Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,654
- 41,323
Mimi sijawahi kuusikia hata huo ushawishi unaopambwa hapa. Kama kweli anao basi aanze kuufanya huko CCM maana hatujawahi kuuona. Juliana kama amerudi nyumbani sidhani kama amefanya kosa. Juliana kama mpiganaji wa CCM alitumwa vitani, amejeruhiwa na hana uwezo wa kupigana tena, ni sharti na ni busara CCM kumchukua na kumpokea vizuri mtu wao maana maana hata kama kwenye uwanja wa vita hakufanikiwa lakini ameumia akiwa kazini.
Nashangazwa na harakati na matusi yanayoendelezwa dhidi ya huyu mwana dada shupavu juliana shonza kisa kutoka chadema na kujiunga ccm. Alikiri mbele ya sekretariati ya ccm kuwa aliipenda chadema kwa dhati lakini amenyanyaswa na kufikiria mara mbili kuendelea kubaki chadema. Akasema yeye bado ni kijana na anaipenda nchi yake na anapenda siasa akafikiria njia nyinginr ya kuwasaidia watanzania kisiasa akaona ccm ndiyo chama kinachoweza kuishi na watu wa namna zote bila kujali tofauti. Sasa kumwita delila nyoka msaliti nadhani ni kufika mbali. Hata kama atazunguka nchi nzima si mpingane naye kwa hoja?? Sioni haja ya hofu. Nadhani katika makala yangu mjoa niliandika hapa kuhusu msimamo wa baadhi ya wasomi wanaomfahamu huyu msichana nao walishangaa chadema kukosa uvumilivu na kumfukuza mtu mwenye uwezo na ushawishi kama juliana. Nadhani wengi wanasema chadema imetupa almasi. Kweli ana iq ya hali ya juu nadhani ilibidi apewe muda wa kusikilizwa kuliko kufukuzwa. Kama chadema ilimfukuza imuache aangalie ustaarabu kwa wengine. Kama atapanda jukwaani kuisema chadema basi inabidi ajibiwe kwa hoja na si kutukanwa kama wengi wa wachangiaji wanavyofanya. Kwanza hiyo inaonesha kuwa bado chadema wanampenda lakini zaidi ni kama wanataka kumwaribia huko alikokwenda asifanikiwe. Labda hili ni onyo kwa chama kuwa na uvumilivu.