Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,924
- 30,272
JOHN KETO
HISTORIA YANGU KUHUSU ELIMU YANGU NA UZOEFU
KATIKA KAZI ZA KUJENGA TAIFA
(Kwa hisani ya Dr. Nzige)
Waliosimama wa nne kulia ni John Keto University of Edinburgh 1953
Nilizaliwa Misozwe katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga (wakati ule ukiitwa Jimbo la Tanga tarehe 15/08/1917.
Kwa kuwa baba yangu alikuwa mwalimu nilipata bahati ya ya kuanza elimu katika shule ya misheni ya U.M.C.A (University Mission to Central Africa)pale Misozwe mwaka 1922.
Baba alipohamia Magila Msalabani kwa ajili ya kusomea kazi ya ushemasi,ikabidi nihamie huko na kuendelea na masomo yangu ya shule ya msingi kwenye shule ya St. Martins (zamani ikiitwa Hemvumo).
Mwaka 1928 (baba wakati huo akiwa Padre) nilihamia shule ya central school kiwanda kwa kuwa baba alihamishiwa kutoka Magila kwenda kuwa Padre wa Mtaa wa Kizara.
Hapo kiwanda nilisoma na kupata cheti cha Territorial St x (central school leaving certificate) mwaka 1932; na mwaka uliof uata (1933) nilikwenda minaki kusomea kazi ya ualimu. Nilipokuwa hapo minaki nilisomea kwanza cheti cha ualimu wa grade I na kufaulu , mwaka huohuo nikajaribu mtihani wa kwenda Makerere na nikafaulu. Kwa hiyo badala ya kupelekwa kufundisha nilipata nafasi ya kuendelea na masomo zaidi ya Diploma in Educationb kule Makerere.
Mwaka 1940 nilifaulu kupata cheti change cha Diploma in Education pamoja na Cambridge School Certificate na kurudi Tanzania ili kuanza kazi yangu ya Ualimu.
Shule yangu ya kwanza kufundisha ni U.M.C.A Korogwe Middle School ambapo nilianzishwa St. VII. Nilifundishwa Korogwe kwa miaka miwili 1940 na 1941 nikiwa mwalimu mkuu, na mwaka 1942 nikahamishiwa kwenda kufundisha Minaki.
Wakati nikifundisha Minaki nilijiandikisha katika Woolssey Hall College ya London, Uingereza ili kupata masomo kwa njia ya Posta . Masomo hayo pamoja na cheti nilichopata cha London Matriculation ndivvyo vilivyoniwezesha kukuballiwa kupata Scholarship Ya British Council mwaka 1950 kwenda kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh, Scotland, Uingereza.
Huko Edinburgh nilisoma kwa miaka mitatu na kupata degree yangu ya M.A katika masomo yafuatayo:- Political Economy,Economy History,British History,Constitutional Law, Botanical Science,Moral Philosophy na English Literature. Mwaka 1954 nikarudi nyumbani na kwenda Minaki kuendelea kufundisha wakati huo nikiwa makamu wa mkuu wa chuo.
Niliporudi mwaka 1954 nilikuta chama cha siasa cha TANU (Tanganyika African National Union) kimekwisha kuanzishwa, kwa hiyo nikajiunga nacho na nikachaguliwa kuwa mwenyekiti wa Tawi la TANU Wilaya ya Kisarawe.
Nilijitahidi kuongoza TANU katika Uzaramo hadi mwaka 1958 wakati nilipoteuliwa na chama kuwa mgombea Mwafrika wa kiti cha ubunge wa Jimbo la Tanga. Nilifaulu na ikabidi kufanya shughuli za ubunge huku nikiendelea na kazi ya ya kufundisha Minaki, baada ya kuafikiana na mkuu wangu wa Chuo (Fr. Nash) kuwa itanilazimu kwenda Tanga ikiwa kkutakuwa na jambo lolote la kisiasa litakalonihitaji jimboni kwangu.
Kwa bahati mbaya kanuni za TANU hazikuruhusu mwanachama kupokea mshahara zaidi ya mmoja ikiimaanisha kuwa mtu kama mimi kupokea mshahara wa ualimu na malipo ya ubunge. Kwa hiyo ilipofika awamu ya pili ya uchaguzi mwaka 1960 sikuweza kugombea tena ubunge, kwa kuwa nilikataa kuacha kazi yangu ya ualimu kwa sababu ambazo nilimweleza Rais Nyerere na akanikubalia.
Mwaka 1961 tulipopata uhuru wetu Rais Nyerere aliniita ofisini kwake Dar es salaam akaniuliza kama niko tayari kwenda Dar es salaam ili kuwa mwenyekiti wa Public Service Commission. Nilimpa sababu zangu nilizopata kupampa huko nyuma zikiwamo uhaba wa walimu kwenye shule yangu ya Minaki, Yeye allinijibu kwamba atanisaidia kuondoa hilo tatizo kwa kutuletea walimu wawili wazungu badala yangu. Kwa hiyo tuliafikiana na nikahama kwenda Dar es Salaam.
Mfumo wa Huduma za pamoja za mawasilano wa Africa ya Mashariki ulipotengenezwa upya. Tanganyika ilipewa huduma ya Posta kwa hiyo mwaka 1964 Rais Nyerere alimtuma waziri Amir Jamal kuja kuniomba niende Nairobi kushika wadhifa wa Postmaster General wa Africa nilikuwa pia mwenyekiti wa kampuni ya Posta na Simu( Post & Telecommunicationb Company Ltd).
Mwaka 1969 baada ya kuundwa kwa Jumuiya ya Africa Mashariki 1967, Makao makuu ya Posta yalihamishwa kwenda Kampala Uganda, Ambako nilikaa mpaka nilipostaafu mwaka 1976 na kurudi nyumbani Tanzania.
Niliporudi nyumbani kwangu Korogwe, Kwamba mwaka 1977 nilikuta Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekwis ha kuanzishwa kwa hiyo nikajiunga na wanachama wengine wa kijiji katika kuhimiza vikao vya chama na kuendesha miradi ya siasa ya kujitegemea kwa mujibu wa miongozo ya Chama. Nilikuwa pia mwanachama wa ushirika wa uzalishaji mali vijijini.
Mwaka 1978 nikapata ujumbe kkutoka magila Muheza kuniomba nikawe mkuu wa Shule ya Hegongo (iliyoitwa Muheza Secondary School hapo awali) badala ya Mw. Stephene Mhando. Nilianzia kazi hiyo tarehe 1/06/1978 nikiwa 1985 nilipostaafu na kurudi Korogwe.
Kwa sasa nipo hapa Majengo nikiwa mwenyekiti wa sehemu ya Wazee wa CCM na mwanachama wa kikundi cha mradi wa kufuga nyuki wa TASAF.
Mungu Uibariki Afrika
Mungu Uibariki Tanzania
…………………..
Majengo Korogwe
10/05/2012
CURRICULUM VITAE
OF
MR. JOHN KETO
1. Date and place of Birth
Born on 15th August, 1917, at Misozwe in Muheza District of Tanga Region.
Married (now widow) with six children, two of them now dead
2. Education
i. At Kiwanda Central School and Minaki
Teacher Training College (1928 – 1937)
Awarded Grade II and Grade I Teachers Certificates
ii. At Makerere College, Uganda(1938 – 1940)
Awarded Cambridge school certificate and Diploma in Education
iii. At Edinburgh University, Scotlad (Oct 1950 – July 1954) awarded M.A degree in following subjects.
· Political History : Constitutional law
· Botanical Science: Moral Philosophy
· English Literature
3. Career
i. Teacher at Korogwe Middle School(1941)
ii. Teacher at Minaki (1942 to Sept 1950) and again 1954 to 1961
iii. Chairman Public Service Commission Tanzania 1961 – 1964
iv. Postmaster General, East Africa 1964 to 1968
v. Director General E.A.P and T. Corporation 1968 TO 1976
vi. Chairman E.A. External Telecoms 1964 to 1976
vii. Headmaster Hegongo Secondary School 1978 to 1985
4. Part Time Activities
a. Member of Council University College
Dar es Salaam
b. Member, East Africa (Swahili) Literature
c. Diwani Muheza and Korogwe District Council
d. Member of Legislative Council
Prepared by Mwalimu John Keto, Majengo Korogwe
HISTORIA YANGU KUHUSU ELIMU YANGU NA UZOEFU
KATIKA KAZI ZA KUJENGA TAIFA
(Kwa hisani ya Dr. Nzige)
Waliosimama wa nne kulia ni John Keto University of Edinburgh 1953
Nilizaliwa Misozwe katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga (wakati ule ukiitwa Jimbo la Tanga tarehe 15/08/1917.
Kwa kuwa baba yangu alikuwa mwalimu nilipata bahati ya ya kuanza elimu katika shule ya misheni ya U.M.C.A (University Mission to Central Africa)pale Misozwe mwaka 1922.
Baba alipohamia Magila Msalabani kwa ajili ya kusomea kazi ya ushemasi,ikabidi nihamie huko na kuendelea na masomo yangu ya shule ya msingi kwenye shule ya St. Martins (zamani ikiitwa Hemvumo).
Mwaka 1928 (baba wakati huo akiwa Padre) nilihamia shule ya central school kiwanda kwa kuwa baba alihamishiwa kutoka Magila kwenda kuwa Padre wa Mtaa wa Kizara.
Hapo kiwanda nilisoma na kupata cheti cha Territorial St x (central school leaving certificate) mwaka 1932; na mwaka uliof uata (1933) nilikwenda minaki kusomea kazi ya ualimu. Nilipokuwa hapo minaki nilisomea kwanza cheti cha ualimu wa grade I na kufaulu , mwaka huohuo nikajaribu mtihani wa kwenda Makerere na nikafaulu. Kwa hiyo badala ya kupelekwa kufundisha nilipata nafasi ya kuendelea na masomo zaidi ya Diploma in Educationb kule Makerere.
Mwaka 1940 nilifaulu kupata cheti change cha Diploma in Education pamoja na Cambridge School Certificate na kurudi Tanzania ili kuanza kazi yangu ya Ualimu.
Shule yangu ya kwanza kufundisha ni U.M.C.A Korogwe Middle School ambapo nilianzishwa St. VII. Nilifundishwa Korogwe kwa miaka miwili 1940 na 1941 nikiwa mwalimu mkuu, na mwaka 1942 nikahamishiwa kwenda kufundisha Minaki.
Wakati nikifundisha Minaki nilijiandikisha katika Woolssey Hall College ya London, Uingereza ili kupata masomo kwa njia ya Posta . Masomo hayo pamoja na cheti nilichopata cha London Matriculation ndivvyo vilivyoniwezesha kukuballiwa kupata Scholarship Ya British Council mwaka 1950 kwenda kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh, Scotland, Uingereza.
Huko Edinburgh nilisoma kwa miaka mitatu na kupata degree yangu ya M.A katika masomo yafuatayo:- Political Economy,Economy History,British History,Constitutional Law, Botanical Science,Moral Philosophy na English Literature. Mwaka 1954 nikarudi nyumbani na kwenda Minaki kuendelea kufundisha wakati huo nikiwa makamu wa mkuu wa chuo.
Niliporudi mwaka 1954 nilikuta chama cha siasa cha TANU (Tanganyika African National Union) kimekwisha kuanzishwa, kwa hiyo nikajiunga nacho na nikachaguliwa kuwa mwenyekiti wa Tawi la TANU Wilaya ya Kisarawe.
Nilijitahidi kuongoza TANU katika Uzaramo hadi mwaka 1958 wakati nilipoteuliwa na chama kuwa mgombea Mwafrika wa kiti cha ubunge wa Jimbo la Tanga. Nilifaulu na ikabidi kufanya shughuli za ubunge huku nikiendelea na kazi ya ya kufundisha Minaki, baada ya kuafikiana na mkuu wangu wa Chuo (Fr. Nash) kuwa itanilazimu kwenda Tanga ikiwa kkutakuwa na jambo lolote la kisiasa litakalonihitaji jimboni kwangu.
Kwa bahati mbaya kanuni za TANU hazikuruhusu mwanachama kupokea mshahara zaidi ya mmoja ikiimaanisha kuwa mtu kama mimi kupokea mshahara wa ualimu na malipo ya ubunge. Kwa hiyo ilipofika awamu ya pili ya uchaguzi mwaka 1960 sikuweza kugombea tena ubunge, kwa kuwa nilikataa kuacha kazi yangu ya ualimu kwa sababu ambazo nilimweleza Rais Nyerere na akanikubalia.
Mwaka 1961 tulipopata uhuru wetu Rais Nyerere aliniita ofisini kwake Dar es salaam akaniuliza kama niko tayari kwenda Dar es salaam ili kuwa mwenyekiti wa Public Service Commission. Nilimpa sababu zangu nilizopata kupampa huko nyuma zikiwamo uhaba wa walimu kwenye shule yangu ya Minaki, Yeye allinijibu kwamba atanisaidia kuondoa hilo tatizo kwa kutuletea walimu wawili wazungu badala yangu. Kwa hiyo tuliafikiana na nikahama kwenda Dar es Salaam.
Mfumo wa Huduma za pamoja za mawasilano wa Africa ya Mashariki ulipotengenezwa upya. Tanganyika ilipewa huduma ya Posta kwa hiyo mwaka 1964 Rais Nyerere alimtuma waziri Amir Jamal kuja kuniomba niende Nairobi kushika wadhifa wa Postmaster General wa Africa nilikuwa pia mwenyekiti wa kampuni ya Posta na Simu( Post & Telecommunicationb Company Ltd).
Mwaka 1969 baada ya kuundwa kwa Jumuiya ya Africa Mashariki 1967, Makao makuu ya Posta yalihamishwa kwenda Kampala Uganda, Ambako nilikaa mpaka nilipostaafu mwaka 1976 na kurudi nyumbani Tanzania.
Niliporudi nyumbani kwangu Korogwe, Kwamba mwaka 1977 nilikuta Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekwis ha kuanzishwa kwa hiyo nikajiunga na wanachama wengine wa kijiji katika kuhimiza vikao vya chama na kuendesha miradi ya siasa ya kujitegemea kwa mujibu wa miongozo ya Chama. Nilikuwa pia mwanachama wa ushirika wa uzalishaji mali vijijini.
Mwaka 1978 nikapata ujumbe kkutoka magila Muheza kuniomba nikawe mkuu wa Shule ya Hegongo (iliyoitwa Muheza Secondary School hapo awali) badala ya Mw. Stephene Mhando. Nilianzia kazi hiyo tarehe 1/06/1978 nikiwa 1985 nilipostaafu na kurudi Korogwe.
Kwa sasa nipo hapa Majengo nikiwa mwenyekiti wa sehemu ya Wazee wa CCM na mwanachama wa kikundi cha mradi wa kufuga nyuki wa TASAF.
Mungu Uibariki Afrika
Mungu Uibariki Tanzania
…………………..
Majengo Korogwe
10/05/2012
CURRICULUM VITAE
OF
MR. JOHN KETO
1. Date and place of Birth
Born on 15th August, 1917, at Misozwe in Muheza District of Tanga Region.
Married (now widow) with six children, two of them now dead
2. Education
i. At Kiwanda Central School and Minaki
Teacher Training College (1928 – 1937)
Awarded Grade II and Grade I Teachers Certificates
ii. At Makerere College, Uganda(1938 – 1940)
Awarded Cambridge school certificate and Diploma in Education
iii. At Edinburgh University, Scotlad (Oct 1950 – July 1954) awarded M.A degree in following subjects.
· Political History : Constitutional law
· Botanical Science: Moral Philosophy
· English Literature
3. Career
i. Teacher at Korogwe Middle School(1941)
ii. Teacher at Minaki (1942 to Sept 1950) and again 1954 to 1961
iii. Chairman Public Service Commission Tanzania 1961 – 1964
iv. Postmaster General, East Africa 1964 to 1968
v. Director General E.A.P and T. Corporation 1968 TO 1976
vi. Chairman E.A. External Telecoms 1964 to 1976
vii. Headmaster Hegongo Secondary School 1978 to 1985
4. Part Time Activities
a. Member of Council University College
Dar es Salaam
b. Member, East Africa (Swahili) Literature
c. Diwani Muheza and Korogwe District Council
d. Member of Legislative Council
Prepared by Mwalimu John Keto, Majengo Korogwe