Elections 2010 JK anatoa maagizo kama Rais au kama mgombea kupitia CCM?

Ngolinda

Senior Member
Apr 12, 2010
125
25
Katika pitapita zangu kwenye blogs..nilikutana na swali au maoni yaloandikwa na mmoja wa wadau na yanasomeka hivi:

"Ninagusia suala moja tu, 'agizo' la Raisi kwa Wakala. Nawaza na kujiuliza ikiwa agizo hili la Raisi latolewa kama Raisi katika shughuli zake za Kiserikali au kama Mgombea wa Uraisi kupitia CCM katika kampeni?

Sina ufahamu wa miiko ya Katiba na Sheria ya Uchaguzi, hivyo mniwie radhi kwa kuwaza hivi, pengine ikipelekwa kesi mahakamani au ukapotolewa ufafanuzi, nitapata uelewa wa kunisaidia kutofautisha kauli za Raisi wa nchi kwa sasa dhidi ya kauli za Mgombea wa Uraisi kupitia CCM ambaye ni Raisi wa nchi kwa sasa.

Nasema hivi kufuatia kauli ya CHADEMA kuishitaki CCM/Raisi Kikwete kwa anaosema na kuagiza ndani ya kipindi hiki cha kampeni, inakuwa kama "unfair advantage" kwa kuwa yeye ni Raisi kisha anagombea Uraisi.

Yaani ni sawa na kusema kwamba, kwa vile yeye kwa sasa ni Raisi na vile vile yeye ni mgombea Uraisi, basi anatumia kofia mbili kama msumeno kukata kuwili, yaani kutoa agizo kama Raisi na kisha kufanya kampeni kama Raisi mtarajiwa. Unakosekana mpaka (a clear demarcation) wa hili ni agizo haliingiliani na sera. Je, ilipaswa auze sera za CCM Tunduma kisha aondoke, na apange safari nyingine upya, au akiwa katika ofisi yake ya Kitawala, atoe agizo kama Raisi kuhusu Wakala wa ununuzi Tunduma? (waweza kubadili pia kuwa alipaswa atoe agizo kama Raisi na kisha afunge safari ya kampeni ambayo hapaswi kutoa maagizo bali kunadi sera zake). Kwa ilivyo sasa, ni vigumu sana kutofautisha (1) Aliyefika hapa na kutoa agizo ni Raisi wa nchi Jakaya Kikwete na (2) Aliyefika hapa ni Mgombea wa Uraisi Tanzania kupitia CCM, Jakaya Kikwete."

Maswali haya yanatokana na Mgombea huyo wa urais Jakaya Kikwete kumuagiza Wakala wa Hifadhi ya Chakula (SGR) kuongeza kiwango cha ununuzi wa nafaka kutoka tani 150,000 hadi 400,000 ili kuwapa soko la uhakika wakulima huko Tunduma.


 
Siasa za nchi zetu hizi ni takataka kabisa! Unadhani katika hali hiyo kuna usawa wa kufanya kampeni? Nadhani kupunguza hali hii ni vizuri kungekuwa na sheria ya mgombea akiwa rais inabidi akaimu hiyo nafasi kwa spika wa bunge mpaka hapo atakapochaguliwa tena au mtu atakapoichukua nafasi hiyo. Sasa ni vurugu tu, jamaa anfanya hongo kwa wananchi wakati huu.
 
Kisheria yeye ni Rais hadi atakapo patikana Rais mwingine. Na kwa sababu hiyo ndiyo maana ananafasi kubwa sana ya kutoa ahadi na pengine kuzitimiza wakati huu wa kampeni ili kuwashawishi wananchi wampigie kura.

Hii ndiyo Tanzania.
 
Conflict of interests!
Nadhani ni busara madaraka ya Uraisi yakome pale tuu anapoanza kampeni
 
Katika pitapita zangu kwenye blogs..nilikutana na swali au maoni yaloandikwa na mmoja wa wadau na yanasomeka hivi:

"Ninagusia suala moja tu, 'agizo' la Raisi kwa Wakala. Nawaza na kujiuliza ikiwa agizo hili la Raisi latolewa kama Raisi katika shughuli zake za Kiserikali au kama Mgombea wa Uraisi kupitia CCM katika kampeni?

Sina ufahamu wa miiko ya Katiba na Sheria ya Uchaguzi, hivyo mniwie radhi kwa kuwaza hivi, pengine ikipelekwa kesi mahakamani au ukapotolewa ufafanuzi, nitapata uelewa wa kunisaidia kutofautisha kauli za Raisi wa nchi kwa sasa dhidi ya kauli za Mgombea wa Uraisi kupitia CCM ambaye ni Raisi wa nchi kwa sasa.

Nasema hivi kufuatia kauli ya CHADEMA kuishitaki CCM/Raisi Kikwete kwa anaosema na kuagiza ndani ya kipindi hiki cha kampeni, inakuwa kama "unfair advantage" kwa kuwa yeye ni Raisi kisha anagombea Uraisi.

Yaani ni sawa na kusema kwamba, kwa vile yeye kwa sasa ni Raisi na vile vile yeye ni mgombea Uraisi, basi anatumia kofia mbili kama msumeno kukata kuwili, yaani kutoa agizo kama Raisi na kisha kufanya kampeni kama Raisi mtarajiwa. Unakosekana mpaka (a clear demarcation) wa hili ni agizo haliingiliani na sera. Je, ilipaswa auze sera za CCM Tunduma kisha aondoke, na apange safari nyingine upya, au akiwa katika ofisi yake ya Kitawala, atoe agizo kama Raisi kuhusu Wakala wa ununuzi Tunduma? (waweza kubadili pia kuwa alipaswa atoe agizo kama Raisi na kisha afunge safari ya kampeni ambayo hapaswi kutoa maagizo bali kunadi sera zake). Kwa ilivyo sasa, ni vigumu sana kutofautisha (1) Aliyefika hapa na kutoa agizo ni Raisi wa nchi Jakaya Kikwete na (2) Aliyefika hapa ni Mgombea wa Uraisi Tanzania kupitia CCM, Jakaya Kikwete."

Maswali haya yanatokana na Mgombea huyo wa urais Jakaya Kikwete kumuagiza Wakala wa Hifadhi ya Chakula (SGR) kuongeza kiwango cha ununuzi wa nafaka kutoka tani 150,000 hadi 400,000 ili kuwapa soko la uhakika wakulima huko Tunduma.



ITS CALLED THE INCUMBENCY FACTOR......and it is legitimate advantage even in the most developed democracies..Opposition should stop lamenting and learn how to deal with it
 
Back
Top Bottom