Kagoda Haina Kesi, hawafikishwi Mahakamani Ng'o!

Hivi ile kamati ya kuchunguza EPA tiyari imemaliza kazi?
kwani watuhumiwa ndo wameibukia kwenye tenda za matrekta.
Sina imani na Kilimo Kwanza tokea yule mtuhumiwa wa EPA
kuteuliwa na mkulu kwenda TIB.
 
Pole sana pasco. Tulishayasema haya humu. Aliyerudisha fedha ni manji kwa niaba ya kina ra. Na ndiye pekee aliyefanya hivyo kwa hiari. Hivi watu hamjajiuliza kwa nini fedha zilizorejeshwa zimepelekwa kwenye kilimo? Si inaitwa kagoda agriculture?
Asante MMKJJ, kwa mujibu wa mtoaji habari wangu, aliyerudisha fedha za Kagoda sio Manji, mtoa habari huyo aliidefendi Kagoda kuwa kama ni fedha fedha za Kagoda zilitumika kufanikisha uchaguzi wa CCM, mtoa habari huyo akaniuliza sasa hawa Kagoda walipata wapi hiyo bilioni 40 iliyorudishwa!.
Kwa maoni yangu, ni kweli Kagoda alichota hizo bilioni 40 pia ni kweli ndizo zilizoibeba CCM na JK wake. Ila haijarudishwa hata senti 5, bali paperwork imefanyika kuonyesha pesa imerudishwa. Wahusika wote wakuu wanalijua hili, ndio maana wanampigia magoti all the time.
Sitta ilikuwa ang'olewe, amenusuriwa sio kwa sababu anakubalika, bali kuondoa uwezekano wa kumeguka na pande kubwa, but his days are numbered na jamaa atahit back big blow baada ya bunge kuvunjwa Ijumaa ya Agosti 6, 2010.
 
Kagoda alias Rostam Aziz ni sterling hata movie ikiisha yeye bado atakuwa kasimama. Pale Ikulu tuna njemba lakini mwenye madaraka zaidi ni Kagoda 'aka' RA huyu ataendelea kula kuku zake bila kuguswa na yeyote yule.
Jamaa he is indeed a king maker, ukiona wabunge wanavyomyenyekea hapa bungeni Dodoma utafikiri ni kimungu fulani. Niko nae hoteli moja, jamaa hupenda kukaa nje open air, basi si foloni hizo, mabalozi wa EU wako hapa Dodoma nao pia wamepiga magoti to show respect
This man bwana.. wee mwache tuu, nakuambia Six ataanguka na EL atarudi juu.
 
Hivi ile kamati ya kuchunguza EPA tiyari imemaliza kazi?
kwani watuhumiwa ndo wameibukia kwenye tenda za matrekta.
Sina imani na Kilimo Kwanza tokea yule mtuhumiwa wa EPA
kuteuliwa na mkulu kwenda TIB.
Usikute mteuzi mwenyewe ndiyo huyo huyo king maker, JK kazi kutangaza tuu.
 
Swali zuri
Lazima tutafsiri wezi, mwizi ni nani, na sifa zake ni zipi. Mwenye mamlaka kisheria kutangaza nani ni mwizi nani si mwizi kwa mujibu wa katiba ni mahakama pekee, kinyume cha hapo zinabaki kuwa ni tuhuma tuu.
Kagoda kachota bilioni 40, hakutumia hati bandia, hakufoji chochote na aliyepitisha dondoo la Kagoda na kuidhinisha malipo ni Mama Meghji baada ya kuridhika ni fedha za UWT kufanyia kazi nyeti. Pesa zikatoka wameiba vipi?.

Hiyo kazi nyeti ni pamoja na kuingiza kontena 4 40ft za scalf, fulana na kofia toka Chini, TRA ilizizuia bandarini mpaka zilipiwe kodi, oda ikatoka juu zikapita. Hivi jamani kugawa fulana, kofia na scalf kwa wananchi ili wakichague Chama cha Mapinduzi sio kazi nyeti?.

JK kachaguliwa kwa kazi nzuri iliyofanywa na Kagoda, sasa kaiba wapi?.

Haya baada ya hiyo kazi nzuri, paper work imefanyika vizuri kuthibitisha fedha zimerudishwa, sasa Kagoda hadaiwi, tatizo liko wapi?.
Ndio maana nimesema Kagoda is as clean as CCM itself, hawa wanaotaka kukichafua chama kwa kisingizio cha kupiga vita ufisadi, ndio watasafishwa ili kusafisha njia kwa 2015 atakaporejea mwana mfalme.
 
Jamco_Za tatizo letu watanzania hatutaki kuthubutu. Uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita wengi wetu kwa sababu tuna means of living hatujishughulishi na vitu kama hivyo kwa kisingizio cha kuwa busy pasipo kujua kuwa serikali inaanzia mtaani na kama viongozi wa mtaani ni wabovu ni wazi kwamba hata huko juu watakuwa wabovu maana mbinu za uchafu zinaanzia mtaani. Hebu tuwe serious na kugrab opportunities kama hizi ili kwamba hao wabovu watakaotaka kuingia huko juu wakose mwanya kwenye ngazi za mtaa na mashina. Hebu fikiria unanunua kiwanja au property lazima upite kwa kiongozi wa mtaa akugongee mihuri. Hii ina maana pasipo yeye wewe huwezi kufanya chochote. Indirectly yeye ndiye rais wa mtaa. Wasomi hebu tujifunze katika hili la serikali za mtaa ili next year tuweze kujitokeza kwa wingi na kugombea nafasi za udiwani na kuendelea. Naamini kwa kufanya hivyo hutaweza kurubuniwa na kanga au tshirt maana uongozi wako si wa kuganga njaa kama ambavyo tumeaacha wenyeviti wa serikali katika uchaguzi uliopita ambao wengi wao ni watu wasiokuwa na ajira na upeo mdogo wa kuchambua mambo.
 
Sasa macho yangu yamefunguka kwani nilikuwa najiuliza Rai walikuwa wanaikandia kauri ya kilimo kwanza na kusema inatokea South Africa na Muasisi wake ni Nelson Mandela Rais msitafu wa SA, kumbe wanajaribu kuamisha concentration kutoka kwa kagoda Ltd na kuipeleka SA.

Hapa kama hatuko macho mapesa yaliyorudishwa yote yanarudi kwa manji kwa kauri mbiu ya kilimo kwanza kwani kagoda inajishugulisha na kilimo hata wakipewa tutaambiwa tenda ilitangazwa wakashinda wakapewa mapesa hayo.

Hivi sisi watanzania tumerogwa au, na kama tumerogwa basi aliyeturoga ameshakufa hata dawa hatutaipata.

Hivi wanaboard niambieni mbona sioni chama kilichoserious katika kutetea haki za watz, wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa, mtaani kwetu chama cha upinzani kilikuwa CUF tu na walisimamisha mtu ambaye kwangu mimi nasema hafai kulingana na quality za uongozi na ndio kilichotokea wakashindwa vibaya sana.

Sasa tutawezaje kusimamisha ujinga wa CCM bila kuwa na uongozi mbadala wa kutusaidia?

Jamco_Za; Tunachotofautiana na viongozi ni ule uwezo wao wa kuona mbele kuliko wale wanaoongozwa hiyo ndio tofauti iliyopo, sasa shida inakuja ni pale kiongozi anapokuwa fisadi na mzandiki, maana anachokiona yeye huko mbele badala ya kutuongoza kwa faida yetu wote wao wanatungoza kwa faida yao.

Hivyo huenda ni sahihi (Sina uhakika) hii kauli mbiu ya kilimo kwanza ilitengenezwa ili kukidhi ufisadi wa walio mbele, kutufumba macho sisi wadanganyika.

Swala la kulogwa kwa wadanganyika huenda ni kweli lakini bado naamini sio wote waliorogwa wapo ambao hawajarogwa ipo siku watatukomboa kwa faida ya wote.
 
.
Haiwezi kuwaondoa madarakani kama ni dhambi hii hii ndiyo iliyowaweka madarakani, wataitumia kuhakikisha wanatawala milele.

Kama alivyosema Kambarage "UKISHAKULA NYAMA YA MTU[BINADAMU] HUWEZI KUACHA" na hawa mafisadi watabuni EPA nyingine ya kuwavusha 2010 kama sio KILIMO KWANZA basi itakuwa MRADI WA VITAMBULISHO!!
 
Lazima tutafsiri wezi, mwizi ni nani, na sifa zake ni zipi. Mwenye mamlaka kisheria kutangaza nani ni mwizi nani si mwizi kwa mujibu wa katiba ni mahakama pekee, kinyume cha hapo zinabaki kuwa ni tuhuma tuu.
Kagoda kachota bilioni 40, hakutumia hati bandia, hakufoji chochote na aliyepitisha dondoo la Kagoda na kuidhinisha malipo ni Mama Meghji baada ya kuridhika ni fedha za UWT kufanyia kazi nyeti. Pesa zikatoka wameiba vipi?.

Hiyo kazi nyeti ni pamoja na kuingiza kontena 4 40ft za scalf, fulana na kofia toka Chini, TRA ilizizuia bandarini mpaka zilipiwe kodi, oda ikatoka juu zikapita. Hivi jamani kugawa fulana, kofia na scalf kwa wananchi ili wakichague Chama cha Mapinduzi sio kazi nyeti?.

JK kachaguliwa kwa kazi nzuri iliyofanywa na Kagoda, sasa kaiba wapi?.

Haya baada ya hiyo kazi nzuri, paper work imefanyika vizuri kuthibitisha fedha zimerudishwa, sasa Kagoda hadaiwi, tatizo liko wapi?.
Ndio maana nimesema Kagoda is as clean as CCM itself, hawa wanaotaka kukichafua chama kwa kisingizio cha kupiga vita ufisadi, ndio watasafishwa ili kusafisha njia kwa 2015 atakaporejea mwana mfalme.
Pasco mkuu, maneno yako nimeyasoma kwa uchungu mkuu sana. Sasa naanza kuamini yale yaliyosemwa humu jamvini siku za nyuma kuwa NCHI YETU IMELAANIWA. Iweje haya yote yanafahamika na hakuna linalofanyika?
 
Kagoda agriculture then imekuja kilimo kwanza???1!!,then Jeetu patel tenda ya kuleta matrekta,kwanini wasipewe jfang amabo wanayauza hapa nchini tayari tutumie midle man?yale yalee ya radar!then kuna kiumbe huku kasema matreka ni msaada toka India bil50.sasa hapa mimi napatwa kizunguzungu,hii sio coincidence CCM wana jambo hapa tena siri nzito,manji mihela mingi pia fungamano na ra,na mkuu wa kaya yupo tu either ndani ya racket au nje anafungwa mdomo sifahamu!!
 
Ni kweli kabisa hakuna mtuhumiwa wa kupelekwa mbele ya sheria? Basi hata Liyumba naye apewe uhuru wake maana atakuwa anaonewa
 
Mhh! karudisha bilioni 40? Kwa nini asirudisha na riba? Kwani amekaa na pesa hizo kwa Muda gani na alizifanyia nini kama si kupata faida? Basi angeweka na interest! Lakini yote ni bure kwani kesi ya nyani itasililizwa vipi na Kima?

Tukubali imekula kwetu!
 
Back
Top Bottom