Kama waziri Mwigulu anakataa kuwa pesa hazijaibiwa serikalini, ina maana kuwa anapingana na ripoti ya CAG?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Wakati akifunga mjadala wa bajeti ya wizara ya Fedha ya mwaka 2023/2024 waziri Mwigulu alinukuliwa akiwaambia wabunge kuwa, kama ripoti ya CAG inadai kuwa pesa nyingi zimeibiwa serikalini, je pesa yote anayoitoa Rais Samia kwenye miradi mbalimbali nchini, angezitoa wapi, iwapo pesa nyingi zimeibiwa serikalini?

Akauliza pia, kama Rais Samia ametoa pesa nyingi zaidi kwenye miradi mbalimbali, kuliko Rais mwingine yeyote, tokea nchi yetu ipate uhuru wake mwaka 1961, je hao Marais wengine waliowahi kuongoza nchi hii, pesa za nchi hii, walikuwa wakizipeleka wapi?

Kiukweli ni kuwa katika hotuba yake ya kufunga bajeti ya wizara ya Fedha ya mwaka 2023/2024, waziri Mwigulu Nchemba, alitumia sehemu kubwa ya hotuba yake, akitoa sifa kemkem Kwa Rais Samia na kuwaomba watanzania kuwa Mama anastahili kupewa maua yake, hadi nikajiuliza hivi waziri Mwigulu, amekuwa ndiye "chawa" mkuu wa Rais Samia Suluhu Hassan??

Kwa tafsiri nyingine, ni kama waziri Mwigulu alikuwa akimanisha kuwa Marais wote, waliowahi kuongoza nchi hii, ndiyo walilkuwa "wapigaji" wa pesa za nchi hii na Rais Samia Suluhu Hassan, ndiye Rais ambaye utawala wake hauna ufisadi hata kidogo!

Je nini maoni yako mwana JF
 
CAG hajawahi sema mahala popote kwamba pesa zimeibiwa ila alijenga hoja ambayo Serikali walitakiwa kujibu ndio maana hoja ya CAG haiwezi kuwa.ushahidi.wa.moja.kwa.moja.mahakamani..

Mwisho wizi upo ila.sio.kwa.kiwangi ambacho wapotoshaji wanataka kuaminisha watu,ingekuwa hivyo Nchi ingekuwa haiendi.
 
CAG hajawahi sema mahala popote kwamba pesa zimeibiwa ila alijenga hoja ambayo Serikali walitakiwa kujibu ndio maana hoja ya CAG haiwezi kuwa.ushahidi.wa.moja.kwa.moja.mahakamani..

Mwisho wizi upo ila.sio.kwa.kiwangi ambacho wapotoshaji wanataka kuaminisha watu,ingekuwa hivyo Nchi ingekuwa haiendi.
ChoiceVariable
Hivi unafikiri ripoti yote ya CAG kuwa pesa "zimepigwa" Kwa mabilioni ya shilingi, kuwa hiyo ripoti ni feki?
 
ChoiceVariable
Hivi unafikiri ripoti yote ya CAG kuwa pesa "zimepigwa" Kwa mabilioni ya shilingi, kuwa hiyo ripoti ni feki?
CAG alisema "zimepigwa"...au hili Neno "zimepigwa"lipo Kwa ripoti?

CAG akisema "matumizi mabaya"au pesa hazina "maelezo"...not necessarily ndo "zimepigwa"...

Naomba uelewe sijasema hakuna wizi au hakuna pesa zimeliwa na wajanja...
Nachojaribu kusema hapa uelewa wa ripoti za kihasibu nao Una changamoto zake Kwa watu wengi ...inapelekea upotoshaji
 
CAG hajawahi sema mahala popote kwamba pesa zimeibiwa ila alijenga hoja ambayo Serikali walitakiwa kujibu ndio maana hoja ya CAG haiwezi kuwa.ushahidi.wa.moja.kwa.moja.mahakamani..

Mwisho wizi upo ila.sio.kwa.kiwangi ambacho wapotoshaji wanataka kuaminisha watu,ingekuwa hivyo Nchi ingekuwa haiendi.
Jizi wewe, tanzania mwizi anaanzia mfagiaji wa ofisi hadi mtu wa cheo cha juu ofisini halafu unasema wizi haupo kwa kiwango kikubwa, unaota wewe
 
CAG alisema "zimepigwa"...au hili Neno "zimepigwa"lipo Kwa ripoti?

CAG akisema "matumizi mabaya"au pesa hazina "maelezo"...not necessarily ndo "zimepigwa"...

Naomba uelewe sijasema hakuna wizi au hakuna pesa zimeliwa na wajanja...
Nachojaribu kusema hapa uelewa wa ripoti za kihasibu nao Una changamoto zake Kwa watu wengi ...inapelekea upotoshaji
Mwanza huko cag aliomba risiti na maelezo ya mamilioni ya hela walishindwa kumpa leo kaondoka yupozake Dodoma wanamwambia njoo risiti zimeonekana sasa huo sio wizi?
 
Wanaosikitisha ni CHAWA.

Pengine yale mapambano dhidi ya WAUPINDEA yangewaangazia na hawa CHAWA, ni kichocheo kikubwa!
 
lazima akatae kwani yeye ndie ananyooshewa vidole vya moja kwa moja!
Ana kiburi na majivuno ya kipekee sana huyu mtu, anajiona anajua kuliko wengine kumbe hamna kitu!
Nahisi serikali hii kuna matatizo ya hawa watendaji kuliko awamu nyingine zote ndio maana ya hivi viburi!
bado tunamkumbuka alivyotuambia kama hatutaki tozo twende Burundi!
 
Kama unataka stress fatilia serikali , otherwise Deal na Mrembo wako na familia yako
 
CAG alisema "zimepigwa"...au hili Neno "zimepigwa"lipo Kwa ripoti?

CAG akisema "matumizi mabaya"au pesa hazina "maelezo"...not necessarily ndo "zimepigwa"...

Naomba uelewe sijasema hakuna wizi au hakuna pesa zimeliwa na wajanja...
Nachojaribu kusema hapa uelewa wa ripoti za kihasibu nao Una changamoto zake Kwa watu wengi ...inapelekea upotoshaji
Hii Nchi walah kutoka kweny wizi na kua wazalendo labda hiki kizaz kitoweke kwanza na si vinginevyo!!!
 
CAG hajawahi sema mahala popote kwamba pesa zimeibiwa ila alijenga hoja ambayo Serikali walitakiwa kujibu ndio maana hoja ya CAG haiwezi kuwa.ushahidi.wa.moja.kwa.moja.mahakamani..

Mwisho wizi upo ila.sio.kwa.kiwangi ambacho wapotoshaji wanataka kuaminisha watu,ingekuwa hivyo Nchi ingekuwa haiendi.
Calibre ya watu aina hii ni waz Tanzania haiwez songa mbele kupambana na wabadhirifu na mafisad, nadhan waliopo sasa watoweke wote ndipo kije kizaz kingine. But sio calibre hizi za praising!!
 
Wakati akifunga mjadala wa bajeti ya wizara ya Fedha ya mwaka 2023/2024 waziri Mwigulu alinukuliwa akiwaambia wabunge kuwa, kama ripoti ya CAG inadai kuwa pesa nyingi zimeibiwa serikalini, je pesa yote anayoitoa Rais Samia kwenye miradi mbalimbali nchini, angezitoa wapi, iwapo pesa nyingi zimeibiwa serikalini?

Akauliza pia, kama Rais Samia ametoa pesa nyingi zaidi kwenye miradi mbalimbali, kuliko Rais mwingine yeyote, tokea nchi yetu ipate uhuru wake mwaka 1961, je hao Marais wengine waliowahi kuongoza nchi hii, pesa za nchi hii, walikuwa wakizipeleka wapi?

Kiukweli ni kuwa katika hotuba yake ya kufunga bajeti ya wizara ya Fedha ya mwaka 2023/2024, waziri Mwigulu Nchemba, alitumia sehemu kubwa ya hotuba yake, akitoa sifa kemkem Kwa Rais Samia na kuwaomba watanzania kuwa Mama anastahili kupewa maua yake, hadi nikajiuliza hivi waziri Mwigulu, amekuwa ndiye "chawa" mkuu wa Rais Samia Suluhu Hassan??

Kwa tafsiri nyingine, ni kama waziri Mwigulu alikuwa akimanisha kuwa Marais wote, waliowahi kuongoza nchi hii, ndiyo walilkuwa "wapigaji" wa pesa za nchi hii na Rais Samia Suluhu Hassan, ndiye Rais ambaye utawala wake hauna ufisadi hata kidogo!

Je nini maoni yako mwana JF
suluhisho ni katiba mpya tu vinginevyo CAG ataonekana kituko,mwongo na mpotoshaji.tuidai katiba mpya haraka ili mambo yaende vzr.
 
Wakati akifunga mjadala wa bajeti ya wizara ya Fedha ya mwaka 2023/2024 waziri Mwigulu alinukuliwa akiwaambia wabunge kuwa, kama ripoti ya CAG inadai kuwa pesa nyingi zimeibiwa serikalini, je pesa yote anayoitoa Rais Samia kwenye miradi mbalimbali nchini, angezitoa wapi, iwapo pesa nyingi zimeibiwa serikalini?

Akauliza pia, kama Rais Samia ametoa pesa nyingi zaidi kwenye miradi mbalimbali, kuliko Rais mwingine yeyote, tokea nchi yetu ipate uhuru wake mwaka 1961, je hao Marais wengine waliowahi kuongoza nchi hii, pesa za nchi hii, walikuwa wakizipeleka wapi?

Kiukweli ni kuwa katika hotuba yake ya kufunga bajeti ya wizara ya Fedha ya mwaka 2023/2024, waziri Mwigulu Nchemba, alitumia sehemu kubwa ya hotuba yake, akitoa sifa kemkem Kwa Rais Samia na kuwaomba watanzania kuwa Mama anastahili kupewa maua yake, hadi nikajiuliza hivi waziri Mwigulu, amekuwa ndiye "chawa" mkuu wa Rais Samia Suluhu Hassan??

Kwa tafsiri nyingine, ni kama waziri Mwigulu alikuwa akimanisha kuwa Marais wote, waliowahi kuongoza nchi hii, ndiyo walilkuwa "wapigaji" wa pesa za nchi hii na Rais Samia Suluhu Hassan, ndiye Rais ambaye utawala wake hauna ufisadi hata kidogo!

Je nini maoni yako mwana JF
Huko anapoenda kukopa akipogwa stop ndo ndo tuje hapa tuulizie alikuwa anatoa wapi
 
Back
Top Bottom