Bunguabongo
Member
- Jan 12, 2011
- 27
- 22
Jukwaa la katiba limetoa tamko kuhusu tume ya Nchimbi. Tamko likisomwa na mwenyekiti wa jukwaa hilo limesema; "kwanza ile siyo tume ni kamati iliyoundwa na nchimbi, kamati hii haitambuliki. Jukwaa linamtaka RAISI aunde tume ya kuchunguza mauaji ya mwandishi DM. Nchimbi hawezi kuunda tume maana yeye, pamoja na IGP wake na jeshi lote la polisi linastahili kuchunguzwa. Jukwaa limeenda mbali zaidi kwa kuitaka tume itakayoundwa,baada ya uchunguzi kukamilika, ipeleke majibu Bungeni kwa ajiri ya kupata ushauri wa kibunge. Mwenyekiti alimalizia kwa kusema...hatudanganyiki!" Aidha jukwaa la katiba linaitaka serikari kutoa tamko la kuisaidia familia ya DM kuisaidia kwa muda wa miaka ishirini ili watoto wa marehemu mpaka wafikie umri wa kujitegemea. Kwa maoni yangu jukwaa limenena vizuri kabisa, kwa mujibu wa sheria na kwa kuangalia familia ya marehemu, mjane na watoto. source; Star TV, Habari ya saa nne asubuhi ya leo.