Kafulila afichua siri za watumishi - kuna wanaolipwa 20,000,000/= kwa mwezi

Msiwaonee hao wanaolipwa mapesa mengi wako kwenye eneo la income generation centre ya serikali wanaizalishia serikali mabilioni ya pesa kama gawio kwa serikali na kodi walipazo na mapato ya kodi ambayo ndiyo yatumikayo kulipa hiyo mishahara kwa watu ambao wako katika sekta ya matumizi tu (expenditure only sector) kama wabunge.wafanyakazi wa serikali n.k

Dunia nzima watu wanao-generate mapato wanalipwa sana iwe kampuni binafsi au serikali.Watu kama wa marketing au wale washughulikao na mauzo au dealing kwenye mabenki binafsi, makampuni ya simu na makampuni ya mafuta kwa mfano hapa nchini mishahara yao na bonus inapita kwa mbali hata ya huyo gavana na huyo wa NSSF.Hivi huyo kafulila anaiingizia serikali mapato ya shiliingi ngapi na hao wabunge na madaktari wanaiingizia serikali shilingi ngapi? Sana sana hao madaktari wanaitia hasara serikali sasa hivi serikali kwa kusababisha vifo vya walipa kodi mawodini na kusababisha mapato ya serikali kutokana na marehemu hao kupungua

Tusiwachokonoe hao watu wanaozalisha mabilioni ya pesa za kuingiza serikalini.Hakuna kazi ngumu duniani kama kuzaalisha mapato(Income).Hao wasipolipwa vizuri wakakata tamaa janga litaibuka la kitaifa hizo posho wabunge wanazollilia zitashushwa Kaangalie vitabu vya mahesabu vya makampuni ya hao wanaolipwa sana yakiwemo bandari,BOT,TRA n.k utagundua kuwa ukiangalia wanachoiingizia serikali na wanachopata wala haviendani kabisa.

Mwisho Kafulila bado kijana kama anaona ubunge haulipi anayo nafasi ya kubadilisha fani asome hasa aende huko anakoona kunalipa kama BOT,TRA,NSSF N.K .Mishahara ndivyo itakiwavyo kuwa mzalishaji mapato anatakiwa alipwe zaidi ya mtumiaji.
Inaonekana nyumbani kwako pale meza ya chakula wewe unatengewa kuku na vitoto vyako vinahangaika na dagaa na maharagwe kila siku kwa vile tu wewe ni mleta mapato ya hapo nyumbani kwako. Na vile vile kwa sababu hiyohiyo unavaa nguo za dhamani kubwa na watoto wanatinga viraka... KULETA MAPATO HOME SI JUSTIFICATION YA KUKOSA UWIANO KATIKA KUGAWANA MAPATO.
 
Weye kafulila unatafuta beef nyingine! kwani hujui mishahara bongo ni siri kama mikataba ya uwekezaji ilivyo siri pia? shauri yako
Kama umeshawahi kusoma tangazo la kazi la serikali utagundua kuwa mishahara ya serikali siyo siri. Kama wasipotaja kiwango (x to y) basi watataja scale TG....
 
Hii picha ya wasira nzuri sana. Kwa nchi zingine inatosha kabisa mwenyewe kesho yake kujiuzulu kabla ya kumsumbua rais kukufuta kazi. Lakn tz wassira analala kila siku bungeni na bado eti anataka urais 2015
 
Hii picha ya wasira nzuri sana. Kwa nchi zingine inatosha kabisa mwenyewe kesho yake kujiuzulu kabla ya kumsumbua rais kukufuta kazi. Lakn tz wassira analala kila siku bungeni na bado eti anataka urais 2015

Shibe kwa sana, mazoezi ziro!
Pia hivi viti vinabembeleza sana wabunge wangekalia vigoda kwenye mjengo au mabenchi, wote wangekuwa atentive.
 
hivi mishahara ya wanasiasa inapaswa kuwa juu ya wataalamu hiyo nchi itakuwa inaelekea wapi?

kafulila kachemsha............mshahara siyo cheo ila ni tija............tija ya mbunge au waziri ni kiduchu ikilingaishwa na watendaji wataalamu.....................
 
Always narrow mind attack personality instead of issues!

Sure,
Nilitarajia memba mzoefu km yeye ajadili inequality za mishahara kama anavyodadavua Kafulila, lakini yeye kaweka chuki binafsi. Hizi tofauti za mishahara ndo zinaleta wizi katika mashirika na taasisi za umma.
 
serikali hii mishahara na posho na safari za nje inategemea wewe unafanya kazi wapi. haijalishi umesoma kwa kiwango kipi. kama uko kwenye Mamlaka za serikali zinazokusanya Mapato kama vile THA, TCRA, TCAA, TRA, SUMATRA, BOT mshahara wako ni mkubwa kuliko wa Daktari hata kama unapika Chai ofisini. kama hautaonyeshwa kwenye Pay Slip kuna posho nyingi tu za kuboost Mshahara wako. wako waliomaliza form4 wakaenda kozi miezi mitatu wanaitwa Proffessionals. mshahara kwa mwezi milion 3,5, 4 na safari za nje zenye kulipiwa na mamlaka kila mwezi . wenzetu wana mishahara Benki wasiyoitumia in terms of Billions. wanakula tu posho za Safari na za madaraka. Kila mwaka wa Serikali huongezwa mshahara na wanasema hautoshi wakati wengine hizo nyongeza za serikali ni ndoto. tumebaki kusema laiti na sisi tungekuwa wahasibu katika mamlaka za serikali kuliko kuwa mhasibu wa serikali Kuu. Daktari lazima mshahara wake uwe mdogo japo kasoma muda mrefu kwa sababu hakusanyi kodi wala mapato mengine. Piteni kwenye hzio mamlaka muone mishahara ya hao watu ndio mtajua nchi hii hakuna usawa ila kulipwa vizuri inategemea unafanya kazi wapi.
 
Tukumbuke kuwa mishara inayojadiliwa hapa ni mishara ya taasi za serikali/agencies. Ukitaka kuziangalia, hizi taasisi/mashirika yameanzishwa kisheria kwa ajili ya kuregulate masuala fulani either fedha, hifadhi za jamii, miindombinu, mawasiliano, biashara, afya nk. Hawa wanafanya kazi independently na central/local government. Hawa ni kama semi-government, wanajiamulia mambo yao wenyewe, including mishahara.
Sioni kama haya mashirika yanatakiwa yalaumiwe kwa kuwa na kiwango kikubwa cha mishahara cuz ni kutokana na majukumu na dhamana waliyoibeba. Ndani ya hayo mashirika kuna madaktari, waalimu, wahandisi, wahasibu na watu wa kila professional!
Chamuhumu hapa ni kuangalia serikali itainua vipi mishahara ya watumishi wake wa Central n Local government ireflect current state ya economy na mfumuko wa bei uliopo!

Wanatumia kodi zipi na hizo sheria zimetungwa nchi gani?. Chanzo cha mishahara yote ya watumishi wa umma ni hazina ambayo inawakamua maskini kwa kodi au michango ya hifadhi za jamii ambyo wanachama hawanufaiki nayo.

Tatizo ni ubinafsi ndio maana % kubwa ya waajiriwa kwenye hizo taasisi ni wenye majina yaliyowahi au yaliyomo kwenye siasa.

Swala la agency na porojo nyingine ni hoja nyepesi
 
Hatutaki kukubali wala kuamini kwamba Itikadi ndizo zinajenga msimamo wa chama na serikali, leo hii hatupo ktk Ujamaa wala hatupo ktk Ubepari na sii vyama wala wananchi wenyewe.

Hakika, yaani tupo tupo tu. Sasa tutumie nafasi hii ya uandishi wa katiba mpya kuamua itikadi kuu ya taifa na dola kwa ujumla.

MFUMO WA MALIPO YA MISHAHARA NA MARUPURUPU YA ENZI ZA SERA YA 'UJAMAA NA KUJITEGEMEA' INAPOLAZIMISHWA KUTUMIKA KATIKA KIPINDI KIPYA TAIFA LINAPOFUATA MFUMO WA 'UBEPARI NA NGUVU YA SOKO' JUMLA YAKE NI MIGOMO ISIOISHA NA KUKIMBIWA NA WATAALAM KUFAIDI UTANDAWAZI KWINGINEKO DUNIANI

Kweli mkuu. Halafu, tatizo ni kwamba, viongozi waandamizi wa serikali na mashirika ya umma wenyewe wanajipa mishahara ya kibepari, ilhali watumishi wengi wa kati na chini wa umma, wanalipwa mishahara ya kijamaa!!

CCM, ukweli wa mambo ni kwamba kiuhakika hatuwezi kuendelea hivi na mfumo wa zamani wa kulipana mishahara na marupurupu kama tulivyokua tukifanya enzi za sera za UJAMAA NA KUJITEGEMEA wakati santuri tayari tumeubadilisha wenyewe kupitia Azimio la Zanzibar.

Mkuu hilo santuri halijabadilishwa rasmi! Si unaona viongozi wetu wanavyoimba kijamaa, huku wakicheza kibepari?! Yaani hata wenyewe hawafahamu aina ya santuri inayopigwa!!

Kimsingi, haiwezekani wengine waonekane kufanya kazi ya kanisa hapa wakati wenzao wengine wanakula na kusaza wakati soko lao ni lile lile Kariakoo anakoenda mwalimu wa shule ya Msingi Hananasif kule Kinondoni na vivyo hivyo ndivyo afanyavyo mke wa Gavana wa BoT; tutaonan wabaya hapa!!!!!!!!!!

Hakika hili nalo ndilo jambo la kushangaza kabisa. Yaani mchanganyiko wa 'supermarket' na 'magenge' katika mtaa mmoja!!
Mke wa waziri anamtuma housegirl gengeni, na housegirl huyo anagongana na mlalahoi mmoja katika genge hilo hilo!! Wakati mwingine wawili hao ugongana na kupigana vikumbo wakati wa "special offer" za sikukuu kwenye "supermarket"!!!
 
Mh!! hii serikali si mchezo! Sijui tutadhulumiwa haki zetu hadi lini, mtumishi wa kada ya chini analipwa Tsh 135,000 kwa mwezi, Gavana analipwa Tzs 20,000,000/= na hawa wote wanakwenda soko la aina moja. gavana nae ananunua sukari say tzs 2,000 na huyu mtumishi (135,000) nae bei ni hiyohiyo! Hivi hili gap kati ya HAVES and HAVE NOTS tutafika kweli! our gvt must be serious!
 
Sasa kama vigogo hawa wanalipwa mishahara minono kiasi hiki bado wanaiba. Kuna sababu gani kuwalipa mishahara mikubwa kama haiwaondolei tamaa ya kuiba na wala hatuoni tija ya maana itokanayo na malipo hayo manono?
 
Huyu kashapotea...sina hata hamu ya kumsikiliza!!
Rejao, politics aside, are you saying you are ok with the way allowances are paid to these people? Kama uko ok nayo, basi una problem kubwa. The guy is not saying anything against the CCM system that you seem to like so much, but he is questioning the fairness of the system. Sasa kama una problem na hiyo, basi unayo kasoro kwenye thinking yako!
 
Tukumbuke kuwa mishara inayojadiliwa hapa ni mishara ya taasi za serikali/agencies. Ukitaka kuziangalia, hizi taasisi/mashirika yameanzishwa kisheria kwa ajili ya kuregulate masuala fulani either fedha, hifadhi za jamii, miindombinu, mawasiliano, biashara, afya nk. Hawa wanafanya kazi independently na central/local government. Hawa ni kama semi-government, wanajiamulia mambo yao wenyewe, including mishahara.
Sioni kama haya mashirika yanatakiwa yalaumiwe kwa kuwa na kiwango kikubwa cha mishahara cuz ni kutokana na majukumu na dhamana waliyoibeba. Ndani ya hayo mashirika kuna madaktari, waalimu, wahandisi, wahasibu na watu wa kila professional!

Chamuhumu hapa ni kuangalia serikali itainua vipi mishahara ya watumishi wake wa Central n Local government ireflect current state ya economy na mfumuko wa bei uliopo!

:frusty::frusty::frusty::nono::nono::nono::nono::high5::high5:
 
Ni sahihi kabisa hata walipwe mil 30 huwezi ukafananisha utendaji wa afisa BOT na daktari jaribuni kuheshimu fani za watu
 
Back
Top Bottom