JK atuambie amechukua hatua gani

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,014
JK atuambie amechukua hatua gani

John Bwire Machi 18, 2009
Raia Mwema~Muungwana ni vitendo

PAMOJA na gazeti hili, kupitia safu zake mbalimbali, kuitahadharisha serikali, kwa muda mrefu, kuhusu kuchukua hatua za kujihami dhidi ya anguko la uchumi wa dunia ambalo lilikuwa njiani, hakuna kope serikalini zilizopepesa.

Na hata athari za anguko hilo la uchumi zilipoanza kuzitafuna nchi tajiri za Marekani, Uingereza na Japan, watawala wetu nchini waliendelea kututia moyo kwamba tuko salama; kwamba hatutaathirika kwavile asasi zetu za fedha hazifungamani moja kwa moja na asasi za fedha za mataifa hayo tajiri zilizotetereka. Wakaonyesha hata takwimu kwamba uchumi wetu unakua!

Lakini, baada ya majuzi kuja nchini Mkurugenzi Mkuu wa IMF, Dominique Strauss-Khan na kutuambia kwamba sasa ni zamu ya bara la Afrika kuanza kuathirika na anguko hilo la uchumi wa dunia, watawala wetu wakazinduka usingizini.

Wakati mwanzoni walituambia kwamba hatuwezi kuathirika kwa kuwa asasi zetu za fedha hazifungamani moja kwa moja na asasi za fedha za mataifa tajiri zilizosambaratika, sasa wanakiri kwamba dunia ni kijiji na kwamba kinachowaathiri walioko Ulaya kitawaathiri walioko Tanzania.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na BBC, yaliyosikika alfajiri ya Ijumaa iliyopita (Machi 13), Rais Kikwete alisema kwamba nchi zetu duniani zimefungamana (interlinked), na kwamba kinachotokea na kuathiri London pia kitaathiri Dar es salaam.

Tuonavyo, hicho alichokisema Rais Kikwete ndiyo ukweli wenyewe, na ndiyo maana, kwa mara nyingine, tunaihimiza serikali kuchukua hatua haraka za kujihami, maana kuchelewa kwao kutakuja kuleta kilio na kusaga meno kwa Watanzania wakati athari za anguko hilo la uchumi zitakapoanza kututafuna kikweli kweli.

Kama watawala wetu walikuwa wanasubiri kuamshwa, basi, kengele ya kuwaamsha imeshapigwa na Strauss-Khan. Tunachokitarajia sasa kutoka kwao ni kututangazia ni hatua gani wanazichukua kukabiliana na athari za anguko hilo la uchumi wa dunia.

Tunasema hivyo kwa sababu, mpaka sasa, Rais wetu Jakaya Kikwete hajautangazia umma namna serikali yake inavyopambana/ itakavyopambana na athari za anguko hilo la uchumi wa dunia. Haitoshi tu kwenda London kuhudhuria mkutano wa G20 wakati nyumbani hajachukua hatua zozote kubwa.

Ijumaa ya wiki iliyopita tuliisikia serikali ya nchi jirani ya Kenya ikitangaza kwamba imeishiwa fedha kutokana na anguko hilo la uchumi wa dunia, na kwa sababu hiyo imechukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kusimamisha ajira zote serikalini, kusimamisha safari zote za nje kwa maofisa wa serikali na kusimamisha semina na makongamano kwa asasi zote za serikali.

Je, sisi hatuwezi kufuata nyayo za wenzetu wa Kenya kabla mambo hayajaanza kutuharibikia kabisa? Au tuamini kwamba bado tuko salama?

Tunajua kwamba ni jambo gumu kusimamisha ajira katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi; hasa kwa chama kilichoahidi kuongeza ajira, lakini je, hata safari za nje, semina na manunuzi yasiyo muhimu navyo hatuwezi kuvisimamisha kwa muda huu?

Wakati tukiisubiri serikali yetu itutangazie inachukua hatua gani kukabiliana na athari za anguko hili la uchumi wa dunia, wito wetu kwa wananchi ni kuwa makini na matumizi ya vipesa kidogo walivyonavyo; kwani kipindi kugumu cha maisha kinakaribia kupiga hodi.
 
Tunaweza kujifunza jutoka Venezuela kwa Hgo Chavez, baadhi ya hatua alizo chukua ni hizi hapa na zingine atatangaza hivi karibuni

"Promising the government's seriousness to counter the impact of the global economic crisis, Venezuelan President Hugo Chavez has announced his "anti-crisis" measures, which include trimming his budget to counterbalance the fall in oil revenues, and increasing planned government financing by three times.

The President's Saturday announcement - close on the heels of the government move to send army to take over the country's chief air and sea ports - provides for a 6.7 percent cut in the 2009 budget, and increase in sales taxes from 9 to 12 percent. The socialist Chavez, a former army officer who condemns capitalism, intends offsetting the plunging oil revenues that comprise nearly one-half of the national budget. Cutting this year's budget to $72 billion, Chavez said the announced measures imply "the socialist spirit to protect social programs, the people and the workers." The President has raised the minimum wage by 20 percent, and increased the planned government financing to $16 billion from $5.6 billion.

Furthermore, Chavez has promised to slash the salaries of senior public officials, as also the habitually-lavish ministerial spending on cars and entertainment.

While proposing the aforesaid measures, Chavez overlooked the economists who had suggested the devaluation of the fixed rate currency - a measure that would likely have covered the budget shortfall, but would have also led to an increase in inflation! Source (TopNews, 2008)

Read more: "Venezuelan President Chavez announces “anti-crisis” measures | TopNews United States" - http://topnews.us/content/24516-venezuelan-president-chavez-announces-anti-crisis-measures#ixzz0AmUxskXk
 
Kwanza nafurahi kuona kwenye rekodi kwamba kuna watu walilisema hili hata kabla ya mkutano wa IMF, kwa hiyo JK siyo tu hakujua cha kufanya, bali pia hakuwa akifuatilia magazeti ya nchini -seuze ya nje- yanasemaje.

JK alishatoa msimamo kwamba hatufanyi chochote tofauti, sasa mnataka msimamo gani tena?

Kama hukubaliani na msimamo huo onyesha mapungufu yake na mwaga pointi zako.Ukitoa hapo alipobofya na ku "cut and paste" kutoka Kenya, muandishi hajatuonyesha idea, achilia mbali idea original.

Ingawa nakubali kwamba kutoa policy si kazi ya muandishi, ningefikiri kuwa mtu mwenye kutoridhika kwa kiwango hiki, hususan muandishi wa siku nyingi kama bwana Bwire, angekuwwa na maoni yanayoweza kuleta mipango itakayotekelezeka. Ni rahisi kuona chombo kinaenda harijojo, hilo hata watoto wa shule za upili wenye akili wanaliona, kitu ambacho si rahisi kukijua ni jibu la swali, je tufanye nini?

This article is the personification of a wasted opportunity to raise a number of alternatives to combat the prevalent crisis.
 
Last edited:
Jamani JK alikuwa London kuona Mlupo wake VK wala sikuhudhuria mkutano wa G20. Kama ukifatilia kwa makini nchi nyingine ziliwakilishwa na mawaziri.

Muulize JK the causes of Global of Economic Recession atakuonyesha meno yake sasa unategemea aje na mikakati ya kupambana nayo!! Jamani tuwe serious
 
Huyu kwa sasa yuko anakula maraha majuu hana habari na unachosema mdau wewe, very unfortunate! Hata hivyo nakupongeza wewe kwa kuona hili.
 
Labda wamezongwa na issue za ufisad na kuchafuana hawana time so long as akaunti zao huko jersey zipo salama ukiachilia hawa SFO wanaowaletea gozgoz
 
Jamani JK alikuwa London kuona Mlupo wake VK wala sikuhudhuria mkutano wa G20. Kama ukifatilia kwa makini nchi nyingine ziliwakilishwa na mawaziri.

Muulize JK the causes of Global of Economic Recession atakuonyesha meno yake sasa unategemea aje na mikakati ya kupambana nayo!! Jamani tuwe serious

..............ha ha haaaaaaaaaaaaa, sasa mkuu basi tuanzishe ukingship Bongo ili JK awe King halafu tuwe tunachagua waziri mkuu maana jama anapenda sana madaraka japo uwezohaba. LoL!

Wito wangu kwa watanzania wenzangu. 2010 uchaguzi ile jamaa akichukuwa form ya urais kama kawaida yao tu, demonstration nchi nzima. Reason, hatakama ni haki yakee kugomea hatutaki agombee tena inatosha maana anaweza shinda kinamna. Yaani nawambia ikifanyika move hiyo walahi atawithdraw form yake ya kuwania tena urais.
 
JK 'kaput'! Hakuna anachoelewa kuhusu 'Global financial crisis'. Aliulizwa akasema tunafanya vilevile km zamani,sasa unategemea mabadiliko ndani ya wiki chache tu? Tatizo la JK ni kuwa hayuko makini na teuzi zake, hivyo usishangae kwa hili kwani wanauchumi aliowaweka kumshauri ni vilaza,hawana wanachojua!!
 
yap ni kweli aliulizwa swali na Isha Sesay lakini hakuwa na jibu zaidi ya kujiwekaweka vizuri kwenye kiti chake na kutabasamu na jibu hakuwa nalo zaidi ya kusema tutaendelea vile vile mpka nilimuonea huruma. Anyways kama mambo ya uchumi mbaya yalitangazwa na serikali yetu bado walinunua mashangingi 700 unadhani tunajiandaa au bendera inafuata upepo tuu? Mhmmm tutafika tuu.
 
yap ni kweli aliulizwa swali na Isha Sesay lakini hakuwa na jibu zaidi ya kujiwekaweka vizuri kwenye kiti chake na kutabasamu na jibu hakuwa nalo zaidi ya kusema tutaendelea vile vile mpka nilimuonea huruma. Anyways kama mambo ya uchumi mbaya yalitangazwa na serikali yetu bado walinunua mashangingi 700 unadhani tunajiandaa au bendera inafuata upepo tuu? Mhmmm tutafika tuu.

JK as a head os state he has to today something to tackle this economic criss, Thailand serikali yao inawagawia pesa wananchi kupunguza makali ya maisha nimeona kwenye leo! Tanzania mzee mzima alipayuka siku moja eti what is happening in London is not gonna happen in Dar es Salaam puuh wat is that?
 
Back
Top Bottom