Kamati ya Zitto yaishukia PPF Juu ya Malipo ya Mamilioni ; Yaagiza kusitishwa malipo mapya!

Status
Not open for further replies.
Zitto NA WENGINEO,

Naomba kuuliza ili kuepekana na hizi policy za serikali hasa katika pension funds na marupurupu ya kujilimbikizia kwanini wakurugenzi (directors) na utawala wasiwe wanapewa contract za miaka 5. Na katika contract za miaka 5 malipo yao kuwepo na mshahara (lump sum), na incentive based on PERFORMANCE???

Swali jengine ni malipo ya wakurugenzi wakuu wa hizi pension kwanini SSRA isiweke kipengele kuwa kila mwaka malipo haya yatolewe in public ijulikane?

Nauliza tu kutaka kufahamu.

Swali zuri, ila katika nchi hii ya Tanzania ambayo mshahara wa Rais na marupurupu yake ni "SIRI" nadhani hili jambo ni gumu. Henu tuanze kudai kwanza kujua mishahara ya viongozi wakuu wa nchi kama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, Spika wa Bunge, IGP, CFD, DG wa usalama wa taifa, DG wa PCCB, mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, etc ndiyo tuhamie wakuu wa mashirika ya umma kama PPF, NSSF, BoT, TIB, TRA, nk
 
Duh! Nilipoanza tu kuisoma ile original post nikai-dismiss easily kuwa leo ni April fools' day:tea:. Nikamaliza na nikawa na amani yangu saafi. Niliposoma first line ya post ya mh. Zitto nika-confirm ok..."Habari ya kuisifia PPF imetoka Jamboleo. Ni uongo. Its a spin." But nikiendelea nikaanza kushtuka kdogo, heee...mbona imekanushwa like 70% hivi tuu?! Ina maana kuna kiasi kidogo cha ukweli kumbe?....Amani yangu imetoweka as of now! Hivi ni mimi tuu nnawaza vibaya? "Malalamiko" yote haya ya wananchi CAG hajayaskia,fine,yawezekana yalimpita kdogo,alisafiri labda, halafu sio member wa JF. Aliyewapa tuzo nae pengine hakuweza kuyaona,fine. Sasa na kamati nayo iliwapongeza kwa tuzo "utawala bora" kabla au baada ya kujua "malalamiko" hayo? Au ni mpaka yathibitishwe kwanza na "vyombo vinavyohusika" ndipo wanaweza kulichukua vinginevyo?
Nimesema hansard nitaweka hapa. Kuhusu tuzo ya utawala bora tuliwapongeza. Kuhusu hati safi tuliwapongeza. Tumewakaripia kuhusu malipo na TUMEYAZUIA. Kupata gratuity na group endowment is against the public service act. Double payment hairuhusiwi. CAG ameagizwa kukagua malipo ya nyuma ya PPF na kama yalikwenda kinyume na sheria waliolipwa lazima warejeshe. Nimelisema wazi hilo jana.
Tuzo ya ubora ya EAC is a small matter here and we didn't even discuss it. Hati safi kila shirika sasa linapata kwa kuwa CAG anakuwa hayaoni haya ambayo wananchi wanayalalamikia.
Hii sio kwa PPF tu, tumemwambia aende mashirika yote. Tayari kamati imepiga stop kwa TPA mwaka jana na wamefuta.
You get pension, its a right. Endowment is an incentive, powa. Gratuity without endowment is ok. Gratuity plus endowment is wrong. Ni mfumo wa wizi kwa watu wachache. Tumeupiga marufuku. Kwa mashirika yote ya umma.
Pia endowment schemes za mashirika ziwe managed na fund managers na sio shirika lenyewe. Those were major decisions.

Kuhusu jamboleo nimemjulisha katibu wa Bunge awaite na kuwahoji wajieleze.
 
Kwenye post zake humu JF, Mzee Mwanakijiji ameweka invoice za malipo ya Group Endowment Scheme ambayo menejimenti ya PPF wamelipwa mamilioni ya pesa akasema hii ni corruption kumbe ni utaratibu unaoruhusiwa na hata kamati ya POAC imeshauri TANAPA nao wauanzishe.

Kinachokatazwa ni double payment ya Group Endowment Scheme na gratuity kwa mtu mmoja. Lakini ieleweke kuwa malipo ya gratuity yanatokana na uamuzi wa serikali yenyewe kusema menejimenti ya PPF wawe kwenye ajira ya mikataba na si ajira ya kudumu.

Hapa suluhisho ni dogo tu. Serikali itangaze kuwa menejimenti ya PPF na mashirika mengine yote ya umma iwe kwenye ajira ya kudumu (permanent and pensionable employment) ili kuondokana na malipo ya gratuity.

Kuna mtazamo kuwa menejimenti inapokuwa mkataba wa muda wanakuwa hawana uzalendo sana na hawazingatii maslahi ya kudumu ya shirika kwani wanajua kuwa ajira yao ni ya mkataba wa muda mfupi.

Menejimenti wanapokuwa kwenye mkataba wa kudumu wanakuwa motisha zaidi na kuwa na ownership zaidi na shirika wanaloliongoza.
tatizo la permanent ni pale performance inapokosa kuwa kigezo cha kuondoa mtu
 
Swali zuri, ila katika nchi hii ya Tanzania ambayo mshahara wa Rais na marupurupu yake ni "SIRI" nadhani hili jambo ni gumu. Henu tuanze kudai kwanza kujua mishahara ya viongozi wakuu wa nchi kama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, Spika wa Bunge, IGP, CFD, DG wa usalama wa taifa, DG wa PCCB, mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, etc ndiyo tuhamie wakuu wa mashirika ya umma kama PPF, NSSF, BoT, TIB, TRA, nk

niulize tu ...mbona hamtuletei taharifa za kamati zingine za bunge ama ndo yaleyale ya Zitto,Zitto,Zitto...tunashukuru tumeziona za Zuberi,tupeni za wengine k.v nishati na madini...,maliasiri na utalii n.k
 
Habari ya kuisifia PPF imetoka Jamboleo. Ni uongo. Its a spin.

Kamati imewakaripia PPF na tumemwagiza CAG achunguze malipo yakiyokwisha fanywa, tumesimamisha malipo ya sasa na tumepiga marufuku double payments ie gratuity na endowment scheme. The citizen wameandika sawa na hata Dailynews wameandika sawa. Maslahi ya JamboLeo ni nini kupotosha habari ya kamati?

Mfumo wa ajira za mikataba kwa mashirika ya umma ni mwanya wa senior staff kujilipa mabilioni ya fedha za Mashirika. CAG ameelekezwa na kamati kukagua mfumo huu kwa mashirika yote ya umma kwa kuanzia na mifuko ya pensheni kisha mashirika makubwa kama TANAPA, TCRA, EWURA nk. Mwaka jana kamati iliagiza TPA kuachana na mfumo huu na vile vile Katibu Mkuu utumishi alitoa waraka kuzuia mfumo wa aina hii.

Endowment scheme ni kwa wafanyakazi wote wa shirika na inakubalika. Gratuity ni ufujaji wa mali na ni marufuku kwa mtu mmoja kufaidika na gratuity na wakati huo huo endowment scheme.

Nitamletea mod hansard ya kikao cha kamati ili wasomaji wa JF waone ukweli wa mjadala na habari ya jambo leo ambayo ni spin ipuuzwe!

Kaka, mojawapo ya vitu ambavyo vinatokea (ukiangalia zile invoice) ni kuwa watu wanapata mikopo toka kwenye mashirika (wa nyumba au gari) say kama milioni 40, ambazo atatakiwa kulipa katika muda fulani. Halafu baadaye anapata endowment ya milioni 120 ambayo anatumia kulipa mkopo/mikopo yake na bado anabakia na fedha taslimu.

Kimsingi utaona kuwa huyu mtu kajengewa nyuma na kununuliwa gari bure...! Maana hajakatwa mshahara wala kitu chochote!!
 
Swali zuri, ila katika nchi hii ya Tanzania ambayo mshahara wa Rais na marupurupu yake ni "SIRI" nadhani hili jambo ni gumu. Henu tuanze kudai kwanza kujua mishahara ya viongozi wakuu wa nchi kama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, Spika wa Bunge, IGP, CFD, DG wa usalama wa taifa, DG wa PCCB, mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, etc ndiyo tuhamie wakuu wa mashirika ya umma kama PPF, NSSF, BoT, TIB, TRA, nk

This is flawed reasoning ndugu yangu; kwanini tufanye hivi halafu baadaye ndiyo "tuhamie" kwingine? Yaani, tuwaache wengine waendelee kuboronga halafu baadaye ndio tuwashukie?
 
Kwenye post zake humu JF, Mzee Mwanakijiji ameweka invoice za malipo ya Group Endowment Scheme ambayo menejimenti ya PPF wamelipwa mamilioni ya pesa akasema hii ni corruption kumbe ni utaratibu unaoruhusiwa na hata kamati ya POAC imeshauri TANAPA nao wauanzishe.

Nadhani bado hujaelewa kinachogombewa ni nini? Hatukusema kuwa GES ni corruption! Tulichoonesha na ambacho tutaonesha mbeleni ni kuwa wakurugenzi wa PPF walitumia ambiguity ya sheria/ taratibu zao wenyewe kujifanya wanastahili malipo ya GES wakati tayari walikuwa wanalipwa gratuity ya 25% ya mishahara yao. Walichokifanya ni kukubaliana kuwa "wao wanastahili" mwisho wa mkataba.

Tatizo ni kuwa GES ni malipo kwa mtu aliyemaliza ajira siyo mkataba. Sasa wao walipolipwa 2008 ingekuwa wameondoka PPF ingeonekana hata labda kuna kukubaliana lakini ulikuwa ni "mwisho wa mkataba" mmoja na wakaanza mkataba mwingine. Walitumia nafasi zao kujistahilisha na baadaye kuhalalisha malipo ambayo vinginevyo wasingeyastahili; huu ndio ufisadi.

Lakini vile vile, kanuni ya GES ni ipi? Kwa hiyo ukiondoa hilo kuna suala la kiwango cha malipo; ni mfanyakazi gani wa PPF ambaye ametumikia shirika hilo na siyo Mkurugenzi ambaye atapata GES ya milioni 220!?

Kinachokatazwa ni double payment ya Group Endowment Scheme na gratuity kwa mtu mmoja. Lakini ieleweke kuwa malipo ya gratuity yanatokana na uamuzi wa serikali yenyewe kusema menejimenti ya PPF wawe kwenye ajira ya mikataba na si ajira ya kudumu.

Hapa suluhisho ni dogo tu. Serikali itangaze kuwa menejimenti ya PPF na mashirika mengine yote ya umma iwe kwenye ajira ya kudumu (permanent and pensionable employment) ili kuondokana na malipo ya gratuity.

Kuna mtazamo kuwa menejimenti inapokuwa mkataba wa muda wanakuwa hawana uzalendo sana na hawazingatii maslahi ya kudumu ya shirika kwani wanajua kuwa ajira yao ni ya mkataba wa muda mfupi.

Menejimenti wanapokuwa kwenye mkataba wa kudumu wanakuwa motisha zaidi na kuwa na ownership zaidi na shirika wanaloliongoza.

To tell you the truth; natofautiana na Zitto kwenye hili: Watendaji hawa walistahili kulipwa Gratuity kwa mujibu wa mikataba yao na siyo GES. Kwa vile wao walikuwa ni waajiriwa wa mkataba basi walikuwa waongozwe na mikataba hiyo. GES ni kwa ajili ya watumishi wa kudumu wa PPF. HIvyo, Wakurugenzi hawa wa mikataba hawakustahili kulipwa kutoka GES.
 
Nimesema hansard nitaweka hapa. Kuhusu tuzo ya utawala bora tuliwapongeza. Kuhusu hati safi tuliwapongeza. Tumewakaripia kuhusu malipo na TUMEYAZUIA. Kupata gratuity na group endowment is against the public service act. Double payment hairuhusiwi. CAG ameagizwa kukagua malipo ya nyuma ya PPF na kama yalikwenda kinyume na sheria waliolipwa lazima warejeshe. Nimelisema wazi hilo jana.
Tuzo ya ubora ya EAC is a small matter here and we didn't even discuss it. Hati safi kila shirika sasa linapata kwa kuwa CAG anakuwa hayaoni haya ambayo wananchi wanayalalamikia.
Hii sio kwa PPF tu, tumemwambia aende mashirika yote. Tayari kamati imepiga stop kwa TPA mwaka jana na wamefuta.
You get pension, its a right. Endowment is an incentive, powa. Gratuity without endowment is ok. Gratuity plus endowment is wrong. Ni mfumo wa wizi kwa watu wachache. Tumeupiga marufuku. Kwa mashirika yote ya umma.
Pia endowment schemes za mashirika ziwe managed na fund managers na sio shirika lenyewe. Those were major decisions.

Kuhusu jamboleo nimemjulisha katibu wa Bunge awaite na kuwahoji wajieleze.

Zitto pengine wewe ndiyo unajaribu kufanya spin hapa. Nimeongea na watu watatu tofauti waliokuwepo kwenye hicho kikao cha kamati yako wamesema gazeti la Jambo Leo limeandika ukweli. Gazeti hilo halijaandika uongo hata kidogo kama unavyodai wewe. Weka hiyo hansard hapa haraka tuione.

Kwa mujibu wa mashuhuda hao, Zitto alitoa pongezi zisizopungua 3 kwa PPF:

(i) Pongezi kwa PPF kwa kuwa na hati safi ya ukaguzi
(ii) Pongezi kwa PPF kwa kuwa mfuko unaoweza kudumu kwa miaka mingi kuliko mifuko yote
(iii) Pongezi kwa PPF kwa kupata tuzo ya kimataifa ya utawala bora

Pamoja na pongezi hizo kwa PPF, wewe na wajumbe wengine walionesha kutoridhika na baadhi ya mambo PPF ikiwemo hiyo double payment ya Group Endowment Scheme na Gratuity, Mbunge kuwa mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa PPF, Director of Internal Audit kuwa kwenye menejimenti, na kutoa maagizo Endowment Fund ya PPF iendeshwe na fund managers nje ya PPF.

Kwa hiyo ulitoa "karipio" kama ulivyosema mwenyewe na pia ulitoa "pongezi" kwa PPF kwa mambo kadhaa. Sasa ni haki ya waandishi wa habari wenyewe kuamua wanaandika habari kwa kuchagua "angle" gani. Wewe huwezi ku-dictate story iandikwe kwa mwelekeo gani. Ni sawa na kuwa na glasi ya maji iliyo nusu. Mmoja anaweza kuone iwe half empty mwingine akaona ni half full.

Kusema Jambo Leo wameandika uongo si sahihi. Zitto kudai eti amemjulisha katibu wa Bunge awa "summon" Jambo Leo na kuwahoji wajieleze ni vitisho vya kitoto. Zitto weka hiyo hansard hapa tuone kama hujatoa pongezi kwa PPF. I dare you!
 
Swali zuri sana.... imefikia wakati magazeti yaache utani na mambo ya maslahi kwa taifa.... nadhani bunge lina nguvu sana na adhabu kwa jambo leo italeta heshima, walifungie gazeti, mwandishi, mhariri na yeyote aliehusika... kwenye professionalism, misconducts may lead to deletion or suspension ya kupractice

waliohusika wafungiwe kabisa kufanya hiyo kazi
bunge lipi ndugu yangu la mama au?
 
CAG, Katibu Mkuu Kuingozi, au Wizara ya Fedha wanatakiwa watoe waraka kuhusu nani anastahili kuweko kwenye Group endowment scheme au wafute contract employment kwa wafanyakazi wa menejimenti ili kuondoa gratuity.

Wakati watu wameshajilipa na kujilipia madeni?
 
Nadhani bado hujaelewa kinachogombewa ni nini? Hatukusema kuwa GES ni corruption! Tulichoonesha na ambacho tutaonesha mbeleni ni kuwa wakurugenzi wa PPF walitumia ambiguity ya sheria/ taratibu zao wenyewe kujifanya wanastahili malipo ya GES wakati tayari walikuwa wanalipwa gratuity ya 25% ya mishahara yao. Walichokifanya ni kukubaliana kuwa "wao wanastahili" mwisho wa mkataba.

Tatizo ni kuwa GES ni malipo kwa mtu aliyemaliza ajira siyo mkataba. Sasa wao walipolipwa 2008 ingekuwa wameondoka PPF ingeonekana hata labda kuna kukubaliana lakini ulikuwa ni "mwisho wa mkataba" mmoja na wakaanza mkataba mwingine. Walitumia nafasi zao kujistahilisha na baadaye kuhalalisha malipo ambayo vinginevyo wasingeyastahili; huu ndio ufisadi.

Lakini vile vile, kanuni ya GES ni ipi? Kwa hiyo ukiondoa hilo kuna suala la kiwango cha malipo; ni mfanyakazi gani wa PPF ambaye ametumikia shirika hilo na siyo Mkurugenzi ambaye atapata GES ya milioni 220!?



To tell you the truth; natofautiana na Zitto kwenye hili: Watendaji hawa walistahili kulipwa Gratuity kwa mujibu wa mikataba yao na siyo GES. Kwa vile wao walikuwa ni waajiriwa wa mkataba basi walikuwa waongozwe na mikataba hiyo. GES ni kwa ajili ya watumishi wa kudumu wa PPF. HIvyo, Wakurugenzi hawa wa mikataba hawakustahili kulipwa kutoka GES.

Issue ni kuwa serikali kupitia Bodi ya Wadhamini iliamua mwaka 2002 kuwa menejimenti ya PPF wawe kwenye mikataba. Wakati uamuzi huu unafanywa, menejimenti ya PPF walikuwa wafanyakazi wa kudumu na wako kwenye Group Endowment Scheme (GES). Hivyo walivyoingia kwenye ajira ya mikataba wakaendelea kupata GES na gratuity kila mkataba ukiisha.

Sidhani kama kuna sheria yoyote iliyo wazi inayosema kuwa GES lazima awe ni mwajiriwa wa kudumu na wale wa mikataba hawaruhusiwi. Pia hakuna usimamizi/waraka/sera wa hizi GES unaofanywa na Hazina hivyo kutokea huu utata.
 
Nimesema hansard nitaweka hapa. Kuhusu tuzo ya utawala bora tuliwapongeza. Kuhusu hati safi tuliwapongeza. Tumewakaripia kuhusu malipo na TUMEYAZUIA. Kupata gratuity na group endowment is against the public service act. Double payment hairuhusiwi. CAG ameagizwa kukagua malipo ya nyuma ya PPF na kama yalikwenda kinyume na sheria waliolipwa lazima warejeshe. Nimelisema wazi hilo jana.
Tuzo ya ubora ya EAC is a small matter here and we didn't even discuss it. Hati safi kila shirika sasa linapata kwa kuwa CAG anakuwa hayaoni haya ambayo wananchi wanayalalamikia.
Hii sio kwa PPF tu, tumemwambia aende mashirika yote. Tayari kamati imepiga stop kwa TPA mwaka jana na wamefuta.
You get pension, its a right. Endowment is an incentive, powa. Gratuity without endowment is ok. Gratuity plus endowment is wrong. Ni mfumo wa wizi kwa watu wachache. Tumeupiga marufuku. Kwa mashirika yote ya umma.
Pia endowment schemes za mashirika ziwe managed na fund managers na sio shirika lenyewe. Those were major decisions.

Kuhusu jamboleo nimemjulisha katibu wa Bunge awaite na kuwahoji wajieleze.

This reminds me of the ORIGINAL ZITTO ZUBERI KABWE... Keep it up mheshimiwa...tuna imani na wewe all the way to MAGOGONI.
 
As cited by Hon. Zitto that the two papers (Dailynews & Thecitizen) reported this matter correctly; I hereby bring in this platform what "Thecitizen" reported for your easy follow-up:
"By Frank Kimboy, The Citizen Reporter
Dar es Salaam. A parliamentary committee has directed the Controller and Auditor General (CAG) and the Treasury to review agreements of all contractual employees in public organisations to ensure they don’t pocket unrealistic benefits upon expiry of their terms.

The directive came after the Public Organisations Account Committee (POAC) smembers were informed that the Parastatal Pensions Fund (PPF) in 2009 paid three workers a total package of Sh1.2 billion in response to contracts which they had entered with the Fund. This was revealed by the PPF director general, Mr William Erio, when presenting PPF’s 2009 performance statement.

Mr Erio told the committee that PPF will this year pay about Sh300 million as further group endowment allowances and as gratitude allowances to three directors whose contracts would have expired.Mr Erio also told POAC that in 2009 PPF paid Sh1.2 billion as group endowment fund and as gratitude allowances to several contractual employees. However, some of those who were paid the allowances were rehired under a contractual basis and continued in their capacities, Mr Erio told POAC members. He told the committee that according to the Pension Funds’ Act, all directors should be employed on a five-year contractual term.
Issuing the directive, POAC chairperson Zitto Kabwe (Kigoma North-Chadema) said the CAG and the Treasury should start investigations on pension funds, where the problem has been detected, before moving to other public organisations.

Mr Kabwe said CAG has also been instructed to scrutinise those who have benefited from the system for the past five years to see if the laws were adhered to when contracting them.“Once an agreement with a contractual employee comes to an end he or she is supposed to be paid gratitude allowance for his services to the organisation and leave employment. How come the same person is involved in the group endowment scheme?” Mr Kabwe wondered.

Earlier, Mr Erio told POAC that PPF has been paying between Sh132 million to Sh220 million as endowment and gratitude allowance to directors whose contracts expire. Commenting on the decision, a member of the committee Kangi Lugola (Mwibara - CCM) said it was hard to believe that there were some people who were pocketing millions of tax payers’ money in pretence that they have retired only to go back to their offices.

“You cannot fetch more than Sh200 million as your retirement benefit after every five years only to go back to your office. This cannot be tolerated,” he warned. Mr Kabwe said CAG should also review the contracts in line with a circular issued on December 2009 by the Public Services Management ministry.

The circular, according to Mr Kabwe, requires all the managements of public organisations to make sure that all contractual employments are not renewed upon their expiry, unless the said employee opts to be employed permanently.

The committee also directed PPF Board of Trustees vice chairman, Dr Kassim Kapalata, to write to the minister of Finance asking him to remove Ms Rosemary Kirigini from the board as the law doesn’t allow an MP to serve on it.
“Parliament passed a law that prohibits any MP from serving as a member of the board of directors or trustees in any financial institution. I wonder why Ms Kirigini is still on the board… You should bring your report on this matter during our next meeting,” he directed.

The committee also ordered PPF to float a tender for other pension funds which would manage its group endowment scheme. He said it was not right for PPF to manage its own scheme.In his report, Mr Erio said by December 2009 the fund had grown by Sh125.5 billion compared to 2008 when the growth recorded was Sh499.3 billion.

Mr Erio said currently PPF was paying between Sh50,000 to Sh6.2 million to each of the 20,000 retirees as monthly pension allowances. He added that in 2009 PPF used Sh47.19 billion as pension allowances to retirees.
However, he said many PPF members have been complaining about the methods the fund has been using to calculate pensions. But the PPF director general added that currently the government was working hard to ensure that the method used to calculate pension allowances under PPF resembles the one used by PSPF and LAPF".
 
Habari ya kuisifia PPF imetoka Jamboleo. Ni uongo. Its a spin.

Kamati imewakaripia PPF na tumemwagiza CAG achunguze malipo yakiyokwisha fanywa, tumesimamisha malipo ya sasa na tumepiga marufuku double payments ie gratuity na endowment scheme. The citizen wameandika sawa na hata Dailynews wameandika sawa. Maslahi ya JamboLeo ni nini kupotosha habari ya kamati?

Mfumo wa ajira za mikataba kwa mashirika ya umma ni mwanya wa senior staff kujilipa mabilioni ya fedha za Mashirika. CAG ameelekezwa na kamati kukagua mfumo huu kwa mashirika yote ya umma kwa kuanzia na mifuko ya pensheni kisha mashirika makubwa kama TANAPA, TCRA, EWURA nk. Mwaka jana kamati iliagiza TPA kuachana na mfumo huu na vile vile Katibu Mkuu utumishi alitoa waraka kuzuia mfumo wa aina hii.

Endowment scheme ni kwa wafanyakazi wote wa shirika na inakubalika. Gratuity ni ufujaji wa mali na ni marufuku kwa mtu mmoja kufaidika na gratuity na wakati huo huo endowment scheme.

Nitamletea mod hansard ya kikao cha kamati ili wasomaji wa JF waone ukweli wa mjadala na habari ya jambo leo ambayo ni spin ipuuzwe!

Mh. Zitto. Nina kajihadithi kanakohusu tatizo lililoonyeshwa kwa maandishi mekundu hapo juu.
JamboLeo si bure na wala si wao tu. Naomba nikuonye hata wewe unaweza kujikuta umeangukia ktk tatizo hilo. Tatizo ni PPF. Tumekuwa tukizungumzia tatizo la PPF kuwahonga waandishi wa Habari kwa kutumia pesa hizo hizo. Kumbuka mwaka jana Waziri wa fedha alipotoa Hotuba ya kutatanisha juu ya mifuko mingine akiwa Arusha hata isiyokuwa ndani ya wiazara yake, lakini akawasifu PPF. Ilifahamika baadaye kwamba hotuba hiyo ilitoka PPF!

Vyombo vyote vya habari vimekuwa vikishindwa kabisa kuandika ubaya wa PPF isipokuwa TBC kuna wakati ilikubali kuandika mambo kama yalivyo. ITV pia ilishindwa kueleza utatanishi wa PPF na wanachama wake. PPF kila wakiona wanaelekea kuandamwa kwa mabaya yao, wataitisha kongamano na mara nyingi wamekuwa wakikutana huko Morogoro na hapo ndo waandishi wetu hupewa vibahasha. Kuna wakati walipewa tour ya kutembelea Mikumi na baada ya hapo waligeuka kuwa mashabiki wa PPF 100%

Kwa kipindi kirefu PPF wamekuwa na migogoro ya malipo ya pensheni. Mgogoro huu unmekuwa ukisimamiwa na waalimu wa vyuo vikuu. Taarifa niliyopewa ni kwamba ilifikia wakati PPF wakaingilia hata mchakato wa kutatua tatizo hilo. Hata Katibu Mkuu Kiongozi alianza kutoa tamko la kutatanisha na kuonyesha ushabiki wake kwa PPF. Kila kikao akaonekana kuwa upande wa PPF pamoja na kukubali kwamba wanayoyafanya hayafai.

Ndo maana nasema kaa chonjo baada ya marufuku hiyo usione ajabu ukafuatwa na mfuko wa Rambo uliojaa noti. Kama hutaelwa huenda wanakamati wenzako watakusakama! Si unafahamu makovu ya uchaguzi?

PPF tunawajua, lakini kama ulivyoona ktk vocha zilizozungushwa hapa JF. Kuna watu wema ndani ya PPF wanatumegea maovu hayo.

Uliona mchanganuo ulioambatana na vocha hizo? Hao wakurugenzi takribani wote walikuwa na mikopo ya nyumba na baadhi walitaka kulazimisha kusamehewa deni hilo, ingawa ilishindikana lakini Huyo Mkurugenzi mkuu, Erio, alikwisha kubali wasamehewe.
Ni mengi na naamini unazitumia habari za jf vizuri. Fikeni hata huko kwenye Bima ya afya ya Taifa kama iko ndani ya himaya yenu mujionee.

Mashamba ya bibi ni mengi.
 
Zitto pengine wewe ndiyo unajaribu kufanya spin hapa. Nimeongea na watu watatu tofauti waliokuwepo kwenye hicho kikao cha kamati yako wamesema gazeti la Jambo Leo limeandika ukweli. Gazeti hilo halijaandika uongo hata kidogo kama unavyodai wewe. Weka hiyo hansard hapa haraka tuione.

Kwa mujibu wa mashuhuda hao, Zitto alitoa pongezi zisizopungua 3 kwa PPF:

(i) Pongezi kwa PPF kwa kuwa na hati safi ya ukaguzi
(ii) Pongezi kwa PPF kwa kuwa mfuko unaoweza kudumu kwa miaka mingi kuliko mifuko yote
(iii) Pongezi kwa PPF kwa kupata tuzo ya kimataifa ya utawala bora

Pamoja na pongezi hizo kwa PPF, wewe na wajumbe wengine walionesha kutoridhika na baadhi ya mambo PPF ikiwemo hiyo double payment ya Group Endowment Scheme na Gratuity, Mbunge kuwa mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa PPF, Director of Internal Audit kuwa kwenye menejimenti, na kutoa maagizo Endowment Fund ya PPF iendeshwe na fund managers nje ya PPF.

Kwa hiyo ulitoa "karipio" kama ulivyosema mwenyewe na pia ulitoa "pongezi" kwa PPF kwa mambo kadhaa. Sasa ni haki ya waandishi wa habari wenyewe kuamua wanaandika habari kwa kuchagua "angle" gani. Wewe huwezi ku-dictate story iandikwe kwa mwelekeo gani. Ni sawa na kuwa na glasi ya maji iliyo nusu. Mmoja anaweza kuone iwe half empty mwingine akaona ni half full.

Kusema Jambo Leo wameandika uongo si sahihi. Zitto kudai eti amemjulisha katibu wa Bunge awa "summon" Jambo Leo na kuwahoji wajieleze ni vitisho vya kitoto. Zitto weka hiyo hansard hapa tuone kama hujatoa pongezi kwa PPF. I dare you!

Inaonyesha kama gazeti liliandika half of the story
 
Habari ya kuisifia PPF imetoka Jamboleo. Ni uongo. Its a spin.

Kamati imewakaripia PPF na tumemwagiza CAG achunguze malipo yakiyokwisha fanywa, tumesimamisha malipo ya sasa na tumepiga marufuku double payments ie gratuity na endowment scheme. The citizen wameandika sawa na hata Dailynews wameandika sawa. Maslahi ya JamboLeo ni nini kupotosha habari ya kamati?

Mfumo wa ajira za mikataba kwa mashirika ya umma ni mwanya wa senior staff kujilipa mabilioni ya fedha za Mashirika. CAG ameelekezwa na kamati kukagua mfumo huu kwa mashirika yote ya umma kwa kuanzia na mifuko ya pensheni kisha mashirika makubwa kama TANAPA, TCRA, EWURA nk. Mwaka jana kamati iliagiza TPA kuachana na mfumo huu na vile vile Katibu Mkuu utumishi alitoa waraka kuzuia mfumo wa aina hii.

Endowment scheme ni kwa wafanyakazi wote wa shirika na inakubalika. Gratuity ni ufujaji wa mali na ni marufuku kwa mtu mmoja kufaidika na gratuity na wakati huo huo endowment scheme.

Nitamletea mod hansard ya kikao cha kamati ili wasomaji wa JF waone ukweli wa mjadala na habari ya jambo leo ambayo ni spin ipuuzwe!


Good reaction, Hongera kwa kazi nzuri, hao jamaa wa gazeti la Jamboleo wanastahili kuchukuliwa hatua, hakuna kitu kingine kinachorudisha maendeleo nyuma zaidi ya uwongo. uwongo ni namba 1.

Sasa kaka Mheshimiwa Zitto, mi niulize kidogo, Hiyo mifuko ya hifadhi ya jamii, huwa inajishughulisha na miradi mbalimbali ya kiuchumi, hizo faida zinazopatikana zinakwenda wapi? kwa nini watumishi hawaongezewi kwenye mafao yao?

Kwa nini mifuko hiyo haikopeshe wafanyakazi wanaohusika kuweka mafao yao huko? manake mfuko kama PSPF hukopesha mtumishi aliyefikisha miaka 50 eti ajenge nyumba. kwa nini asikopeshwe akiwa angalau ametumika kazini miaka hata nane (8) ili ajenge kujikwamua na maisha ya kupanga nyumba? Au hata ikopeshe watumishi wanaotaka kujiendeleza ki elimu!?.

Unajua, kuboresha maisha ya wafanyakazi si mpaka miaka hamsini, Mi nadhani kupitia kamati yenu tungeni sheria ipelekwe bungeni ambayo itaruhusu wadau wa Mifuko hiyo kukopa pesa ili ziwasidie kuboresha maisha. Hai-sound kabisa kutokopesha mdau huku anahifadhi pesa zake. After all hiyo mifuko inajihusisha na miradi kibao ya uzalishaji.

TUSAIDIENI NDUGU Maisha NI Magumu MNO.
 
jana wakati tunajadili malipo haya hapa JF niliandika sentensi moja tu kuwa namuamini sana Zito. Baadhi ya watu hawakunielewa. naamini leo baada ya maelezo ya Zito mtanielewa kwa nini nilisema vile.
 
Asante Zito kuja na ufafanuzi. Mimi sichangii zaidi maana nina maslahi kwenye mifuko hiyo upande wa walalamikiwa.:tape::bored:
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom