Kamati ya Dk. Wilbroad Slaa yalamba posho mara mbili
12 May 2009
Na Mwandishi Wetu
MAELEZO yalivowahi kutolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, kwamba wapo baadhi ya wabunge wanaopokea posho mara mbili, yamethibitishwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh.
Ripoti hiyo ya CAG inathibitisha hali hiyo kutokana na ukaguzi wa hesabu za Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, ikidhihirika kuwa malipo yaliyofanywa kupitia vocha ya malipo yenye namba 1/8/066145, yaliyosainiwa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo yalitumika kulipa wabunge posho.
Katika hali ya kawaida, wabunge hulipwa posho na ofisi ya Bunge hususan wanapokuwa katika shughuli za kawaida zinazohusiana na kamati za Bunge.
Katika ukaguzi tulioufanya tuliweza kubaini matumizi yasiyostahili yenye thamani ya Sh 8,472,200 ambayo yasingeweza stahili kulipwa kwa kutumia fedha za miradi ya TASAF, anasema CAG kupitia ripoti yake ya ukaguzi kwa mwaka ulioshia Juni 30, mwaka 2008, ripoti ambayo hata hivyo imekwishawasilishwa bungeni.
Maelezo yaliyotolewa kwa CAG kuhusu malipo hayo yanasema; Posho kwa ajili ya vikao vya kamati ya Bunge ya hesabu za serikali za mitaa Agosti 7 hadi 16 mwaka 2007 yalikuwa Sh 1,050,000.
Kutokana na kubainika kwa hali hiyo huenda hadhi ya wajumbe wa kamati hiyo inayoongozwa na Dk. Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu, ikaingia doa mbele ya umma wa Watanzania.
Aprili 2, mwaka huu, Dk. Hosea aliwaeleza wabunge waliojaribu kuhoji uhalali wake wa kuiongoza TAKUKURU wakati akiwa anakabiliwa na tuhuma za kusafisha kashfa ya zabuni ya mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond, kuwa kama watafanya hivyo basi nao pia wawe tayari kusikia kashfa zao mbele ya umma. Mara baada ya kutoa kitisho hicho kwa wabunge wakati wa semina ya miundombinu ya uadilifu iliyoandaliwa na Takukuru na Chama cha Wabunge wa Afrika (APNAC) na kufanyika kwenye Hoteli ya Whitesands, jijini Dar es salaam, Dk. Hosea alijikuta katika wakati mgumu.
Inakuwaje wakati wa mjadala wa Richmond, wewe mkururugenzi wa Takukuru ulikanusha kuwapo rushwa na uchunguzi wa kamati ya Bunge ulibaini kuwepo rushwa ndani ya kampuni hiyo?
Je ni nani mwenye dhamana ya kukuadhibu wewe na taasisi yako kuhusu rushwa alihoji Mbunge wa Busega, Dk.Raphael Chegeni katika semina hiyo.
Swali hilo halikutegemewa na Dk Hosea na lilionekana kumuudhi na kulazimika kuchukua kipaza sauti na kusitisha maswali na kuanza kujibu kwa ghadhabu.
Hapa siyo jukwaani hivyo tusilete siasa. Nipo hapa kwa ajili ya kufundisha na kama ni suala la Richmond waziri mkuu alishaliongelea na ndiyo mwenye dhamana ya kujibu hilo. Mimi sina jibu kwa hilo na kama mtu hapendi kuvuliwa nguo kwanini umvue mwenzako, alisema Dk Hosea.
Mjadala huu aachiwe Waziri Mkuu Mizengo Pinda na aliyeuliza swali hilo hanitendei haki kwani hakuna hoja nyingine ya maendeleo kwa jamii ambalo inaweza kujadiliwa mbona mnangangania kujibu hilo pekee.
Najua kuna watu wanatumiwa ili niongee halafu nibabaike katika kujibu na nishindwe kufanya kazi yangu. Mbona mnangangania jambo hilo tu wakati kuna hoja nyingine za maendeleo kwa jamii. Kuhusu suala la Richmond sijibu ngo.
Chanzo: Gazeti la Kwanza Jamii
12 May 2009
Na Mwandishi Wetu
MAELEZO yalivowahi kutolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, kwamba wapo baadhi ya wabunge wanaopokea posho mara mbili, yamethibitishwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh.
Ripoti hiyo ya CAG inathibitisha hali hiyo kutokana na ukaguzi wa hesabu za Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, ikidhihirika kuwa malipo yaliyofanywa kupitia vocha ya malipo yenye namba 1/8/066145, yaliyosainiwa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo yalitumika kulipa wabunge posho.
Katika hali ya kawaida, wabunge hulipwa posho na ofisi ya Bunge hususan wanapokuwa katika shughuli za kawaida zinazohusiana na kamati za Bunge.
Katika ukaguzi tulioufanya tuliweza kubaini matumizi yasiyostahili yenye thamani ya Sh 8,472,200 ambayo yasingeweza stahili kulipwa kwa kutumia fedha za miradi ya TASAF, anasema CAG kupitia ripoti yake ya ukaguzi kwa mwaka ulioshia Juni 30, mwaka 2008, ripoti ambayo hata hivyo imekwishawasilishwa bungeni.
Maelezo yaliyotolewa kwa CAG kuhusu malipo hayo yanasema; Posho kwa ajili ya vikao vya kamati ya Bunge ya hesabu za serikali za mitaa Agosti 7 hadi 16 mwaka 2007 yalikuwa Sh 1,050,000.
Kutokana na kubainika kwa hali hiyo huenda hadhi ya wajumbe wa kamati hiyo inayoongozwa na Dk. Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu, ikaingia doa mbele ya umma wa Watanzania.
Aprili 2, mwaka huu, Dk. Hosea aliwaeleza wabunge waliojaribu kuhoji uhalali wake wa kuiongoza TAKUKURU wakati akiwa anakabiliwa na tuhuma za kusafisha kashfa ya zabuni ya mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond, kuwa kama watafanya hivyo basi nao pia wawe tayari kusikia kashfa zao mbele ya umma. Mara baada ya kutoa kitisho hicho kwa wabunge wakati wa semina ya miundombinu ya uadilifu iliyoandaliwa na Takukuru na Chama cha Wabunge wa Afrika (APNAC) na kufanyika kwenye Hoteli ya Whitesands, jijini Dar es salaam, Dk. Hosea alijikuta katika wakati mgumu.
Inakuwaje wakati wa mjadala wa Richmond, wewe mkururugenzi wa Takukuru ulikanusha kuwapo rushwa na uchunguzi wa kamati ya Bunge ulibaini kuwepo rushwa ndani ya kampuni hiyo?
Je ni nani mwenye dhamana ya kukuadhibu wewe na taasisi yako kuhusu rushwa alihoji Mbunge wa Busega, Dk.Raphael Chegeni katika semina hiyo.
Swali hilo halikutegemewa na Dk Hosea na lilionekana kumuudhi na kulazimika kuchukua kipaza sauti na kusitisha maswali na kuanza kujibu kwa ghadhabu.
Hapa siyo jukwaani hivyo tusilete siasa. Nipo hapa kwa ajili ya kufundisha na kama ni suala la Richmond waziri mkuu alishaliongelea na ndiyo mwenye dhamana ya kujibu hilo. Mimi sina jibu kwa hilo na kama mtu hapendi kuvuliwa nguo kwanini umvue mwenzako, alisema Dk Hosea.
Mjadala huu aachiwe Waziri Mkuu Mizengo Pinda na aliyeuliza swali hilo hanitendei haki kwani hakuna hoja nyingine ya maendeleo kwa jamii ambalo inaweza kujadiliwa mbona mnangangania kujibu hilo pekee.
Najua kuna watu wanatumiwa ili niongee halafu nibabaike katika kujibu na nishindwe kufanya kazi yangu. Mbona mnangangania jambo hilo tu wakati kuna hoja nyingine za maendeleo kwa jamii. Kuhusu suala la Richmond sijibu ngo.
Chanzo: Gazeti la Kwanza Jamii