abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
http://www.mzalendo.net/habari/jee-...badala-ya-makambi-yote-kujaa-wakuria#comments
Jee nikwa nini tusiwe na vijana wetu wenyewe ktk JWTZ Zbar Badala ya makambi yote kujaa Wakuria?
Mimi nahisi hii ndio kutawaliwa ki-Jeshi na watu tusio wafahamu wala wasio na asili ya Zanzibar. Haingii akilini kuwa makambi yote ya kijeshi yalio inezwa mitaani Zanzibar ukiangalia yamerundikana wanajeshi wa kigeni Wasio na baba,babu dada wala kaka Zanzibar jee tunategemea nini upepo ukibadilika.
Hii ni hatari tena kama Baraza letu BLW halikusikiliza kilio chetu basi hata wao iko siku watajuta, Hawa wanaweza kuja kufanya vitimbi na sisi Wzanzibar na viongozi wetu tukajitafuta. Nisawa na msemo usemao zimwi likujualo halikuli likakwisha? lakini jee hawa ni Mazimwi wenye kutujuwa? jee ingekuwa kuna vijana wetu ktk makambi si tungeona tuna home boys wetu ktk territory yao?.
Kwanza ktk Jeshi la JWTZ lina ubaguzi mkubwa, huwezi kupata nafasi ya Jeshi kama ni Mzanzibar mwenye asili ya kihindi,kiarabu,kingazija na hata ukiwa mweusi basi asili yako iwe imetokea Bara nitabu kuona mtu mweusi baba mama ni Mzanzibar na kuwa ktk Jeshi la JWTZ a.).
B.) Ukiwa Mzanzibar ktk Jeshi la JWTZ basi huekwi Zanzibar unatupwa Bara tena Mikowani ili uwe mbali na Zanzibar kabisa, jee hii si mbinu ya kutawaliwa sisi kijeshi Zanzanzibar?. kwani kuna kosa gani la kuwa kambi za kijeshi Zanzibar kusimamiwa na Wzanzibar wenyewe na kuwa na vijana wetu wenyewe kulinda nchi yao?.
Mimi na hisi hivi sasa nilazima makambi ya Jeshi yasimamiwe na vijana wetu sio kuletewa Sura za Tanganyika kujazwa katika makambi lengo ni nini? tuseme ccm/smz hawajiamini kwa raia wao? lakini wajuwe tu kuwa upepo unaweza kuwageukia wao smz na wakishapewa amri hata Raisi wa Watu wa Zanzibar Dr Shein wampeleke kinguvu Bara basi hawajali wanampeleka.
Mimi huona ushungu sana kumuona Raisi wetu siku za Sherehe za mapinduzi ya Zanzibar January 12 kukaguwa vikosi vya JWTZ ukiangalia hizo sura zenyewe ni Wakuria watupu, hii ni aibu kwa ulimwengu mzima kuwa vijana wetu tunao lakini tumeleta wageni kuwa wanajeshi ni (sad & shame).
Bado tu smz hamuja soma? niasari ngapi hutuletea hawa Wakuria Zanzibar kuna kipindi kulichamiri wizi wakutumia silaha na ktk uchunguzi ilionekana JWTZ wanashiriki kikamilifu kufanya ujambazi huu, kuna mara ngapi vilikuwa vikikamatwa vitu tv,mafrege,pikipiki vyawizi vimo ktk meli lao la kijeshi lile la Kasa vikisafirichwa kupelekwa Bara?.
Hawa ni majambazi na tunawalea wenyewe na ndio ukaona hata wakati wa uchaguzi hugeuka na kuonyecha rangi zao za unyama ku-rape na kufanya mambo mengi tu yakinyama ktk jamii ya kizanzibar na hufanya hivi kwa kuwa hawana damu yao hapa.
Lakini vijana wetu sizani kuwa wanaweza kufanya unyama huu kwa ndugu zao, wahame bwana kwanza vipi kambi zijengwe mitaani au na sisi tunataka tutokezewe na mabomu ya Gongolabota? kawaida ya majeshi ulimwenguni hukaa mipagani sio mitaani kama hawa, lakini hawa hawalindi ulinzi wa mipaka wanalinda itikati za chama na kututawala kijeshi. mungu ibariki nchi yetu Zanzibar.