dazu
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 365
- 76
Katibu wa bunge bwana Kashillillah aliita waandishi wa habari kuelezea minyukano iliyojitokeza katika mkutano wa 3 wa bunge hili la 10, aliuleza umma kwamba kilichosababisha ni ugeni wa wabunge na sio udhaifu wa Spika. Alienda mbali zaidi kutolea mfano wa mbunge wa Arusha Mh. Godbless Lema kwamba kitendo chake cha kusema 'funga mlango tupigane' kinatokana na uchanga wake bungeni na kwamba hana wala hajasoma kanuni za bunge. Maoni yangu ni kwamba katibu hajamtendea haki Mhe. Lema kwa sababu
1. Ni wabunge wengi ambao walijibizana maneno wakiwemo wakongwe na mawaziri (tulisikia wengine wakisema 'atoke nje');
2. Si kweli kwamba mhe. Lema hana kanuni za bunge;
3. Kila bunge jipya huja na wabunge wapya lakini haya hajajitokeza huko nyuma;
Mtazamo wangu ni kwamba yaliyojitokeza ni mwanzo tu wa kuonesha dhahiri kwamba spika wa sasa hakuwa amewiva vya kutosha kuvaa viatu vya Sitta. Aidha kitendo cha ufafanuzi huu kutolewa na katibu wa bunge ni ushahidi mwingine kwamba Spika kashindwa. Naomba kuwasilisha.
1. Ni wabunge wengi ambao walijibizana maneno wakiwemo wakongwe na mawaziri (tulisikia wengine wakisema 'atoke nje');
2. Si kweli kwamba mhe. Lema hana kanuni za bunge;
3. Kila bunge jipya huja na wabunge wapya lakini haya hajajitokeza huko nyuma;
Mtazamo wangu ni kwamba yaliyojitokeza ni mwanzo tu wa kuonesha dhahiri kwamba spika wa sasa hakuwa amewiva vya kutosha kuvaa viatu vya Sitta. Aidha kitendo cha ufafanuzi huu kutolewa na katibu wa bunge ni ushahidi mwingine kwamba Spika kashindwa. Naomba kuwasilisha.