CCm itaendelea kuwa juu tu. Tanzania hakuna chama cha siasa hata kimoja vyote ni vyama vya harakati na kutangaza harakati badala ya sera. CCM oyeeeeeeeeeee!
Chama cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa Vyama vya Upinzani, kinaweza kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, "potelea mbali:" wakachagua Chama cho chote, ilimradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa Nchi yetu unataka yasemwe. (Ukurasa 61)
Mwalimu hakuishia hapo, bali aliongezea namna hii:
Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha Chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila hofu na wasi wasi! (Ukurasa 66)
Wana jf mliotazama habari startv saa mbili usiku huu mtakuwa mashaidi wangu!Hivi Huyu Siyoi hajui kweli Mwanry ni mbunge WA jimbo gani?
Duh poor SIYOI...
Atakuwa aliandikiwa desa na majimarefu au Lusinde wamemlisha kasa. Naskia jamaa huwa anaandikiwa usiku mambo ya kuzungumza kesho yake ili akalili usiku kucha na kugandamizia ndumu (bangi) asubuhi ili apate stimu ya kupandia jukwaani. Akipata ubunge huyo jamaa hadhi ya kuwa mbunge nchi hii itashuka sana
Mkuu nilifuatilia habari ya ITV vizuri.
Lusinde alisema hivi, "Mchagueni Siyoi, anatokea ukoo mkubwa wa CCM"
Yaani alimaanisha vyama vya siasa ni 'koo' na CCM ambayo ni moja ya vyama hivyo, ni ukoo mkubwa yaani chama kikubwa.
Tusipotoshe jamanijapo tunahitaji mabadiliko.