kasyabone tall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2009
- 254
- 59
Habari nilizo nazo ni kuwa kadi mpya za kupigia kura Tarehe 31-10-2010, bado zinatolewa kwa wapiga kura ambao sio rasmi( ambao hawatambuliwi na NEC). Lakini pia kuna tatizo kubwa sana,watu waliojiandikisha katika kituo kimoja na kufanya marekebisho ya kujiandisha upya sehemu nyingine alizohamia, majina yao yametokea sehemu zote mbili. Licha ya kasoro hizo kutokea, bado kadi mpya zinatolewa na bila shaka ni hayo majina ambayo yanatokea sehemu mbili. Je kwingineko hilo jambo likoje?
Wale waliojiandikisha na wakabadili vituo waangalie majina yao kule walikokuwa wamejiaandikisha awali. Pia wafanye uchunguzi wa kina juu ya kutolewa kadi mpya za kupigia kura kipindi hiki katika maeneo yao, japo zatolewa kwa siri mno.
Wale waliojiandikisha na wakabadili vituo waangalie majina yao kule walikokuwa wamejiaandikisha awali. Pia wafanye uchunguzi wa kina juu ya kutolewa kadi mpya za kupigia kura kipindi hiki katika maeneo yao, japo zatolewa kwa siri mno.