Kama Slaa, Migiro, Salim, Lowassa, Shein hawafai kuwa Rais; nani atatufaa 2015?

mwalimu nyerere alituonya kutaja majina kabla ya sifa...... sijui lakini kwa vile umetulazimisha kutaja majina basi nadhan kwa sasa labda mwakyembe!!!
 
mwalimu nyerere alituonya
kutaja majina kabla ya sifa...... sijui lakini kwa vile umetulazimisha
kutaja majina basi nadhan kwa sasa labda mwakyembe!!!

Sisi tuna mupigia upatu Dr slaa ndiye candidate wetu wa rais 2O15.CCM tunaomba mutupe jina moja tu la mtu munaye ona anafaa kua rais kutoka chama chenu musitupe majina mengi tunaomba jina moja tu
 
Hapa mtu anayefaa kuongoza TZ ni dr.W.P.SLAA tu,huyu pekee ndiye mwenye uchungu na umaskini wa taifa letu,hana urafiki na wezi,mafisadi,wala rushwa na wahujumu uchumi.wengine waliobaki wote ni zao la ufisadi.hao lowasa na wenzake ndio waasisi wa ufisadi ha pa nchini,wameshiriki katika maamuzi mengi haramu yaliyotufikisha hapa tulipo wakiwa mawaziri na wajumbe wa cc ya chama chake.ili nchi ipige hatua itoke kwenye mkwamo inamuhitaji dr slaa tu.
 
Sisi tuna mupigia
upatu Dr slaa ndiye candidate wetu wa rais 2O15.CCM tunaomba mutupe jina
moja tu la mtu munaye ona anafaa kua rais kutoka chama chenu musitupe
majina mengi tunaomba jina moja tu

Kama mwakyembe ndio candidate wa ccm urais 2015 basi atapambana na Dr slaa na huo ndio utakua mwisho wa utawala wa ukoo wa panya
 
hata hivo nasikia cdm wanampango wa kutokumsimamisha Slaa eti wanataka kumsimamisha Mnyika au Lissu ili kuwasuprise watanzania kwa mara nyingine,HAPO VIPI? Magamba yote
 
Last edited by a moderator:
Kiukweli nionavyo mimi viongozi ambao wanafaa kuliongoza taifa letu kwa 2015 ni wafuatao:

1. William Ngeleja (Mr Megawatt)
2. Zitto Kabwe
3. Dr Mwinyi
4. Shamsi vuai Nahodha

Uzuri wa hawa jamaa wako smart, waelewa, wazalendo, si wanafiki, ni wakweli, ni wachapakazi na wana misimamo, hawababaishwi na ushabiki wa kisiasa. Aida, ni watu wenye hekima na watulivu, hawana jaziba kwa umma hata kama wanashutumiwa.

Vinginevyo ni majanga matupu!
 
Nipo mimi hapa nichagueni. Ila nitaandaa viboko vya kutosha ili tuwekane sawa ndani ya miezi sita ya kwanza. Haya mambo ya ujinga ujinga wa kuvunja sheria ndogo ndogo, kama za barabarani na nyinginezo, ni kulamba viboko vya haja hadharani tu. Jela tutazitumia kuwafunga mafisadi, majangiri na watu kama hao waliotufikisha hapa tulipo baada ya kutaifisha mali zao za wizi.
 
Usitusumbue, Rais wa JMT anajulikana hata tungefanya uchaguzi huru na haki leo hii.
 
"Kwa nini tusifikirie majina kama haya:
•Emmanuel Nchimbi
•Zitto Zuberi Kabwe
•John Mnyika
•January Makamba
•William Ngeleja
•Nape Nnauye
•Halima Mdee
•n.k

Afazali Zitto mi namkubali, Lakini hawa wengine mmmmh.... Mungu apishie mbali

Makosa yaleyale ya 2010. Still tunaangalia rangi ya paka badala ya kuangalia uwezo wa Paka kukamata Panya.
Mbona watanzania hatujifunzi makosa, tutaendelea kuumiza wananchi wasio na hatia mpaka lini?

Nafasi ya Urais si ya kukurupuka, huyo aliepo si aliungwa mkono na Vijana na kauli za asali na maziwa, yamefika wapi.
 
Katika ulowataja yupo aneyefaa.Mi naona hata kama hafai tuwachague tu mbona Kikwete hakufaa tukamchagua!Tehe tehe teheee tumpe Migulu Michemba au naye keshatajwa ktk kashfa.ila kama ni ile ya kuua mi ndo nnayoijua na sijamtaja !
 
Kiukweli nionavyo mimi viongozi ambao wanafaa kuliongoza taifa letu kwa 2015 ni wafuatao:

1. William Ngeleja (Mr Megawatt)
2. Zitto Kabwe
3. Dr Mwinyi
4. Shamsi vuai Nahodha

Uzuri wa hawa jamaa wako smart, waelewa, wazalendo, si wanafiki, ni wakweli, ni wachapakazi na wana misimamo, hawababaishwi na ushabiki wa kisiasa. Aida, ni watu wenye hekima na watulivu, hawana jaziba kwa umma hata kama wanashutumiwa.

Vinginevyo ni majanga matupu!

Mkuu nahisi wakati unaandika hii utakuwa ulishatupia Zanzi bila shaka
 
Uongozi ni hekima ndg siyo Muonekano wa mtu Mungu atampa amtakaye kwa wakati wake
 
Mimi kama Mtanzania mpiga kura ,siwezi kumpigia kura Slaa ikiwa atakuwa mgombea wa Uraisi kupitia Chadema.Huyu ukiangalia ana tatizo la ndoa,unaweza kusema ni private lakini haikubaliki kuwa hivyo ,kwani kuiba au kuchukua mke wa mtu na kuzusha kuwa alitalakiwa na kuitumia nafasi hiyo kuwa wako ,huko siko na si kweli kwani bado kuna kesi au ilikuwepo kesi. wacha yote hayo lile tendo la kuchukua mke wa mtu hadi kufikishana mahakamani si la kiungwana na halikufaa kuwepo kwa mgombea Uraisi.

Slaa hafai kuwa mgombea kwani hili jambo limemuengua kimaadili ,inaonyesha hana maadili mema ,na hata kuukimbia Upadre nalo pia ni suala la kuwa si mtu mwenye msimamo ,zaidi ni mwenye kuonyesha dalili za mtu mwenye tamaa na asieridhika.

Ingawa anaonyesha ni mpiganaji hodari katika duru za kisiasa ,yeye ni bora angebakia hukohuko kwenye ngazi za chini za ubunge na nyinginezo Uraisi kwa mtu wa aina hii ni mwiko na hafai kabisa.

Hayo ni yako.ugaragale,ulie na hata ufanyeje,dr Slaa ndio kipenzi cha watz na ndie rais wao ajae.
 
"Kwa nini tusifikirie majina kama haya:
•Emmanuel Nchimbi
•Zitto Zuberi Kabwe
•John Mnyika
•January Makamba
•William Ngeleja
•Nape Nnauye
•Halima Mdee
•n.k

Afazali Zitto mi namkubali, Lakini hawa wengine mmmmh.... Mungu apishie mbali
Sasa hayo majina kwenye red si ni vituko tu hapa jamvini au unataka umefanya balance kwa vyama vikuu nchini,afadhali kwa ccm ungemweka mtu kama Filikunjombe ningekuelewa mkuu.
 
Wanasiasa wengi wa CCM wamekuwa wakitajwa kwamba ama wanania ya kutaka kugombea au wanatakiwa kugombea nafasi ya uraisi itakapofikamwaka 2015 katika uchaguzi mkuu. Watu wengi tumekuwa tukijiuliza, je kwa miongohii ya karibuni CCM inaweza kutupatia raisi bora kwa sasa. Haya ndioyanayosemwa mtaani kwetu;

Edward Lowasa

Side A
Mtu wa maamuzi
Amefanikiwa ki-utendaji, hasa kwa kipindi alichokuwa waziri mkuu-kama ujenzi washule za kata n.k
Mtu wa maamuzi magumu (kama anavyoamini yeye mwenyewe uamuzi wa kuingia mkatabana RICHMOND ulikuwa mgumu,kwa nia njema japo baadae ulikuwa na madhara)-akijitanabaishani bora uchukue maamuzi magumu kuliko kutochukua maamuzi.
Kiutenndaji amewahi kuwashughulikia wakurugenzi au mainjiniawazembe ‘on the spot’.

Side B
Amehusika na kashfa ya RICHMOND, kwa kulazimisha kampunihiyo ipewe zabuni pasipokuwa na vigezo, hata mchakato wa kuipa zabuni haukufuatasheria ya manunuzi ya uma. Sakata hili limeshalipatia taifa hasara kubwa mno.
Anadaiwa kuwa na matumizi makubwa katika kuusakauraisi-misaada makanisani, misikitini, na vikundi mbalimbali vya kijamii-swalini kwamba kwanini anautaka sana uraisi na kama akiupata fedha alizotumiazitarudi vipi
Mtazamo wa baba wa taifa juu yake-kwa kutambua nafasi yababa wa taifa (J.K Nyerere)katika nchi hii,akitoa maoni juu ya jambo lolotehatuwezi kuyapuuza-inadaiwa aliwa kuhoji ukwasi alionao Edo ukilinganisha naumri wake mdogo
CCM vijana wa Pwani wamewahi kutoa tamko raisi ajaye (2015) hatatokakaskazini.

Benard Membe

Side A
Ana uzoefu wa siasa za kimataifa, ana ‘connection’ kwaniamewahi kuwa balozi kabla ya kuwa waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikanowa kimataifa
Nguvu yake nyingine inayotajwa ni uhusiano wa karibu alionaona mkubwa wa kaya pamoja na familia yake.

Side B
Kuna watanzania ambao hawakuridhishwa na msimamo wake wakuunga mkono Tanzania ijiunge na OIC
Kama kiongozi mkubwa nchini hajawahi kufanya jambo loloteexceptional la kiutendaji-amekuwa akitimiza majukumu kwa namna ya kawaida sana –watupia wametazama namna alivyo-deal na ishu ya Malawi pamoja na East AfricanCommunity

Samweli Sita

Side A
Alijizolea sifa sana kwa uongozi wa bunge lililopita, yeyemwenyewe akiliita ni ‘bunge la viwango’-anaonekana alifanya kazi ya uspikavizuri ukilinganisha na uongozi wa bunge la kabla na baada yake (baada ya mfumovyama vingi kuanza)
Angalau kwa maneno amekuwa akipinga ufisadi naakijitanabaisha na kundi ndani ya CCM linalopambana na ufisadi

Side B
Wapo wanaodai alikuwa mbabe kipindi anaongoza bunge
Kutoeleweka kimsimamo-amehusishwa na kuanzisha chama cha CCJkabla ya kuwaacha solemba wale aliowatanguliza
Akiwa spika alijenga ofisi ya spika wa Bunge la Jamuhuri yaMuungano wa Tanzania kule Urambo (jimboni kwake) akijua kwamba hatakuwa spikamilele-ofisi ingeweza kujengwa hata Dar-es-salaam kama haipo.
Aliwahi kuwaita upinzani (akijibu swali kwa niaba ya wazirimkuu bungeni) kazi yao ni unafiki-huo ni unafiki kwakuwa hata yeye alihusishwana CCJ (upinzani) kabla ya kukosa usajili. Kwa namna anavyojibainisha kamampambanaji dhidi ya maovu na rushwa hakupaswa kuwatuhumu unafiki watu ambaowanapigana vita hiyohiyo. Kwa nafasi anayoitaka (uraisi) akiipata, kamaanawatazama wapinzani kuwa kazi yao ni unafiki, demokrasia ya vyama vingi inawezakuwa pabaya.
Wapo pia wanaozani, baada ya ‘kupigwa chini’ kwenye mchakato wa spika kwa kigezo cha ‘sasa niwakati wa kuwa na spika mwanamke’, asingekubali nafasi ya kupozwa ya uwaziri waAfrika Mashariki, kwa kukubali aliisaliti nafsi yake.

John Magufuli

Side A
Anatajwa kama ni mtu wa maamuzi, ambaye hajali watu,wakiwepo wakubwa wake wa kazi watasema nini kuhusu maamuzi (sahihi) yake
Kiutendaji ana CV nzuri tu, akiwa wizara ya ujenzi, uvuvi,na baadae ujenzi tena

Side B
Inasemekana wakati mwingine haangalii madhara ya maamuziyake kabla ya kuamua-pamoja na kufuata sheria pia kwa kiongozi wa ngazi za juuinashauriwa kutumia busara wakati mwingine
Amewahi kukumbwa na kashfa ya kujiuzia nyumba yeye, nduguyake na mwanamke mmoja kipindi cha cha uuzaji wa nyumba za shirika lataifa-hayo ni matumizi mabaya ya nafasi uliyonayo katika utumishi wa uma kwamaslahi binafsi

Harrison Mwakyembe

Side A
Mchapakazi, mthubutu, siyetiwa hofu na watu wengine,mpambanaji dhidi ya ufisadi na maovu

Side B
Machoni pa watu, sikiongozi wa kushika nafasi za juu kama uraisi-pengine aishie uwaziri mkuu
Wakosoaji wengine wanadai, akiwa mwenyekiti wa tumeiliyotafiti sakata la ufisadi-RICHMOND- hakusema yote kwa wananchi, kwaniangefanya hivyo serikali ingeanguka,tunajiuliza kwanini hakusema yote,ilikuwakwa masilahi ya nani waakati hata kwa yale yaliyosemwa yaliingusha serikali
Ushiriki wake kwenye serikali ambayo yeye mwenyewe alidaihaikuchukua hatua kwa watu wanaowinda maisha yake pia unakosolewa, ni kamaamesaliti nafsi yaake

Salim A. Salim

Side A
Anatajwa kama mtu mwenye busara
Mtu mwenye uzoefu kimataifa
Mzanzibari-Wapo wanaoona uchaguzi ujao ni zamu ya Wazanzibarikukalia kiti cha uraisi wa Muungano, baada ya Watanganyika kuongoza mihulamiwili mfululizo

Side B
Alichafuliwa katika uchaguzi wa ndani wa CCM wa kumtafutamgombea uraisi mwaka 2005 kwa kudai
Ana mahusiano na kifo cha raisi wa kwanza wa Zanzibar,tuhuma ambazo inadaiwa ni matokeo ya siasa chafu
Pia katika siasa za majitaka, alihusishwa kuwa karibu nachama cha HIZBU, chama cha Wazanzibari waarabu ambao hawakuunga mkono mapinduziya Zanzibar
Wapo wanaodai pia, pamoja na sifa nzuri alizonazo ‘personally’,chama alichopo hakiwezi kumtoa mgombea safi, kwa imani kwamba nguvu yawachache/mmoja haiwezi kupingana mfumo ‘ozo’.

Fredrick Sumaye

Side A
Anaunganishwa na mafanikio ya kiuchumi ya serikali ya awamuya tatu, kwani wapo wanaoamini kwa maendeleo ya kiuchumi serikali ya awamu yatatu ilifanya vizuri kuliko serikali zilizopita na iliyofuata, anapewa sifakwakuwa yeye ndio alikuwa waziri mkuu wa wakati huo
Angalau kwa matamko amekuwa akikemea uovu na ufisadiulivyoshamiri nchini

Side B
Hawezi kujitenga na matukio ya kifisadi yaliyotokea awamu yatatu, katika awamu hiyo tumeshuhudia ufisadi ulifanyika kwa kuzingatia hichondio ilikuwa kipindi cha uuzwaji wa mashirika ya uma (ubinafsishaji). Pia kunasakata kama la EPA lilitokea zama zake
Kwa kipindi sasa amekuwa akigombea ardhi na wananchi, kwamfano maeneo ya kiluvia ya Kisarawe kijiji cha Tondoroni kuna ugomvianaohusishwa yeye na wananchi kuhusu umiliki ardhi, na inadaiwa jeshi limekuwalikitajwa kumiliki eneo hilo kama njia ya kutisha wananchi kwa maslahi ya mtubinafsi

SWALI;
Kwa watu hawa nani anafaa, au ndani ya CCM hakuna kabisa mtuanayefaa kupewa dhamana hii (uraisi) nzito kuliko zote katiaka taifa letu?
 
Mtapata shida sana ila mnasaau kuna yule ambaye hasubiri nyinyi mmpitishe na atawamaliza tu kwa hela mtake msitake make nyinyiem mwenye hela ndo anaonekana msafi na mwenye kustahili uongozi
 
Mkuu wanatajwa wengi tu:

Dr. John Pombe Maghufuli
Mr. Membe
Mr. Six
Mr. Sumaye
Mr. Mwinyi
Ms. Tibaijuka, nk.

Mkuu analysis yako ni nzuri kwa hao watu uliowataja lakini bahati mbaya hujatuwekea umri wao ifikapo October 2015 ambao ni mwezi wa uchaguzi.

Matatizo yangu ni kwamba watu humu JF tumekuwa tukisema wazee wetu ni vyema wakapumzika kama tulivyotoa maoni kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi. Lakini linapofika suala la Urais tunawaangalia watu ambao wako beyond 60 years! Hawa wanatakiwa wawe wameenda kupumzika baada ya kuutumikia umma (Najua urais hauna retirement age).

Nadhani kwa mantiki ya kutaka vijana watwae madaraka basi ni vyema wakatwaa na Urais pia. Ningefurahi kuona wana JF wanakuwa chachu katika hili kwa kuwapendekeza vijana na si wazee ambao wanatakiwa wawe washauri tu kama mzee Mtei, Kisumo, nk.

Ningefurahi kuona tunawapigia chapuo vijana na wala si babu zetu (najua wana JF wengi ni .com na Tab).

Kwa nini tusifikirie majina kama haya:
  • Emmanuel Nchimbi
  • Zitto Zuberi Kabwe
  • John Mnyika
  • January Makamba
  • William Ngeleja
  • Nape Nnauye
  • Halima Mdee
  • n.k
Lakini wawe of age but below 60 years by October 2015. Kila siku wazeee wazeee. Ni muda muafaka wa kutafuta vijana na kuwakabidhi mikoba. Ila wasiwe wavuta shisha tu!

Nchimbi???
Ngeleja???
Nape???
ha haa ha ha ha ha ha ha ....uuuuuuwiii' Du! umeichoka Tz yetu...
 
Back
Top Bottom