Sjiui hii tabia kwamba kila aendapo rais (ndani ya Tanzania) anaenda na kiti chake ni idea ya nani? haya ni madharau makubwa wa wananchi wa kawaida, na naweza kusema ni PR blunder kubwa sana. Kama wamejiwekea protocol kwamba kila aendapo rais lazima akalie kiti hicho hicho au kinachofanana, kwa nini wasibabane na hivyo viti wakati akiwa nje ya nchi? Ina maana Rais hana shida kukalia kiti cha aina yoyote nje ya nchi, lakini hapa Tanzania yeye is too special lazima awe na kiti tofauti na maskini? Nyerere alikuwa anakalia mpaka vigoda. Na kati ya vitu vilivyomfanya Nyerere akakubalika kwa wananchi ni kule kutokujifanya yeye ni special.
Niliona hii tabia kwa Mkapa sasa naona Kikwete anaiEndeleza lakini ni wakati wakiwa ndani ya nchi. Mdharau kwao - mtumwa!
Niliona hii tabia kwa Mkapa sasa naona Kikwete anaiEndeleza lakini ni wakati wakiwa ndani ya nchi. Mdharau kwao - mtumwa!