Wana JF,
Nimejaribu kufikiria dira ya uongozi wa JK nimeshindwa. Miaka mitano imepita, sijajua alikuwa ana lengo gani hasa ambalo alilivalia njuga kuhakikisha linafanikiwa. Nilichokiana ni kwamba lengo lake kuu ilikuwa ni kukaa kwenye uraisi miaka kumi na hatimaye aweze ku influence mrithi wake atakayemridhia.Nina baadhi ya sababu zinazonifanya niamini hivyo:
1. JK aliyavumilia makundi makubwa yaliyokigawa chama chake , si kwa sababu yeye ni mvulivu, la . Lengo lake ilikuwa asiyaudhi hayo makundi ili ayatumie kuukwaa tena uraisi kwa kipindi cha pili; kinyume na uvumi uliokuwa unazagaa kwamba he was meant to be a one term president!
2.Hakuwa na nia ya dhati ya kuwatumikia watanzania na ndiyo maana alikuwa mgumu sana kuchukua maamuzi.Lengo lake kubwa ilikuwa ukubwa; mengine ni by the way. Kwa ujumla , alitumia nguvu kubwa kufika ikulu si kwa sababu ya kulisaidia taifa, bali ilikuwa kutimiza mradi wake wa kuamini kwamba alikuwa chagua la Nyerere na Mwinyi kumrithi Mwinyi, ila upepo ukageuka kwenda kwa Mkapa ( Kwa sabubu za wazi bila shaka)
3.Napata shida kujua kwamba anajali au hajali mambo yanayo waumiza wananchi. Kwa mfano kulikuwa na malalamiko mengi ya watu kuhusiana na jinsi blog ya Ze Utamu ilivyokuwa inawachafua watu wasio na hatia ikiwemo viongozi mbalimbali wa nchi, lakini hapakuchukuliwa hatua yoyote ya kudhibit vitendo hivyo. Ni pale kashfa hii ilipomgusa yeye moja kwa moja ndipo serikali yake ikaurupuka na kuufunga mtadao huo. Je hapa aliufunga kwa kunusuru watu wake, au alifunga kwa ubinafsi wa kwamba "bwana mkubwa ameguswa"? Kwa maana nyingine ni kwamba blogu hiyo ingeendelea kuwepo hadi leo, kama si mwenye blogu kumgusa Mr. untouchable.
4.Kumekuwa na tuhuma miaka yote mitano ya uongozi wake kuhusu yeye kulinda marafiki zake ambao wamechafuka sana kwa tuhuma za ufisadi. JK aliwavumilia na kuwatetea kwa nguvu zake zote na hata kuwapigia kampeni kuwa ni watu safi. Akaingilia hadi Takukuru ( refer weakleaks) kuwakingia kifua wasipelekwe mahakamani. Ameendelea kuwavumilia mpaka wakaingia kwenye kamati nyeti kabisa za bunge na wakadhibiti bungu. JK kimya. LAKINI GHAFLA BIN VUU LEO ANASEMA ANAJIVUA GAMBA, KULIKONI? Jibu ni rahisi: Marafiki zake walishaanza kumzidi kete kuelekea uchaguzi wa 2015. Walishafanikiwa kuzitikisa jumaia zote za CCM kuhakikisaha kwamba come 2012, wampige chini asiwe mwenyekiti wa CCM. Ni baada ya kuguswa maslahi yake , ndo leo anasema anajivua gamba. Tena ni mkali kwelili kweli . Vipi? Mbona hivyo? Kwanini leo, na kwanini Lowasa, Chenge na Rostam"? Mbona akina Mkapa , Kigoda na wengineo hawatoswi? Wale akina Mulla kule Mbeya ambao ni kama wanaserikali yao vipi wale? Kwamba akina Wasira ni wasafi? Tena ghafla, eti iundwe timu ya Wazee ili washauri chama, mbona walipigwa madongo walipojaribu kukinyooshea chama vidole na wakaitwa wahuni na rafiki yake mkuu Makamba? Hata JK mwenyewe alisema " Nilijua watasema , lakini nitawajibu" yaani akiwaponda watu wa kongamano la Nyerere. Leo hii wamekuwa na busara?
Kwanini ghafla waonekane wana busara. Si ni kwa vile amezidiwa nguvu na marafiki zake; hajafanya hivyo kwa sababu ana uchungu na nchi hii, la hasha! Ni project yake ya kuelekea 2015 ili aweke mtu atakaye endeleza usultani wao.
Siwatetei akina Lowasa, ila siamini kwamba ndo pekee mafisadi ndani ya CCM na serikali kwa ujumla.
Ukiangalia jinsi watumishi wa umma wa mashirika kama NSSF, TANAPA, NCAA, TANESCO nk walivyojilimbikizia mali, huwezi ukasema CCM leo imejivua gamba. Hakika imevaa kavu zaidi, na mwisho wake utakuwa mbaya kuliko. Kama mwandishi mmoja alivyoandika kwenye Mwanahalisi " CCM ikijivua gamba itavuja kweli" naanza kuamini. Nasubiri reactions za kundi la Lowasa na wenzake, jinsi zitakavyo litikisa taifa hili.
Siombei...ila ungozi huu wa kukamiana na kuamua kwa maslahi binafsi haufai.
3.
Nimejaribu kufikiria dira ya uongozi wa JK nimeshindwa. Miaka mitano imepita, sijajua alikuwa ana lengo gani hasa ambalo alilivalia njuga kuhakikisha linafanikiwa. Nilichokiana ni kwamba lengo lake kuu ilikuwa ni kukaa kwenye uraisi miaka kumi na hatimaye aweze ku influence mrithi wake atakayemridhia.Nina baadhi ya sababu zinazonifanya niamini hivyo:
1. JK aliyavumilia makundi makubwa yaliyokigawa chama chake , si kwa sababu yeye ni mvulivu, la . Lengo lake ilikuwa asiyaudhi hayo makundi ili ayatumie kuukwaa tena uraisi kwa kipindi cha pili; kinyume na uvumi uliokuwa unazagaa kwamba he was meant to be a one term president!
2.Hakuwa na nia ya dhati ya kuwatumikia watanzania na ndiyo maana alikuwa mgumu sana kuchukua maamuzi.Lengo lake kubwa ilikuwa ukubwa; mengine ni by the way. Kwa ujumla , alitumia nguvu kubwa kufika ikulu si kwa sababu ya kulisaidia taifa, bali ilikuwa kutimiza mradi wake wa kuamini kwamba alikuwa chagua la Nyerere na Mwinyi kumrithi Mwinyi, ila upepo ukageuka kwenda kwa Mkapa ( Kwa sabubu za wazi bila shaka)
3.Napata shida kujua kwamba anajali au hajali mambo yanayo waumiza wananchi. Kwa mfano kulikuwa na malalamiko mengi ya watu kuhusiana na jinsi blog ya Ze Utamu ilivyokuwa inawachafua watu wasio na hatia ikiwemo viongozi mbalimbali wa nchi, lakini hapakuchukuliwa hatua yoyote ya kudhibit vitendo hivyo. Ni pale kashfa hii ilipomgusa yeye moja kwa moja ndipo serikali yake ikaurupuka na kuufunga mtadao huo. Je hapa aliufunga kwa kunusuru watu wake, au alifunga kwa ubinafsi wa kwamba "bwana mkubwa ameguswa"? Kwa maana nyingine ni kwamba blogu hiyo ingeendelea kuwepo hadi leo, kama si mwenye blogu kumgusa Mr. untouchable.
4.Kumekuwa na tuhuma miaka yote mitano ya uongozi wake kuhusu yeye kulinda marafiki zake ambao wamechafuka sana kwa tuhuma za ufisadi. JK aliwavumilia na kuwatetea kwa nguvu zake zote na hata kuwapigia kampeni kuwa ni watu safi. Akaingilia hadi Takukuru ( refer weakleaks) kuwakingia kifua wasipelekwe mahakamani. Ameendelea kuwavumilia mpaka wakaingia kwenye kamati nyeti kabisa za bunge na wakadhibiti bungu. JK kimya. LAKINI GHAFLA BIN VUU LEO ANASEMA ANAJIVUA GAMBA, KULIKONI? Jibu ni rahisi: Marafiki zake walishaanza kumzidi kete kuelekea uchaguzi wa 2015. Walishafanikiwa kuzitikisa jumaia zote za CCM kuhakikisaha kwamba come 2012, wampige chini asiwe mwenyekiti wa CCM. Ni baada ya kuguswa maslahi yake , ndo leo anasema anajivua gamba. Tena ni mkali kwelili kweli . Vipi? Mbona hivyo? Kwanini leo, na kwanini Lowasa, Chenge na Rostam"? Mbona akina Mkapa , Kigoda na wengineo hawatoswi? Wale akina Mulla kule Mbeya ambao ni kama wanaserikali yao vipi wale? Kwamba akina Wasira ni wasafi? Tena ghafla, eti iundwe timu ya Wazee ili washauri chama, mbona walipigwa madongo walipojaribu kukinyooshea chama vidole na wakaitwa wahuni na rafiki yake mkuu Makamba? Hata JK mwenyewe alisema " Nilijua watasema , lakini nitawajibu" yaani akiwaponda watu wa kongamano la Nyerere. Leo hii wamekuwa na busara?
Kwanini ghafla waonekane wana busara. Si ni kwa vile amezidiwa nguvu na marafiki zake; hajafanya hivyo kwa sababu ana uchungu na nchi hii, la hasha! Ni project yake ya kuelekea 2015 ili aweke mtu atakaye endeleza usultani wao.
Siwatetei akina Lowasa, ila siamini kwamba ndo pekee mafisadi ndani ya CCM na serikali kwa ujumla.
Ukiangalia jinsi watumishi wa umma wa mashirika kama NSSF, TANAPA, NCAA, TANESCO nk walivyojilimbikizia mali, huwezi ukasema CCM leo imejivua gamba. Hakika imevaa kavu zaidi, na mwisho wake utakuwa mbaya kuliko. Kama mwandishi mmoja alivyoandika kwenye Mwanahalisi " CCM ikijivua gamba itavuja kweli" naanza kuamini. Nasubiri reactions za kundi la Lowasa na wenzake, jinsi zitakavyo litikisa taifa hili.
Siombei...ila ungozi huu wa kukamiana na kuamua kwa maslahi binafsi haufai.
3.