Kama kweli kilichopitishwa Bungeni siyo Mkataba bali ni makubaliano, basi Bunge nalo limevunja Katiba

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,498
37,792
Ibara ya 63(3)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inalipa mamlaka Bunge la nchi kujadili na kupitisha mikataba inayoingiwa Kati ya Tanzania na Mataifa mengine. Siku ya majadiliano nilimsikia Spika Tulia na baadhi ya Wabunge akiwemo Kitila Mkumbo wakinukuu Ibara hii kwamba ndiyo imewaba Bunge nguvu ya kujadili na kisha kupitisha mkataba na Dubai Emirate.
Cha kushangaza Jana Spika Tulia kageuka anasema walichopitisha si Mkataba ni makubaliano.
Sasa naomba Wapambe wake mtusaidie ni Ibara ipi ya Katiba inayosema makubaliano nayo yatajadiliwa na kupitishwa na Bunge? Vinginevyo mtuambie labda Spika Tulia analazimisha kutofautisha Mkataba na makubaliano!!
20230629_125811.jpg
 
1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO), je makubaliano yanaweza kusema tunakupa bandari zote alafu mkataba ukasema tunakupa bandari moja tu?

Si spika Tulia, waziri mkuu wala Rais mwenyewe wala wale vikaragosi wengine wanaotumwa kutetea mkataba aliyeweza kujibu swali hili.
2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
elimu yetu ni kichekesho, huyu dada et ni msomi tena mtaalamu wa kuandaa vijana kwenye nyanja ya sheria duh...niliwahi kuwaambia watu kuwa dokta anayefundisha chuo kikuu bongo akienda ulaya ni tutorial asistant tu, content hawana.
 
Ibara ya 63(3)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inalipa mamlaka Bunge la nchi kujadili na kupitisha mikataba inayoingiwa Kati ya Tanzania na Mataifa mengine. Siku ya majadiliano nilimsikia Spika Tulia na baadhi ya Wabunge akiwemo Kitila Mkumbo wakinukuu Ibara hii kwamba ndiyo imewaba Bunge nguvu ya kujadili na kisha kupitisha mkataba na Dubai Emirate.
Cha kushangaza Jana Spika Tulia kageuka anasema walichopitisha si Mkataba ni makubaliano.
Sasa naomba Wapambe wake mtusaidie ni Ibara ipi ya Katiba inayosema makubaliano nayo yatajadiliwa na kupitishwa na Bunge? Vinginevyo mtuambie labda Spika Tulia analazimisha kutofautisha Mkataba na makubaliano!!View attachment 2673115
Bogas kabisa haaa wanawake
 
Shetani na mawakala wake hawana kabisa mlango wa kutokea kwenye hili la bandari, kila utetezi wa hovyo wanaojaribu kuja nao, wanapewa majibu mazito yenye uthibitisho kisheria.
 
Back
Top Bottom