KAFULILA aeleze alipata wapi Shahada ya "BBA" na Mwaka gani

hivi hawa wabunge hawasubmit vyeti vyao bungeni kabla ya kupost profile zao?hii inaweza kuleta aibu.
 
udsm hakuna hyo course ya BBA labda km diploma,angalieni course zinazotolewa pale UDBS hiyo course haipo. Nipo pale huu ni mwaka wng wa 3 huo ni uzushi. Hyo course ipo RUCO,TUMAINI,St.JOHN na CBE.

kuwepo kwako hapo si kwamba unajua kila kitu kinachotokea au kufanyika hapo.
 
Hebu niwekeni sawa wana JF, hapa tunajadili elimu tuu au na sifa za kuwa mbunge?? Mbunge kiwango change cha usomi ni kipi?
Kama ni just Elimu yake, no comment, ila kama ni elimu yake na uhusiano na ubunge wake, i think STD Vii wapo na Form four poor wapo,
I am blind sometimes

Mageuzi

1. Hawa ndo wanakaa kwenye kamati kujadili budget kabla hatujaletewa na wanai-discuss on our behalf

2. Hawa ndo wanapitisha miswada na kutunga sheria na sera

3. Hawa ni mawaziri watarajiwa.....anytime aweza kuteuliwa kama itamridhisha mteuaji

Kama tunawekeza kwenye elimu kwa level ya kata ni wazi kuwa tunalubali na kutekelza kwa matendo kwamba elimu ni sehemu ya maendeleo. If so mwenye elimu ni more likely kuenedelea yeye na kuendeleza wenzake thus hawa ni muhimu sana kwao kuwa wameelimika kuendana na zama hizi tunazoishi na si kwa mujibu wa katiba
 
tuletea mambo ya maana hapa kama hajasoma si akasome? Madam anayo division 3 ya form 6.anasifa na pesa anayo
nami pia ni form four lakini nina mpango wa kusoma diploma, na nimeamua kuiandika kwenye cv yangu sasa ili iwe inatumika hadi hapo nitakapoimaliza rasmi!

 
Ukiwa mwanasiasa lazima ufuatiliwe, kama waliweka kwa bahati mbaya kwenye website ya bunge basi wafanye marekebisho.
 
Ninachojua ni kuwa alidisco mwaka wa pili na siyo kufukuzwa ila ana uwezo mkubwa kuliko wenye vyeti vya PhD
 
msemakweli tulimpongeza sana kulipua vigogo wa CCM wenye vyeti bandia lakini Malagarasi hatutaki kumpongeza pengine kafulila naye ana vyeti bandia na amefanya hivyo kwa sababu anajua sifa ya kuwa mbunge ni kusoma na kuandika kwa hiyo elimu ya juu sana si ya kuhoji sana ni kama added advantage

Mkuu kagonge kwanza kikombe kimoja cha kahawa kisha urudi jamvini. Nahisi you are so tied, kwa sababu kinachobishaniwa hapa siyo suala la kuwa na elim kubwa kama kwalification ya kuwa mp au post yeyote ile. Hoja kuu hapa ni kwamba Kafulila kalidanganya bunge kwa kuainisha kuwa ana education status kwa level ya BBA. Kinachotafutwa kwa Kafulila ni kudhibitisha kuwa hakudanganya au akiri kuwa alidanganya, watu warisike na maisha yaendelee mbele. Sawa kaka?
 
nadhani kama kafulila alikuwa UDSM akafukuzwa kwa migomo, bado anahaki ya kutuambia aliaanza wakati huo huko nyuma, ila kama ali-disco hilo ni tatozo jingine
 
Inamaaana wakati david kafulila anasoma hiyo bba hakuna watu walio mwona anasoma/classmates?
 
jamaa si angekomaa tu aikamate hiyo BBA.Matatizo yameanza sasa.Hivi inawezekana kwa Tanzania,mbunge kuvuliwa ubunge kwa kosa la kudanganya elimu yake?

Na bora iwe hivyo. kiongozi kudanganya danganya iwe mwiko. Hii iende hadi kwenye ahadi kipindi cha kampeni. kwanza sijui kwa nini wanaahidi.
 
Ni kweli, Kafulila aliagirisha Masomo mwaka 2008, ila kwa mujibu wa tovuti ya Bunge inaonyesha alisoma mwaka 2006 mpaka 2008 ni ni graduate, huo ni uwongo!

Angalia update za tovuti ya bunge utaelewa
 
2006-08 ni miaka miwili, alipata vip hii shahada wakati hutolewa miaka 3.mwenye meelezo mazuri aweke maana CV hii inaonekana kuchakachuliwa

acha ujinga wewe, hiyo inamaanisha hiyo shahada hakuimaliza alisitisha hapo ndo ikaendelea tena.
Hivi watu wajinga wanatoka wapi humu jf, yani watz tunauvivu mpaka wa kufikiri, loh!
 
Ninachojua ni kuwa alidisco mwaka wa pili na siyo kufukuzwa ila ana uwezo mkubwa kuliko wenye vyeti vya PhD

We Jinga!! Hakudisco, alisimamishwa kwa sababu ya ada, mbona hamsomi nyie watu mnabwabwaja tuu
 
[mimi nadhani suala la kafulila ni too personal.wewe kama wewe huitaji kutuambia kwamba ana elimu gani.kama bunge lina kumbukumbu kuwa ni graduate wewe unaumia kiasi gani?kama sikosei hata karo hukumlipia wewe elimu yake inakuhusu?let us discuss burning issues prevailing in our country.we do have so many things to discuss.mcolor="#00ff00"][/color]
 
Bado ninsistiza, atueleze aliipata wapi na vyeti vyake vipo wapi? inaeleweka kuwa mpo wapenzi wa kafulila ambao mliwahi kuwashikia bango mawazili kadhaa kuwa ni mafisadi wa elimu, tunamtaka na jamaa yenu atueleze alisoma na kupata wapi shahada yake ya kwanza katika BBA na siyo kuja kubwabwaja? Atueleze, amezoea kusema uwongo sasa amekamatwa pabaya waziwazi, ktk hili hawezi kukwepa, akanunue vyeti udsm tuone kama anaweza. Aliipata wapi shahada yake? Umma unataka kujua, siyo kusema sema uongo halafu adhani hatujui


Kama elimu yake ndogo na amenunua vyeti hebu tupe vya kwako kwanza ambavyo ni orijino. Kafulila kaelimika mavyeti ya nini
 
SalutationHonourableMember picture
1688.jpg
First Name: David
Middle Name: Zacharia
Last Name:Kafulila
Member Type:Constituency Member
Constituent: Kigoma Kusini
Political Party: NCCR-MAGEUZI
Office Location: Box 22 Uvinza, Kigoma
Office Phone: +255 716 426220
Ext.:
Office Fax:
Office E-mail: dkafulila@parliament.go.tz
Member Status: Current Member
Start date:
End date:
Date of Birth 15 February 1982
EDUCATIONS
School Name/Location Course/Degree/Award Start DateEnd DateLevel
Uvinza Primary SchoolPrimary Education19911996PRIMARY
Kiganamo Primary School, KasuluPrimary Education19971997PRIMARY
Chumvi Secondary School, UvinzaO-Level Education19982001SECONDARY
Shinyanga Secondary SchoolA-Level Education20022004HIGH SCHOOL
National Democratic Institution (NDI)-20092009CERTIFICATE
Fedrick Elbert Stiftung (Foundation) FES-20072007CERTIFICATE
University of Dar Es SalaamBBA20112013NOT COMPLETED
University of Dar es SalaamBBA20062008
CERTIFICATIONS
Certification Name or TypeCertification No. IssuedExpires
No items on list
EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From DateTo Date
The Parliament of TanzaniaMember - Kigoma South Constituency20102015
NCCR-MageuziDirector20092010
MRDDirector20092010
POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position FromTo
NCCR-MageuziParty Secretary General2009
CHADEMAInformation Officer2008
CHADEMAInformation Officer - Youth 2007
PUBLICATIONS
Description Published Date
No items on list
SPECIAL SKILLS
Skill Name or Description Years Experience Acquired Through Skill Level
No items on list
RECOGNITIONS
Recognition Type Recognition DateReasonAction TakenIssued by
No items on list
 
tunataka atueleze aliipata wapi? hata machali ana haki ya kuhoji iwapo anaelewa kuwa kafulila kalidanganya bunge kuhusu elimu yake?hoja ya msingi ni kafulila atueleze alisoma wapi na lini? kwa kuwa ni kfulila maneno kama ya chuki yameanza,ila kwa lukuvi, nchimbi,mkulo wakihojiwa elimu zao na kuitwa mafisadi wa elimu safi. Atueleze ilipata wapi hiyo BBA

Mkuu, kwanza nikupe pole kwa kupandishwa hasira kwa ufisadi wa inayosemekana elimu ya Mhe. Kafulila.
Labda nianze kwa kukuuliza, kwa elimu yake ya kidato cha sita, anastahili kuwa mbunge?
Swala la pili ni, je huko katika chama chenu (NCCR, I presume), wakati wanachama wanapowasilisha maombi ya kuomba kuteuliwa kugombea ubunge, huwa hamuwaagizi wagombea kuthibitisha viwango vyao vya elimu kwa kuonesha walau nakala za vyeti vyao?
Kama haupo utaratibu huo basi uanzisheni, kuliko kutuletea zogo hili hapa Jf na kufanya wanajamii kuacha kujadili mada za maana na kuipitia mada kama ya kwako.
 
Back
Top Bottom