Jinsi Mpesa ilivyofanikiwa Afrika ikashindwa kwenye soko la Ulaya - Funzo wa madevelopers

Nafaka

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
12,155
31,058
Katika ubunifu ambao umefanikiwa sana Afrika ni mobile money hasa ikizaliwa kutoka Safaricom Mpesa. Ubunifu huu tofauti na ubunifu uliozoeleka kuanzia ulaya ukaletwa Afrika, huu ulitengenezwa mahususi kwa mazingira ya kiafrika na ndio maana mbile money imefanikiwa sana afrika.
Vodafone kuona mafanikio haya akaamua kuexpand Mpesa na kuipeleka kwenye sokoa la Ulaya. Mwaka 2014 ikawa launched kwa mara ya kwanza nchini Romania akilenga itumiwe na wateja milion 7 aliokuwa nao huko Romania.
Lakini tofauti na Afrika, Waromania hii huduma hawakuipenda yani waliona haiwezi kuwa mbadala wa huduma nyingone walizonazo za masuala ya pesa.
Kufikia 2018 M-pesa ya Romania ilikuwa ikitengeneza hasarana kupelekea Vodafone kusitisha hii huduma kabisa na mpango wao wa kuisambaza Ulaya.
Funzo ni kwamba, kila product inabidi iendane na mazingira husika na ndio maana developers wengi wanacopy apps za nje wanatengeneza zao tofauti jina baada ya miezi wanaachana nazo amaana watu hawazitumii.
 
Mpesa hata south africa ilifeli vibaya sana Sijui ni vp East africa imefanikiwa
Imefanikiwa kwa sababu watu wengi hawakuwa wameunganishwa kwenye huduma za kibenki na kutokana na hilo ilikuwa ni rahisi kutuma pesa in real time na haikuhitaji mtu kuwa na smartphone au internet. Ile implimentation ya Ussd ilisolve mengi. Ukitaka kujua hilo, japo mitandao ya simu imeunda app za mobile money na watu wana smartphone bado watu wako addicted na ussd.
 
kwa wenzetu huko washazoea kufanya malipo yote kwa credit card, mifumo ya kutumiana pesa ilisharahisishwa zaidi kwa apps na internet banking toka zamani.

hii mpesa ni kwajili yetu huku ambako tupo nyuma zaidi kiteknolojia, Internet yenyewe tu tunauziwa kama ndonya za mchele na tunawasha data kwa manati kuepuka vifurushi kuisha haraka, Na hii ndio sababu hatuujui urahisi wa internet banking tupo bize na kubofya manyota na mareli,

kuipeleka mpesa huko ulaya ni sawa na kwenda kuwauzia mitumba.
 
Mpesa ana hizi mobile payments ni kw kwa ajili ya nchi ambazo hazina mifumo iliyokamilika ya fedha.

Hii sio mifumo ambayo ni sustainable kwa huko mbele. Miaka 30 ijayo mpesa inaweza kua ni huduma iliyosahaulika kabisa pale idadi kubwa ya watu watakapokua wamejiunga kwenye mifumo rasmi ya kufedha.
 
Katika ubunifu ambao umefanikiwa sana Afrika ni mobile money hasa ikizaliwa kutoka Safaricom Mpesa. Ubunifu huu tofauti na ubunifu uliozoeleka kuanzia ulaya ukaletwa Afrika, huu ulitengenezwa mahususi kwa mazingira ya kiafrika na ndio maana mbile money imefanikiwa sana afrika.
Vodafone kuona mafanikio haya akaamua kuexpand Mpesa na kuipeleka kwenye sokoa la Ulaya. Mwaka 2014 ikawa launched kwa mara ya kwanza nchini Romania akilenga itumiwe na wateja milion 7 aliokuwa nao huko Romania.
Lakini tofauti na Afrika, Waromania hii huduma hawakuipenda yani waliona haiwezi kuwa mbadala wa huduma nyingone walizonazo za masuala ya pesa.
Kufikia 2018 M-pesa ya Romania ilikuwa ikitengeneza hasarana kupelekea Vodafone kusitisha hii huduma kabisa na mpango wao wa kuisambaza Ulaya.
Funzo ni kwamba, kila product inabidi iendane na mazingira husika na ndio maana developers wengi wanacopy apps za nje wanatengeneza zao tofauti jina baada ya miezi wanaachana nazo amaana watu hawazitumii.
Unajua hasara ambayo makampuni ya ATM,VISA yangepata? Wazungu wajanja sana hulinda tech zao zisife na kipata hasara.
Sawa na 5G ilipozinduliwa China kabla ya ulaya, ilipigwa propaganda ili kuizuia Huawei kuua kampuni za ulaya.
Mashart waliopewa Huawei wauze/copyright.
Kilichojiri tunajua wote.
 
Unajua hasara ambayo makampuni ya ATM,VISA yangepata? Wazungu wajanja sana hulinda tech zao zisife na kipata hasara.
Sawa na 5G ilipozinduliwa China kabla ya ulaya, ilipigwa propaganda ili kuizuia Huawei kuua kampuni za ulaya.
Mashart waliopewa Huawei wauze/copyright.
Kilichojiri tunajua wote.
Ilifail kwa sababu haikutengenezwa kwa mazingira yao wala si propaganda. Toka mwanzo lengo la mpesa ilikuwa ni kuwahudumia watu ambao hawana huduma za kibenki na limited access na internet.
 
Ilifail kwa sababu haikutengenezwa kwa mazingira yao wala si propaganda. Toka mwanzo lengo la mpesa ilikuwa ni kuwahudumia watu ambao hawana huduma za kibenki na limited access na internet.
Huoni kutokwenda bank kunaokoa muda? Kwa hio wazungu hawapendi kuokoa muda?
 
Bank zimeisha kuwa integrated to mpesa.
Wazungu Hawako sahihi muda wote.
MPesa is very adv tech kulinganisha na ma ATM. Mzungu Hawaii kukubali Afrikabuwe Mbeki yake kumbe huwezi kuwa mbele kwa kila kitu.
Monopoly ECONOMY ndio inaowasumbua.
Mbona wameikubali PayPal inatofauti gani na mpesa.
 
mimi nadhani ni mifumo tu ya kulinda system nyingine za kifedha za huko kwao..

Mfano huku kwetu elon musk alivyotaka kuleta internet yk imekuwa blocked na nchi nyingi kwa sababu teyari kuna mifumo ya internet na serikali imekopa billioni of money kwa ajili ya mifumo hiyo kuruhusu ushindani ambao utaiuwa mifumo hiyo ni hatari na hasara kubwa kwa serikali.
 
Huoni kutokwenda bank kunaokoa muda? Kwa hio wazungu hawapendi kuokoa muda?
Wana internet, wanawaweza lipa vitu online kwa kutumia card za bank, wanaweza kulipa vitu popote kwa kutumia kadi, now hata kwa simu kwa kusogeza simu na kifaa kilichoconnected na kadi zao, wana huduma nyingi za kuconnect kadi au benki zao zinazotoa cashback so hiyo ina maana hawana haja ya kwenda benki na huduma zao ziko reliable zaidi. Pia kumbuka wana huduma za credit card.
 
mimi nadhani ni mifumo tu ya kulinda system nyingine za kifedha za huko kwao..

Mfano huku kwetu elon musk alivyotaka kuleta internet yk imekuwa blocked na nchi nyingi kwa sababu teyari kuna mifumo ya internet na serikali imekopa billioni of money kwa ajili ya mifumo hiyo kuruhusu ushindani ambao utaiuwa mifumo hiyo ni hatari na hasara kubwa kwa serikali.
Ilifail kwa sababu hebu fikiria ni simple tu.
We una pesa benki na una kadi connected na benki yako ambayo unaweza kuitumia kulipia chochote iwe sokoni, supermatket, bar, online, kwenye usafiri ukitaka mtumia mtu pesa watmtumia from your card via labda paypal instantly utahitaji mpesa kwa ajili ya shughuli gani?
Huku kwetu ilifanya kazi kwa sababu kuna sehemu hata mabenki hayakuwepo au tawi la benki liko mbali. Mawakala wa mpesa walisolve hilo ndiyo maana hata mabenki yamebidi yafuate model za kuweka mawakala ili kuwasogezea watu huduma karibu.
 
Wana internet, wanawaweza lipa vitu online kwa kutumia card za bank, wanaweza kulipa vitu popote kwa kutumia kadi, now hata kwa simu kwa kusogeza simu na kifaa kilichoconnected na kadi zao, wana huduma nyingi za kuconnect kadi au benki zao zinazotoa cashback so hiyo ina maana hawana haja ya kwenda benki na huduma zao ziko reliable zaidi. Pia kumbuka wana huduma za credit card.
Kutumia kadi na kutumia karatasi ya mpesa ipi ni rahisi na gharama nafuu ktk uendeshaji?
Li ATM mashine lina gharamai kubwa. Max malipo ilikufa kwa sababu gani.
Malipo yalikuwa more digitized kuliko Max malipo.
Transaction ya card ina makolokolo mengii wakati mpesa ni simple tu simu ya elf 15.
Hayo makorokoro yako uliotaja hap siyaelewi
Uendesgaji wake una gharama.
Mpesa bado ipo mbele ya hayo makolokolo.
Ulaya wameachwa mbali sana na China ktk mfumo wa pesa, wao wanaamini ukiritimba na sio ubora na gharama.
 
Kutumia kadi na kutumia karatasi ya mpesa ipi ni rahisi na gharama nafuu ktk uendeshaji?
Li ATM mashine lina gharamai kubwa. Max malipo ilikufa kwa sababu gani.
Malipo yalikuwa more digitized kuliko Max malipo.
Transaction ya card ina makolokolo mengii wakati mpesa ni simple tu simu ya elf 15.
Hayo makorokoro yako uliotaja hap siyaelewi
Uendesgaji wake una gharama.
Mpesa bado ipo mbele ya hayo makolokolo.
Ulaya wameachwa mbali sana na China ktk mfumo wa pesa, wao wanaamini ukiritimba na sio ubora na gharama.
Unaongelea gharama hizo Afrika sio kwao wao. Kwa wao ni gharama ziko cheap kuliko gharama unazokatwa na bank yao na bado wanakupa cashback bonus. Na kumbuka sio lazima utembee na ATM. mimi mfano nina atm ya payoneer toka wanitumie sijawahi hata kwenda kuichukua nilicho nacho ni namba za kadi na CVV na bado naitumia nimeconnect na apps payment za simu.
Narudi, hii huduma kwao haikufaulu kwa sababu haikuweza kutatua chochote haikuwapa sababu ya kwanini wadump huduma walizo nazo kwa ajili ya M-pesa. Hii huduma ilifaulu Afghanistan kwa sababu nao walikuwa na shida kama za kwetu.
Na kumbuka wao wanaprefer kufanya cashless transactions kitu ambacho kadi za benki zinatimiza hilo.
Japokuwa gharama za atm kwetu ziko juu, ila bado ni cheap kuwithdraw 400,000 atm kuliko kuitoa kwa wakala. Hata report ya WB ya mwaka 2018 ilionyesha gharama za hizi huduma kwa mtumiaji ziko juu.
 
Back
Top Bottom