Kamwe Haiwezekani kuwashinda maadui watatu!!

kipindupindu

JF-Expert Member
Dec 16, 2010
1,053
170
Je tujiulize mwalimu Nyerere alikua anafikiria nini?

Alisema maadui wanaotukabili kama taifa ni watatu yaani UJINGA, MARADHI NA UMASIKINI.

Naamini huu ndio msingi uliomuongoza mwalimu katika kujaribu kuleta maendeleo nchini.

Kwa maoni yangu naamini huwezi kupambana na maadui watatu kwa pamoja halafu utegemee ushindi,kamwe haiwezekani!
Je wanazuoni wafuasi wa mwalimu Nyerere mnaelezea vipi hii falsafa ya Nyerere?

Binafsi naona adui yetu ni mmoja tu -UJINGA.watanzania bado ni wajinga sana wanahitaji elimu,kwa bahati mbaya hata wale wanaoitwa wasomi; wataalamu au viongozi bado ni mbumbumbu mno.

Ukweli huu unanifanya niseme kwamba ni vyema tupambane na adui mmoja yaani UJINGA.Tukifanya hivi tutashinda!

Nawasilisha:
 
Achana na siasa za Nyerere. Adui yetu mkubwa ni UFISADI.

Tukiondoa ufisadi, hayo mambo mengine yataji set yenyewe
 
Ujinga mbaya ni ule wa watu wanaojidai kwenda shule na ma Phd na hawajui/hawataki kuwasaidia watanzania,wale wasiojua kabisa ni rahisi kuwavuta
Kwa sasa hivi adui Ufisadi ndiye mkubwa kuliko wote
 
Naona mnazungumzia sera za Nyerere ambayo kwa sasa hivi havizingatiwi na tuko kwenye zama ambazo kama taifa hatujui maadui wetu ni wapi? Leo tunashuhudia serikali ina vipaumbele zaidi ya kumi kwa wakati mmoja! Hili hamulioni ni ambigous kuliko siku zote?
 
Achana na siasa za Nyerere. Adui yetu mkubwa ni UFISADI.

Tukiondoa ufisadi, hayo mambo mengine yataji set yenyewe

mkuu ufisadi ni ngumu kuuondoa,nadhani hakuna nchi isiyokuwa na ufisadi.tatizo la msingi ni ujinga,ujinga huu unatufanya kuwachagua viongozi wale wale ambao tunaambiwa ni mafisadi.ujinga unatufanya tushindwe kutambua athari za ufisadi katika maisha yetu ya kila siku,pia ni ujinga huo huo unawafanya mafisadi wasiwe na mbinu za kutafuta utajiri zaidi ya 'kufisidi' ujinga unawafanya waliopewa mamlaka ya kuzuia ufisadi waogope kutumia mamlaka hayo kuzuia au kuchukua hatua dhidi ya ufisadi.ujinga wetu unatufanya tusihoji au kuchukua hatua dhidi ya madhalimu wachache.tuondoe ujinga kwanza ndipo tutakapoweza kupambana na maadui wengine.
Nyerere alikuwa sahihi kuwataja hawa maadui watatu lakini alishindwa au hakujua ni yupi aliye hatari zaidi ambaye anahitaji mashambulizi makali.
 
kaka nakubaliana na wewe kwani mtu anaweza akawa amesoma lakini elimu yake haija msaidia kitu kwani mwanafalsafa mmoja aliwahi kusema 'respectability is the cloak under which the fool hide their stupidity'.{kwa tafsiri isiyo rasmi mtu anaweza akawa amesoma sana,anacheo kikubwa na anavaa vizuri sana lakini yote ni kificho cha ujinga wake hivyo mimi naona adui yetu mkubwa bado ni ujinga
 
Back
Top Bottom