Karibu Prof. Mama Anna Tibaijuka ndani ya JamiiForums!

Status
Not open for further replies.
Yuko wapi sasa huyo Anna Tibaijuka?

Mimi ningependa kumuuliza ile bomoa bomoa yake ya pale mwanzoni alipoanza hii kazi yake ya sasa imeishia wapi?

Maana alikuja na kasi kwelikweli lakini sasa hatuisikii tena hiyo bomoabomoa. Kulikoni? Nguvu ya Mountain Dew au Fanta Pineapple?
Mmeanza!
 
Karibu mama yetu jamvini, mimi ningependa sana hoja yako ya kwanza ambayo ni kubwa mno kuizungumzia ni ile ya mji mpya wa kigamboni, hii inagusa sana hisia za wakazi wa mji huu ambao wanatakiwa kupisha mradi mpya.


1. Waziri Mkuu alifafanua kwamba tathmini ifanyike upya sababu mambo mengi hayakufuata sheria za re-allocation, sasa hili unalizungumziaje, maana hatujaona watathimini wowote toka wizarani kwako wakianza kazi mpaka sasa hivi?

2. Je serikali italipa fidia nyingine kwa wananchi wa eneo hili baada ya kuwazuria kutoendeleza makazi yao kwa miaka miwili -- stop order ya serikali mwaka 2008 - 2010? katika eneo hili?

3. Kuna eneo kubwa sana baada ya Dar Zoo, hilo lipo wazi ambalo linafika hadi Tundwi Songani, Kimbiji, Mbutu nk, ni km 25 - 50 toka katikati ya jiji. hilo halijaendelezwa na linafaa kabisa kujenga mji huu mpya wa kisasa, kwa mantiki hii serikali haitaingia gharama kubwa za ulipaji wa fidia, je mweshimiwa hii hoja unaionaje?

4. Je serikali inapata kigugumizi kipi kuweka kwazi kwamba wananchi wa eneo hili watafute wawekezaji wenyewe na kuingia nao mikataba (wabia kwenye ardhi) ili kujenga mji mpya kufuata ramani iliyopo? kuna hisia za wananchi kwamba serikali inafanya udalali (mtu wa kati) kati ya wananchi na wawekezaji.

Mwisho karibu sana JF.

Namuona ona Dr.F Ndugulile ana like post yako,ili kudanganya watu
kwamba ana fuatilia saaaana mambo ya jimboni kwake.

Niliwahi kumwambia kuhusu wizi na uonevu wanao fanyiwa wafanyakazi wa
TIPER ambao 85% ni wakazi wa jimbo lake akafyata mkia. Hovyoooo.

Wote ni wale wale,ukisha ingia CCM hata uwe msafi kama theluji utanuka shombo tu.
 
Last edited by a moderator:
Karibu sana Mama Tibaujuka, Tunategemea ushirikiano wako wa karibu katika kujibu hoja kwa uhalisia bila kuchakachua/kupika majibu kama ilivyo kawaida ya viongozi wengi. Ila kwa imani tulionayo kwako tunatarajia majibu yenye uzito sawa na hoja na sio majibu mepesi kwa hoja nzito na zenye maslahi kwa taifa letu kwa ujumla.
 
Ana akili sana huyu mama, nimewahi Kuongea nae ana kwa ana mara 4 hivi, nikagundua ni mtu mwerevu sana, tatizo kubwa ni uozo wa hii nchi nadhani hata yeye amekata tamaa, swali langu kwako mh kwanini hampimi maeneo hapa Dar, hivi hizi squatter zitaisha lini, hamkereki kuona miji iliyokaa hovyo hovyo nyie kama serikali jamani...hebu nijibu kwanza...
 
Nami nichukue fursa hii kukukaribisha kama mwanajamvi nina imani na utendaji wako wa kazi, hofu yangu ni kuwa baadae chama chako wanaweza kukuambia ujitoe kama mlivyoambiwa wakati ule wa kunadi sera kupitia TBC
 
Kaibu mama Anna T, ukiwa huko uwazirini ukikutana na Wassira mwambie nae tunamkaribisha hapa
 
Nami nichukue fursa hii kukupongeza mama najua unachapa kazi na utatusaidia katika mambo mengi humu jamvini hofu yangi ni moja kuwa unaweza ukaambiwa na wakubwa zako ujitoe kama mlivyoambiwa wakati wa mchakato majimboni.
 
Hapa ni zaidi ya vikao vya NEC,
Mawazo mbalimbali yaliyo huru hutolewa,
Majibu yenye tija twahitaji
Pia wewe unaruhusiwa kuuliza kuongeza uwezo wako zaidi
 
Mama usisahau kutembelea na majukwaa mengine! kuna raha sana JF, karibu sana.
 
Kwanza nikupongeze sana Mama yetu Prof Anna Tibaijuka kwa uamuzi wako murua wakujiunga na jukwaa hili linaloaminika kuwa ni mwiba mchungu kwa waaminio ni alfa na omega katika nchi hii.

Ninakutia moyo mama yangu kuwa jasiri wa kuuruhuru moyo wako na akili yako vipokee hata yale ambayo hukupenda kuyasikia,

Ninakuomba sana endelea kuwashawishi na waheshimiwa mawaziri na wabunge wajiunge hapa jamvini na ikiwezekana Mh rais nae ajiunge nasi katika kulijenga taifa kwanjia ya jamvi hili.

Mkuu Yeriko Mheshimiwa Raisi yupo huku na ukijua jina lake hata hutaamin. Mpaka ban ashakula
 
Karibu Mama yetu,wewe ni jembe.

Huyu ni moja ya viongozi ambao hawapendi ukiritimba,ukimpigia simu kuomba kuonana nae ofisini anakupa appointment straight away labda kama hata anapokuwa tight anakuambia politely. Shule yako imetulia achana na hizo Masters za Economics.
 
Karibu sana mama Ana Tibaijuka kwani utakuwa mtu wa muhimu kwetu kuhusu matatizo ya ardhi na jinsi gani twaweza kupata hati kwa wale tulionunua viwanja bila kupata hati ya ardhi. Na vilevile mama utatusaidia sisi watanzania wazawa kumiliki japo roho heka ya ardhi kwani sisi ni watanzania tumekuwa tunanyanyaswa sana na raia wa nje karibu mkombozi wetu jukwaani
 
Mimi nina maswali mengi sana kwa huyu mama. Nasubiri mods mkishafungulia mjadala.

Muhimu ningependa mods mumkaribishe pia Mwakyembe na Magufuli katika mjadala huo kama wageni, sababu wizara zao zinakaribiana sana.
 
Prof Anna Tibaijuka,

..karibu sana jamii forums.

..angalia tu usije ukawa "RADICALIZED" na kuanza kuchukia UFISADI na CCM.

..maswali yangu ni haya:

1. Kwanini ulijiunga na CCM chama kilichotamalaki kwa UFISADI?

2. I know u wanted to serve and bring changes to your community and the country at large. Je, kufanya hivyo ilikuwa ni lazima ujiunge na CCM? What would u have missed kwa kujiunga na vyama vingine? Kwanini unafikiri mchango wako ulihitajika zaidi CCM na siyo vyama vingine ambavyo ni vichanga??

3. What part ya matatizo ya Tanzania -- kiuchumi,kisiasa,kijamii, can be attributed to sera mbovu, na uongozi mbaya wa CCM, and what part can be attributed kwa wa-Tanzania wenyewe??

4. Bila kuegemea ktk kujadili masuala la vyama vingine vya siasa, kwanini unafikiri CCM inastihili kuendelea kushika hatamu za uongozi wa nchi yetu. Kuna ripoti imetoka ikieleza kwamba wa-Tz ni masikini kuliko Waganda ambao tuliwakomboa toka makucha ya udikteta mwaka 1978/79.

cc: Nguruvi3, Barubaru, gombesugu, Jasusi, Nyani Ngabu, Kiranga
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom