Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,110
Leo bungeni mhe.Mwigulu Nchemba amemkumbusha Speaker kuhusu JJ Mnyika kuwasilisha ushahidi vile alimtuhumu kwamba alishiriki kwa namna moja ama nyingine katika ufisadi wa EPA. Kumekuwa na nadharia kwamba Mhe.Nchemba hakuhusika kwakuwa alianza kazi baada ya ufisadi kutokea.Namtaka Mwigulu Nchemba awaeleze Watanzania yafuatayo: 1.Kwa kuwa M/kiti wa chama chake aliwahi kukiri kwamba,fedha za EPA zilikuwa zinarudisha je,aliwajua wale waliokuwa wanarudisha? 2.Kama alikuwa hajui, je yuko tayari kukiri kwa Watanzania kwamba ana nidhamu ya uoga kwani hata pale aliposikia,hakuumuliza mwenyekiti wake wa chama? 3.Kwa kuwa Nchemba anadai hakuhusika,lakini yeye ndiye mtunza hazina wa chama cha mapinduzi ambacho M/kiti wake Rais Kikwete alikiri urudishwaji wa mali,sasa ni kwa kadri gani hakushiriki kutunza hazina za kifisadi- kwa kujua ama kutokujua? 4.Aliwasaidiaje maofisa wa TAKUKURU ili wapate ushahidi akiwa kama raia mwema?