Kampa mwanamke mimba anadai bado ananipenda

Mrs minel

Member
Sep 3, 2014
64
53
Habari JF,

Mimi ni binti nilikua na mpenzi wangu tuliyedumu kwa miaka miwili, ingawa hakua officially ila alijulikana kwetu. Kuna kipindi tulikwazana mwezi mzima baadae tukaelewana.

Sasa hivi majuzi, nimegundua ana mwanamke na ana mimba yake. Tukakaa chini kuzungumza anadai alikutana na huyo mwanamke kipindi tumekwazana na anajutia sana kwani mimi ndiye chaguo lake so anaomba nimvumilie mpaka huyo mwanamke ajifungue then atanioa.

Anaogopa kumkwaza huyo mwanamke kwa sasa, atatoa mimba yake. Na pia anasema huyo mwanamke ana tatizo la moyo so asije akadhurika, kwahiyo mimi nivumilie tu awe nae mpaka atakapojifungua atarudi kwangu.

Jamani, naumia na nipo njia panda.
Kumpenda nampenda mno na yeye kuniacha hataki kabisa naumia jamani.

Nisaidieni ushauri
 
wewe mwenyeo una maamuzi gani, unajua uyo mwanamke alomtia mimba ana msimamo gani, kama uyo alomtia mimba unamjua basi mchunguze
 
wewe mwenyeo una maamuzi gani, unajua uyo mwanamke alomtia mimba ana msimamo gani, kama uyo alomtia mimba unamjua basi mchunguze
nimeshachunguza huyo mwanamke mwenye mimba ana mtoto mdogo na yupo kwenye process za talaka means alikua ameolewa
 
nimeshachunguza huyo mwanamke mwenye mimba ana mtoto mdogo na yupo kwenye process za talaka means alikua ameolewa
pyuuuu huna bf hapo aiseee.. unategemea apewe talaka amuache huyo mpenzio .. bibi wewe tafuta mwanaume mwingine
 
Mioyo ni midanganyifu always

Hiko kimeo kinaku enjoy tu
na nna uhakika hiyo hadithi ya huyo mwanamke kuumwa moyo ni ya kutunga

kwa ufupi umeambiwa usim disturb 'the real mrs'..
wewe ushapangwa uwe mchepuko
napenda watu walio open km wewe ingawa inauma thanks for the advice
 
Back
Top Bottom