wa serikali ambayo itasimamia watumishi wa serikali wasie politicized. Tume hii isimamie pi vyombo vyote vya dola . Tume iwe inawajibika kwa bunge, siyo kwa rais.

(g) Mikataba yote inayofanywa na serikali iwe inapata baraka za bunge. Bile bunge kukubali mkataba usitekelezwe.

machache kwa leo. Kuna mambo mengine kama Muungano na udhibiti wa pesa za umma ambayo yanatakiwa kuwekwa bayana.
 
1)wagombea binafsi au huru waruhusiwe kwenye chaguzi zote.
2)Nafasi ya Raia kuhoji uwezo wao viongozi kiutendaji iwekwe wazi kikatiba.
3)ielezwe bayana Takrima katika Chaguzi zozote ni Rushwa
4)Rasmi za Mikataba yote inayohusu TAIFA iwe wazi kwa raia wote kabla na baada ya kupitishwa kama mkataba
5).Haki ya Raia kupata maelezo au habari toka serikalini iweke wazi kikatiba.
nitaendelea baadae kidogo
 
Naomba nichangie kidogo hii mada.

Kwanza naomba tuwe makini sana tunavyochangia hii mada ili tueleweke tunaongelea nini.

Kama mtu unaona rais asiteue majaji toa mapendekezo yako majaji wateuliwe kwa njia gani. Ninavyojua mimi rais hawezi kumteua JJ kuwa jaji, hana sifa hizo. Katia uteuzi wa majaji rais anaongozwa na miongozo iliyopo kuteua majaji.

Naonga mkono kuhusu teuzi za rais zipitishwe na bunge ingawa natambua tutakuwa tunawaongezea posho tu wabunge. Kama richmonduli alikosa kura moja wakati anapitishwa na bunge ni kivipi teuzi nyingine zitaenda vizuri. Hii sheria itakuwa very futuristic.

Naonga mkono pia hoja ya kumzuia rais kuteua mawaziri toka kwenye wabunge wao wenyewe wametuambia mikataba haiwezi kupelekwa bungeni wakati huyo huyo anayesema na aliyepitisha ni mbunge sasa sijui ana tofauti gani na wabunge wengine.

Kuhusu uteuzi wa wakuu wa mikoa na wilaya nadani nitaacha watu wengine wachangie ila ninavyoelewa mimi kama na wao watapigiwa kura inamaanisha tunaunga mkono utawala wa kimajimbo. Kwa upande wangu nadhani bado hatujafika huko, ndiyo tutaimarisha demokrasia lakini kwa historia iliyopo wapiga kura wa Tanzania bado wanachagua watu wasiofaa nadhani dawa iliyopo ni kuchagua rais bora ambaye atachagua watu bora kumsaidia. Sitashangaa kusikia Manji ni mkuu wa mkoa wa dar es salaam kama kutakuwa na uchaguzi. Mimi siamini mambo ya demokrasia ya kupiga kura ndiyo maana JK ni rais wetu. It doesn't matter kama anaweza kazi au la hilo silo kosa lake ametumia haki yake ya kugombea na amepata.

Nadhani nimalizie na hii issue ya kiongozi wa shughuli za bunge. Ukimuondoa waziri mkuu kuwa kiongozi wa shughuli za serikali bungeni inaaanisha tunabadilisha hicho chombo sasa sijui tutakiita Congress?
 
(e) Wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wasiteuliwe na raisi bali wagombee kama wabunge.


Sikubaliani na hili pendekezo: Litasababisha tuwe na chaguzi lukuki...napendekeza hao wakuu wa wilaya wasiwepo kabisa badala yake bunge lichague Wakuu wa Mikoa ambaye atafanya kazi za Mkoa wake akishirikiana na Wabunge.
 
Sam,
Hapa tupo katika mchakato wa kupata maoni ya katiba tunayoihitaji na kutoa uhuru zaidi kwa Bunge na wananchi kwa ujumla na hata kupunguza madaraka ya viongozi wakuu ambayo wanayatumia vibaya.

Nafikiri swala la Waziri Mkuu kuwa Kiongozi wa bunge limechangia mambo mengi ya serikali kutohojiwa ipasavyo na hata yanapohojiwa basi yanakuwa hayatoi muelekeo kamili,kwani inapotokea wabunge wengi ni wachama kimoja kama hivi sasa basi mkuu huyo washughuli za bunge hutumia wasaa na nafasi yake kutoa ushawishi ili aungwe mkono au kukwamisha mijadala mbali mbali kupitiia mawasiliano na spika kupitia nafasi yake.Hivi kuna nchi ngapi ambazo Waziri Mkuu ni mkuu wa shughuli za bunge?je nchi zote zenye mawaziri wakuu pia huwa wakuu wa shughuli za bunge?

Kwani kuna ulazima tunapomuondolea madaraka hayo itabidi tubadili na jina ?Tafadhali naomba ufafanuzi.
 
Nd. Kichuguu nakuunga mkono!
Mawaziri ambao ni wateule wa Rais wasitoke bungeni!
Na kila mteule wa Rais kama Mabalozi, Mawaziri, Majaji, wakuu wa Taasisi kubwa wathibitishwe na bunge!
 
Wakati wa maneno matupu umepitwa na wakati, lazima tuweke vitendo.

Hii mada yaweza kuwa ndio chanzo cha mabadiliko kama tutaweka shime, na ili kupata mtiririko mzuri ningependa mada hii tuijadili kipengele kwa kipengele, ni vyema tukaipitia katiba ili michango yetu iwe ni ya kujenga.

Admin. naomba uingilie kati ili mwisho wa siku, kama sheria inaruhusu tuoa draft ya katiba iliyoandaliwa na JF kisha tuisambaze kwa wadau wachangie zaidi na kuiboresha. katiba hii itawekwa wazi kama watawala wakiamua kuchukua sawa, wakigoma iko siku tutapata kiongozi atakeyeifanyia kazi.

Mfano, sura ya pili ya katiba yetu inazungumzia Serikali ya jamuhuri ya Muungano, hapa tunaweza kujadili kwa undani muundo wa serikali tunataka uweje, uteuzi wa viongozi, miiko ya uongozi.

Vili vile kazi mke wa rais zitamkwe wazi kwenye katiba
 
Kazi ndiyo kipimo cha utu

Kama tunataka tuijenge hii forum watu waje humu na waone tunaongea mambo ya maana lazima tujue tunaongea nini. Mara ya kwanza nilijua umekosea tu kuandika, Waziri Mkuu siyo kiongozi wa bunge wote humu tunajua kiongozi wa bunge ni nani. Waziri mkuu ni kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, kuna tofauti kubwa sana hapo.

Labda wewe uniambie sasa ni nchi gani ambayo ina bunge na waziri mkuu siyo kiongozi wa shughuli za serikali bungeni. Ninaweza kukupa mfano mmoja labda unaweza kunielewa naongelea nini. US hakuna waziri mkuu na hakuna bunge. Wana chombo kinaitwa Congress ambacho kimegawanywa sehemu mbili. Uingereza wana bunge ambalo PM ndiye kiongozi wa shughuli za serikali bungeni. Jinsi bunge la uingereza linavyoendeshwa ndivyo na letu linatakiwa liwe hivyo hivyo, hakuna sheria inayokataza mbunge kumuuliza waziri mkuu swali lolote ila chama cha akina shy ndicho kinaaribu.
 
Wakati wa maneno matupu umepitwa na wakati, lazima tuweke vitendo.

Hii mada yaweza kuwa ndio chanzo cha mabadiliko kama tutaweka shime, na ili kupata mtiririko mzuri ningependa mada hii tuijadili kipengele kwa kipengele, ni vyema tukaipitia katiba ili michango yetu iwe ni ya kujenga.

Admin. naomba uingilie kati ili mwisho wa siku, kama sheria inaruhusu tuoa draft ya katiba iliyoandaliwa na JF kisha tuisambaze kwa wadau wachangie zaidi na kuiboresha. katiba hii itawekwa wazi kama watawala wakiamua kuchukua sawa, wakigoma iko siku tutapata kiongozi atakeyeifanyia kazi.

Mfano, sura ya pili ya katiba yetu inazungumzia Serikali ya jamuhuri ya Muungano, hapa tunaweza kujadili kwa undani muundo wa serikali tunataka uweje, uteuzi wa viongozi, miiko ya uongozi.

Vili vile kazi mke wa rais zitamkwe wazi kwenye katiba


mgumu,

Hoja yako ni ya msingi lakini nadhani niruhusiwe tu kuongoza huu mjadala ili usipoteze mwelekeo.

Hapa nahitaji jambo moja tu kujua kama kuna zaidi ya members 3 wanaoona hili linafaa kufanywa na mimi. Naweza kuwa natoa kipengele kimoja baada ya kingine (toka kwenye katiba) kila siku 3 ili tukifikirie kwa mapana na kukijadili kwa manufaa ya taifa letu.

Sidhani kama tupo kuipinga katiba ya Jamhuri ya Muungano bali kuangalia wapi pamesahaulika, wapi parekebishwe, kukumbushana wajibu kama raia wa Tanzania n.k.

Nadhani tunaongelea hii:

Toleo la Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya Mwaka 1977, ambalo limezingatia na kuweka pamoja mabadiliko yote yaliyofanywa katika Katiba ya Muungano tangu ilipotungwa mwaka 1977 hadi tarehe 30 Aprili, 2000.

Kwa wasiokuwa na muda wa kui-download mimi nitakuwa naiweka kipengele kimoja baada ya kingine.

Kumradhi sikuwa online kwa muda kutokana na matatizo ya hapa na pale. Am back though occupied.
 
Invisible, kuna mabadiliko ya Katiba 14 (2005) sikumbuki kama yalishapitishwa .... Katiba yenye mabadiliko hayo ndiyo sahihi kuijadili, hiyo ya 2000 ina vipengele ambavyo vimeshaondolewa na vingine vimeongozwa, au kubadilishwa.
 
Ni kweli Mzee Mwanakijiji,

Nitafanya kitu kimoja, naomba uvumilivu hadi kesho niitafute 'soft copy' ya katiba ambayo ni 'Ammended' na 'Latest' ili tuwe na reference yenye uhakika.

Aidha kama kuna mwenye nayo anirushie kwenye barua pepe yangu
 
Kichuguu,
Nipo nawe bega kwa bega! safi sana.

Kazi ndio kipimo cha Utu,
Hoja yako kuhusu waziri mkuu ni muhimu sana kwa sababu inaonyesha hakuna sheria inayombana waziri mkuu kutokuwa mbunge akiwa bungeni ila bado hujisikia kama serikali ipo juu ya bunge wakati wote na kuwa bunge sio baraza huru ila chini ya serikali.
Inatakiwa sheria ama utaratibu ambao unahakikisha kuwa waziri mkuu ni mwakilishi wa serikali bungeni. nadhani pia nguvu yake ktk kujibu hoja itapungua sana kama mawaziri wote walioteuliwa hawatakuwa kati ya wabunge.

Sam,
Mjomba hilo swala la wakuu wa mikoa na wilaya kusema kweli gumu sana kulipatia dawa. Nadhani kuchaguliwa na wananchi inaweza kuwa sii mbaya sana ikiwa huyu RC lazima awe na kiwango fulani cha ELIMU, pia sharti kubwa zaidi ni mkazi wa sehemu hiyo. Kuwepo na sifa fulani ambayo wababaishaji vigumu kuwa nayo.

Invisible,
Mimi nakubaliana na ushauri wa Mgumu, ila tu tuwe makini tusije poteza baadhi ya maelezo yaliyotangulia. Mwanakijiji, bingwa wetu weka mavituz!
 
Kichuguu,
Nipo nawe bega kwa bega! safi sana.

Kazi ndio kipimo cha Utu,
Hoja yako kuhusu waziri mkuu ni muhimu sana kwa sababu inaonyesha hakuna sheria inayombana waziri mkuu kutokuwa mbunge akiwa bungeni ila bado hujisikia kama serikali ipo juu ya bunge wakati wote na kuwa bunge sio baraza huru ila chini ya serikali.
Inatakiwa sheria ama utaratibu ambao unahakikisha kuwa waziri mkuu ni mwakilishi wa serikali bungeni. nadhani pia nguvu yake ktk kujibu hoja itapungua sana kama mawaziri wote walioteuliwa hawatakuwa kati ya wabunge.

Sam,
Mjomba hilo swala la wakuu wa mikoa na wilaya kusema kweli gumu sana kulipatia dawa. Nadhani kuchaguliwa na wananchi inaweza kuwa sii mbaya sana ikiwa huyu RC lazima awe na kiwango fulani cha ELIMU, pia sharti kubwa zaidi ni mkazi wa sehemu hiyo. Kuwepo na sifa fulani ambayo wababaishaji sii vigumu kuwa nayo.

Invisible,
Mimi nakubaliana na ushauri wa Mgumu, ila tu tuwe makini tusije poteza baadhi ya maelezo yaliyotangulia. Mwanakijiji, bingwa wetu weka mavituz!

Nimekuelewa na kwa vile huu ni mchakato wa nini tunakitaka ndiyo maana nikasema tumnyime uwezo huo kisheria katika katiba mpya tunayoihitaji.Tusubiri hayo marekebisho ya katiba ya 14 :2005 ili tuyaone tuende sawia nayo kwa kuona mapaungufu zaidi na kuyafanyia kazi.
 
Mimi hoja yangu siku zote ni kuandikwa katiba mpya wala sio kubadilisha. Sababu za kuandika katiba mpya ni nyingi, lakini ya msingi kabisa ni kuwa wananchi wa Tanzania hawajawahi kushiriki katika kupambanua mambo wanayotaka yawe kwenye katiba yao. Kwa hiyo ni wazi kabisa katiba uhalali wa katiba yetu hasa katika mazingira ya leo ni jambo lenye kuzua maswali mengi kuliko majibu.
 
mwanasiasa,

You're right (maybe), tatizo nimekumbana na ugumu kupata katiba yenye amendments za 2005. Kama unaweza kunipa mtu wa kunisaidia kwa hilo inaweza kuwa vema sana.

Am now in Dar. You can PM me. Unajua tungeenda kwa kuangalia kwanza vipengele vilivyomo kwenye katiba (current) na tukaangalia mapungufu yake then tuka-propose nyingine na kuwasiliana na Bunge letu tukufu tungekuwa tumecheza 'heko'.

Sijui kama nasomeka au lah...
 
Invisible, hapo zamani kulikuwa na duka la vitabu vya serikali somewhere along Samora Ave... ukienda hapo bila ya shaka unaweza kupata nakala ya Katiba.. ila sijui kama Samora Avenue bado ipo, kama bado haijauzwa kwa wachimba madini!
 
Invisible, hapo zamani kulikuwa na duka la vitabu vya serikali somewhere along Samora Ave... ukienda hapo bila ya shaka unaweza kupata nakala ya Katiba.. ila sijui kama Samora Avenue bado ipo, kama bado haijauzwa kwa wachimba madini!

Bado ipo, na hiyo katiba ipo pale. Niliyo nayo mimi hapa nilinunua hapa Septemba 2006 nilipotembelea Dar.
 
Nashukuru kwa kunitonya,

Napafahamu, nitafuatilia kesho kunako asubuhi. Bongo usiku mnene mida hii. Mwnkjj get online thru MSN.
 
Back
Top Bottom