RAIS Jakaya Kikwete, amewaonya watu watakao fanya fujo watashughulikiwa na vyombo vya sheria ikiwemo kufikishwa mahakamani kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya Katiba.
Kauli ameitoa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwaapisha wajumbe wa tume ya kuratibu mabadiliko ya Katiba ya nchi, ambapo alisema kutokana na umuhimu wa kazi hiyo Serikali itahakikisha itatoa ulinzi wa kutosha mara tume hiyo itakapo anza kazi rasmi ya kuratibu maoni kwa wananchi kwa kuhakikisha ina imarisha ulinzi kwa wajumbe wa tume hiyo ikiwemo kupambana na watakaofanya fujo kwa kuchukuliwa hatua na vyombo vya dola.
Rais Kikwete, alisema pamoja na kazi hiyo wamewataka Watanzania kutambua kuwa kazi ya tume hiyo ni kuratibu maoni ya Katiba mpya, na sio ya kujadili kuwepo au kutokuwepo Muungano ila ni mchakato wa kupata katiba bora itakayoendesha Taifa la Tanzania.
Wajumbe hao wa tume ya mabadiliko ya Katiba walioapishwa na Rais Kikwete ni pamoja na Mwenyekiti wake Jaji mstaafu Joseph Warioba, Makamu Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji mstaafu Augustino Ramkadhani pamoja na wajumbe wake ambao ni Profesa Mwesiga Baregu, Riziki Shahari Mngwali, Dk. Sengodo Mvungi, Richard Lyimo , John Nkolo, Alhaj Said EL- Maamry, Jesca Mkuchu, na Profesa Palamagamba Kabudi.
Wengine ni Humphrey Polepole, Yahya Msulwa, Esther Mkwizu, Maria Kasonda, Al-Shaymaa Kwegyir na Mwantumu Malale pamoja na Joseph Butiku.
Wengine ni Dk.Salim Ahmed Salim, Fatma Said Ali, Omar Sheha Mussa, Raya Suleiman Hamad, Awadh Ali Said, Ussi Khamis Haji, Salma Maoulid, Nassor Khamis Mohammed, Simai Mohamed Said, Muhammed Yussuf Mshamba, Kibibi Mwinyi Hassan, Suleiman Omar Ali, Salama Kombo Ahmed, Abubakar Mohammed Ali, Ally Abdullah Ally Saleh.
Pamoja na Katibu wa tume hiyo Assaa Ahmad Rashid na Naibu Katibu wake Casmir Sumba Kyuki.
Rais Kikwete, alisema kutokana na kazi hiyo Tume hiyo inayoongozwa na Jaji mstaafu Joseph Warioba, itafanya kazi ya kukusanya maoni kuhusu katiba na maslahi ya Wananchi wa pande mbili zinazounda muungano.
Alisema kwa muda mrefu kumekuwepo na hali ya kutoaminiana kati ya Serikali na wadau hasa mara ulipotangazwa muswada wa mabadiliko ya katiba huku baadhi ya vyama vya siasa kuona havina uwezo wa kukishinda Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hata kuibua hoja mra kwa mara ya kuhitaji mabadiliko ya katiba ya nchi.
"Kuzinduliwa rasmi kwa tume hii ya kuratibu maoni ya kupata katiba mpya ya nchi ni ishara tosha ya Taifa letu kuingilia katika historia iliyotukuka kwa kuanza safari mpya ya kuelekea kuzaliwa kwa Katiba mpya itakayotokana na maoni ya Watanzania wenyewe.
"Pamoja na hili kwetu sisi upande wa Serikali tutahakikisha tunatoa ulinzi wa kutosha kwa tume hii mara itakapoa anza kazi ya kuratibu maoni kwa wananchi na tunajua wapo wale wakorofi ikiwa wataleta fujo watashughulikiwa na vyombo vya dola kwa mujibu wa sheria.
"Mbali na hilo tutawawezesha kikamilifu ikiwemo vitendea kazi pamoja ikiwemo usafiri pamoja na fedha ili mfanye kazi hii ya Watanzania kwa ufanisi wa hali ya juu kama ilivyokusudiwa.
"Tangu nilipotangaza uteuzi wenu kwa kweli Watanzania wengi wameupokea vizuri, nanyi mna wajibu wa kufanya kazii kwa niaba ya Watanzania wote na sio kuteta misimamo ya vyama vyenu au taasisi zenu. Kuwepo kwenu katika tume hii hakika mmekuwa wawakilishi kwa kila Mtanzania katika kuifanya kazi hii ambayo nina aamini italeta mafanikio makubwa kwa Taifa letu," alisema Rais Kikwete.
"Mwalimu Julius K. Nyerere, alisema mawazo hayapingwi kwa rungu bali hujibiwa kwa mawazon yaliyobora zaidi. Ni vema mtambue kuhamaki si jibu ila jambo jema ni kutoa mawazo yako yaliyobora zaidi. Kama Watanzania tutaifanya kazi hii kwa moyo tutafanikiwa kupata katiba iliyo bora itakalolilea Taifa letu katika miaka 50 ijayo," alisema
Rais Kikwete, alisema tangu mwaka 1984, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haikuwa na haki nyingi za raia ambapo kutokana na hali hiyo hivi sasa Taifa linahitaji kuwa na katiba ambayo itaingizwa haki nyingi za msingi za Watanzania kutokana na rasilimali zilizopo nchini na zinazoendana na matamko ya umoja wa mataifa.
Kauli ameitoa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwaapisha wajumbe wa tume ya kuratibu mabadiliko ya Katiba ya nchi, ambapo alisema kutokana na umuhimu wa kazi hiyo Serikali itahakikisha itatoa ulinzi wa kutosha mara tume hiyo itakapo anza kazi rasmi ya kuratibu maoni kwa wananchi kwa kuhakikisha ina imarisha ulinzi kwa wajumbe wa tume hiyo ikiwemo kupambana na watakaofanya fujo kwa kuchukuliwa hatua na vyombo vya dola.
Rais Kikwete, alisema pamoja na kazi hiyo wamewataka Watanzania kutambua kuwa kazi ya tume hiyo ni kuratibu maoni ya Katiba mpya, na sio ya kujadili kuwepo au kutokuwepo Muungano ila ni mchakato wa kupata katiba bora itakayoendesha Taifa la Tanzania.
Wajumbe hao wa tume ya mabadiliko ya Katiba walioapishwa na Rais Kikwete ni pamoja na Mwenyekiti wake Jaji mstaafu Joseph Warioba, Makamu Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji mstaafu Augustino Ramkadhani pamoja na wajumbe wake ambao ni Profesa Mwesiga Baregu, Riziki Shahari Mngwali, Dk. Sengodo Mvungi, Richard Lyimo , John Nkolo, Alhaj Said EL- Maamry, Jesca Mkuchu, na Profesa Palamagamba Kabudi.
Wengine ni Humphrey Polepole, Yahya Msulwa, Esther Mkwizu, Maria Kasonda, Al-Shaymaa Kwegyir na Mwantumu Malale pamoja na Joseph Butiku.
Wengine ni Dk.Salim Ahmed Salim, Fatma Said Ali, Omar Sheha Mussa, Raya Suleiman Hamad, Awadh Ali Said, Ussi Khamis Haji, Salma Maoulid, Nassor Khamis Mohammed, Simai Mohamed Said, Muhammed Yussuf Mshamba, Kibibi Mwinyi Hassan, Suleiman Omar Ali, Salama Kombo Ahmed, Abubakar Mohammed Ali, Ally Abdullah Ally Saleh.
Pamoja na Katibu wa tume hiyo Assaa Ahmad Rashid na Naibu Katibu wake Casmir Sumba Kyuki.
Rais Kikwete, alisema kutokana na kazi hiyo Tume hiyo inayoongozwa na Jaji mstaafu Joseph Warioba, itafanya kazi ya kukusanya maoni kuhusu katiba na maslahi ya Wananchi wa pande mbili zinazounda muungano.
Alisema kwa muda mrefu kumekuwepo na hali ya kutoaminiana kati ya Serikali na wadau hasa mara ulipotangazwa muswada wa mabadiliko ya katiba huku baadhi ya vyama vya siasa kuona havina uwezo wa kukishinda Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hata kuibua hoja mra kwa mara ya kuhitaji mabadiliko ya katiba ya nchi.
"Kuzinduliwa rasmi kwa tume hii ya kuratibu maoni ya kupata katiba mpya ya nchi ni ishara tosha ya Taifa letu kuingilia katika historia iliyotukuka kwa kuanza safari mpya ya kuelekea kuzaliwa kwa Katiba mpya itakayotokana na maoni ya Watanzania wenyewe.
"Pamoja na hili kwetu sisi upande wa Serikali tutahakikisha tunatoa ulinzi wa kutosha kwa tume hii mara itakapoa anza kazi ya kuratibu maoni kwa wananchi na tunajua wapo wale wakorofi ikiwa wataleta fujo watashughulikiwa na vyombo vya dola kwa mujibu wa sheria.
"Mbali na hilo tutawawezesha kikamilifu ikiwemo vitendea kazi pamoja ikiwemo usafiri pamoja na fedha ili mfanye kazi hii ya Watanzania kwa ufanisi wa hali ya juu kama ilivyokusudiwa.
"Tangu nilipotangaza uteuzi wenu kwa kweli Watanzania wengi wameupokea vizuri, nanyi mna wajibu wa kufanya kazii kwa niaba ya Watanzania wote na sio kuteta misimamo ya vyama vyenu au taasisi zenu. Kuwepo kwenu katika tume hii hakika mmekuwa wawakilishi kwa kila Mtanzania katika kuifanya kazi hii ambayo nina aamini italeta mafanikio makubwa kwa Taifa letu," alisema Rais Kikwete.
"Mwalimu Julius K. Nyerere, alisema mawazo hayapingwi kwa rungu bali hujibiwa kwa mawazon yaliyobora zaidi. Ni vema mtambue kuhamaki si jibu ila jambo jema ni kutoa mawazo yako yaliyobora zaidi. Kama Watanzania tutaifanya kazi hii kwa moyo tutafanikiwa kupata katiba iliyo bora itakalolilea Taifa letu katika miaka 50 ijayo," alisema
Rais Kikwete, alisema tangu mwaka 1984, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haikuwa na haki nyingi za raia ambapo kutokana na hali hiyo hivi sasa Taifa linahitaji kuwa na katiba ambayo itaingizwa haki nyingi za msingi za Watanzania kutokana na rasilimali zilizopo nchini na zinazoendana na matamko ya umoja wa mataifa.