Inanambo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 3,985
- 2,770
Mwaka jana 2011 Staa wetu Joseph Shamba (Vengu) alikuwa anaumwa amelazwa hospitali ya MUHI2 na habari hizo nilizipata humu kwenye Jukwaa letu la Jamii Forum. tulimhurumia sana na kumwombea juu ya afya yake ili aweze kupona na kuendelea na kazi yake ya kuburudisha watanzania kwa vichekesho. Mwaka huu sijasikia habari zake kama maombi yetu yamejibiwa na yeye kupona au bado ni mgonjwa au ameshatwaliwa kama Mzee Kipara(Mungu amrehemu). Tafadhali mwenye taarifa za afya yake anijulishe. Natanguliza shukrani.