John Cheyo: Hakuna chama cha upinzani ambacho ni kikubwa kuliko vyama vingine

Nyabukika

JF-Expert Member
Jun 15, 2022
1,402
942
Mwenyekiti wa Chama cha UDP anasema hakuna chama cha upinzani ambacho ni kikubwa kuliko vingine.

"Tunaona kuna chama tawala na kuna chama kinajiita sisi kikubwa!, hakuna chama cha upinzani kikubwa kuliko vingine, namshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kutaka mchakato wa Katiba mpya uwe Shirikishi maana hatutafuti katiba ya vyama viwili"

"Wanapoanza kuzungumza kwenye mikutano kwamba kuna vyama vingine ni vyama vya mfukoni mara vyama vya namna gani, mara kuna vyama vimeolewa na CCM hii sio sawa, sisi kama UDP hilo tunaona litatugawa".

"Njia nzuri ya kufikia mchakato wa Katiba mpya ni kufuata maelekezo ya Mhe. Rais Samia aliyotoa, kwamba mchakato uwe shirikishi, wote tushirikishwe, na wananchi ndio wapewe kipaumbele sio chama kimoja wala viwili." - Mzee John Momose Cheyo.
 
Hivi mzee kama huyu aloshindwa hata kumpa mtu mwengine uenyekiti ndani ya chama chake miongo na miongo yeye ndie mwenyekiti naye anataka ashirikishwe kwenye katiba mpya kweli ukistaajabu ya musa utayaona ya firauni watu kama hawa unaweza kubaliana na hao wanawaita vyama vya mifukoni bora mzee wa ubwabwa naweza muelewa kuliko vyama ambavyo ndani yake tu vimeshindwa kufanya mabadiliko ya katiba zao ili wenyeviti wapewe na wengine halafu wanataka katiba mpya
 
Kwani kuna vyama pinzani hapa nchini au vikundi vya wahuni????
 
Mwenyekiti wa Chama cha UDP anasema hakuna chama cha upinzani ambacho ni kikubwa kuliko vingine.

"Tunaona kuna chama tawala na kuna chama kinajiita sisi kikubwa!, hakuna chama cha upinzani kikubwa kuliko vingine, namshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kutaka mchakato wa Katiba mpya uwe Shirikishi maana hatutafuti katiba ya vyama viwili"

"Wanapoanza kuzungumza kwenye mikutano kwamba kuna vyama vingine ni vyama vya mfukoni mara vyama vya namna gani, mara kuna vyama vimeolewa na CCM hii sio sawa, sisi kama UDP hilo tunaona litatugawa".

"Njia nzuri ya kufikia mchakato wa Katiba mpya ni kufuata maelekezo ya Mhe. Rais Samia aliyotoa, kwamba mchakato uwe shirikishi, wote tushirikishwe, na wananchi ndio wapewe kipaumbele sio chama kimoja wala viwili." - Mzee John Momose Cheyo.
Cheyo hajitambui, ukubwa wa chama una factors nyingi sana. It's either ni kwa sababu ya uzee au ameamua kuwa chawa wa CCM, kuna vyama ni kama havipo kiasi kwamba hata Sukuma gang wasiojielewa ambau hushambulia kila kitu isipokuwa Mwendakuzimu hauwe kukuta wakivishambulia vyama hivyo. Yaani ni kama havipo.
Hauwezi kusikia Sukuma gang wakilialia kwamba Cheyo aachie ngazi kwani amekuwa mwenyekiti wa hicho chama tokea akianzishe.
 
Mwenyekiti wa Chama cha UDP anasema hakuna chama cha upinzani ambacho ni kikubwa kuliko vingine.

"Tunaona kuna chama tawala na kuna chama kinajiita sisi kikubwa!, hakuna chama cha upinzani kikubwa kuliko vingine, namshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kutaka mchakato wa Katiba mpya uwe Shirikishi maana hatutafuti katiba ya vyama viwili"

"Wanapoanza kuzungumza kwenye mikutano kwamba kuna vyama vingine ni vyama vya mfukoni mara vyama vya namna gani, mara kuna vyama vimeolewa na CCM hii sio sawa, sisi kama UDP hilo tunaona litatugawa".

"Njia nzuri ya kufikia mchakato wa Katiba mpya ni kufuata maelekezo ya Mhe. Rais Samia aliyotoa, kwamba mchakato uwe shirikishi, wote tushirikishwe, na wananchi ndio wapewe kipaumbele sio chama kimoja wala viwili." - Mzee John Momose Cheyo.
Huyu anaelewa anachosema kweli? Nini kigezo cha ukubwa wa chama? Anadhani chama chake kjnalingana na Chadema?
 
Mzee Cheyo "Bwana Mapesa" kumbe yupo!
Kuishi kwingi ni kuona mengi jamani! Navuta picha 1992 mzee Cheyo amekuja Sumbawanga kutafuta saini za wadhamini na wanachama ili aanzishe chama cha UDP nikiw kijana mdogo nikifuatilia vyema siasa za nchi enzi hizo na vikwazo vya mikopo ya maendeleo toka mabeberu (Structural Adjustment Program-SAP) enzi hizo vilivyomnyima usingizi Ticha na Mzee Ruksa na serikali yake. Maana ili hawa jamaa wakuunge mkono kwenye maendeleo waliweka kigezo kwanza nchi iruhusu Ubepari na iruhusu Mfumo wa vyama vingi, na Mzee Ruksa ikabidi aweke uhuru wa soko kulikuwa hamna namna maana dah mabeberu wasikie tuu wasingetupa noti.😁

Nirudi kwenye mada. Kiufupi hawa Cheyo,Mrema,Mabele & Co ndio ile syndicate/Crew ambayo Mchonga/ Ticha aliwaita mezani vijana wabobezi wa "Kimedani" wakiwa wachanga kabisa kwenye jumba jeupe wakilelewa na mtu ambae badae alikuja kuwa PM enzi za JK toka Katavi huko. Mrema akiwa amebobea na kufuzu masomo ya siasa na propaganda.
Mabele mwanasheria kijana na Momose Cheyo akawaambiwa wampe draft mezani kama "stunts" wa upinzani maana tunataka dunia ione kwamba tumeukubali na tumeuanza mfumo wa vyama vingi bongo hii, hasa mabeberu wa Bretton Woods (IMF & WB) ambao walitia ngumu kishiriki maendeleo mpaka tuukubali mfumo wa vyama vingi.

Ticha akaona isiwe nongwa, vijana hawa wakapewa mpunga mrefu sana na kila aina ya nyenzo waanzishe vyama na wengine wakakuta vimeshaanzishwa ila vinawasubiri walete figisu figisu ila zisizoumiza😁.

Na vijana hawa wakafanya kazi iyo waliopewa ikiratibiwa kwa ukaribu na jengo jeupe basi ndo ikawa hivyo. Hawa ni watu wanaoheshimika sana kwenye jengo jeupe na wapo kwenye "Payroll" za tozo hizi na ni matajiri kwelikweli. Fikiria 1994 mtu anazunguka nchi nzima ikiwa na mijndombinu mibovu akinadi sera zake alikuwa na pesa kiasi gani?
Naona wanazeeka sasa hawa ma "legends" wengine naona washatangulia mbele za haki.

Nchi hii imetoka mbali na siasa ina mengi na wingi wa siasa ndio siasa yenyewe😁
 
Back
Top Bottom