Mimibaba
JF-Expert Member
- Jul 1, 2009
- 4,557
- 1,291
Nimelazimika kukushangaa. CCM miaka yote ina katiba, ilani hata mikakati inayosimamiwa na dola na kusahau wananchi ambao hawana habari na katiba, ilani(kwa maana ya ahadi hewa zisizo na rasilimali za utekelezaji hasa rasilimali watu) na mikakati hiyo. Ingekuwa ina nia ya kukabili upinzani ingeruhu democrasia ichukue mkondo wake iruhusu hata wasio na chama washiriki kwenye siasa wa kudhihirisha mwelekeo mbadala wa siasa. Maana yake ni kuwa na katiba ya nchi ya kidemocrasia.Malalamiko yenu nimeyasoma vizuri na mengine yanahita kujibiwa. Lakini kabla sijajibu, hebu nielezeni ni nini kipya ambacho wapinzani wamesha fanya ili niamini kweli wana nia ya kujenga taifa?
Ukisoma katiba za wapinzani, zote hazina jipya zaidi ya kukopi na kuamend katiba ya CCM chama pekee chenye uongozi bora na uwazi.
Karibuni CCM,
Nakuarifu mimi nilikuwa mwana CCM mara ya mwisho mwaka 1983/4 kilipobinafsishwa. Ahsante