Kamati Teule ya Bunge kumchunguza Jairo imetumia kiasi gani?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Kamati hii teule ilikuwa na wajumbe 5 ambao ni:

(i) Mhe. Eng. Ramo Matala Makani, (Mb.) - Mwenyekiti
(ii) Mhe. Martha Jachi Umbulla, (Mb.)
(iii) Mhe. Gosbert Begumisa Blandes, (Mb.)
(iv) Mhe. Mch. Israel Yohana Natse, (Mb.)
(v) Mhe. Khalifa Suleiman Khalifa, (Mb.)

Kamati hii ilikuwa na wajumbe wa Sekretariati wafuatao (kimsingi watendaji wa kamati)

Ndugu Nenelwa Mwihambi-Wankanga
(ii) Ndugu Lukago Alphonce Madulu
(iii) Ndugu Asia Paul Minja
(iv) Ndugu Mswige Dickson Bisile

Kamati hii teule ilipewa muda usiozidi wiki nane (kuanza kazi Sept 5, 2011). Na Kamati hii iliweza kufanya mahojiano na watu wapatao 146 ambao aidha walilazimika kwenda kwenye kamati hiyo au kamati ilikutana nao. Ili kuweza kufanikisha shughuli zake za uchuanguzi wa mambo haya bila ya shaka kamati iliingia gharama mbalimbali. Binafsi ningependa sana kujua kama kiasi kilichotumika kimeendana na huduma ambayo tumeipata kama taifa (value for money). Hasa ni muhimu kujua kama watendaji wote watachukuliwa hatua za kawaida za kinidhamu au kutochukuliwa hatua kabisa na kupewa maonyo tu.

Kwa sababu kama mwisho wa siku hakuna atayeondolewa au hata kufikishwa mahakamani (kustaafu ukiwa na mafao yako siyo adhabu) basi Watanzania watakuwa wamepoteza mara mbili.

a. Wamepoteza kwenye fedha ambazo zinadaiwa kuchotwa kiaina kufuatia agizo la Jairo
b. Wamepoteza mara mbili kwenye fedha za posho na gharama nyingine ambazo Kamati Teule imeingia - hivi wabunge wanapokaa kwenye vikao vya kamati teule wanalipwa posho ya kiasi gani au wanafanya bure?

Tusipoangalia kama taifa tutakuwa tumechezeshwa mchezo wa "chekundu cheusi" a.k.a kuingizwa mjini yaani tumeliwa double hadi "king"!
 
kuwa kwenye kamati ni dili ila kama hukosan na madam speaker mana ukiwa unamkera na mambo yako ya miongozo na kumwambia anacheza badala ya kua refa umeumia mpapa unamaliza mda wako hutawahi kua mwanakamati wa kamati yeyote ile na ndo nchi inavyoeendeshwa unakula kwa urefu wa kamba yako
 
Mzee Mwanakijiji kuna c. umesahau, kuna vijisenti vilitumika wakati wa ukaguzi maalumu wa CAG aliyempa taarifa Katibu Mkuu kiongozi na ikasemekana DJ hana kosa la kinidhamu. Boresha kidogo ili tuwe na vijigharama zaidi. Ntarudi.
 
fine, ni vyema kupima 'value for money' kila unapoamua kufanya jambo lolote husussani kama linatumia hela 'nyingi'. Japo gharama, hata kama nyingi, haiwezi kuwa kigezo peke yake cha kuamua kufanya au kutofanya jambo fulani, zipo sababu nyingine muhimu, ambazo zinapaswa kuzingatiwa.

kuhusu haya masuala ya uchunguzi unaohusiana na matumizi ya fedha, umuhimu wake hauzingatii tu gharama inayotumika kuendesha uchunguzi, bali kubaini kuthibitisha kuwa hakuna ubadhilifu, na pale wanaposhindwa, kinyume chake ndiyo huwa matokeo ya nuchunguzi.

kwa nini ni muhimu kufanya hivi, hata ikigundulika hakuna fedha zilizofujwa? Ni kwa ajiri ya kuwahabarisha wale walio katika hatari ya kutumia vibaya madaraka kufuja mali za umma, wajue kwamba hata ikiwa ni fedha kidogo namna gani zilizofujwa ipo siku watafuatiliwa, kwa maana hiyo uchunguzi kama huu unaweza kuokoa fedha nyingi sana kwa kuzuia ubadhilifu wa hapo baadaye. Hii ni moja tu ya sababu mhimu

Kuhusu kuchukuliwa au kutochukuliwa hatua wahusika, hiyo tusiitwike kamati wala bunge, wao pamoja na matatatizo yao mengine wamefanya kazi yao.. kwa hakika wangekuwa na uwezo huo, wangeshachukua hatua hata bila ya kuunda kamati hiyo, maana suala lenyewe lilikuwa wazi mno.

Serikali na CCM wasipochukua hatua, hiyo nayo ni muhimu maana waliokuwa hawajui kwamba hatua hazichukuliwi hata kwa mambo yaliyowazi watapata nafasi ya kubaini hilo
 
Kamati hii teule ilikuwa na wajumbe 5 ambao ni:

(i) Mhe. Eng. Ramo Matala Makani, (Mb.) - Mwenyekiti
(ii) Mhe. Martha Jachi Umbulla, (Mb.)
(iii) Mhe. Gosbert Begumisa Blandes, (Mb.)
(iv) Mhe. Mch. Israel Yohana Natse, (Mb.)
(v) Mhe. Khalifa Suleiman Khalifa, (Mb.)

Kamati hii ilikuwa na wajumbe wa Sekretariati wafuatao (kimsingi watendaji wa kamati)

Ndugu Nenelwa Mwihambi-Wankanga
(ii) Ndugu Lukago Alphonce Madulu
(iii) Ndugu Asia Paul Minja
(iv) Ndugu Mswige Dickson Bisile

Kamati hii teule ilipewa muda usiozidi wiki nane (kuanza kazi Sept 5, 2011). Na Kamati hii iliweza kufanya mahojiano na watu wapatao 146 ambao aidha walilazimika kwenda kwenye kamati hiyo au kamati ilikutana nao. Ili kuweza kufanikisha shughuli zake za uchuanguzi wa mambo haya bila ya shaka kamati iliingia gharama mbalimbali. Binafsi ningependa sana kujua kama kiasi kilichotumika kimeendana na huduma ambayo tumeipata kama taifa (value for money). Hasa ni muhimu kujua kama watendaji wote watachukuliwa hatua za kawaida za kinidhamu au kutochukuliwa hatua kabisa na kupewa maonyo tu.

Kwa sababu kama mwisho wa siku hakuna atayeondolewa au hata kufikishwa mahakamani (kustaafu ukiwa na mafao yako siyo adhabu) basi Watanzania watakuwa wamepoteza mara mbili.

a. Wamepoteza kwenye fedha ambazo zinadaiwa kuchotwa kiaina kufuatia agizo la Jairo
b. Wamepoteza mara mbili kwenye fedha za posho na gharama nyingine ambazo Kamati Teule imeingia - hivi wabunge wanapokaa kwenye vikao vya kamati teule wanalipwa posho ya kiasi gani au wanafanya bure?

Tusipoangalia kama taifa tutakuwa tumechezeshwa mchezo wa "chekundu cheusi" a.k.a kuingizwa mjini yaani tumeliwa double hadi "king"!

This is great thinking!!! Mara nyiongi tumezoea kusubiri baada ya CAG ku-report ndo tunastuka.

MKJJ, kwa mfumo wa system yetu, ambayo imekataa kata kata dhana ya CDM ya kujiangalia upya na kupunguza matumizi hasa maposha yasiyo kuwa ya lazima. Nina uhakika wametumia hela nyingi.

Kwa kweli kama serikali haitakuwa tayari kuondoa matumizi yasiyo ya lazima katika mfumo wake, haya yataendelea kuwa ngojera. Nimecheka sana leo, nimesoma habari kuwa Waziri wa fedha Bw. Mkulo, amewabwatukia wahisani walioahidi kuchangia GBS kuwa rate ya kuwasilisha michango yao ni ndogo sana maana ndo kwanza wametoa around 7% wakati kwa sasa ilipaswa kuwa wamekwisha changia about 97% katika quoter hii!!!

Nikawaza, hivi serikali pamoja na matusi ya kina kamerun bado tu, hatuwa revise tukusanye kutoka ndani na kuangalia servings kutoka katika kubana matumizi yetu!!!!
 
Nakubaliana kabisa na MMK.

Sifahamu vizuri sheria zinazosimamia mamlaka ya viongozi wa umma, lakin nafikiri hawa jamaa ambao wamekuwa implicated kwenye matumizi mabovu ya kodi ya wananchi wangetakiwa kufikishwa mahakamani - kwa kupokea fedha ambayo wanajua kimsingi hawastahili au haiendani na taratibu za usimamizi wa fadha ya umma - HILI NI WAZO LANGU, SIJUI SHERIA INASEMAJE.

Lakini kwa upande mwingine MMK, tukio zima linaweza kuwa na impact katika wakati ujao kwa msingi kuwa watendaji sasa watakua makini juu ya matumizi mbalimbali ya ofisi walizopewa kusimamia. Kwa kweli hawa viongozi wetu wamepata fedheha kubwa sana hata mbele ya familia zao - wewe Ngeleja, ana shiida gani ya kumfanya achukue mil 4 atie mfukoni huku Watanzani zaidi ya milioni 40 wanakufa kwa maradhi, hawana maji safi na salama, hakuna umeme, hali ya maisha dni na mbaya ....? ni akili kweli waweza hata kumsimulia mwanao kwanini alichukua kiasi hiko cha pesa?

Lakini pia mfumo wa utendaji wa serikali hii unaonekana kuwa dhaifu, uliokosa ubunifu, usiokuwa na usimamizi, uliokosa uadilifu, umejaa ubinafsi,..... na ambao uwezo wake wa kufanya maamuzi unatia shaka sana.

Wiki sasa inakwisha, maamuzi yalishafanywa, kwanini wanasita kuchukua hatua?

Huwa najiuiza sana swali hili, "WHO CARES?"Kwa Tanzania nashindwa hata kupata jibu. Nobody cares for anything. tupo kama miti unaosubiri ndege waje kutua,wapate pumziko lao, hewa safi, then wanajisaidia wanaondoka zao.

Nimesoma heading moja na Raia Mwema this week yasema 'Wameshindwa kazi, wanategemea tume"

THEN WHAT?

Huu ujinga unaanzia pale dodoma kwa kuwa na wabunge wengi wa ccm ambao kila jambo ni makofi tu. Nani atamuuliza mtendaji mkuu wa serikali pale bungeni kuwa maazimio ya richmond yameishia wapi? EPA? (zaidi ya watuhumiwa kuhamishwa idara)
.

TUSUBIRI
 
Mkuu ulichozungumza ni jambo la msingi sana. Tulipofikishwa na CCM hadi sasa ni pabaya. Rushwa,uroho wa madaraka,wizi wa rasilimali ya taifa,wigo uliopo kati ya wenye nacho na wasionacho unazidi kuongezeka. Masikini anazidi kunyang'anywa kidogo alicho nacho.
Kama alivyowahi kusema baba wa taifa rip kuwa rushwa/ufisadi ikikomaa serikali iyopo madarakani haitoweza kulikabili tatizo hilo zaidi ya kuliacha lijitatue lenyewe sababu hakuna mwenye ubavu wa kukabiliana nalo. Huko ndiko tunakoelekea na tukifika huko rasmi tumekwisha.
Tusitegemee jipya katika utekelezaji wa maamuzi ya kamati teule,viongozi wetu wa juu hakika wamezidiwa vibaya,hawana maamuzi yoyote magumu wanayoweza kuyatoa kwa sasa zaidi ya kuyaacha yajitatue yenyewe na kwa namna watz tulivyopitiwa na pepo mbaya tutayasahau yote.
 
Mkuu MMJ,
Umenena vema. Value ya kamati ina maana kubwa sana katika kupelekea matokeo mazuri ya mapendekezo yaliyotolewa. Tuambiwe ni shs ngapi?
Pili,hata kama mapendekezo hayatatokea kama ilivyopangwa bado kama mchangiaji mmoja alivyosema awali, watendaji aidha watapunguza (si kuacha) au wataendelea kula ila kwa kuficha sana.
All in all, mi pia nimekuwa nasubiri sana watu wapelekwe mahakamani. Ila si jambo dogo, maana wa kushughulikia mapendekezo hayo naye ni mtuhumiwa, Rais atashauriwa na nani? Ametukosea sana.
Nina imani, jambo hilo litatokea. Na ndiyo itakuwa zawadi ya uhuru wa miaka 50.
 
Nimewahi kusikia habari ya taasisi moja ya Kimarekani iliyokuwa imeunda jopo la wataalamu kufanya utafiti wa jinsi gani Wamarekani wangeweza kupunguza matumizi ya chumvi ya mezani wakati wa kula. Jopo hilo lilituia karibu dola milioni 1.5. Walikuja na ripoti ndeefu sana ambapo walipofikia hitimisho wake huwezi kuamini.

1. Kupunguza matundu ya salt shaker!
 
Bunge lilituhumu, likachunguza, likashtaki kisha likatoa hukumu. Vyombo vingine kama mahakama na dola havina la kufanya ili kuepuka kuingilia mhimili huu?

Mimi nadhani Bunge lilijivika majukumu mengine ambayo siyo ya kwake. Mwisho wangependekeza vyombo kama TAKUKURU na Polisi vifanye uchunguzi,na kupeleka mashitaka Mahakamani. Mahakama ndiyo itatwambia hawa ni wahalifu ama la. Nasema hivyo kutoka katika mfano wa Kamati ya Bunge iliyochunguza Kampuni ya Richmond ambayo kadri siku zinavyosogea tunapata habari mpya,na inatuonyesha kwamba kuna habari muhimu zilifichwa kwa manufaa ya baadhi ya viongozi huku wengine wakisulubishwa kwa makosa ya kutungwa na chuki.
 
kwa upande wangu mi naona hata kama kamati ingetumia bilioni moja bado value for money ingekuwa imezingatiwa kwa sababu
  1. Report iliyotolewa na kamati inazuia matumizi mabaya ya fedha umma nyingi kuliko walizo tumia; namaanisha ofisi nyingi ambazo zilikuwa na tabia za kijairo zimeotishwa na hivyo aidha kama walikuwa na tabia za kijairo wataacha au kama walikuwa wanampango wa kuanza wataogopa wataogopa; mfano mimi ni mtumishi wa umma baada ya kutoka ile report ya kamati meneja wa mamlaka ambapo mimi nafanya kazi alituita na kutupa nakala ya report na kutuambia tuipitie halafu tuonane baada ya kuisoma; tulipoonana alituambia katika malipo anayoidhinisha anaamini hakuna ufisadi na hivyo asingependa siku moja tufikie hatua ya kuundiwa tume. haya pia ni matokeo ya report ya kamati ambayo yametumia kiasi kile kile kilichotumika lakini watu wengi hawayajui. na naamini yamefanyika katika maofisi mengi.
 
Bunge lilituhumu, likachunguza, likashtaki kisha likatoa hukumu. Vyombo vingine kama mahakama na dola havina la kufanya ili kuepuka kuingilia mhimili huu?

Mkjj hizo pesa zimepotea bure, ni ufisadi unaoendelezwa na Bunge. hivi unakumbuka ile kamati ya kuwapatanisha Mengi na nani vile. na nyingine nyingi. ni njia ya wabunge kuishi. mimi sioni tofauti ya matumizi mabaya ya wabunge VS yale ya JAIRO infact hata hizo semina zinazoongelewa ni wabunge waliofaidi. wabunge waliohongwa hawathubutu kusema chochote maana wanajua kitakachowapata.

hapa panachanganya sana mwenye kutoa hukumu kisheria ni nani? hata mimi nilidhani wangetafuta ushahidi kisha wawapelekee wahusika ili jamaa wafunguliwe mashtaka. hii kusema jamaa wanamakosa na pia wafukuzwe kazi inaleta utata sana kwani ni kama tu ile ya RICHMOND ambayo mpaka sasa utekelezaji wake unakuwa mgumu.

kwa sheria za TZ hili swala ni la polisi + TAKUKURU na mwendesha mashtaka wa serikali ili wakiona kuna kesi waipeleke mahakamani
 
Mimi nadhani Bunge lilijivika majukumu mengine ambayo siyo ya kwake. Mwisho wangependekeza vyombo kama TAKUKURU na Polisi vifanye uchunguzi,na kupeleka mashitaka Mahakamani. Mahakama ndiyo itatwambia hawa ni wahalifu ama la. Nasema hivyo kutoka katika mfano wa Kamati ya Bunge iliyochunguza Kampuni ya Richmond ambayo kadri siku zinavyosogea tunapata habari mpya,na inatuonyesha kwamba kuna habari muhimu zilifichwa kwa manufaa ya baadhi ya viongozi huku wengine wakisulubishwa kwa makosa ya kutungwa na chuki.
Ngoja niulize kizushi:
NEC ya CCM na BUNGE la JMT ni mapacha "identical" au "fraternal" ? Maamuzi yao, mijadala yao, inafanana sana hata katika masuala mazito ya kitaifa yanayogusa maslahi yetu sote!
 
mambo ya pesa bado ni siri kubwa Tanzania! Vitu kama hivi vinahitaji kuwekwa wazi. Hii ndio mianya ya panya wengi tuliojaza ghala!
 
Halafu kwenye ripoti kwa nini hawaweki gharama zilizotumika? Kwa mfano watuandikie:-

Mheshimiwa Spika,
Katika kuandaa ripoti hii tume imetumia gharama/jumla ya pesa taslimu Tshs.... kwa mchanganuo ufuatao:-
  • Posho Tshs....
  • Mawasiliano Tshs....
  • Stationery Tshs....
  • Overtime Tshs....
  • :spy:
  • :spy:
  • ..............................
 
Back
Top Bottom