911
Platinum Member
- Aug 22, 2008
- 852
- 499
Wakati kukiwa na mambo lukuki ambayo wananchi wangependa mh.Rais ayatolee tamko,yeye ameamua 'kupambana' na watoto 14...Ok,swali langu ni kuwa hivi hivyo vituo vya redio na televisheni vitakavyoonesha 'komedi' hiyo vinalipwa?Na nani?I mean kutoka fungu lipi?Yule dogo aliyemuulizaga Eddo kuhusu vijana kuwa taifa la kesho...nilisikia aliandamwa kweli na UwT,nadhani hawa watakuja na hoja soft soft.
Kutoka katika gazeti la Mwananchi;
Na Sadick Mtulya
BAADA ya kufanya mazungumzo na wananchi kwa njia ya redio na televisheni, Rais Jakaya Kikwete sasa atasikiliza hoja na maswali kutoka kwa watoto.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu na Watoto (Unicef), ambalo limeendaa mpango huo, limesema hiyo ni sehemu ya uhamasishaji nauungaji mkono wa kupitishwa kwa sheria mpya ya watoto nchini.
Sheria hiyo imepitishwa hivi karibuni bungeni na Rais Kikwete anasubiriwa kuisaini ili ianze rasmi kutumika
Kikwete, ambaye alizungumza na taifa kwa mara ya mwisho Septemba 9 mwaka huu alipozungumza na wananchi kwa dakika 90, atapambanana watoto 14 watakaokuwa wamechaguliwa kutoka mikoa saba ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Kwa mujibu wa Unicef, katika mpango huo wa aina yake utakaofanywa katika kipindi ambacho dunia inaadhimisha miaka 20 ya kuanzishwa kwa sheria ya mtoto, Rais ataulizwa na kujadilina na watoto wenye umri kati ya miaka 10 na 18 tu.
Shirika hilo limefafanua kwamba mpango huo ni wenye lengo la kuwapa matarajio watoto katika jitihada zao za kuboresha maisha na haki zao za msingi katika mabadiliko ya maendeleo ya dunia.
"Watoto wenye umri kati ya miaka 10 hadi 18 wakiwakilishwa na wenzao 14 kutoka mikoa saba ya Tanzania Bara na Zanzibar watatumiaaina mpya ya kuwasiliana na Rais Kikwete kwa kusikiliza hoja zao, kwa kujibu maswali yao, kusikiliza ushauri wao na kupata maoni juu ya mambo yanayohusu mustakabali wa nchi yetu, serikali yetu na maendeleo yetu," inaeleza taarifa ya Unicef, tawi la Tanzania.
"Mazungumzo hayo yatafanyika mwishoni mwa mwezi Novemba mara baada ya kukamilika kwa mazungumzo baina ya UNICEF na vyombo vya habari vitakavyorusha matangazo hayo moja kwa moja kupitia televisheni na redio."
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, watoto hao watazungumza moja kwa moja kupitia vituo vya redio na televisheni vya Shirika la Utangazaji (TBC) na vyombo vingine vya utangazaji nchini.
Taarifa hiyo inafafanua kwamba "mbali na TBC, televisheni nyingine za ITV, Channel Ten na Star Tv zinatarajiwa kuonyesha mazungumzo hayo."
Taarifa hiyo imevitaja vituo vitakavyotangaza moja kwa moja mazungumzo hayo kuwa ni TBC-Taifa, Radio One, Radio Clouds na Radio Free Afrika.
Kipindi hicho kitakachorushwa kwa dakika 30 kitafanyika baada ya watoto hao kuchujwa kutoka Zanzibar na katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Mtwara, Mbeya na Mwanza.
Uchujaji wa watoto hao utafanyika katika tarehe tofauti kuanzia Novemba 10 hadi 19 mwaka huu kupitia vituo vya kulelea watoto.
Katika mkoa wa Mwanza kituo cha Mwanza Children Fund (Mwachif) kitafanya uchujaji huo Novemba 10 na 11, katika mikoa ya Arusha ni kituo cha World Vision Tanzania na Dar es Salaam kituo cha DogoDogo Centre vyote Novemba 12 na 13.
Mkoa wa Lindi ni kituo cha Save the Children na Dodoma ni kituo cha World Vision Tanzania vyote Novemba 14 na 15 na mkoa wa Mbeya ni kituo cha Kiwohede Novemba 17 na 18.
Kutoka katika gazeti la Mwananchi;
Na Sadick Mtulya
BAADA ya kufanya mazungumzo na wananchi kwa njia ya redio na televisheni, Rais Jakaya Kikwete sasa atasikiliza hoja na maswali kutoka kwa watoto.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu na Watoto (Unicef), ambalo limeendaa mpango huo, limesema hiyo ni sehemu ya uhamasishaji nauungaji mkono wa kupitishwa kwa sheria mpya ya watoto nchini.
Sheria hiyo imepitishwa hivi karibuni bungeni na Rais Kikwete anasubiriwa kuisaini ili ianze rasmi kutumika
Kikwete, ambaye alizungumza na taifa kwa mara ya mwisho Septemba 9 mwaka huu alipozungumza na wananchi kwa dakika 90, atapambanana watoto 14 watakaokuwa wamechaguliwa kutoka mikoa saba ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Kwa mujibu wa Unicef, katika mpango huo wa aina yake utakaofanywa katika kipindi ambacho dunia inaadhimisha miaka 20 ya kuanzishwa kwa sheria ya mtoto, Rais ataulizwa na kujadilina na watoto wenye umri kati ya miaka 10 na 18 tu.
Shirika hilo limefafanua kwamba mpango huo ni wenye lengo la kuwapa matarajio watoto katika jitihada zao za kuboresha maisha na haki zao za msingi katika mabadiliko ya maendeleo ya dunia.
"Watoto wenye umri kati ya miaka 10 hadi 18 wakiwakilishwa na wenzao 14 kutoka mikoa saba ya Tanzania Bara na Zanzibar watatumiaaina mpya ya kuwasiliana na Rais Kikwete kwa kusikiliza hoja zao, kwa kujibu maswali yao, kusikiliza ushauri wao na kupata maoni juu ya mambo yanayohusu mustakabali wa nchi yetu, serikali yetu na maendeleo yetu," inaeleza taarifa ya Unicef, tawi la Tanzania.
"Mazungumzo hayo yatafanyika mwishoni mwa mwezi Novemba mara baada ya kukamilika kwa mazungumzo baina ya UNICEF na vyombo vya habari vitakavyorusha matangazo hayo moja kwa moja kupitia televisheni na redio."
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, watoto hao watazungumza moja kwa moja kupitia vituo vya redio na televisheni vya Shirika la Utangazaji (TBC) na vyombo vingine vya utangazaji nchini.
Taarifa hiyo inafafanua kwamba "mbali na TBC, televisheni nyingine za ITV, Channel Ten na Star Tv zinatarajiwa kuonyesha mazungumzo hayo."
Taarifa hiyo imevitaja vituo vitakavyotangaza moja kwa moja mazungumzo hayo kuwa ni TBC-Taifa, Radio One, Radio Clouds na Radio Free Afrika.
Kipindi hicho kitakachorushwa kwa dakika 30 kitafanyika baada ya watoto hao kuchujwa kutoka Zanzibar na katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Mtwara, Mbeya na Mwanza.
Uchujaji wa watoto hao utafanyika katika tarehe tofauti kuanzia Novemba 10 hadi 19 mwaka huu kupitia vituo vya kulelea watoto.
Katika mkoa wa Mwanza kituo cha Mwanza Children Fund (Mwachif) kitafanya uchujaji huo Novemba 10 na 11, katika mikoa ya Arusha ni kituo cha World Vision Tanzania na Dar es Salaam kituo cha DogoDogo Centre vyote Novemba 12 na 13.
Mkoa wa Lindi ni kituo cha Save the Children na Dodoma ni kituo cha World Vision Tanzania vyote Novemba 14 na 15 na mkoa wa Mbeya ni kituo cha Kiwohede Novemba 17 na 18.