Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Rais wa Zanzibar, Amani Karume hajahudhuria kwenye sherehe za Muungano katika uwanja wa Uhuru. Sababu kubwa iliyoelezwa ni kuwa hali mbaya ya hewa imesababisha ashindwe kutoka Zanzibar kwa ndege kuja kwenye sherehe hizo. Lakini...
Kuna ndege nyingi nimeshuhudia zikitua na kuruka Dar na hizo \inahusisha ndege ndogo zinazotokea Zanzibar. Nimeszishuhudia ndege hizi kwa sababu hapa ninapoishi ni kati ya uwanja wa ndege Dar na Zenji, huwa zinakatisha hapa.
Pia, ipo helkopta ya jeshi ambayo imeweza kutoka Zanzibar hadi Dar, na ikakatiza Uwanja wa Uhuru na mshereheshaji akaatangazia watu kuwa helkopta hiyom ilikuwa inaangalia/inapima hali ya hewa ili kuona kama ndege itakayombeba Rais Karume itafika Dar.
Lakini kuna ndege mbili (za kivita) zimepita uwanja wa Uhuru kama sehemu ya maonyesho ya sherehe hizo.
Ndio maana nimebaki najiuliza kwa nini rais Karume ameshindwa kufika Dar kwenye sherehe hizi? Sikubaliani na hili la hali ya hewa kwa sababu hali ya hewa haikuwa mbaya kiasi cha kuzuia Ndege ya Rais Karume kutoka Zanzibar na kutua Dar.
Najiuliza, kwa nini Rais Karume amekacha sherehe za Muungano mwaka huu?
Kuna ndege nyingi nimeshuhudia zikitua na kuruka Dar na hizo \inahusisha ndege ndogo zinazotokea Zanzibar. Nimeszishuhudia ndege hizi kwa sababu hapa ninapoishi ni kati ya uwanja wa ndege Dar na Zenji, huwa zinakatisha hapa.
Pia, ipo helkopta ya jeshi ambayo imeweza kutoka Zanzibar hadi Dar, na ikakatiza Uwanja wa Uhuru na mshereheshaji akaatangazia watu kuwa helkopta hiyom ilikuwa inaangalia/inapima hali ya hewa ili kuona kama ndege itakayombeba Rais Karume itafika Dar.
Lakini kuna ndege mbili (za kivita) zimepita uwanja wa Uhuru kama sehemu ya maonyesho ya sherehe hizo.
Ndio maana nimebaki najiuliza kwa nini rais Karume ameshindwa kufika Dar kwenye sherehe hizi? Sikubaliani na hili la hali ya hewa kwa sababu hali ya hewa haikuwa mbaya kiasi cha kuzuia Ndege ya Rais Karume kutoka Zanzibar na kutua Dar.
Najiuliza, kwa nini Rais Karume amekacha sherehe za Muungano mwaka huu?