Kailima Ramadhan: Uchaguzi 2015 ulikuwa huru na wa haki, CHADEMA imeshindwa kihalali! Hakuna upendeleo kwa CCM, NEC ni Tume huru

CCM wazandiki, wanafiki na wafitini wakubwa, tena waliollkosa haya bini soni. Polisi ni yao, magereza ni yao, time ya uchaguzi ni yao, utawabia nn?

Wanatumia nguvu hawakamatwi, wanatoa rushwa hawakamatwi, wanatukanwa hawahojiwi, n.k.
 
kiukweli hapa hatuna tume huru ya uchaguzi bali tume ya uchaguzi. chini ya tume hii siwezi panga foleni kamwe.
 
Wanabodi,

Baada ya figisu figusu za uchaguzi wa marudio wa madiwani, nimebahatika ya kufanya mahojiano na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhani Kailima, yaliyofanyika ofisini kwake jioni hii, kuhusu uchaguzi huo, katika kipindi cha Habari Zaidi ya Habari na PPR, ambacho kinarushwa kupitia Vituo 5 vya TV, TBC, ITV, STAR TV, Channel Ten, Azam TV, Clouds TV na kwenye Youtube.


Hizi ni Baadhi ya Dondoo za Mahojiano Hayo.
  • Zoezi la Uchaguzi limekwenda vizuri kwa asilimia 95%, hakukuwa na kasoro yoyote kubwa kuathiri uchaguzi huo, hivyo uchaguzi umekamilika na taarifa rasmi, itatolewa punde itakapokamilika.
  • Uchaguzi huo ulikuwa ni uchaguzi huru na wa haki, licha ya kutokea mapungufu madogo madogo, lakini matokeo ni matokeo halali, aliyeshinda ameshinda kihalali kwa haki, aliyeshindwa, pia ameshindwa kihalali kwa haki.
  • Hakuna hata chama kimoja, kilicholalamikia jambo lolote kuhusu uchaguzi huo, mpaka sasa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi, haijapokea malalamiko yoyote, kutoka chama chochote, au mgombea yoyote kwa mujibu wa utaratibu wa kujaza fomu za malalamiko.
  • Hakuna chama kilichojitoa rasmi, ila kama ilivyo kushiriki uchaguzi ni hiyari, vivyo hivyo vyama viko huru kujitoa wakati wowote, lakini mpaka zoezi la uchaguzi linamalizika, hakuna chama kilichojitoa rasmi kwa mujibu wa taratibu za kujitoa.
  • Mawakala wa vyama, wanapatikana kwa mujibu wa sheria, taratkanuni, mtu ambaye hajakidhi taratibu za uchaguzi, hawezi kuruhusiwa
  • Ameelezea kuwa Tume yake ni Tume huru, inayoendesha chaguzi kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, hakuna chama chochote, kimewahi kulalamikia kipengele chochote cha uchaguzi kinachonyima haki, kitakachoifanya tume isiwe huru.
  • Amesisitiza Tume yake haijawahi kuingiliwa na chombo chochote, wala kupokea maagizo au maelekezo kutoka kwa yeyote.
  • Tume yake haijawahi kufanya upendeleo wowote kwa chama chochote, hata CCM nayo pia inailalamikia tume yake, hata uchaguzi wa Madiwani CCM Arusha wamelalamika.
  • Pia nimeuliza kuhusu Mkurugenzi, Mwenyekiti wa NEC na makashna kuteuliwa na rais ambaye ni mwenyekiti wa chama kimoja, wataweza kutenda haki?, pia amelijibu.
My Take.
Its high time vyama tuanze kutake responsibilities kwa matokeo ya utendaji wa vyama vyetu kwenye chaguzi, kwa pale ambapo uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, tukubali kushindwa kihalali, asiyekubali kushindwa sio mshindani, badala ya kutafuta visingizio.

Kama hali ya uwezo wa ushindani kwa vyama vyetu vya upinzani nchini Tanzania, jee hali itakuwaje uchaguzi wa 2020?. Kama wapinzani hawatabadili strategies, za namna ya kushindana na CCM kwenye sanduku la kura, kuna hatari ya CCM, kuyarejesha majimbo yote ya upinzani mwaka 2020, hivyo Tanzania kuanza safari ya kuelekea kuwa ni nchi ya vyama vingi jina tuu, lakini ukweli tunaelekea kuwa nchi ya chama kimoja.

NB. Kipindi kikiwa tayari, nitakipandisha humu umsikilize mwenyewe.

Wasalaam.

Paskali

Hivi kampuni yako haijawahi kuwa na mkataba wa kibiashara/huduma na Tume ya Uchaguzi? Inaonekana hukufanya mahojiano na huyu mtu yenye lengo la kulisaidia taifa, bali kuisaidia tume, na mwisho wa siku wewe mwenyewe kuwa sehemu ya tatizo!
 
Umemletea Pasco hoja nyepesi hivyo?
Atakuacha mbali sana,

Kiboko ya pasco ni Mchambuzi, Nguruv3, Joka Kuu, kobello, na Mnyama Kiranga
 
Kwa hivyo wangejitoa wakati vitimbi vimeanza baada ya uchaguzi kuanza? Shameless kabisa
Ninyi stahiki yenu ni hii

20 Ole wao wasemao kwamba uovu ni wema, na kwamba wema ni uovu; watiao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza; watiao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu!
Isaya 5 :20


Kwenu mtu akifa huwa mnasubiri daktari aandike ripoti kuwa huyu kafa? Si we mwenyewe unaona tu mtu kweli kafa na dokta anakwambia tu kafa then taarifa baadae?

Ninyi ndiyo waandishi mnaotuharibia nchi hii sio siri.

Nimeongea nikiwa huru sina kadi ya chama hapa
Nakubaliana na wewe asilimia zote!
 
Inasikitisha sana wewe hoja ya msingi kwako ni BUNGE LIVE na mikutano, watanzania hawataki kusikia hoja za kijinga namna hii. Endeleeni kupasha benchi joto mpaka mtakapopata akili.
Hivi Ile Ripoti Maalum Ya Kamati Ya Ulinzi Na Usalama Ya Bunge Kuhusu Kushambuliwa Kwa Mh. Tundu Lissu Tuliyoambiwa Itasomwa Kwenye Bunge La Mwezi Wa 11 Ilipotelea Wapi? Mbona Hiyo Ripoti Hatujaisikia?
 
Mkuu BAK, uchaguzi ni process yenye sheria, taratibu na kanuni, zikiwemo taratibu za kuripoti malalamiko yoyote, kama hayo yote yametokea na hakuna yoyote aliyelalamika rasmi, hadi uchaguzi unakamilika, hakuna yoyote aliyelalamika!, na hata kule kujitoa kwa Chadema, haikujitoa bali ilisusa tuu, kama ilivyo kanuni, unakuwa mgombea kwa kujaza fomu, na kujitoa ni kwa kutoa taarifa rasmi ya maandishi, na sio kuwaambia tuu waandishi wa habari. Tangazo lile ya kujitoa, lilipaswa kufuatiwa na kujaza fomu ya malalamiko, na kutoa taarifa rasmi ya kujitoa. Kama hakuna malalamiko yoyote registered, then tume iko right, no one complained!.

Paskali
Pascal Mayalla unapaswa uelewe kuwa Tume iliratibu uhuni uliofanyika jana. Huu sio uchaguzi wa kwanza kufanyika Tanzania. Figisu tulizoziona jana kimsingi zinafuatia agizo la Rais la kutaka Wagombea wa CCM watangazwe hata kama hawajashinda. Mana alisema "inashangaza watu tunawalipa mishahara, tunawapa magari na tunawawekea Mafuta halafu mnawape ushindi wapinzani". Hii kauli ndio iliyopelekea Polisi kuwa eyes off, hands on katika kuhakikisha CCM inashinda kwa dhurma hata ikibidi kuua. Hakuna siri tena kuwa figisu za tume za kutokuwaapisha wasimamizi kwa wakati na kwa utaratibu ulio wazi ilikuwa ni sehem ya mkakati huo.

Binafsi wala sioni haja ya kupeleka malalamiko popote mana ndivyo utawala ulivyotaka iwe. Itatupasa tukae na kutathmini ni kwa namna gani tujipange kukabiliana na chaguzi zijazo. Ila tujue kuwa hii maana yake ni kuwa chaguzi zijazo zitakaribisha mapigano na mauaji ya halaiki. Nadhani ndio utawala unachotaka kukiona. Mana nnachofahamu mimi huwezi kung'ang'aniza kumtawala mtu asiyekuhitaji umtawale. Ni sababu hizi hizi ziliwafanya wazee wetu wapambane na mkoloni kwa silaha za jadi hadi wakamtimua pamoja na silaha nzito alizokuwa nazo.

Ila kilichotokea jana kimeiacha Tume uchi na kuudhihurishia umma kuwa Tume haina tena uwezo wa kutenda haki kwa vyama vya upinzani. Nadhani hapa Katiba mpya ndio itakuwa suluhisho. Kwa kilichotokea jana Chama cha Mapinduzi kimejiingiza katika fedheha kubwa na CCM imejipambanua kuwa ni chama cha Kihuni. CCM tuliyoiona jana sio CCM ile ya Mwalimu JK Nyerere. Jana tuliiona CCM katika sura mpya ya chama cha kihuni, chama dhurumati na cha kinyang'anyi. Hii ni hatua muhimu sana kwenye kukiondoa madarakani, vyama vyote duniani vilivyoondolewa madarakani vilipitia hatua kama hizi na hatimaye vikaondoka mchana kweupe.

Binafsi nayachukulia matokeo ya uchaguzi wa jana kuwa yamesababisha kukisogeza chama cha mapinduzi katika sehemu nzuri zaidi ya kukiondoa, iwe kwa sanduku la kura au kwa utaratibu mwingine. Ila kimekaribia kumwagika, CCM ya leo haiamini tena kwenye haki mana inajua haki ikitendeka basi wao wameondoka. Hii ni hatua nzuri mana inamaanisha kuwa CCM ishapoteza mvuto ilichobakia nacho sasa ni mabavu tu.

Ila wewe kama Mwandishi mkongwe inasikitisha sana kama katika kilichotokea jana hadi sasa hujaweza kuandika kitu kuhusu mustakabali wa Taifa letu. Hii inadhihirisha waandishi wetu mpo Kimaslahi zaidi. Kwenye nchi za Wenzetu vyama vya siasa vinaogopa kufanya ushenzi kama wa jana mana vinajua reputation yao itaharibiwa maana Media itahangaika nao. Ila kwetu media imetulia utadhani hawakuona uhuni uliofanywa jana.

Ila jua faida mnazozitarajia kwa kulea huu ujinga ni just short term. Mtapata hela mtajenga nyumba nzuri kwa kuwa mawakala wa kutetea huu ujinga ila cku nchi ikichafuka hizo nyumba mtazikimbia wenyewe na hizo hela mtazijutia. Nawasihi sana tupambane kila mtu kwa nafasi yake kuhakikisha amani tuliyonayo haitoweki. Naona CCM inajiinua sasa kutaka kuvuruga amani nchini. Ila jueni kuwa amani ikivurugika ni wote tutakuwa tumepoteza.
 
kama wewe umeshindwa kukemea mauaji kwenye uchaguzi siwezi kushangaa kwanini unapinga hoja hizo
Mauaji yapi kwenye uchaguzi yametokea? Jana na leo nimeangalia taarifa za habari chanel 10, azam na itv sijasikia taarifa ya mauaji.
Alafu hayo 'mauaji' ndo yangezuiliwa na bunge live unalotaka??
Ufipa mnasomeshwa ujinga.
 
Hii kitu chukulieni maguzi lakini madhara yake sio kwa mihemko tujione kwa kuwa ni ccm basi haina madhara kwetu. Madhara yetu ktk chama yako wazi yaani hatujuamini kutokana matendo yetu ndo yanatutafuna
Matendo yapi??
 
Hivi Ile Ripoti Maalum Ya Kamati Ya Ulinzi Na Usalama Ya Bunge Kuhusu Kushambuliwa Kwa Mh. Tundu Lissu Tuliyoambiwa Itasomwa Kwenye Bunge La Mwezi Wa 11 Ilipotelea Wapi? Mbona Hiyo Ripoti Hatujaisikia?
Unaniuliza mimi kama nani??
 
Pascal mayalla mm namfananisha na viongozi wanachuo waliokuwa wanahudumu jikoni kwanza walafi wachoyo wafitini waongo wana mashavu kama paka mwizi huyu mayalla ni mmoja wao
 
Kutokubali kushindwa ni tabia ya vyama vya upinzani vya hili bara la giza
So sijashangazwa na taarifa za CHADEMA za kutokubali matokeo
ila pia kutokukubali kushindwa kwa vyama tawala ni tabia ya hili bara la giza, kwa kutumia vyombo vya dola vinavyomilikiwa na serikali ya chama tawala ilikuendelea kuwepo
 
Inasikitisha sana wewe hoja ya msingi kwako ni BUNGE LIVE na mikutano, watanzania hawataki kusikia hoja za kijinga namna hii. Endeleeni kupasha benchi joto mpaka mtakapopata akili.
Kama.sheria ya kujenga kwenye mita zisizokubalika imepelekea sehemu jengo la Tanesco kubomolewa,kuwq na cheti feki ni kosa la jinai na wafanyakazi wa hivyo wameondolewa kwenye nafasi zao.
Je leo mikutano ya vyama vya siasa na maandamano ni sheria.je kuipinga siyo jinai?
 
Hata Spika wa bunge alisema hakupokea barua ya Nyalandu ya kujiuzulu ila dk chache alipokea barua ya CCM ya kumfukuza Nyalandu uanachama... kwa hiyo sintoshangaa kwa hili
 
Mauaji yapi kwenye uchaguzi yametokea? Jana na leo nimeangalia taarifa za habari chanel 10, azam na itv sijasikia taarifa ya mauaji.
Alafu hayo 'mauaji' ndo yangezuiliwa na bunge live unalotaka??
Ufipa mnasomeshwa ujinga.
Mku ss ni watanzania yaani ni wamoja sio mpaka mtu afe ndo tuone kunashida imetoka mtu awe amezuiwa kutimiza haki yake ya kikatiba kama amezuiwa kwa virungu au kwa uonevu hii ni mbaya hata kwa amwaccm mkomavu haiwezi kutusapoti chama kwani hawezi kujitetea chama mbele ya jamii kwa maswali yatakuwa mengi kutoka ktk hiyo jamii .
Hiki kipindi ni Mungu atunusuru na haya majaribu yasiyoyakitanzani
 
Pascal mbali na mazuri yake ila anasumbuliwa na ule ugonjwa sugu ambo huwezi kuuficha maradhi ya ukanda ni mabaya sana kuliko HIV
 
Hizi siasa za kuuana sio nzur kiukweli watanzania hatujafikia hatua hii hv kwann mtu anajitoa ufahamu kabisa anakuja na comments za ajabu kwenye thread yani anajifanya km hayaoni vile wenzetu walianza hvi hvi mwisho wa siku wakaelekea kubaya km watanzania tunapaswa kuweka itikadi zetu pembeni na kuangalia utu wetu ila ndo kuna wengine wanajifanya haya km maigizo au hawayaoni na kuna watu wanaona upinzani km kikwazo cha maendeleo na bado wanaaminisha watu hvi jamani upinzani ni kuleta changamoto na kuikosoa serikali ila kwenye mapungufu au kwenye uwalakini kurekebishwe sasa anayesema upinzani kusifia kila kukicha huyo atakua anajitoa ufahamu kwamba 2×3 jibu 6 yy anasema nane siasa za kuuana si nzuri watanzani wenzangu kumbukeni kuna maisha baada ya uchaguzi.........MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom