Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wana JF, ma hasa wale Waisilamu napenda kuwafahamisha kwamba kuna uwezekano mkubwa JK hakuwa ana mazoea ya kufunga Mwezi Mtukufu wa Ramadhani -- ila ameanza kutimiza nguzo hiyo miaka hii alipoukwaa Urais. Rafiki yangu mmoja aliyekuwa akifanya kazi Wizara ya Fedha wakati JK akiwa Waziri wa Wizara hiyo mapema miaka ya 90 amenieleza alikuwa hafungi.
Hii inaweza kutoa mwanga kwa kiasi kikubwa matatizo yake ya sasa ya kuangukaanguka kunakosemekana kinatokana na kuzidiwa na swaumu.
Halafu pili, hivi katika mafundisho ya kufunga inaruhusiwa kwa Muisilamu kuwatangazia umma kwamba yeye amefungulia? Ndivyo alivyotangaza JK pale Jangwani baada ya kupewa glucose na kurudi jukwaani alisema "Nimefungulia"
Kanuni ya kufunga inasema kwamba kama mtu amefungulia kwa sababu yoyote ile (yaani pamoja na agizo la daktari) haifai kutangaza. Unachotakiwa ni kwamba wewe kula tu kimya kimya na unatakiwa ulipe siku hizo ulizokula baada ya Ramadhani.