Kashilila aichefua CHADEMA upya

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

25 NOVEMBER 2011


*Wamshangaa kauingilia mambo yao, kupotosha umma
*Wamtaka awataje wabunge wachanga wasiojua sheria
*Mnyika amshukia Makinda, asema alipuuza wabunge

Na Benjamin Masese

SIKU moja baada ya Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilila, kudai mazungumzo kati ya Rais Jakaya Kikwete na Kamati teule ya
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hayatabadili maamuzi yaliyopitishwa na Bunge, chama hicho kimeibuka na kusema kuwa, kiongozi huyo hana msaada wowote kwa bunge bali anaeneza sumu, chuki na kuchonganisha makundi ndani ya jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mbunge wa Ubungo, Dar es Salaam, ambaye pia ni Katibu wa wabunge CHADEMA, Bw. John Mnyika, alisema wameshangazwa na kitendo cha ofisi ya bunge kuwa mstari wa mbele kupotosha umma juu ya muswada wa mabadiliko ya katiba mpya 2011.Alisema juzi Dkt. Kashilila alitoa taarifa kupitia vyombo vya habari kuwa, baadhi ya wabunge wa Bunge la Muungano ni wachanga na hawajui sheria ambazo walipaswa kuzitumia kujenga hoja.

"CHADEMA inamtaka Dkt. Kashilila awataje wabunge hawa kwa majina na kueleza kwa nini alishindwa kuwashauri mapema ili waweze kutimiza lengo la muswada huo kutosomwa bungeni kwa mara ya pili," alisema.

Alisema kitendo cha kusema majadiliano kati ya Rais Kikwete na kamati teule ya chama hicho hayawezi kubadili maamuzi ya bunge ni kutaka kupotosha Watanzania na dhamira ya Kamati Kuu ya CHADEMA kutaka muafaka kwa njia ya majadiliano.

"Hili suala ni bichi, upo uwezekano wa kutolewa maamuzi makubwa yasiyotarajiwa, Dkt. Kashilila anapaswa kusoma ibara ya 62(1) na 62(3) ya katiba ya Tanzania.

Alisema Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda aliwapuuza wabunge waliojitokeza kuonesha jitihada za kupinga muswada huo usisomwe kwa mara ya pili lakini si kweli kwamba wabunge hawajui sheria.

Bw. Mnyika alisema alikusudia kutumia kanuni ya 86(3)(a) kupinga muswada usisomwe kwa mara ya pili lakini alipuuzwa hata alipotumia kanuni ya 55 (3)(b) ili kutoa hoja ya kuahirisha mjadala.

"Huyu Dkt. Kashilila ndiye hajui sheria, alishindwa kulisaidia Bunge na kumshauri Spika wake, umma uliona yaliyokuwa yakitendeka, hata kanuni ya 86 (3) (b) ilipotumika, wabunge walisimama ili kuunga mkono hoja lakini haikusikilizwa.

"Kimsingi suala la kupitisha muswada huu lilikuwa limepangwa, nawaomba wananchi mpuuze kauli za Dkt. Kashilila, jambo la msingi tupiganie haki yetu ya kushirikishwa katika mchakato wa kupata katiba ambayo itatuongoza miaka 50 ijayo," alisema.

Aliongeza kuwa kama Dkt. Kashilila atashindwa kuwataja wabunge wasiofahamu sheria na kueleza sababu za kushindwa kumshauri spika, watakutana na kutafakari hatua za kuchukua.



 
Kama kweli huyu Dr wa bunge kasema hayo, basi hana msaada wowote kwa jamii ya kitanzania kwenye hii karne ya 21. hajui kwamba yeye hatakiwi kuegemea upande wowote! Anyway, hujasema maneno yote aliyosema huyo Dr. pengine taarifa ilianzia sehemu nyingine.
 
na akiegemea hoja ya chadema atakuwa upande gani? Ninachojuwa wao chadema wanaenda kujiridhishatu na mazungumzo yao hayawezi kubadili maamuzi ya bungu, ukweli ndo huo.na kama wana mapendekezo yao wameyatowa wapi? Wamekusanya wapi maoni hayo?,,nafikiri hy kamati yenyewe ndo itaenda kupewa maelezo na sababu zilizopelekea muswaada kusomwa kwa mara ya pili.
 
Kashilila ni hawo hawo Maccm..........anatetea maslahi yake na si ya watanzania,yeye yuko bungeni na bunge ni mhimili unaojitegemea iweje aingilie mhimili mwingine ambao ni rais kwa kusema hakuna kitakachobadilika!!

JK soma alama za nyakati, huu mchakato wa katiba mpya uliopitishwa bungeni na maccm ni wa maccm na marais 2 na si wa wananchi hata Profesa Shivji amesema hivyo, kamwe hatutaukubali na tuko tayari kwa lolote, hii nchi si ya maccm wala ya kikundi cha watu wachache bali ni ya watanzania wote. Mungu tupe nguvu. Amina
 
Kwa nini Dr Kashilila anasema mazungumzo kati ya CHADEMA na rais hayatabalisha chochote? Na inakuwaje katibu wa bunge ambaye kimsingi kazi yake ni kusogeza makaratasi mezani kwa Spika anajiingiza kwenye malumbano na wawakilishi wa wananchi (wabunge)? Katumwa na nani huyu bwana kusema aliyosema?

Hii si mara ya Kwanza huyu Dr. Kashilila kujiugeuza mbunge lakini kwa suala nyeti kama KATIBA ya nchi nilidhani amevuka mipaka - kabisa. Haikubaliki hata kidogo kwa katibu wa bunge kuita wawakilishi wa wananchi mbumbumbu! Ana ujuzi gani huyu kwenye mambo ya sheria? Amefanya nini cha maana tangu apewe hiyo kazi na rais? Yeye na Makinda wanaweza kutumbia ni lini hili bunge lake la mipasho litatoa report ya Lema?
 
MAMA ANNA MAKINDA KWA NINI UMECHAGUA KUUDHALILISHA 'UBINADAMU, HAKI NA UTU WA MTANZANIA' KWA KUTUMIA USPIKA WAKO VIBAYA???:spy:

Hivi huyu mama alipokua amekaa pale mbele na kushinikiza saaana kupitishwa muswada huu ambao hivi sasa umebatizwa jina 'Muswada wa Makinda', alijibidisha hata kidogo tu kulifunua ndani akajionea jinsi ilivyo HATARI KWA USALAMA WA TAIFA letu kwa kukiuka mkataba wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa kuvipa FURSA MPYA vyombo vya Zanzibar kutungia sheria mbalimbali Tanzania Bara na kuonekana mbuzi ndani ya gunia kiasi hicho?

Je, huyu mama anajua kweli tofauti kati ya marekebisho ya sheria ukilinganisha UUNDWAJI UPYA KWA KATIBA ya nchi kama ambavyo wananchi wa Tanzania tulivyoomba?

Je, mama Makinda anayo habari kwamba kwa Demokrasia ilivyoanza duniani kule Mesopotamia (Iraq ya leo) hali halisi ilikua ni ilikua ni kwa wananchi wote wa taifa hilo kujiendea bungeni (Direct Democracy) kujiamulia jinsi gani ardhi zenye rutuba za pale Ephrates na Tigris zingeweza kugawiwa uzuri kwa kila mwananchi akapata kulima. Je, anatambua ya kwamba ilikua tu ni baadaye sana tu ndipo mtaalam mmoja wa Hisabatia wa nchini Samos ajulikanaye kama Pythagorus alipoombwa tu NA BUNGE ZIMA LA WANANCHI WOTE ili aje kuwasaidia juu ya ugawaji ardhi kwa haki Pythagoras Theorem kutumika katika lengo hilo?

Je anayo habari kwamba yeye ni spika tu na yule ni mbunge tu kwa sababu siku hizi kutokana na idadi ya watu kuongezeka kukaonekana ni vema kutumia mfumo wa demokrasia ya uwakilishi (Representative Democracy) badala ya ile ya kila mtu kwenda bungeni?

Hali hii inamaana kwa hasa kwetu Tanzania kwa kukubali kufuata mfumo huu mpya ya uwakilishi bunge ni kwamba ni kweli wananchi TUMEAMUA KWA DHATI KABISA KUKASIMU MADARAKA yetu kwenu ili kila mlitendalo bungeni, mahakamani na huko serikali kuu ni SHARTI IENDESHWE KWA KUZINGATIA MATAKWA YETU na jinsi ambavyo tunawatumeni huko mkafanye. Mama Makinda iweje katika huu muswada nyeti na hatarishi wewe uamue tu kutuweka kando wananchi unafanya hivo kwa maelekezo na maslahi ya nani??

Mama spika, mbali na sisi kuhiari kukasimu madaraka yetu kwenu kutuwakilisha huko bungeni kwa kutunga sheria mbali mbali zinazotokana moja kwa moja na ndoto na matumaini zetu huku uraiani,
NANI KAKUAMBIA KWAMBA HATA MADARAKA YETU YA KUKALIA USHUKANI KUJIUNDIA KATIBA YA NCHI YETU NAYO TULIKASIMU KWA MTANZANIA MMOJA TU AITWAYE RAIS AU KWA WAKATI MWINGINE JAKAYA MRISHO KIKWETE na maswahiba wake?
:spy:
 
Kwa kauli yake hiyo huyo katibu wa bunge, inadhihirisha kuwa swala hilo la kupitisha muswada lilishapangwa hata kabla ya Mswada kupelekwa BUNGENI,. Kadhihirsha kuwa hata kama Wananchi wakifanya wapendavyo hakuna mabadiliko yatakayotokea.

Anatakiwa aulizwe kama ndo Maamuzi ya serikali hayo au ni yake binafsi. Huyo Dr hajui wananchi wanataka nini? Swala hili si la CDM ingawa wao ndo walikuja na Mada hiyo...

Swala hili ni la wananchi na kwakuwa CDM wanawasikiliza wananchi watakacho ndo maana wakawawakilishia swala hili la katiba...
 
Dr Kashilila ni MWAKILISHI wa jimbo gani nchini na alichaguliwa na kura ngapi ndipo akatutemee mate usoni kiasi hicho? Huyu anayeripotiwa humu ni Dr Kashilila mtumishi wetu serikalini au Dr Kashilila mwakilishi wetu bungeni??

Yaani kauli nyingine bwana mpaka mtu unapata na ushawishi kuhoje kama hizo herufi zilizomtangulia jina ni za kupewa au za kupashwa?
 
Dr Kashilila ni MWAKILISHI wa jimbo gani nchini na alichaguliwa na kura ngapi ndipo akatutemee mate usoni kiasi hicho? Huyu anayeripotiwa humu ni Dr Kashilila mtumishi wetu serikalini au Dr Kashilila mwakilishi wetu bungeni??

Yaani kauli nyingine bwana mpaka mtu unapata na ushawishi kuhoje kama hizo herufi zilizomtangulia jina ni za kupewa au za kupashwa?

Ni mtumishi tunaempa mshahara wetu mkubwa kwa kazi ya kutuvurugia utaratibu Bungeni, Hana maana kama huyu sijawahi kuona, ikumbukwe kuwa nae pia ameteuliwa na Rais kuwa pale alipo. Mwenye CV yake angetumwagia tuhangaike nae.
 
Kasoma shule zipi na hizo herufi kweli ni U-PhD kweli au ni zile za bwana mifugo huyu mitaani kwetu; CV tafadhali.
 

25 NOVEMBER 2011


Alisema kitendo cha kusema majadiliano kati ya Rais Kikwete na kamati teule ya chama hicho hayawezi kubadili maamuzi ya bunge ni kutaka kupotosha Watanzania na dhamira ya Kamati Kuu ya CHADEMA kutaka muafaka kwa njia ya majadiliano.

"Hili suala ni bichi, upo uwezekano wa kutolewa maamuzi makubwa yasiyotarajiwa, Dkt. Kashilila anapaswa kusoma ibara ya 62(1) na 62(3) ya katiba ya Tanzania.

Kifungu cha katiba 62(1) "Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ambalo litakuwa na sehem mbili, yaani Rais na Wabunge"

Kifungu cha katiba 62(3) "Iwapo jambo linahitaji kuamuliwa au kutekelezwa na sehemu zote mbili za bunge kwa mujibu wa masharti ya katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote, basi jambo hilo halitahesabiwa kuwa limeamuliwa au limetekelezwa ipasavyo mpaka liwe limeamuliwa au limetelekelezwa na Wabunge na vilevile Rais, kwa mujibu wa madaraka yao kuhusu jambo hilo"

Hapo tunaona wazi katibu wa Bunge alivyo, tena eti Dkt! ama kweli ndiyo maana Regia aliwaambia hawana tofauti na std!!!
 
Huyu bwana anajiharibia....anapunguza heshima yake kwa wabunge...yeye ni nani mpaka aingilie na kutoa matokeo ya mazungumzo ambayo hayajafanyika? Anafanya hivyo kwa jeuri ya nani?
Anatafutwa kung'atwa huyu.
 
Kashilila, nimependa sana maneno kwenye wino mwekundu hapo chini yakituthibishia wewe mwenyewe ukisema kwa PhD yako hiyo uchwara kwamba SERIKALI IMEONDOA MUSWADA hivyo Wa-Tanzania wote tulikua tukisubiri hiyo hiyo serikali ikae ijipange KULETA UPYA AU KWA KUSOMWA KWA MARA YA KWANZA bungeni Muswada ambao hawakulazimika kuuondoa bungeni wenyewe.

Huu usanii wote mnaoufanya hapa kwa kutamani kutufungia nje wananchi juu ya hili ndilo hasa linalotupeleka barabarani hivi karibuni kuandamana mpaka kieleweke; kama ulidhani ni utani shauri yako.


Constitutional Review Bill may be renamed

By Felister Peter

28th April 2011

Kishilla.jpg


Dr Thomas Kashililah, Clerk of the National Assembly, stresses a point at a news conference on the Constitutional Review Bill held in Dar es Salaam yesterday.

The Constitutional Review Bill, 2011 withdrawn from Parliament early this month, may have its title changed to correspond with the contents, Clerk of the National Assembly, Dr Thomas Kashilila, has said.

The current name had led to some people confusing the bill as heralding the review of the constitution, while the draft document was actually meant to facilitate the setting up of a presidential commission to supervise the entire process, said Dr Kashilila.

"The Constitutional Review Bill, 2011 was to be passed by the Parliament to allow for the formation of the commission. It wasn't for the constitution review process," Dr Kashilila said when talking to journalists in Dar es Salaam yesterday.

He admitted that some lawmakers refused to pass the Bill simply because they didn't understand it. He said even the chaos that occurred at the start of the exercise was largely caused by people's ignorance of the Bill, as most of them thought the process of making the new constitution had already started.

"Was there really a need for people to demonstrate on this? We are delaying the whole process unnecessarily," he noted.

So far most of the people who have contributed to the Bill have suggested that all issues should be discussed during the review process, he said, adding that the Parliamentary Committee on Constitutional Affairs has taken onboard all the opinions and that human rights, judiciary and union matters are now likely to be discussed.

On the parliament's move to table the Bill under certificate of urgency, Dr Kashilila admitted that it qualified to be tabled as an ordinary motion because it had already been published in the Government Gazette on March 11, this year.

"Law and regulations require bills to be published in the Government Gazette 21 days before they are tabled in Parliament. When first tabled in the House on April 7, this year, the Constitutional Review Bill had already been published 25 days before," he explained.

Answering a question on the Speaker's competence, the Clerk Dr Kashilila said the recent chaos witnessed in the august House meetings was caused by lack of understanding of parliamentary regulations by new lawmakers who constitute over 69 per cent of all MPs.

He said almost all the new MPs have little experience on House matters because many of them have never worked before in government or taken part in big debates. He said the Speaker of the National Assembly, Anne Makinda is competent enough to handle the Parliament, but hesitated to punish them because she knew they were still ignorant of the House regulations.

The Legal and Human Rights Centre (LHRC) has singled out use of 'abusive language' and poor attendance as some of the glaring shortcomings tainting the third meeting of the 10th Parliamentary session.

A recent report by the Legal and Human Rights Centre (LHRC) classified the April Parliament session in Dodoma as the most chaotic ever, whereby MPs clearly flouted Parliamentary regulations.

It said that legislators were expected to fulfill their obligations as committed people's representatives. It said booing and uttering provocative remarks like ‘close the doors, let us fight,' or ‘let them go to Loliondo for the healing cup,' were unwarranted and a waste of time.

Mid this month, the National Assembly withdrew the criticised Constitutional Review Bill, 2011 and gave more time for public consultations and contributions to the document. The Bill attracted fierce criticism from academicians, students, legislators, government leaders and other stakeholders from Tanzania Mainland and Zanzibar.

The parliamentary committee that coordinated the public hearings recommended to the government to draft a Kiswahili version of the Bill, to allow more Tanzanians understand the contents of the document and contribute meaningfully.

SOURCE: THE GUARDIAN



.
 
Si kila mwenye PhD ni msomi ila wengi wao huacha akili huko waliko somea na kuchukua karatasi gamba na nyie kuendekeza kuwata ma Dr ndiyo maana wanaleta dharau .Mie nina mshukuru huwa sipendi kumwita mtu kwa title a Dr au Prof bali mie hugonga majina yao moja kwa moja .Ndiyo maana niko huru .
 
na akiegemea hoja ya chadema atakuwa upande gani? Ninachojuwa wao chadema wanaenda kujiridhishatu na mazungumzo yao hayawezi kubadili maamuzi ya bungu, ukweli ndo huo.na kama wana mapendekezo yao wameyatowa wapi? Wamekusanya wapi maoni hayo?,,nafikiri hy kamati yenyewe ndo itaenda kupewa maelezo na sababu zilizopelekea muswaada kusomwa kwa mara ya pili.
akiegemea kwa chadema ina maana maana ameegemea kwa wananchi walio wengi. pili ibara 62(1) ya katiba ya nchi ya mwaka 1977 inasema nanukuu, 'kutakuwa na bunge la jamhuri ya muungano ambalo litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge' kwa maana hiyo Wabunge tayari wameshatimiza wajibu wake, na Rais nae atatimiza wajibu wake yaani kusaini au kutosaini muswada, na kinachotegemewa kutosaini mkataba ili aegemee upande wa wananchi walio wengi.
 
Dah! nchi hii inawasomi wazuri tu! lakini! lakini! masikini! wakishapewa kazi na rahisi wanakuwa kama hata mtoto wa kindagarden afadhali!!
 
Back
Top Bottom