Jussa: Tanganyika kama hamtaki Muungano semeni Tugawane mbao hata sisi tumechoka, ya Bandari yenu sisi hayatuhusu!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,036
142,123


Kaimu Kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo Jussa amesema Tanganyika suala dogo tu la Bandari kelele kila kona wakati wao wameipora Zanzibar vitu kibao kuanzia 1964

Jussa amesema Zanzibar Ilikuwa na Polisi wake, Ilikuwa na Jeshi lake, Ilikuwa na Passport, Ilikuwa na Mabalozi, Ilikuwa na fedha yake, Ilikuwa na Kiti UN na mambo mengine chungu nzima lakini yote yameporwa na Tanganyika

Jussa amesema suala la Bandari wao Zanzibar haliwahusu so Watanganyika wapambane na hali zao

Jussa ameonya wanaozungumzia kuvunja Muungano kwamba wao wako tayari hata kesho wameshachoka

Jussa alikuwa akihutubia Mkutano wa hadhara huko Puja Zanzibar uliohudhuriwa na Makamu wa kwanza wa Rais Masoud Othman

Mlale unono!
 
Ameona dada yake anaiuza Tanganyika kwa nduguze kwa vipande vya fedha ameanza mipasho siyo?

Siku inakuja imani yangu hili halitapita salama ipo siku tutaona wapemba wakitamani kupiga mbizi kurudi kwao Pemba!muungano hauna chochote kinachomnufaisha Mtanganyika ukweli ni huo.
 
Hata Tanganyika ilikuwa na hivyo vyote anavyovisema. Kwanza Zanzibar ndiyo inaitawala Tanganyika ambayo imeuwawa na muungano.

Huu muungano wa kimaghumashi sana. Hata hao kina Jussa nahisi ni mamluki wanaotumiwa kulalamika uongo ili tuone kwamba wao ndo wenye shida. Na hii ilianzia kwa Maalim Seif na mwalimu Nyerere.

Muungano ni wa kinyonyaji kwa Tanganyika. Zanzibar bado ipo na inainyonya Tanganyika. Na pia kuitawala.
 
Zanzibar ni kakisiwa kadogo, ila wakazi wake wana vishindo kweli!!! Kwenye kuchongoa midomo ndio usiseme!!!

Zanzibar kama inavunja muungano, ina uwezo gani kuwa na jeshi lake?
Yaani na wakiwa nje ya nchi wanajiita wa Zanzibar, na wana chama chao cha kijamii,Wazanzibari waiishio ....jina la mji husika huko nje mji wowote/nchi yeyote waliopo.
 
Back
Top Bottom