Kaniacha bila sababu, moyo unaniuma

Jay_the_analyst

JF-Expert Member
Aug 14, 2016
206
151
Ndugu zangu wanajamvi habari za asubuhi.

Nimekuja hapa kuandika uzi huu nikiomba ushauri nikihitaji faraja kutoka kwenu.

Mimi ni kijana miaka 25, mwenzangu huyu 21, nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita, mwenzangu kaishia form 4. Tumekuwa kwenye mahusiano karibu mwaka na nusu. Niseme kweli nilimpenda sana na yeye alinipenda. Nilijitolea sana kwa hali na mali kwa moyo wote kumsaidia katika maisha yake nilimpenda kwa moyo wote. Hali ilibadilika miezi kadhaa tangu tuingie kwenye mahusiano.

Mwenzangu akabadilika ghafla kaanza kunifanyia vituko majibu machafu nikimkosea tena kosa dogo laki binadamu, mwenzangu anachukulia nimefanya makusudi anakuwa mkali ugomvi hauishi wiki nzima. SMS akawa hajibu hata calls zangu hapokei.

Nikachunguza mabadiliko haya nikagundua mitandao ya kijamii ndio imemponza. Nikasema ngoja nipunguze mapenzi. Akajirudi akawa mpole akawa anasema ananipenda. Nikarudisha tena mapenz tena kwake baada ya muda akarudia ile tabia majibu machafu kiburi cha wazi wazi.

Nikaenda kwa mama yake akasema nimvumilie kwa kuwa bado hajakuwa kiakili nikavumilia nikampa onyo akajirekebisha wiki mbili tu baada ya hapo karudia tena tabia ile ile ya kuto nisikiliza anataka asikilizwe yeye tu nikimshauri jambo anajifanya mjuaji sana, kiburi nje nje.

Mimi sikuwahi msaliti na despite ya vituko anavyo nifanyia nilizidi kumwonyesha upendo, mimi nilimlipa kwa mema sijawahi kulipiza kisasi kwake, mpaka ndugu zake walikuwa wakisifia upendo wangu kwake. Lakini mwenzangu alikuwa haoni hilo.

Kila tulipo kosana alitaka tuachane hata kama kosa ni dogo anataka tuachane. Nikikubali anakaa week 1 moja anaomba msamaha na kuahidi kubadilika lakini baada ya hapo tena anarudi madudu.

Jana usiku nilimpigia simu kumsalimia kumjulia hali akakata simu, nikamtumia SMS hajajibu. Nilipompigia mara ya pili akapokea nikamuuliza kwanini anafanya hivyo akasema hajisikii kuwa na mimi nikamuuliza kwanini, ni kosa gani nimekutenda akasema hakuna ila hajisikii tu na ananitakia maisha mema na mahusiano yaishe.

Sasa wadau sijamtenda baya lolote lakini yeye kaamua hivinifanyaje?

Naomben ushauri?
 
hivi mbna unakua kama gari la mkaa wiki moja gereji week moja barabaran..... embu achana nae umri huo unasumbuliwa na kibinti cha early 20's........... na yet hujui nn cha kufanya.
sifa ya mwanaume ni kua na msimamo katika maamuzi kuwa hvyo bas.
Kama kamwaga mboga wew mwaga ugali. Mbona unaonyesha udhaifu mkuu
Ndugu zangu wanajamvi habari za asubuhi.

Nimekuja hapa kuandika uzi huu.. nikiomba ushauri.. nikihitaji faraja kutoka kwenu.

Mim ni kijana miaka 25 , mwenzangu huyu 21. nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita.. mwenzangu kaishia form 4.
Tumekuwa kwenye mahusiano karibu mwaka na nusu. Niseme kweli nilimpenda sana na yeye alinipenda. Nilijitolea sana kwa hali na mali kwa moyo wote kumsaidia katika maisha yake... nilimpenda kwa moyo wote. Hali ilibadilika miez kadhaa tangu tuingie kwenye mahusiano...

Mwenzangu akabadilika gafla.. kaanza kunifanyia vituko.. majibu machafu.. nikimkosea tena kosa dogo laki binadamu ,mwenzangu anachukulia nimefanya makusudi.. anakuwa mkali ugomvi hauishi wiki nzima. Sms akawa hajibu.. hata calls zangu hapokei..

Nikachunguza... mabadiliko haya.. nikagundua mitandao ya kijamii ndio imemponza ..
Nikasema ngoja nipunguze mapenz. Akajirudi akawa mpole.. akawa anasema ananipenda. Nikarudisha tena mapenz tena kwake... baada ya muda akarudia ile tabia... majibu machafu.. kiburi cha wazi wazi..

Nikaenda kwa mama yake ... akasema nimvumilie.. kwa kuwa bado hajakuwa kiakili... nikavumilia ..nikampa onyo... akajirekebisha wiki mbili tu.. baada ya hapo karudia tena tabia ile ile ya kuto nisikiliza.. anataka asikilizwe yeye tu.. nikimshauri jambo anajifanya mjuaji sana..
Kiburi nje nje...

mimi sikuwah msaliti.. na despite ya vituko anavyo nifanyia..nilizidi kumwonyesha upendo, mimi nilimlipa kwa mema.. sijawah kulipiza kisasi.. kwake. Mpaka ndugu zake walikuwa wakisifia upendo wangu kwake. Lakin mwenzangu alikuwa haoni hilo.

Kila tulipo kosana... alitaka tuachane ... hata kama kosa ni dogo.. anataka tuachane..
Nikikubali anakaa week 1 moja .. anaomba msamaha.. na kuahid kubadilika.. lakin baada ya hapo tena anarudi madudu.

Jana usiku nilimpigia simu kumsalimia .. kumjulia hali.. akakata simu.. nikamtumia sms hajajibu. Nilipo mpigia mara ya pili akapokea.. nikamuuliza kwann anafanya hivyo.. akasema hajisikii kuwa na mm... nikamuuliza kwa nn, ni kosa gani nimekutenda.. akasema hakuna ila hajisikii tu.. na ananitakia maisha mema na masiano yaishe.

Sasa wadau.. sijamtenda baya lolote .. lakin yeye kaamua hiv.. nifanyaje.. naomben ushauri?
 
Hizo anazokuonyesha ndiyo tabia yake halisi and ndiyo maana umejitahidi kumuonya ameshindwa kubadilika....

Ukiendelea kumng'ang'ania atakusumbua.

"Birds of the same feathers flock together"

Akipata mwenye kiburi mwenzake wataendana, jipe muda utamsahau utafute muungwana mwenzio.
 
kifupi wewe una mbembeleza mtafutie time kwanza na wewe akipiga usipoke mda mwingine mpe adhabu kama mwezi hivi then utaona wewe una muogopa kumpoteza una onyesha mi wangu alikuwa hivyo ni simple saizi kimya kajielewa
 
Kijana pole sana....mie yamenikuta hayo.niliumia sana tena sana....ila nikaamua kumtumbua jipu tu hamna namna.....ila kikubwa nilivyoona haeleweki nikaamua kumuwekea vikwazo vya kiuchumi...........muacha pasipo mjulisha mwanaume hamwaachi binti kwa maneno magumu.ila usiwe wa kukupeleka peleka ukamrudia....Mungu atakupa mwema,mpole na mwenye mapenzi ya dhati kwako......MUACHE AENDE ATAKUKUMBUKA SANA atapotekwa na vijana wa mwendokasi
 
Back
Top Bottom