Kamati Teule ya Richmond ilitumia sh 400 milioni?!!

Nafikiri tuendako tunahitaji Zero tolerance. Kuna mafisadi na vifisadi.

Ukimchunguza saana Mwakyembe utagundua kuwa kama angelipata nafasi nzuri, mhhhh.........

Kwa habari ambazo mie nimeshazisikia tayari ambazo mwakani zitaanikwa hadharani wakati wa uchaguzi, jamaa si mzuri kiasi hicho.

Hivi kwa nini asingelikuwa ni MFANO WA KUIGWA kama alivyo Dr. Slaa? Kwani anashindwa nini kuwa msafi na hasa ukichukulia alisoma sheria? Kuna vitu anajiingiza kichwa kichwa hadi unamhurumia. Wengi wanamkubali Mwakyembe kwa uwezo wake mkubwa na kama asingelikuwa na papara na akawa ametulia, sasa hivi angelikuwa kashamziba hata Dr. Slaa na nafikiri ndani ya CCM angelikuwa tishio kubwa sana na siyo sasa kila siku yuko busy kujibu mapigo. Mara huku umeme wa upepo, mara kateka watu, mara kagombanisha watu mara kagombana na mkuu wa Mkoa, mara kagombana na madiwani mara kaficha data za bunge..... Mara moja, mbili sawa ila sasa inakuwa too much hadi mtu unaanza kuamini kuwa huyu na yeye mhhhhhhh......

Ila nashindwa kufahamu kuwa hawa watu wa tume, walichaguliwa wale ambao pia wana makosa? Maana wao inakuwa rahisi sana kuwatisha (tishia ya Hosea) kuwa "mkinitenda, ntakutendeni...." Alipomparamia RA, alipigwa kishock cha umeme kidogo tu, akawa akilalamika kila sehemu. Ukweli ukabaki wazi kuwa alitumia data alizozipata kwenye utafiti na yeye akataka kuanzisha kampuni ya kuzaa umeme wa upepo ili na yeye afyonze. Mtu mwenye mapenzi ya nchi yake, lazima angelifahamu kuwa swala la energy, inabidi libaki mikononi mwa nchi milele na hasa kwa nchi masikini.

Mkuu hacha kupotosha watu...unajua wanaohusika IPTL, Songas, Kiwira, Richmond, Artumas, Na project ambazo zimekwama kama Wind-Eetc etc. Unajua ma director wa Tanesco vizuri na nani wanahakikisha watu wao wanawekwa? Issue ya Umeme haipo mikononi mwa wananchi...power pool ya mwakyembe ni briefcase company ambayo hata tender haijapata kokote, it was an idea in its early stages unacompare na Richmond?? Acha kupotosha jamii.
 
Mkuu,

Nakiri ni kubwa kwa kulinganisha na hali ya maisha ya mtanzania. Lakini mkuu unajua JK anatumia kiasi gani kwa mavazi tu kila mwezi? Uliza uambiwe, unaweza kuibamiza pc yako hivihivi!

Unakumbuka ofisi ya Waziri Mkuu ilikuwa imetengewa kiasi gani kwa ajili ya fenicha tu? Bajeti hiyo ni ya kila mwaka kumbuka...

Hii ya kina Mwakyembe as long as ilionesha outcome kwenye public bado naweza kusema ni afadhali. Tena, mwanzisha hoja anasema walipewa Mil 400, ana uthibitisho kuwa hakuna masalia ya kiasi chochote? Manake tusiangalie upande mmoja wa kupewa bila kuangalia marejesho.

Natambua kuwepo kwa mpango wa kuhakikisha 'kina Mwakyembe' wanashindwa kwa gharama zozote, udhaifu wao kupokea posho ambazo hawakujua zingewageukia ndo unawagharimu kwa sasa!

Am not 'pro Mwakyembe' and at the same time am not 'pro Lowassa'!

Invisible,

Ni kweli huko juu wanakula kama hawana akili nzuri hivi na wabaya zaidi ni hawa Wapambe. Nilishaangalia film ya ile sherehe ya Swaziland ambapo mfalme huchagua mke. Unakuta jamaa wanavyompa maneno ya kumpandisha mori mfalme ili ajichagulie kigoli utafikiri si watoto wa watu. Hawa Wapambe nao nafikiri huwa lao hilohilo..... Mzee, achana na Gucci, hapo kuna BOSS. Utavaaje suti ya 3 digitals???

Mie na imani yangu yote, ninaamini kuwa kama BUNGE likisafishwa, basi na wao watamsafisha RAIS. Kuhangaika na Rais kwa sasa ni kupoteza muda. Siku zote atakuambia "sijavunja sheria na bajeti wamenipangia wabunge". Sasa ili kukata MIZIZI, ni kulivaa BUNGE. Hapa itakuwa ni kama ile story ya ... "...ng'ombe akanywa maji, maji yakazima moto, moto ukaunguza fimbo na fimbo akamchapa KALUMEKENGE. Na Kalumekenge akaenda SHULE.
 
Mkumbo, usiingie mkumbo please. Ni kweli kamati ilitumia 438m tshs kwa kazi ile. Lakini sio kweli kuwa kazi ile haikuwa na tija. Kuna makosa fulani fulani ikiwemo kutomhoji Lowasa ambayo itatugharimu sana siku si chache zijazo, lakini ukipima mapungufu hayo na faida unaona kamati ile ilifanya kazi. 438m tshs hazimalizi mgawo na haina maana walipewa kina Mwakyembe mfukoni - kuna nauli za safari humo nk.
Tutafanya dhambi kubwa sana iwapo tutaingia mtego wa kuona kazi yote ile haina thamani. Kazi iliyoangusha serikali nzima? Jamani!

Hata hivyo, ni vema Kamati itwambie bila kumung'unya maneno na kwa vielelezo RICHMOND ni nani? Nilishtuka juzi Dkt. Mwakyembe alilitaka gazeti la Mtanzania litwambie Richmond ni nani. Hapana. Kamati ndiyo ilipaswa itwambie maana tuliwalipa watwambie hivyo na sio magazeti. Mnakumbuka Lowasa alisema alipokuwa anajiuzulu 'put it on the table, who is Richmond'

Pili, kuna suala la gharama za Richmond ambapo tunaamini kuwa gharama za mradi ule ni 172m usd. Hii imerudiwa kweli kweli. Serikali ilisema Richmond hawakuchukua hata senti tano. Sisi kwenye Kamati ya Mashirika ya Umma tulipopitia hesabu za TANESCO zinazoishia Disemba 2008 tulikuta kuwa RICHMOND/DOWANS walilipwa advance ya 30m usd kwa makubaliano ya kuzilipa kutokana na makati ya umeme watakaouza. Walipoanza kuuza umeme wakaanza kukatwa na mpaka tulipovunja mkataba ule na DOWANS zilibaki 8m usd hazijalipwa.

Wiki ijayo ni lazima tuelezwe tunapataje pesa hizi maana dowans tumeshavunja mkataba kabla ya kumaliza deni letu (pamoja na deni la 4m usd kama faini ya kuchelewa kuzalisha umeme). Hizi 12m usd tunazipataje. Haya ndio mambo ya msingi sana kwangu katika mjadala huu wa wiki ijayo.

Gharama zilizotumika na kamati kufanya uchunguzi zina value for money. Zoezi lile pamoja na mapungufu hayo madogo ya juu limeleta nidhamu serikalini sana. Tusibeze kazi ile jamani.

kula tano Mheshimiwa...........
 
Zitto,

..hebu acha kutuchezea wewe.

..mbona Mwanakijiji na wenzake wameleta ripoti yao hapa ulisikia wametumia 400 milion.

..posho za 100,000 per day kwa wajumbe wa hizi Tume unaona ni halali kwa mazingira ya Tanzania?

..usije ukakuta labor cost za Tume ya Mwakyembe ni kubwa kuliko labor cost za Richmond au Dowans.
 
Mkuu hacha kupotosha watu...unajua wanaohusika IPTL, Songas, Kiwira, Richmond, Artumas, Na project ambazo zimekwama kama Wind-Eetc etc. Unajua ma director wa Tanesco vizuri na nani wanahakikisha watu wao wanawekwa? Issue ya Umeme haipo mikononi mwa wananchi...power pool ya mwakyembe ni briefcase company ambayo hata tender haijapata kokote, it was an idea in its early stages unacompare na Richmond?? Acha kupotosha jamii.

Mkuu Kapinga,

Nafahamu wanaohusika na hizo kampuni zote za kuzalisha umeme. Ni viongozi waliopo madarakani na wale waliokuwepo madarakani wa taifa letu la Tanzania. Nafahamu Mkurugenzi wa Tanesco ni mtu anayelalamikiwa kuwa alihusika kwenye scandal ya rada ya ndege. Anayehakikisha wanawekwa hapo kwa maelezo ya Mwanakijiji na King maker. Nafahamu pia kuwa issue ya umeme haipo mikononi wa wananchi. Na ndicho nimekiandika. Mwakyembe na yeye alitaka kuanzisha kampuni yake na sidhani kama ingelitofautiana saana na hizo nyingine. Sasa hapa ninachopotosha ni nini? Wee naona unadandia TGV kwa mbele........ Ile kuwa na WAZO tu la kufungua kampuni sawa na zile zinazoifilisi Tanzania, ni mwanzo wa ufisadi. Kwani hata akina Richmonduli na Dowans na wao si wako kwenye mikoba tu? Hadi leo unaambiwa HAWAJULIKANI. Sasa tofauti yao na Mwakyembe ni moja, mmoja alifanikiwa akaanzisha na mwingine alikuwa mbioni kuanzisha. Ninaamini kama Mwakyembe angelipewa U-PM au Urais huko mbele ya siku, angelipindisha na yeye kila mstari ili kampuni yake izalishe umeme.

Kwa mtu anayependa Tanzania, basi lazima afahamu kuwa Maswala yote ya ENERY, Ulinzi na Usalama, Usafiri mijini, Maji (safi na Taka) na RELI, haya inabidi yabaki mikononi mwa Nchi. Hapo ndipo uchumi wa nchi unaanzia. Hebu ona leo watu wanavyomaliza masaa kadhaa pale Dar kwa ajili ya foleni za magari........ Ona bidhaa ngapi zinaharibika kwa sababu hamna umeme. Uzalishaji unakwama kwa sababu hamna umeme. Kama ingelikuwa imeandikwa wazi kuwa "Umeme ni swala la nchi na hamna umeme wa watu binafsi....." basi TANESCO wangeliachwa wajiendeshe wenyewe na sidhani kama Idris angelipelekwa huko maana ulaji ungelikuwa haba. Huu uzalishaji umeme wa watu binafsi ndiyo umetufikisha hapa. Kila siku watu wanaota kuihujumu TANESCO ili wao wachukue uzalishaji. Wakijua hamna uzalishaji na nyumba zao pia wanapata GIZA, basi watakuja juu sana na umeme utarudi.

By the way: Hivi hizo QUEs za magari pale Dar, Wabunge, mawaziri, makatibu wakuu nk haziwasumbui nyie? Loooo......!!!!!!
 
Wasomi wanasema milioni hizo 400 zingeweza kununua genereta na wananchi wasingeendelea kuwa gizani leo. Kwa uzembe wa kamati hiyo, wananchi wako gizani kwa kutokuwa na umeme leo, ...

Hao wasomi ni wa political science nini? Nadhani hukuwaelewa labda walikuwa na maana ya jenereta la Chuo!

Mi naomba Mungu tuwe na sheria kama za China, mtu akiwa implicated na rushwa au ufisadi ni shaba/jela au kitanzi tu. Huku kuleta post za namna hii, kuanzisha magazeti ya kujitetea nje ya bunge (wakati walikuwa na nafasi kujitetea bungeni) ni kutupotezea muda.

Hawa jamaa tungekuwa at least tumewaweka jela siku nyingi sasa hivi tungekuwa tunaongelea KILIMO KWANZA. Kwa kusikiliza/kujadili utetezi wao usioisha tunapoteza muda sana.

Nawasilisha!
 
mimi na sema kama ufisadi wote uliofanyika hela hazijawatosha hao mafisadi, basi serikali ya ccm watupe hesabu kamili ya hela wanazotegemea kuvuna kutoka nchi yetu hili tuwalipe na wao waturudishie nchi yetu tuanze upya kuliko kuendelea kutafunwa kwa njia ya sasa.we need to vote them out,we hired them and we can fire them.
 
....... Unapomnyooshea mwenzako kidole kimoja angalia vidole vingapi vinakuelekea wewe! Dkt Hoseah kwa kutumia Sheria ya mwaka 1971 hakuweza kubaini rushwa kwenye mkataba wa Richmond, sasa kama kamati ya Mwakyembe iligundua rushwa si ingepeleka kesi mahakamani?

Wakuu tuwe waangalifu tunapojadili haya mambo.......tuwe open minded.............msitake kuwatishia watu wasiseme yale wanayotakiwa kusema eti wakumbuke kuwa nao wana/tanyooshewa vidole.........

Haikuwa kazi ya tume ya Mwakyembe kupeleka Kesi mahakamani.......sehemu kubwa ya kazi ya tume ya Mwakyembe iliishia pale walipotoa ripoti yao bungeni.........

......ni lazima tutambue mapambano haya si lele mama Mafisadi nao wamejiandaa vilivyo.............

.......Mapambano ya Rushwa wakati mwingine ni very tricky...........kwa kifupi Dkt Hosea alichemsha........ukitaka kujua ukweli wa suala la Richmond na TAKUKURU fuatilia kwa karibu TAKUKURU............

........BOUNCING BACK?
 
Mkuu,

Nakiri ni kubwa kwa kulinganisha na hali ya maisha ya mtanzania. Lakini mkuu unajua JK anatumia kiasi gani kwa mavazi tu kila mwezi? Uliza uambiwe, unaweza kuibamiza pc yako hivihivi!
Nasikia analetewa suti 30 kila mwezi zilizoshoneshwa nje na yule tajiri wa Kempiski.
 
Zitto,

Mie nafikiri mngelianzisha kama "kampeni kujisafisha". Wabunge wote wa CHADEMA na wengine wa upinzani na hata baadhi wa CCM watakaokuwa willing kurudisha POSHO hizo walizochukua mara mbili, basi na mfanye hivyo mbele ya Waandishi wa habari. Hata kama nyuma yenu hakutakuwa na neno CHADEMA, ila ujumbe utafika kuwa nani walikuwa waanzilishi wa hii kampeni.

Mwisho niseme, kwa hili naungana na wengine kwa kuwapa TANO CHADEMA.
 
Mil.400 ilikuwa siku ngapi na walienda walisafiri wapi na wapi ...duh..Mwakyembe lol. walewaleeeee kina mengi, Mosha, Simba, na NICOL..wasomi watamaliza nchi hii sisi tunaolipa kodi..to technorat..wanatumaliza sisi a big shame?
Wajenge barabara hapa kinondoni...hivi huo uchunguzi umesaidia Tsh..ngapi?? au umeokoa tsh...? kuibwa au kuibiwa?
 
Nasikia analetewa suti 30 kila mwezi zilizoshoneshwa nje na yule tajiri wa Kempiski.
Jasus, correct me 30 suits a month or 3 suits a month? When will he wear all those suits? 360 per annum, 1800 suits in five years?
 
..hizi ni gharama za kununua madawati zaidi ya 30,000.

..ni gharama za kulipa waalimu zaidi ya 2500.

..ni gharama za kuwalipa wahadhiri wa chuo kikuu zaidi ya 200.

..binafsi nafikiri hizi Tume za Uchunguzi za Bunge au Raisi zinaweza kufanya kazi kwa gharama za chini zaidi.
 
Jasus, correct me 30 suits a month or 3 suits a month? When will he wear all those suits? 360 per annum, 1800 suits in five years?
Hata mimi niliuliza hivyo hivyo. Mzigo huletwa pale Kempiski kila mwezi. Labda nyingine za watoto na ndugu zake, sijui.
 
..hizi ni gharama za kununua madawati zaidi ya 30,000.

..ni gharama za kulipa waalimu zaidi ya 2500.

..ni gharama za kuwalipa wahadhiri wa chuo kikuu zaidi ya 200.

..binafsi nafikiri hizi Tume za Uchunguzi za Bunge au Raisi zinaweza kufanya kazi kwa gharama za chini zaidi.
Joka Kuu,
Unajua masikini ni mtu ambaye hajijui kama yeye ni masikini. Masikini ana sifa ya kufuja na kutojua thamani ya fedha Zitto anajua kabisa hizo pesa siyo ndogo. I have lost my trust in all these creatures called members of Parliament. Zitto now is a super rich in Tanzania standard and this Parliament made him rich so what do you expect from him? ZS400,000,000.00

=

USD302,571.861
 
Lakini mkuu milioni 400 ni lundo la hela, kwa kazi gani hasa walioifanya? Wakati mwingine hawa vinara wetu wa vita dhidi ya ufisadi wanajipiga bao mwenyewe. Milioni 400, posho mbilmbili, ebo!

Alishatuasa Katibu Mkuu wetu Dk Slaa kuwa hii vita dhidi ya ufisadi inahitaji sifa moja kubwa, nayo ni: unyoofu. Sasa hawa wenzetu kila siku wanapoteza sifa za kuwa majemadari wa vita hii. Tutayajua mengi huko tuendako!
si ungeomba breakdown toka kwa mtoa hoja, ili uyaone hayo mabaya ya mwakyembe na kundi lake, ama sivyo hii ina itwa sweeping statement inachukua uchafu na usafi humo humo. kwa yule asiye na uwezo wa kupambanua usafi na uchafu ataliona hili jambo lote ni uchafu, hivyo tunakuwa hatuwatendei haki wananchi wa tanzania hususani wasioweza kupambanua jambo.
 
- Shillingi Millioni 400, the results Waziri Mkuu amejiuzulu, mawaziri wawili wametoka naye, malipo ya dola 154,000 kwa mwezi kwa Richimonduli yakasimamishwa, Rostam akaanza kuuza makampuni yake ya kifisadi na kujificha ficha, kwa mara ya kwanza taifa zima tukagundua kuwa kumbe tuna kundi la Mafisadi, na wao officially na kwa mara ya kwanza wakaanza ku-operate wazi wazi bila kujificha na wote sasa tunawajua, Ika m-cost Lowassa umakamu wa CCM, na kumkosesha kabisa kiu yake ya urais, eti it was not worthy?

- Mnasema ilikuwa sawa Shillingi Millioni 100 kutumika na kesi ya Malima VS Mengi? Kamati ya kurekebisha Muungano ilitumia hela ngapi na matokeo ni nini? Kamati ya kina Mwema ilitumia hela ngapi na matokeo yalikuwa ni nini? Kamati ya Bomani ilitumia ngapi na matokeo yalikuwa ni nini hasa? Kamati ya Warioba ilitumia hela ngapi na matokeo yako wapi jamani?

- Tunazidi kuliua taifa tunapojaribu kuingiza siasa kwenye kila ishu hata zisizohusika, sasa mnasema nini bila ya kutumia hizo Shillingi Millioni 400, tungeishia kuwalipa hela ngapi hawa kina Lowassa, Rostam na Richimonduli? Hawa mafisadi sasa wanatapa tapa baada ya NEC na Sitta, walifikiri nini kwamba wana nguvu sana kwa sababu wana hela zetu walizotuibia?

- Hivi ni lini tutaambiwa hasa madhambi ya kweli ya Mwakyembe kiuongozi na kisiasa badala ya hizi ngonjera zisizokwisha na batili? Mbona hawakupata tabu kummaliza Mtikila, ushahidi ulikuwa wazi na mweupe, sasa Mwakyembe mbona anawasumbua sana na ushahidi wa kweli kuhusu madhambi yake?

Respect.


FMEs!
 
Back
Top Bottom