Jinsi Richmond/Dowans walivyoizunguka TANESCO na Taifa

Habari Muhimu Kama hii inahitaji kusomwa Mara Kwa Mara ili ikae ,idumu katika Vichwa vya Wapambanaji
 
Kweli watanzania tumekuwa mabwege kwelikwlei huu ni mfano wa mmoja bado kagoda, meremeta, iptl, mikataba ya madini, na mengineyo bila kuwa kama tunisia sijui kama tutatoka.
 
View attachment Why Richmond-Dowans.pdf

Nimetumiwa hii document kwa email, simjui author wake ni nani lakini nampongeza kwa jinsi alivyoweza kuchambua kiini cha sakata zima, ukiisoma between the lines utajua kwa undani ni jinsi gani taifa lilivyoingizwa mkenge na wajanja wachache, ingawaje ni ndefu kidogo lakini it worth reading, just take your time and read it to the end halafu tuunganishe nguvu kupaza sauti za kupinga malipo ya Dowans.
 
View attachment 22336

Nimetumiwa hii document kwa email, simjui author wake ni nani lakini nampongeza kwa jinsi alivyoweza kuchambua kiini cha sakata zima, ukiisoma between the lines utajua kwa undani ni jinsi gani taifa lilivyoingizwa mkenge na wajanja wachache, ingawaje ni ndefu kidogo lakini it worth reading, just take your time and read it to the end halafu tuunganishe nguvu kupaza sauti za kupinga malipo ya Dowans.

mmmh kwa kweli tuna kazi..
 
MM,
Utaniwia radhi kwa kuuliza tena na labda tena na tena. Nadhani ni jambo la kawaida na linalokubalika kwamba endapo mahakama imetoa uamuzi ambao wewe huridhiki nao, unaweza ku-appeal ili haki itendeke. Sasa nimewasikia Mzee Sitta na Dr. Mwakyembe wakieleza bayana kuwa Richmond na mrithi wake Dowans ni makampuni ya kitapeli. Binafsi siwezi kupuuza kauli za viongozi hao kwa sababu nina hakika wakati ule wa sakata la Richmond walipata fursa ya kujua mengi kuhusu utapeli huo kuliko hata walichokiandika na kusomwa bungeni. In other words, ninamchukulia Dr. Mwakyembe as a reliable source of data kuhusu utapeli wa hayo makampuni.

Sasa ninachojiuliza, ni je, kama kweli viongozi wetu ni wazalendo, walishindwaje kutumia fursa ya ku-appeal na kupeleka ushahidi mbele ya mahakama unaoonyesha kuwa dowans ni kampuni ya kitapeli tu. Ni kitu gani kimezuia Mwanasheria wetu asichukue hatua hiyo? Je, kipengele ulichogusia kwamba kumbe urithishanaji kati ya Richmond na Dowans ulifanywa kabla hata ya kufikia maridhiano kati ya Tanesco na Richmond, hakiwezi kuwa ni sababu tosha ya kuonesha utapeli wa Dowans? Je, tukiamua kama nchi kutolipa Dowans tutapata madhara gani ambayo wananchi wetu wa kawaida yatawaathiri zaidi ikilinganishwa na madhara watakayopata endapo serikali itajikamua na kulipa mabilioni hayo?

There is an English Saying which goes like "The one who pays the piper chooses a song". Hao akina Werema, Ngeleja ni wanasheria. Lakini hawako upande wa Serikali bali Bosi wa Rostam Azizi ambaye ni mshitiri na mfadhili wao. Sasa unategemea nini?
 
Mzee Mwanakijiji--Nilikuwa bize kwenye sherehe ya Magamba nikashindwa kusoma this very valuable analysis. Ulichoandika hata Jakaya Mrisho Kikwete anafahamu vizuri tu ila kwa kuwa Richmond ni Agenda yake mwenyewe. Mchakato wa kuweka William Ngeleja pale wizara ya Nishati ukisukwa na Rostam pamoja na team ya akina Malima na Jairo. Rais mwaka 2008 alitoa decree ya kwamba mitambo iondolewe pale Ubungo na alikataa ushauri wa kuitaifisha. Hata hivyo alishinikiza fisadi mmoja mashuhuri kutoka Tanesco William Mhando apewe kuwa Managing Director aw Hilo shirika na haraka haraka Dowans ikabatizwa ikaitwa Symbion na kwa usanii mkubwa Hillary Clinton akaingia kimkenge kuizindua. Aliyekuwa company secretary wa Tanesco alikuwa anapinga kwa nguvu zote uwepo wa hiyo mikataba tata. Kwa haraka na baraka za JK aliondolewa kimizengwe na kijana Godson alitoka Vodacom ambako aliwekwa na Rostam akateuliwa kuwa Company secretary. Kwa umafia huo Rostam amefanikiwa kuipatia Symbion mikataba ya kufua umeme pale Ubungo , Tegeta,Dodoma na anazo mikataba ya kuweka mitambo ya disel Huko Arusha na Shinyanga. Hata hiyo Kampuni ya Aggreko ni ya kwake. Kwa mtaji huo amepewa ulaji aw kutosha. Mpango huo umeingia Luba baada ya EWURA kushindwa kupitisha ongezeko la tarrif kwa asilimia 155% pamoja na Jakaya kulipigia debe kwa sana. Bila kumwondoa Jakaya Kikwete madarakani hakuna hatua yoyote itakayochukuliwa. Hao akina Ngeleja na team nzima ya Wizara, Tanesco na TPDC haiwezi badilika mpaka 2015. Habari ndiyo hizo. Sisi tutaandika na kuandikaga. Wote wamewekwa mfukoni na Rostam Aziz. Swali tuone ni Bank gani itawkopesha Tanesco waweze kulipa gharama za umeme wanonunua kutoka kwa Rostam kwani bei wanayonunulia umeme ni Tshs.736/= kwa unit moja ukiongezea upotevu 25% bei inakuwa Tshs.920/= na bei wanayouzia kwa wastani ni Tshs.200/= hiyo tofauti ya Tshs.700/= wataziotoa wapi. Tunaomba Majibu kutoka kwa Ngeleja, Mboma au Mhando of course kwa kuwa Jakaya nae ni mchumi then wakokotoe vinginevyo tuweke kisomo cha hitima ya Tanesco mimi nitanunua ngombe na mchele!
 
Ili kundi la RA wanatuona Watz kama vichaa vile ndio maana wanakula nchi kama wanavyotaka. Hivi JK RA una undugu gani nae kiasi cha kufanya madudu yote haya na ww unaangalia tu, mnanishangaza kabisa kwa kutojali waliowaweka madarakani na kusahau kuwa miaka ya uchaguzi inakuja
 
Nchi hii imeshauzwa na raia kudhulumiwa mgao wao badala ya kila raia kupewa mgao na kwenda kupokelea kwenye halmashauri alikozaliwa. Yani mimi naichukia serikali nzima iliyoko madarakani kwa sasa.
 
Kwanza kwenye hii kesi tanzania iliwakilishwa na nani? Tumjue ili tujue uelewa wake kwenye masuala ya sheria, na ikiwezekana awajibishwe kwa kukiuka maadili ya kazi kwa kujua au kutojua

Mwanasheria aliyetuwakilisha ktk kesi hiyo aliteuliwa na Richmond/Dowans wenyewe. Halafu akaaambiwa akwepe kufika mahakamani na siku alizofika alijifanya kutojua vizuri yaliyoendelea nchini/Wizarani kwake.

Hiyo ndo Drama, sawa na ile ya shule za msingi.
 
Sisi watanzania ni WAJINGA, tunaona kama haya mambo hayatuhusu na hatuna uchungu nayo. Kila kukicha ni madudu matupu yanaibuka na kuendelea, tunalalamika wala hatuchukui hatua. TANESCO wameongeza bili ya umeme kwa 40% ili wapate pesa ya kuilipa DOWANS, tumelalamika mchana-usiku tukalala. Sasa hivi wapendwa wetu wanakufa mahospitalini na vichanga tumboni, tumewaachia wanaharakati mchana-usiku tumelala siku imepita. Rais ameshatujua ujinga wetu, yeye kakwea pipa kaenda ulaya!

Hakyanani ingekuwa ni nchi ya wenye akili, serikali hii isingekuwepo madarakani siku nyingi.
 
Tatizo viongozi wetu wanatuona mazuzu, mabwege na wakuja ndo maana kila kukicha hawaishi kutuibia. Na tungezubaa nahisi hata wake zetu wangekuwa wanaendelea kutuibia. Inaudhi sana kweli.
 
Hivi mlipompa m k w e r e oops alipoiba kura mlifikiria ni kwa nini?
 
Kwa hakika concrete facts zilizomwagwa humu na Mwanakijiji ni fedheha kwa serikali iliyoko madarakani. Haiingii akilini kuiona serikali ikipoteza kesi ya wazi kama hii. Hivi TANESCO na serikalini kuna wanasheria kweli? Tungependa kuelewa majina ya wanasheria waliosimama kwa niaba ya serikali na TANESCO na viwango vyao vya elimu ili tuwaelewe wasaliti wetu. Kwa mujibu wa facts zilizomwagwa humu ambazo hata sisi wengine tulikuwa hatuzifahamu sawasawa zaidi ya kusoma magazetini, Richmond ilifaa kufilisiwa, mali zake kutaifishwa. Sasa nimepata mwanga kwa nini Lowassa anahaha kuutafuta u-Rais mwaka 2015. Bila shaka anaelewa kitakachofuata endapo nchi itachukuliwa na mtu mwenye uchungu na anayeweka maslahi ya Tanzania mbele - kwamba yeye na vibaka wenzake woote wataishia lupango na kurejeshwa kwenye dimbwi la umasikini. Natamani nchi hii ingekuwa China wote hawa tungeshawasahau. Wakati ndiyo huu kwa wabunge wetu wa Upinzani kupeleka hoja bungeni ya kudai hatua za kuchukuliwa kwa wahujumu uchumi hawa.
 
Hivi ni nani mhusika mkuu kwenye sakata la RICHMOND?Kama si Lowasa,ni nani sasa ili watanzania tumjue na asutwe.
 
Hivi ni nani mhusika mkuu kwenye sakata la RICHMOND?Kama si Lowasa,ni nani sasa ili watanzania tumjue na asutwe.

Vile vile je wahusika wa IPTL, MEREMETA, DEEP-GREEN, MINARA PACHA, RADAR, BILLION SWISS BANK, nk nk,... Jazia. Sasa kwa nini iwwe Lowassa peke yake? Tukumbuke yale mashtaka ya mwanamke mzinzi mbele ya BWANA YESU na alivyowajibu washtaki wake...." Ambaye siyo mzinzi kati yenu na awe wa kwanza kumpopoa huyu mwanamke mawe"... na wote "wakaingia mitini". Hivyo basi hakuna aliye msafi kwenye NEC ya sasa na nadiriki kusema kwenye safu ya sasa ya uongozi wa MAGAMBA
 
The most weirdest thing katika huu mjadala wa RICHMOND ambao naona watu wana kila document ni kuwa husikii majina ya:

1. Tender process ilivyokuwa

2. TENDER VALUATION ilivyofanywa

3. Katika Valuation team hakuna anaytajwa

4. Final report ya Valuation team

5. Mapendekezo yaliyopelkwa kwa DG wa TANESCO

6. Majina ya wanasheria wa TANESCO walioridhia haya

7. Majina ya waliokuwa consulted kule WIZARA YA NNISHATI

8. Majina ya waliohusika kule WIZARA YA SHERIA


9. Ushauri wao kwenye hili jambo

10.Role ya PRIVATE law firms kuishauri TANESCO

11. Mchanganuo ulivyofanywa mpaka kuwateua hawa private lawfirms na sababu...PPA ilifuatwa na je PPRA waliridhia?

12.Majina ya hao wahusika from the private law firm

13. Walilipwa Kiasi gani per hour?

14. Comments za DG wa TANESCO zilikuwa zipi?

15. Wanasheria wizara ya NISHATI walikuwa akina nani na walimpa ushauri gani waziri?


16. Wahusika wa PPRA ambao walikuwa consulted na comments zao

naona kila kukicha tunajadili maamuzi ya kesi na hao wanao likisha hizi documents mbona hawaleti full mzigo includi hayo majina?

Unles JF is not as influential as it used to back in the day when people used to trust it with leaked docs...Kulikoni au kitumbua kishaingia mchanga?


Au kama wanavyosema wanywamwezi kuwa the GAME HAS BEEN RIGGED!!

Unless kuwepo public inquiry into this fiasco

It was an emergency plan!

Hayo mambo ya tenda na vikao bureaucracy zinachukua 6 months na posho kibao!

It was the right move kwa serikali sema baadae wakalikoroga! walipoingia na wanasiasa wakaharibu kabisa.

Hizo billioni tunazoilipa Dowans ni lawama kwa bunge la Tanzania.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom