JK umesikia haya ya Machangu DC wa Nzega na Resolute T LTD Nzega ?

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Ile issue tuliyoongea kuhusu PCCB.

Mwaka jana mwezi wa 10 Kampuni Resolute ilitoa donation ya pesa kwa NGO zinazofanya miradi ya HIV/Aids. NGO 3 zilipewa milioni 3 kila moja.

Ofisini ya idara ya mahusiano hapo Resolute ilikuwa na wafanyakazi 3, mmoja wao ni Mariam Mavura amabye ni mkuu wa idara.

Wakati hiyo pesa inatolewa,nilikuwa likizo , Kwa hiyo huyu mama yaani Mariam Mvura ambaye ni mkuu wa Idara hapa akawafuata viongozi wa NGO inayoitwa CHAWATIATA waliopewa pesa akawaomba wampe rushwa ya sh 1.5milion, jamaa wakakataa,pesa hii ilikiwa wagawane na DC Betty Machangu ambaye pia anatembea na Les Taylor ambaye ni mkuu wa Operations Manager Resolute Tanzania LTD, baada ya kuona wamekataa na wanaweza kumsemea, akageuza kibao na kuja kushtaki kazini nilikuwa naomba rushwa.

So baada ya bosi mkubwa yaani Les Taylor kusikia hivyo na issue ikawa imepita kwa DC, DC akapendekeza nifukuzwe kazi.

Wakati huo huo wakaanza kuisakama ile NGO ya CHAWATIATA kwa kuwatumia PCCB Nzega kuwa imetoa rushwa kwangu, so wakawa wanawashinikiza ile NGO itoe malezeo yatakayo niangamiza , ila taratibu zote za kesi zilifanyika pale ofisini na wale watu wa NGO wakaja kutoa ushahidi kuwa huyu mama yaani Mariam Mavura ndiye aliyeomba rushwa na siyo mimi. Sasa wakati vurugu zinaendelea, bosi mkubwa yaanio Les Taylor akawa anafuata sana maelekezo ya DC, na barua aliyoandika huku mgodini akimwelekeza kuwa nifukuzwe kazi; kumbe DC ni bibi yake siye tulikuja kufahamu baadaye.
Huyu DC kuna mambo mengi sana ya siri anayofanya na mgodi, ikiwa ni mgodi kumpatia mabasi ya kufadhili uchaguzi wa UWT bure na kwa siri, ili hali kampuni ikitoa tamko kuwa haijihusihi na siasa hivyo kutotoa pesa kwa Chama chochote cha siasa.

So kesi ikaamuliwa in favour of me ila huyu mama Mariam Mvura huku kwetu akasema hataki kufanya kazi na mimi , so ikabidi niondolewe kazini .

Mmoja wapo wa wale watu wa NGO ambao waliwekwa ndani na PCB ni ndugu wa Warioba aliyekuwa PM zamani, akaamua kuandika malalamiko Ikulu kuhusu unyanyasaji unaofanywa na PCB, huyu mama wa mgodini na DC kuwakandamiza wao.

Baada ya hiyo barua kufika Ikulu, waziri mkuu akamwagiza mkuu wa mkoa wa Tabora aunde tume ije kufuatilia hili suala, hasa kwanini huyu mfanyakazi kapewa mazingira magumu yakamfanya aache kazi.

Tume ya kwanza ikaja ikahoji ikapeleka majibu, baada ya muda ikaja tume ya pili yenye watu wa usalama wa taifa, PCB makao makuu na mkoani, walipokuja kuhoji huyu mama Betty Machangu akawaleta hadi mgodini akawatembeza huku na huko .....baada ya hapo hatujui iliishia wapi.

Majuzi mwezi wa nne, kulitokea wizi hapa mgodini, wakamwagwa askari hapa wa kufa mtu, Tosi akaleta kikosi chake, kabla ya wizi huo mkuu wa wilaya aliagiza PCB wamkamate yule Katibu wa NGO akawekwa ndani siku nne akiishinikizwa kubadili kauli yake kuwa DC na huyu mama wa mgodini hawakuomba rushwa, jamaa akakataa kubadili statement yake, baadaye wakamwachia.

Wizi ulipotokea na kamata kamata ikaanza, huyu mama wa mgodini naye akakamatwa na kuweka ndani siku 11, issue yake ikawa haiwezi kutatuliwa, kila anayeuliza anaambiwa awasiliane na Ikulu. watu waliomkamata mmoja wao ni PCB toka makao makuu na usalama wa taifa.Wizi huu ulikuwa wa dhahabu nyingi tu, na katika kuhojiwa wanakijiji walisema hawana uhusiano mzuri na mgodi kwani huyu mama anakula pesa za miradi ya wananchi.

Wakampeleka hadi benki kucheki akaunti zake wakakuta ana zaidi ya milioni sabini ambazo wakati anahojiwa hakuweza kueleza biashara anayofanya ya kuingiza pesa in between salaries tena kwa amount kubwa!!

Hatujui ilipoishia ila aliwekewa dhamana na akatoka hadi leo hatujasikia kesi ... na anaendelea na mambo yake kama kawaida ila kaanza fitina mgodi mzima kwamba kuna dada mmoja wanafanya naye kazi ndiye aliyemshitaki polisi ama kumtaja huko polisi lakini yeye ana uwezo na pia yeye anafahamiana na wakubwa hivyo hapatakuwa na kesi.
 
apeleke malalamiko tume ya utawala bora hasa kuhusu D.C

Ukisoma vyema utaona kwamba kuna tume 2 kwa agizo la waziri mkubwa zimefika na bado issue ni moto haiguswi .Je Pinda anajua kilicho endelea na kinacho endelea ? Huy Mkuu wa Wilaya Pinda anaweza kumbana tu , ni kweli Serikalo yanatokea wako kimya ? Au huyu DC analinda maslahi ya wakubwa so hata wazalendo wakiumia hakuna shida ?
 
Ukisoma vyema utaona kwamba kuna tume 2 kwa agizo la waziri mkubwa zimefika na bado issue ni moto haiguswi .Je Pinda anajua kilicho endelea na kinacho endelea ? Huy Mkuu wa Wilaya Pinda anaweza kumbana tu , ni kweli Serikalo yanatokea wako kimya ? Au huyu DC analinda maslahi ya wakubwa so hata wazalendo wakiumia hakuna shida ?

Waziri Mkuu hahusiki na Tume ya Utawala bora, Tume zilizokuwa zimeundwa hazihusiani na tume ya Utawala bora.
 
Mkuu Utawala bora Tanzania??? Duh we acha tu inatakiwa tupate kiongozi atakae safisha watu hawa.

Tume ya Utawala bora haijafanya jambo linalopelekea kupoteza credibi;ity mpaka sasa. Ila nadhani wananchi tumeshindwa kuitumia. Kwa mara ya mwissho nikumbuka ilikuwa juu ya issue ya DC wa Loy Thomas Sabaya juu ya kuvunja nyumba za wananchi huko Serengeti. Licha ya kwamba jamaa bado ni DC huko Songea, lakini Tume ya Utawala bora ilitaka aadhibiwe.
 
Endapo taarifa hiyo ina ukweli ndani yake basi mheshimiwa jk ana budi kuwajibisha viongozi kama hao,kwani wanatuonyesha wazi kuwa bado mwanamke anaudhaifu kwenye jambo la mapenzi.Haiwezekani dc mzima uliyetoka ulikotoka kwenda kutawala watu kwa niaba ya rais ukaanze kuanzisha mausiano ya kimapenzi na wale uwatawalao.
 
Iundwe tume huru ili kubaini ukweli...!? Maana ndio mtindo wa uongozi wa serikali yetu kwa sasa, hakuna uwajibikaji tena. Kila anayepewa mamlaka haaminiki, akifanya jambo lolote nje ya utaratibu inabidi aundiwe tume. na kwa mtindo tunaoenda nao hata hizo tume nazo huenda zisiaminike tena maana kila jambo tume juu ya tume.
 
Tume ya Utawala bora haijafanya jambo linalopelekea kupoteza credibi;ity mpaka sasa. Ila nadhani wananchi tumeshindwa kuitumia. Kwa mara ya mwissho nikumbuka ilikuwa juu ya issue ya DC wa Loy Thomas Sabaya juu ya kuvunja nyumba za wananchi huko Serengeti. Licha ya kwamba jamaa bado ni DC huko Songea, lakini Tume ya Utawala bora ilitaka aadhibiwe.

Hao hao tume ya Utawala bora wamechafuka na hawapaswi kubebwa wanaweza wakakuchafua na wewe watamwajibisha nani hapo?
 
Jambo hili nadhani Rais mwenyewe anaweza kuingilia kati.Ama ni zito kama za Hosea na PCCB ? Hawa ma DC ni washikaji wa Rais kawateua yeye na Pinda ni msimamizi tu .DC anatembea na mzungu wa mgodini watu wetu wanaumia na Pinda kesha pewa taarifa ngoma imerudi droo na mama ana mapesa wameona Bank PCCB wako kimya .Mama kaanza kutafuta watu wa ofisi moja na yeye waondolewe ili waendelee kunyanyasa .Pesa zimetolewa wanaomba rushwa akiwamo DC , Pinda kashindwa .JK umepata taarifa hizi uamue ?
 
Yule mama namfahamu ni mtu wa madili toka zamani.

Kwenye hii issue kuna wamama 2 na Baba mmoja sasa wewe wamfahamu vipi ?Hapa watu wa usalama wa Nchi wapo , Usalama wa CCM wapo na Usalama wa Rais wapo wekeni sawa jambo hili kwa kumpa mkulu habari a Hosea ajue kwamba tunamulika hadi resolute .Iussue must be taken seriously as it seems kuwa mfupa mnene na wa chupa Pinda umesha mpindisha .JK you help is needed.Mtu hana kazi kisa mapenzi kudumu baada ya DC wako kushiriki kuomba Rushwa .PCCB ni hao wamekuwa implicated .
 
Huyu mariam mavura alikuwa anajisomesha pale open university MA(DS) sijui kama kamaliza na alionekana kutesa sana kwa vijisenti kumbe ndo mambo yake?? Kweli Watanzania tunaliwa sana, na huyo DC analifedhehesha taifa, kweli anatembea na mzungu ili hali unamwakilisha rais ktk wilaya yako!! Lol
 
Huyu mariam mavura alikuwa anajisomesha pale open university MA(DS) sijui kama kamaliza na alionekana kutesa sana kwa vijisenti kumbe ndo mambo yake?? Kweli Watanzania tunaliwa sana, na huyo DC analifedhehesha taifa, kweli anatembea na mzungu ili hali unamwakilisha rais ktk wilaya yako!! Lol

Ndiyo matokeo ya kuteua ma DC wanawake, kufanywa VIMADA si jambo geni,si machangu tu wapo kibao!
 
Hao hao tume ya Utawala bora wamechafuka na hawapaswi kubebwa wanaweza wakakuchafua na wewe watamwajibisha nani hapo?

wamechafuliwa na nini au nani? mbona hakuna lawama zozote zilizotolewa juu ya tume hii? tatizo wengi hawaifahamu.
 
Ile issue tuliyoongea kuhusu PCCB.

Mwaka jana mwezi wa 10 Kampuni Resolute ilitoa donation ya pesa kwa NGO zinazofanya miradi ya HIV/Aids. NGO 3 zilipewa milioni 3 kila moja.

Ofisini ya idara ya mahusiano hapo Resolute ilikuwa na wafanyakazi 3, mmoja wao ni Mariam Mavura amabye ni mkuu wa idara.

Wakati hiyo pesa inatolewa,nilikuwa likizo , Kwa hiyo huyu mama yaani Mariam Mvura ambaye ni mkuu wa Idara hapa akawafuata viongozi wa NGO inayoitwa CHAWATIATA waliopewa pesa akawaomba wampe rushwa ya sh 1.5milion, jamaa wakakataa,pesa hii ilikiwa wagawane na DC Betty Machangu ambaye pia anatembea na Les Taylor ambaye ni mkuu wa Operations Manager Resolute Tanzania LTD, baada ya kuona wamekataa na wanaweza kumsemea, akageuza kibao na kuja kushtaki kazini nilikuwa naomba rushwa.

So baada ya bosi mkubwa yaani Les Taylor kusikia hivyo na issue ikawa imepita kwa DC, DC akapendekeza nifukuzwe kazi.

Wakati huo huo wakaanza kuisakama ile NGO ya CHAWATIATA kwa kuwatumia PCCB Nzega kuwa imetoa rushwa kwangu, so wakawa wanawashinikiza ile NGO itoe malezeo yatakayo niangamiza , ila taratibu zote za kesi zilifanyika pale ofisini na wale watu wa NGO wakaja kutoa ushahidi kuwa huyu mama yaani Mariam Mavura ndiye aliyeomba rushwa na siyo mimi. Sasa wakati vurugu zinaendelea, bosi mkubwa yaanio Les Taylor akawa anafuata sana maelekezo ya DC, na barua aliyoandika huku mgodini akimwelekeza kuwa nifukuzwe kazi; kumbe DC ni bibi yake siye tulikuja kufahamu baadaye.
Huyu DC kuna mambo mengi sana ya siri anayofanya na mgodi, ikiwa ni mgodi kumpatia mabasi ya kufadhili uchaguzi wa UWT bure na kwa siri, ili hali kampuni ikitoa tamko kuwa haijihusihi na siasa hivyo kutotoa pesa kwa Chama chochote cha siasa.

So kesi ikaamuliwa in favour of me ila huyu mama Mariam Mvura huku kwetu akasema hataki kufanya kazi na mimi , so ikabidi niondolewe kazini .

Mmoja wapo wa wale watu wa NGO ambao waliwekwa ndani na PCB ni ndugu wa Warioba aliyekuwa PM zamani, akaamua kuandika malalamiko Ikulu kuhusu unyanyasaji unaofanywa na PCB, huyu mama wa mgodini na DC kuwakandamiza wao.

Baada ya hiyo barua kufika Ikulu, waziri mkuu akamwagiza mkuu wa mkoa wa Tabora aunde tume ije kufuatilia hili suala, hasa kwanini huyu mfanyakazi kapewa mazingira magumu yakamfanya aache kazi.

Tume ya kwanza ikaja ikahoji ikapeleka majibu, baada ya muda ikaja tume ya pili yenye watu wa usalama wa taifa, PCB makao makuu na mkoani, walipokuja kuhoji huyu mama Betty Machangu akawaleta hadi mgodini akawatembeza huku na huko .....baada ya hapo hatujui iliishia wapi.

Majuzi mwezi wa nne, kulitokea wizi hapa mgodini, wakamwagwa askari hapa wa kufa mtu, Tosi akaleta kikosi chake, kabla ya wizi huo mkuu wa wilaya aliagiza PCB wamkamate yule Katibu wa NGO akawekwa ndani siku nne akiishinikizwa kubadili kauli yake kuwa DC na huyu mama wa mgodini hawakuomba rushwa, jamaa akakataa kubadili statement yake, baadaye wakamwachia.

Wizi ulipotokea na kamata kamata ikaanza, huyu mama wa mgodini naye akakamatwa na kuweka ndani siku 11, issue yake ikawa haiwezi kutatuliwa, kila anayeuliza anaambiwa awasiliane na Ikulu. watu waliomkamata mmoja wao ni PCB toka makao makuu na usalama wa taifa.Wizi huu ulikuwa wa dhahabu nyingi tu, na katika kuhojiwa wanakijiji walisema hawana uhusiano mzuri na mgodi kwani huyu mama anakula pesa za miradi ya wananchi.

Wakampeleka hadi benki kucheki akaunti zake wakakuta ana zaidi ya milioni sabini ambazo wakati anahojiwa hakuweza kueleza biashara anayofanya ya kuingiza pesa in between salaries tena kwa amount kubwa!!

Hatujui ilipoishia ila aliwekewa dhamana na akatoka hadi leo hatujasikia kesi ... na anaendelea na mambo yake kama kawaida ila kaanza fitina mgodi mzima kwamba kuna dada mmoja wanafanya naye kazi ndiye aliyemshitaki polisi ama kumtaja huko polisi lakini yeye ana uwezo na pia yeye anafahamiana na wakubwa hivyo hapatakuwa na kesi.

Lunyungu!

Pole sana. Acha ubaguzi kama huyo DC SIO mke wa mtu then yuko huru kufanya mapenzi na mwanamume wa chaguo lake hata akiamua kuwa changu doa inategemea na aliyempa Job Description. Kama anakula uroda na Mtishi as long as sio wakati wa kazi hayo ni private life !!

Maamuzi ya Rais hayajadiliwi hapa Tanzania hata akimteua mkewe kuwa Prime Minister si katiba inamruhusu?

Kuhusu aliyepigwa paranja kwa kuingilia ulaji wa DC huyo mama nampa pole.

Nilishawaambia hapa jamii kwamba Mgodi wa Resolute unamilikiwa na Rostam Aziz mbunge wa Igunga period. Kesi ya nyani utapeleka kwa ngedere unatarajia nini hakuna kitu!!! Hao akina Tosialitumwa kutafuta dhahabu ya JMK kwani yeye ni shareholder behind the scenes !

Kwa taarifa hiyo andika maumivu na imekula kwako !! Next time be careful usikiguse kitumbua cha DC or else utchovywa kwenye Acid au ulambishwe cynide ukafie kwenu!!! Kalieni majungu tu mnavuna mlichopanda kwenye uchaguzi wa 2005. Si mlisema ana sura nzuri kalieni ugali kama ni ya samaki!!! Kidumu CCM na Rostam Aziz kanyaga twende pambaf!!!
 
Matumizi mabaya ya nafasi na vyombo vya dola siku zao zaja,wachakalike haraka wafyonze rasilimali za nchi kadri wanavyoweza mwisho wa siku wote tutaangamia watakimbilia wapi,ulaya wanakataliwa marekani usiseme uchina hawataki ,kila wanavyonyanyasa wananchi wajue ndivyo chuki ya watanzania inavyozidi zidi yao,naogopa sana jinsi baadhi ya hawa watu wanaoitwa viongozi kila kitu chao wameshika wao tuuu wanakula wanamaliza kila kitu utamwombaje mtu akupe asilimia 50 ya pesa alizopata kwenye NGO wakati anapaswa kuisimamia iwajibike
 
Lunyungu!

Pole sana. Acha ubaguzi kama huyo DC SIO mke wa mtu then yuko huru kufanya mapenzi na mwanamume wa chaguo lake hata akiamua kuwa changu doa inategemea na aliyempa Job Description. Kama anakula uroda na Mtishi as long as sio wakati wa kazi hayo ni private life !!

Maamuzi ya Rais hayajadiliwi hapa Tanzania hata akimteua mkewe kuwa Prime Minister si katiba inamruhusu?

Kuhusu aliyepigwa paranja kwa kuingilia ulaji wa DC huyo mama nampa pole.

Nilishawaambia hapa jamii kwamba Mgodi wa Resolute unamilikiwa na Rostam Aziz mbunge wa Igunga period. Kesi ya nyani utapeleka kwa ngedere unatarajia nini hakuna kitu!!! Hao akina Tosialitumwa kutafuta dhahabu ya JMK kwani yeye ni shareholder behind the scenes !

Kwa taarifa hiyo andika maumivu na imekula kwako !! Next time be careful usikiguse kitumbua cha DC or else utchovywa kwenye Acid au ulambishwe cynide ukafie kwenu!!! Kalieni majungu tu mnavuna mlichopanda kwenye uchaguzi wa 2005. Si mlisema ana sura nzuri kalieni ugali kama ni ya samaki!!! Kidumu CCM na Rostam Aziz kanyaga twende pambaf!!!

Hii Manake nini yaani Rostam kila pembe ya rasilimali ametumbukiza pua yake hivi ni nani nchi hii i wish mtu angemchukua akamtupe katikati ya bahari nachukia sana nguvu alizonazo zimezidi kipimo
 
Mkereme,

Heshima mbele kwa sana. Unayoyaandika sijui huwa ya kweli au laaa. Sipo hapa kukukashfu au kukupa sifa. Ila kwa haraka haraka naona una datas nyingi sana mkuu (kama ni kweli).

Ila jambo moja tu unalonichosha ni staili ya uandishi wako. Ninakuwa na shida ya kuamini kama ni kweli au porojo. Ningeliomba unapoandika maneno mazito namna hivyo, andika kwa uwazi zaidi na si kukatiza katiza na kiutani kwa mbali.

Nasoma sana maelezo yako nikiyaona, hivyo naomba (ombi laweza kukataliwa) kama ukiweza andika kwa uwazi zaidi ili sisi wa shamba tuelewe nini kinaendelea.

Kama nilivyoanza na namaliza, heshima kwa mbele sana na nafaidi michango yako. Keep going strong and strong for the sake of Tanzania/Tabora. Sijui wee ni Mkereme au Mkeremi......
 
wamechafuliwa na nini au nani? mbona hakuna lawama zozote zilizotolewa juu ya tume hii? tatizo wengi hawaifahamu.

Ohhh mkuu Nziku ndauli beela siwipuliha?
Tume tumechoka mkuu hazina jipya wanasafisha tu watu wenye matope na wao sasa wamesha chafuka hawana jipya.
 
Back
Top Bottom