Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

EPISODE 22

“A TRUE STORY BY INSIDER”

Na mimi muda huo niliinuka kuelekea chumbani kwake sikutaka kubisha, niligonga mlango na akasema niingie.

Nilifungua mlango na yeye alikuwa kajilaza kitandani, na muda huo macho yangu yote yalikuwa yakimwangalia Mwanamke mrembo aliyejilaza pale kitandani. Maana alikuwa na kibukta kifupi kinachoishia mapajani katikati, na upande wa juu alikuwa kavaa sport bras.

Sasa ule uzuri wake na vile alivyokuwa nikiona maungo yake vizuri tena live kwa macho nilijikuta nataka kupagawa na mimi sikutaka kuendelea kumtizama maana mnara ulishaanza kusimama wima.

MIMI: “Umeniita nakusikiliza”

IRYN: “Insider nataka unisaidie kutoa vitu humo kwenye makabati, nataka tuvipange vizuri.”

MIMI: “Sawa haina shida.”

IRYN: “Afu Grizmann anakuja mwezi huu, anakusalimia.”

MIMI: “Msalimie pia, mwambie aje na mazaga bhasi.”

Room yake ilikuwa na zile kabati za kutengeneza moja kwa moja. Nilifungua kabati na droo zote moja kwa nyingine.

Sasa kila nikifungua droo nilikuwa nakuta simu na vitu vingine kama chaji, earpods, apple watches na saa. Baada ya kumaliza kukagua drow zote nilihesabu jumla ya idadi za simu na zilikuwa simu 14 ambazo ni Samsung na iphone. Samsung Galaxy S22 ultra (2), Iphone 12 Pro Max (3), Iphone 13 Pro (3) na Iphone 13 Pro Max (6).

Nilishangaa sana asee yaani mtu anakaa na simu nyingi vile ndani na zote zilikuwa ni brand new hakuna hata moja ilofunguliwa. Muda ule nilitamani niibe hata simu moja nifiche lakini ilikuwa ngumu kwa upande wangu. Kuomba simu pia nilikuwa siwezi maana nilipewa simu na Iryn na hakuwai niuliza kuhusu ile simu, nilimpa Mama J na nikachukua simu yake, tulifanya kuexchange na Mama J.

IRYN: “Insider hizo simu zipo ngapi?”

MIMI: “Jumla ziko 14, unakaaje na duka la simu ndani?”

IRYN: “Insidier hizo simu nilipewa kama zawadi tu na watu tofauti, kama hizo iphone 12 Pro Max nilipewa muda mrefu sana toka zinatoka.”

MIMI: “Aisee unabahati sana, unajua uzuri wako unawapagawisha sana wanaume.”

IRYN: “Insider umeanza tena, hizo iphone 12 kuna dada nitawapa saloon, wanani-furahisha sana.”

MIMI: “Na hizo zingine? Si bora hata uuze upate hela maana thamani zinazidi kushuka, na mwaka huu iphone 14 inatoka.”

IRYN: “Sasa naziuzia wapi?”

Nilitamani kumwambia aongee na Muajemi maana anaduka la simu lakini nikaona haitakuwa good idea, Muajemi angejisikia vibaya sana yaani kapeleka zawadi ya simu afu mtu anasimu kibao ndani.”

MIMI: “Niachie hili mimi, nitatafuta mtu wa kumuuzia.”

IRYN: “Okay sawa, nataka now nitumie na Samsung Ultra maana wanaisifia sana.”

Samsung S22 ultra ilikuwa released February lakini Iryn alikuwa nayo tayari tena mbili (2).

MIMI: “Sawa Bossy.”

Alinipiga jicho kali sana maana alikuwaga hapendi kusikia nikimuita hili jina.

MIMI: “Una nipiga jicho na hayo macho yako ya kirembo.”

IRYN: “Insider njoo angalia.”

Na muda huu alikuwa akinionesha picha zake na video mbalimbali alizokuwa Ufaransa.

MIMI: “Ulikuwa unashiriki fashion?”

IRYN: “Niligombea Miss college.”

MIMI: “Ikawaje?”

Na muda huu Iryn alikuwa akitafuta picha ya kunionesha,

IRYN: “Ona nilikuwa wa2, sikushinda. Huyu dada alishinda.”

Huyu dada aliyekuwa akinionesha ambaye ndo alishinda, alikuwa ni mhindi.

MIMI: “Ni kisu hatari.”

IRYN: “Kumbe hata wewe umeona, alishinda huyu alikuwa anasoma Finance.”

MIMI: “Hata hvyo ulijitahidi kuwa wa2 sio kitoto.”

IRYN: “Kupitia haya mashindano ndo nili-miti na Grizmann, kipindi hicho yeye alikua Masters.”

MIMI: “Everything happen for a reason.”

IRYN: “Yeah sure”

MIMI: “Hivi huko Ufaransa Grizz hakucheat kweli?”

Muda huu Iryn aliniangalia akaanza kucheka, ni kama hakutegemea lile swali.

IRYN: “Ana mke na watoto 2.”

MIMI: “Aisee na wewe umeridhika kuwa mchepuko?”

IRYN: “Insider Grizz kuna mambo ananisaidia mengi sana, sometimes we don’t have a choice.”

MIMI: “Ni kweli unachosema ila naona anakupenda sana.”

IRYN: “Yeah he loves me but ni mme wa mtu.”

Sikutaka kuendelea kumwuliza sana kuhusu Grizz na muda huo yeye alitoka kwenda Seblen akiniacha pale chumbani nikiendelea kumpangia vitu vyake.

Wakati amekwenda seblen Mary alikuwa akinipigia simu na Iryn alisikia simu ikiita.

IRYN: “Insider somebody Mary is calling.”

MIMI: “Njoo na simu bhasi.”

Muda huo nilitumia kuongea na Mary, alikuwa akiniuliza kama nipo around ili nikampick ila nikamwambia niko Kijitonyama. Mary pia aliomba kama tutaweza onana muda ule na nikamwambia maybe jumapili nitamcheki.

Na muda huo wakati nikiongea na Mary, kwa upande mwingine Iryn alionekana kuwa makini sana kusikiliza maongezi yetu.

IRYN: “Insider nani huyo?”

MIMI: “Kila nikiongea na mwanamke lazima uulize ni nani.”

Na Iryn kama hakufurahishwa na hili jibu nilimwona kamind flani hivi. Pia kama alijiona ananikosea sana kufuatilia calls zangu.

IRYN: “Ok Insider am sorry”

MIMI: “Usijali najua huna nia mbaya, huyu ni mshikaji wangu.”

IRYN: “Ngoja nikapike chap”

Na mimi nilitoka nikakaa pale seblen na muda huo nilikuwa nikiangalia Tv utafikiri ni Baba mwenye nyumba. Na mimi niliamua kwenda Jikoni kumsaidia kupika muda ule.

“Unanipikia nini Mummy?”

“Nilitaka kupika ndizi na nyama ila nimeona uvivu kumenya ndizi.”

“Si ungesema nikusaidie? Mimi niko kwaajili yako”

“Kesho nitapika usijali.”

“Sasa unapika nini?”

“Tambi za maini.”

Na muda huu mimi niliamua kutengeneza juice ya nanasi na story zikiendelea.

IRYN: “Insider Muajemi anataka twende Zanzibar kutembea”

MIMI: “Aaah mnakwenda lini?”

IRYN: “Ndo najifikiria hapa”

MIMI: “Wewe unapenda?”

IRYN: “Kwenda napenda, ila yule mtu simwamini bado.”

MIMI: “Kwamba unaogopa atakuteka?”

IRYN: “Hamna sio rahisi, anyway nitaangalia.”

MIMI: “Si unakwenda na mimi hapa Bodyguard wako.”

IRYN: “Hahahaah Insider huishiwi vituko”

MIMI: “Nimekwenda jeshini wewe cheka, sikutaka kuwa mjeshi tu.”

Na muda huo nikamwonesha cheti changu cha JKT kile cha Mujibu wa sheria, Iryn haya mambo hajui hivyo alishangaa sana, maana alikuwa haamini kama nilikwenda jeshini.

IRYN: “Insider kumbe umekwenda Jeshi, upo vizuri ndomana mambo yako ni chap sana, na unajali sana muda.”

MIMI: “Nitakulinda kila unakokwenda na hakuna wa kukuzingua.”

Iryn alishiia kufurahi tu muda huu hakuwa na chakusema, pia alisema kesho ambayo ni jumamosi angeenda kuonana na Muajemi. Na mimi niliunga mkono hili jambo kwa asilimia mia kabisa, maana Iryn angekua karibu na Muajemi mimi ningeendelea kufaidi matunda.

MIMI: “Vipi kuhusu kutoka usiku kwenye kazi zako.”

IRYN: “Tutaendelea next week nataka kudeal na wateja wa web tu kwasasa tena ambao wana offa nzuri tu.”

MIMI: “Sawa Bossy Lady.”

Baada ya kumaliza mapishi tulikula chakula na nikamshukuru kwa Dinna, nikamuaga nasepa muda ule, lengo langu ilikuwa kwenda barabarani kuendelea na majukumu ya kusaka pesa.

Wakati nataka kuondoka Iryn aliniita

IRYN: “Insider…. Leo tumeanza mwezi mpya, nikiwa nakulipa naomba upokee hela sijisikii vizuri kuona unakataa hela hata kama tulikuwa kwenye makubaliano.”

MIMI: “Sawa haina shida mummy”

IRYN: “Byee Insider takecare”

Nilitoka pale ilikuwa saa2 usiku tayari na mimi nikaendelea kupiga kazi non-stop, kama mnavyojua kwa Dar weekend ndo watu wanatoka out kutumia hela.

Nilipiga kazi mpaka saa 7 usiku na niliamua kurudi baada ya kupata mteja aliyekuwa anaelekea Mbezi Beach.

*********

Jumamosi niliamka asubuhi sana kama kawaida yangu na nilipiga sana kazi hii siku. Ile Asubuhi kwenye saa5 Msomali alinipigia simu na aliuliza niko wapi nikamwambia niko tabata Baracuda.

Msomali akasema kama nitakwenda mjini nimpigie simu anataka twende Mbweni na alisisitiza sana.

Saa 12 jioni ndo muda ambao nilionana na Msomali na alikuwa pale CBD hotel Gerezani.

Tulitoka hapo kwanza tulianza kupitia Mlimani city kuna mtu alikwenda meet naye na nilisubiri kama 1 hour. Baada ya hapo sasa tukaanza safari ya kwenda Mbweni na tulipitia Barabara ya Mwaikibaki ili kukimbia foleni ya Bagamoyo Road.

MSOMALI: “Insider gari yako ni safi sana na inanukia vizuri.”

MIMI: “Si unajua ofisi lazima iwe safi muda wote, hata hapa umekuta Gari ni chafu.”

MSOMALI: “Kwa hili unajitahid sana hongera.”

MIMI: “Ahsante sana Bossy wangu I really appreciate.”

Saa 3 tulikuwa tumefika Mbweni na tulifika sehemu anayokwenda tukaingia ndani na mimi nilikwenda msubiri kwenye garden

Msomali alitumia kama masaa 2 pale na akatoka akanambia tunakwenda Sea cliff hotel Masaki, ndo nitamwacha pale.

Wakati tuko njiani tulikuwa tunapiga story mbalimbali hasa za Maisha na mademu.

MSOMALI: “Insider kwa kipindi kifupi tulichokutana nimetokea kukubali sana, kuna deal nitakushirikisha by next week, au umeridhika na maisha ya Uber?”

MIMI: “Hapana Bossy sijaridhika maana hii kazi sometimes ni mateso ila ndo hivyo tunapambana kibishi. Kama deal zuri mimi napiga kwasasa nachoangalia pesa tu.”

MSOMALI: “Sawa haina shida Bro!, nitakupigia simu.”

MIMI: “Sawa Bossy nasubiri na nitashukuru sana.”

Tulifika pale Sea cliff na nikamshusha Msomali pale.

MSOMALI: “Bro nikupe kiasi gani? Maana hatukuelewana kabisa.”

MIMI: “Bossy wewe nipe utakayoona haitoniumiza mimi, si unaona wese limepanda bei? Vita ya Ukraine na Russia ndo imeleta majanga.”

MSOMALI: “Ni kweli Bro! vita ya wakubwa hizo sisi wengine ni watizamaji tu, wewe ongea kuwa huru.”

MIMI: “Ok kutoka Posta mpaka Mlimani city 15,000, kutoka Mliman mpaka Mbweni 25,000 na kutoka Mbweni mpaka hapa utanipa 30,000 unipa 70,000 sio mbaya.”

MSOMALI: “Haina shida Bro ngoja nikupe na offa ya bia maana leo weekend”

Msomali alinipa 100,000 na akaondoka pale huku akiahidi kunitafuta kwa ajili ya hilo deal. Na muda huo niliwaza Msomali atakuwa na deal gani?

Na muda huu nilipata request ya mteja alikuwa anakwenda Airpot na alikuwa palepale Sea cliff.
Na huyu mteja alikuwa kauzu sana nakumbuka, maana tulitoka pale Sea cliff mpaka Terminal 3 bila kuongea njiani.

Nilipiga kazi mpaka saa 9 usiku ndo nikarudi kulala, maana nilikuwa na usingizi hatari.

*******

Jumapili saa 4 asubuhi Mama Junior alirudi home na aliletwa na Mamdogo wake home. Niliwapokea na tulishinda na mamdogo pale home mpaka tukala chakula cha mchana na yeye akaaga.

Hii siku nilicheza sana na Junior maana nilim-miss sana, na Junior alikuwa mtundu sana kipindi kile mpaka sasa ni mtundu balaa huyu mtoto.

Mchana Iryn alinipigia simu akasema kama nitapata muda niende kwake ili nipeleke ile mizigo (mashine za saloon) kule Masaki kwa Mama Janeth.

Jioni saa10 nilitoka home na nikamwaga Mama J natoka ila nitawai kurudi tutoke out. Mama J alifurahi sana kusikia hizi taarifa maana ni kama alikuwa amemiss kutoka out na mimi mme wake.

Nilifika kwa Iryn ila sikuingia ndani na niliitoa ile mizigo kibarazani na kuiweka kwa gari. Muda huo nilihisi Iryn atakuwa amelala hivyo sikutaka kumsumbua kabisa. Kwasababu nilikuwa najua ile mizigo inakwenda kwa Mama Janeth nikasema acha niipeleke tu, nikirudi ndo nitamcheki.

Nilipeleka ile mizigo kwa Mama Janeth Masaki, baada ya kufika Mlinzi alinifungulia geti na nilimkuta yuko nje akipanda maua . Nilimsalimia nikamwambia nimeleta mizigo na nikaitoa nikaingiza ndani.

“Mwanangu Ahsante sana.”

Nilimwaga Mama Janeth na mimi nikaondoka kurudi kwa Iryn, na wakati niko njiani Iryn alipiga simu.

“Insider kumbe umepeleka mizigo kwa Mama Janeth.”

“Yeah, wakati nafika hapo ulikuwa umelala, sikutaka kukusumbua.”

“Nilitaka twende wote bhasi lakini.”

“Niko njiani soon nitakuwa hapo.”

Wakati narudi nilitumia njia ya Heilasie Road ambayo inakuja kutokea Bagamoyo Road, kwangu naonaga hii barabara ni rahisi, maana hainaga mambo mengi.

Nilitumia kama dakika 15 kufika Kijitonyama kwa Iryn na nilipark gari nje ya fensi getini, sikutaka kukaa sana pale. Lengo langu lilikuwa nirudi home mapema ili nitoke out na wife.

Niliingia ndani na nilimkuta seblen akichezea laptop yake ya Macbook, nilimsalimia na nikaenda kukaa kwenye kiti.

“Insider…….”

Iryn aliniita na mimi nikamtizama kumsikiliza anataka kusema nini;

“Naam mummy”

“Huyu ni mwanao?

Iryn alikuwa akionesha picha ambayo nilikuwa nimeipost whatsapp status nikiwa na Junior.

TO BE CONTINUED

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
Now
 
EPISODE 25

“A TRUE STORY BY INSIDER”

Mary hata hakutusemesha bali aliomba nifungue gari ili atoe mkoba wake ndani ya gari. Na baada ya kuchukua mkoba wake aliondoka eneo lile.

MIMI: “Hivi Mary anajua kinachoendelea kati yetu?”

PRISCA: “Hapana hajui ila leo kajua na kuprove kabisa. Si unakumbuka nilikwambia kuhusu da Mary?”

MIMI: “Sawa bhana kazi kwako na dada yako. Mimi naondoka naomba utanambia kinachoendelea na urudi home mapema sawa?”

PRISCA: “Sawa haina shida”

Na mimi niliondoka eneo lile kurudi zangu nyumbani kulala, kwa upande mwingine nilifurahi Mary kufahamu kinachoendelea kati yangu na mdogo wake.
***

Jumatatu asubuhi Msomali alinipigia simu na akaniuliza maamuzi niliyoyachukua kuhusu lile deal na mimi nilimdanganya kuwa sipo na niko mkoani mara moja, hivyo nikirudi ningemcheki. Na yeye alisema hakuna shida ananipa muda wa mimi kuendelea kufikiria ili nifanye maamuzi sahihi.

Kwa upande wa wateja zangu nao wabeba, ambao tulikuwa na mikataba, nilikuwa na Mama wa2 na Maggy tu kwa kipindi hiki, maana hata madogo wa kule shule Masaki walikuwa likizo ya Pasaka.

Baada ya kuwapeleka wateja zangu Posta muda ule nilimpigia simu Prisca ili nijue kama walirudi home salama. Na baada ya kumpigia alipokea simu na tukaanza maongezi,

PRISCA: “Hi baby”

MIMI: “Umeamkaje na Unaendeleaje?”

PRISCA: “Niko salama Insider hofu wewe.”

MIMI: “Jana mmerudi sangapi?”

PRISCA: “Tulikaa mpaka saa 8 usiku.”

MIMI: “Aiseeh, yale mambo uliyokuwa unafanya jana bila aibu unakumbuka?”

PRISCA: “Hahahaa kwani vibaya Insider?, Wale ni watu wazima washajua kinachoendelea. Siwezi kuficha hisia zangu kwako kisa wao.

MIMI: “Sawa bhana umefanya vizuri, see you letter. Nilitaka kukujulia hali.”

PRISCA: “Ahsante Insider I love you.”

MIMI: “Byee”

Hii jumatatu pia niliongea kwa simu na Muajemi kupitia Whatsapp na yeye alikuwa bado yuko Saudi Arabia na alikuwa akinijulia hali. Muajemi aliendelea kunisisitiza niendelee kuongea na Iryn ili waende Zanzibar akitoka huko, na alisema hataki kwenda nyumbani ikiwezekana aunganishe moja kwa moja mpaka Zanzibar. Na alisema angerudi mwisho wa mwezi huu April, kwa upande wangu sikutaka kumwambia chochote kinachoendelea kati yangu na Iryn.

Biashara ya Uber ilianza kuwa ngumu hasa upande wa request maana abiria walikuwa wa tabu sana. Kilichokuwa kinanisaidia kipindi hiki ni wale wateja zangu wa bank kuwapeleka sehemu mbalimbali. Wateja wengi walikimbilia kwenye bajaji ili kupunguza gharama za maisha, maana nauli zilikuwa juu sana.

Jumatano Mama wa2 alinipigia simu na akaomba tuonane kwake usiku nikiwa natoka kwenye mishe zangu bhasi nipitie pale nyumbani kwake, na mimi niliukubali ule wito.

Baada ya kumaliza mishemishe zangu saa 2 usiku nilikuwa nimewasili kwa mama wa2 na nilikaribishwa ndani nikakaa seblen na yeye alikuwa jikoni. Na muda huu Pili alikuja seblen na alinisalimia pale,

“Shikamoo.”

“Marahaba mke wangu nimekuja hapa kwaajili yako ujue.”

Pili alionekana kuwa na aibu sana maana hta kuniangalia alikuwa anashindwa. Na wakati huu mama wa2 alikuwa dining akiandaa chakula mezani.

MAMA WA2: “Pili umemwona mme wako? anasema anasubiri umalize shule akuoe.”

Pili hakuwa na chakusema maana alishikwa na aibu sana, nilihisi huenda pili ni Virgin bado sio kwa zile aibu na pia alionekana kujipenda sana, Mama wa2 alikuwa na binti mzuri sana.

MIMI: “Mama mkwe mbona Pili ana aibu hivi? Ana umri gani?”

MAMA WA2: “Sema anakuonea aibu wewe hana lolote. Mwaka huu september anafunga miaka 18.

MIMI: “Pili unasomea nini?”

PILI: “PCB”

MIMI: “Nice kumbe nitaoa doctor.”

Na muda huu Pili alionesha kutabasamu, ila ni lile tabasamu la aibu.

Na muda huu nikaribishwa dining kwaajili ya kula dinna na sikuweza kukataa, japo nilisema nitakula kidogo ili nikirudi home nisigombane na Mama J.

Mimi ndo nilikuwa wa kwanza kumaliza kula na Mama wa2 alishangaa sana.

MAMA WA2: “Insider ongeza chakula hata kidogo maana nilipika kingi kwaajili yako.”

MIMI: “Mama mkwe hata usijali na unanijua vizuri mimi, ukweli ni kwamba navyotoka huko nilikuwa nimekula tayari.”

Nilikwenda kukaa seblen na baada ya dakika 10 Mama wa2 alikuja ili tuongee na alikuwa na bahasha mkononi.

MAMA WA2: “Insider mzigo wako huo hapo.”

Aliiweka ile bahasha mezani na mimi nikaichukua na nilivyoifungua nikaona kuna hela ndani.

MIMI: “Mama mkwe nilijua nina jaza mafomu ya mikopo.”

MAMA WA2: “Insider mkopo mdogo huo huna haja ya kujaza forms nimekusaidia kwa njia nyingine na hakuna riba. Wewe utarejesha hio hio amount, kama utakuwa unakwama marejesho bhasi uwe unasema tujue tunasaidianaje kurejesha.”

MIMI: “Ahsante sana mama mkwe, mimi sikujua unaniitia hili kabisa.”

MAMA WA2: “Kuwa na amani Insider”

Sikutaka kabisa kuuliza maswali sana, niliendelea kukaa pale huku tukipiga story mbalimbali na alisema weekend hii tutakwenda kuangalia nyumba yake anayoijenga Madale.

Niliaga pale kwake na nilimshukuru sana Mama wa2 kwa lile jambo na nikaondoka kurudi nyumbani. Wakati niko njiani nilikuwa na furaha sana kwakweli sikutegemea kupata kile kiasi cha pesa kwa haraka vile.

Habari mbaya kwenye hii week ya kwenda Pasaka, Uber walisitisha huduma za usafiri wa TAX kwenye Application yao, ila huduma za Bajaji na Bodaboda zilikuwa zikiendelea kama kawaida na ilikuwa 14/04/2022 alhamis kitu kama hicho, ila waliendelea na wateja wa Card tu na kampuni ambao walikuwa wameingia nao mikataba.

Hizi zilikuwa ni habari mbaya sana kwa madereva tulikokuwa tukitumia hii App. Kitendo cha Uber kusitisha huduma kwa upande wa magari kilinipa stress sana maana kwa Tanzania wateja wengi wanalipa kwa cash, nikawaza hapa itabidi nitumie Bolt ambayo nilikuwa siipendi.

**********

Ijumaa jioni Mzee Pama alinipigia simu na akaomba jumamosi jioni tuonane kwani ana mazungumzo muhimu na mimi, nilimkubalia na akasema tutakutana pale Budget Bahari Beach. (Mzee wa Ununio mwenye mchepuko wake Kigamboni)

Ijumaa mimi nilikomaa na Bolt na nilipiga kazi mpaka saa8 usiku ndo nikarudi kulala, biashara ilianza kuwa ngumu sana wateja walikuwa wakuokoteza sana. Yaani unaweza kaa hata saa2 bila ya kupata request na hapa ndo nikapata wazo la kununua bajaji, maana nilikuwa nikiwasiliana na madereva wa bajaji walikuwa wanasema kwa kipindi hiki wanapiga sana hela.

Nikakumbuka wife ana pesa kwa Baba yake na kuna kipindi alitaka kuzichukua nikamkatalia, nilimwambia aziache kwanza Baba yake azitunze. Baba yake aliahidi kumpa milion 5 ili zimsaidie kwenye mambo yake. Mzee wake alimwambia zile pesa ambazo anampa zilikuwa ni ada zake za masomo, sababu aliamua kuolewa bhasi atampa zimsaidie kwenye mambo yake.

Nikaplan nitaongea na wife ili tununue Bajaji na itakuwa ya kwake pesa itakayokuwa inapatikana itaingia kwenye mfuko wake. Niliona pale ni wazo zuri maana kama jambo litafanikiwa bhasi nitaweza kupunguza gharama nyingi sana.

Jumamosi ndo siku ambayo nilikuwa na miadi na Mzee Pama, niliamka saa11 asubuhi na hii siku nilipiga sana kazi na angalau pesa niliipata, japo Bolt niikuwa siipendi ila nilikuwa sina jinsi.

Saa11 jioni nilikuwa niko pale Magufuli stand mbezi mwisho nikisubir request na hapo nilikuwa nimeset destination ya Bahari Beach ambako nilikuwa nina miadi na Mzee.

Nilisubiri sana pale lakini sipati request na kuchoma mafuta kutoka mbezi mpaka Bahari beach niliona ni mbali sana afu hasara. Nilisubiri kwa saa 1 na nusu hivi ndo nikapata mteja alikuwa anaelekea Tegeta nyuki karibu na shule ya Canossa.

Baada ya kumshusha abiria nilikwenda na ile barabara ya nyuki inayokuja kutokea Bahari beach ndo nikaunga kwenda Budget.

Nilifika pale saa 2 kasoro lakini kwa upande mwingine mzee alikuwa bado hajafika, na ilimchukua dakika 20 Mzee Pama kufika eneo lile. Mzee Pama alifika moja kwa moja nilikokuwa nimekaa maana nilimuelekeza,

MZEE PAMA: “Nimeona gari yako hapo parking nikajua umefika muda sana, kwanza nisamehe kwa kukuchelewesha najua bado upo kazini.”

MIMI: “Usijali Mzee wangu kuwa na Amani kabisa.”

MZEE PAMA: “Kulikuwa na foleni kali sana pale Africana mpaka najuta kwanini sikupita barabara ya chini.”

MIMI: “Leo ni weekend lazima pawe na foleni, za siku na pole na majukumu Mzee wangu.

MZEE PAMA: “Ahsante sana kijana, kazi zinaendelea vipi kwa upande wako?”

MIMI: “Mzee kwa upande wangu ni ngumu, maana juzi tu hapa Uber wamefunga ofisi yao na wateja wamekimbilia bajaji, nauli ziko juu sababu ya kupanda kwa mafuta.”

MZEE PAMA: “Kweli kabisa bei za Petrol na diezel nimeona ziko juu sana hii ni hatari sana.”

Na muda huu dada alikuwa amefika kutusikiliza, wakati mara ya kwanza amekuja nilimwambia asubiri kidogo.

MZEE PAMA: “Kijana unaweza agiza chochote unachotaka kuwa huru.”

MIMI: “Dada naomba mchemsho wa Kuku na maji ya kunywa”

MZEE PAMA: “Niletee windhock na kuku choma nusu.”

Dada aliondoka na sisi tuliendelea na mazungumzo yetu,

MIMI: “Mzee uliniambia una jambo muhimu unataka kuniambia.”

MZEE PAMA: “Kuna jambo nilitaka unisaidie maana nalifanya kwa siri na sitaki ndugu au mtu yoyote wa karibu yangu alijue. Kwa muda mfupi tuliofanya kazi nimetokea kukuamini sana kijana na wewe ndo unajua siri yangu ya ule mchepuko hakuna anayejua mwingine zaidi yako.”

MIMI: “Kumbe! ni jambo gani mzee usiwe na wasiwasi mimi nitakusaidia kama litakuwa chini ya uwezo wangu.”

MZEE PAMA: “Ile nyumba ya Mbweni nayojenga bila shaka utakuwa unaikumbuka, tulikwenda wote kabla ya kwenda Kigamboni.”

MIMI: “Naikumbuka vizuri kabisa hata sasa naweza kukupeleka, ile mitaa yote ipo kichwani.”

Na muda huu mzee alicheka sana,

MZEE PAMA: “Kijana uko vizuri, sasa ile nyumba ni ya yule mke mdogo, niliamua kumjengea Mbweni ile niwe naye karibu ili hata nikitaka kumwona iwe rahisi. Kwasasa iko kwenye finishing kuna vitu vya kumalizia (kama kuweka makabati jikoni, masink, taa za ndani na nje, kuweka pavings, tiles, kupaka rangi na kutengeneza bustani nknk). Nataka wewe unisaidie kusimamia mpaka finishing ikamalike maana mimi ninasafari na nitarudi 26/04.

Nilishangaa kuona ule mjengo mkali ni wa yule mchepuko wake wa Kigamboni.

MIMI: “Mzee hilo halina shida ni jambo dogo sana kwangu nitalisimamia vizuri kabisa na wewe utafurahi.”

MZEE PAMA: “Sasa nitakukabidhi pesa na nitakupa list ya vitu na material nayohitaji kuweka mle ndani, nakuomba usimamie manunuzi na usitoe hela mpaka kazi iwe imefanyika, Constructor wa kwanza tuligombana alikuwa muhuni huyu ni mpya simwamini bado.”

MIMI: “Mzee hilo ondoa shaka kila kitu kitakwenda vizuri”

MZEE PAMA: “Ahsante sana gharama zako tutaongea nikirudi wewe usiwe na wasiwasi.”

MIMI: “No problem Mzee wangu.”

Tulimaliza maongezi pale na mimi nilikuwa nimemaliza kunywa soup yangu, alifanya malipo na tukaongozana kwenda kwenye gari yake, ilikuwa ni Fortuner mpya kabisa na namba zake za usajili zilisomeka DY.

“Kijana fungua mlango ingia”

Nilivyoingia ndani Mzee alifungua drow na akatoa bunda za pesa ambazo alisema jumla ni 37 million.

MZEE PAMA: “Makubaliano yetu ni 36.5 million, hapo itabaki laki 5 hiyo itakusaidia mafuta, chakula na mambo mengine.”

Na muda huu akatoa karatasi ambayo imeandikwa mahitaji ya kununua kwaajili ya ujenzi.

MZEE PAMA: “Na haya ndo mahitaji yenyewe naomba uwe makini sana kwenye hizi materials, huku ndo tunakopigwa hela sana na unaweza wekewa fake, hakikisha fundi hakuzidi ujanja.”

MIMI: “Mzee hili halina shida kwangu wewe fahamu umekutana na mtu sahihi.”

MZEE PAMA: “Nikirudi tutaonana na ujenzi unaendelea kule, jumatatu unaweza kwenda kuanza kukagua, nitampa namba yako na wewe nitakupa namba ya fundi, mimi naondoka kesho ila tutakuwa tunawasiliana kwa whatsapp”

Mzee alinipa namba ya simu ya constructor na alitoa bahasha ili niweke zile pesa na tukaagana muda huo.

Mimi nilikwenda kwenye gari yangu na nikaziweka zile Pesa kwenye drow na nikaanza safari ya kurudi home. IST ilikuwa imebeba pesa za kununua wenzake kama watatu hivi, zilikuwa Pesa nyingi sana na sikuelewa kwanini Mzee Pama kaniamini sana vile.

Barabarani niliendesha gari kwa spidi sana maana niliogopa nisije kutekwa na Pesa za watu muda ule, na mapema tu nilikuwa nimefika home.

Na huu usiku Mama wa2 alinipigia simu akafanya booking ya gari kwaajili ya kesho ambayo ni Pasaka na tukakubaliana tuonane kwake 08:00 asubuhi.

********

Asubuhi nilimka mapema nikafanya mazoezi ya viungo kwa ujumla na baada ya hapo nikaingia bafuni kuoga na muda huo mama J alikuwa amelala bado.

Wakati navaa ndo nasikia Mama J akiniita,

WIFE: “Baba J asubuhi yote hii unakwenda wapi? Inamaana hujui leo kuna sikukuu?”

MIMI: “Mke wangu nakwenda kutafuta hela si unajua leo sikukuu kazi ni nyingi, hata leo na kazi na mtu.”

WIFE: “Sawa ila sisi tunakwenda kula sikukuu nyumbani.”

MIMI: “Mimi sina tatizo kama umeridhia ni jambo jema kuwa na familia labda unambie utahitaji kiasi gani cha pesa nikupe.”

WIFE: “Tutatoka out pia wewe utakayoona inatosha sawa tu.”

MIMI: “Afu naomba tuongee jambo ili ukienda huko nyumbani uone unafanyaje.”

WIFE: “Jambo gani?”

MIMI: “Nataka tununue Bajaji maana Uber imekuwa ngumu kwa sasa wateja wamekimbilia Bajaji. Ulisema kwa mzee wako kuna hela kama unaweza ongea naye akupe hizo hela, lengo langu hio bajaji iwe yako na Pesa itakayokuwa inapatikana itaingia kwako. Nataka kupunguza gharama si unaona tuna ujenzi kule na pesa zinaishia kule?. Ukifanikisha hili sasa hapo nitakupa mpango mzima.”

WIFE: “Sawa ni jambo zuri sana nitaongea na Mzee na nitakupa mrejesho badae nikirudi.”

MIMI: “Ila usiseme lolote kwa Mzee, wewe angalia ni namna gani utaongea naye ili akupe hizo hela, usiongee masuala yoyote.”

WIFE: “Nimekuelewa Baba J usiwe na wasiwasi.”

Nilitoa laki moja nikampa zimsaidie kwenye matumizi yake ya sikukuu na mimi nikaondoka kuelekea kwa Mama wa2.

Nilifika mapema kabisa pale nyumbani na nilikuwa getini pale nje, nilipiga honi na Mama wa2 alitoka haraka ni kama alikiwa akinisubiri na alitoka na mwanae Pili wakaingia kwenye gari.

“Insider mambo, nataka twende sokoni sasa sijui twende wapi nahitaji na Kuku wa kienyeji wawili wakubwa”

“Hapa uhakika na soko kubwa twende Tegeta nyuki naamini utapata unachotaka.”

“Sawa twende bhasi chap.”

Tulikwenda Tegeta Nyuki sokoni kufanya manunuzi na siku hii soko likikuwa na wateja sana hata parking zilikuwa za shida. Tuliingia sokoni kufanya manunuzi na mimi nilikuwa nikimsaidia kufanya manunuzi na kupeleka mizigo kwenye gari.

Mimi hata niwe smart vipi kwenye suala la kuwasaidia wateja nilikuwa active sana, na hiki kilifanya wateja wanipende sana.

Tulitumia kama 1 hour hivi mpaka kumaliza manunuzi na baada ya hapo tulirudi home.

MIMI: “Mama mkwe mbona leo umenunua vitu vingi sana?”

MAMA WA2: “Na wageni leo ndomana, kuna rafiki zangu wa kazini wanakuja na pia kesho nina ugeni wa mdogo wangu kutoka Moshi.”

PILI: “Mama kumbe mamdogo Joana anakuja kesho.”

MIMI: “Kumbe una mdogo wako hongera sana.”

MAMA WA2: “Ehh Pili anakuja kesho…..Insider kesho tutakwenda AirPort kumpokea wote.”

MIMI: “Sawa haina shida Mama mkwe.”

Tulirudi pale kwa Mama wa2 na nikawasaidia kutoa vitu kwa gari na nikaingia ndani kupata Breakfast.

Na wakati niko kwa Mama wa2, Maggy pia alinipigia simu kuniwishi Pasaka na akanambia kama sitojali niende kwake maana hana kampani.

Mama wa2 hii siku alionekana kuwa busy sana na mimi sikutaka kuendelea kukaa pale na nilitamani sana kuondoka.

MIMI: “Mama mkwe kuna kazi yoyote ya mimi kufanya? Nataka nikukimbie.”

MAMA WA2: “Insider kwakweli hakuna nilitamani sana twende kule Madale ila tutakwenda kesho. Unataka kuondoka na hujala? Subiri chakula.”

MIMI: “Usijali nitakula kesho acha nikawasalimie ndugu zangu.”

Nilitoka pale kwake ilikuwa saa 7 mchana na wakati niko kwenye gari nilimpigia simu Prisca kumuwish sikukuu ya Pasaka. Na pia hii siku nilitamani sana ningeimaliza na prisca.

MIMI: “Hi bae, happy Easter”

PRISCA: “Thank you honey nilikuwa naogopa kukupigia maana nilijua upo nyumbani na mke mkubwa.”

MIMI: “Yeah sure ulifanya vizuri.”

PRISCA: “Honey karibu home bhasi hapa napika vitamu kwaajili yako, are you coming?”

MIMI: “Mmmh hata wewe unajua kupika? Hahahahahaha.”

PRISCA: “So unanicheka kwamba sijui kupika?, Insider hizo dharau has to stop.”

MIMI: “Baby utani tu unachukia, nilitaka kuspend na wewe leo vipi it’s possible?”

PRISCA: “Kwa leo ngumu maana mzee yupo na amesema tutatoka out kama family badae, pia niko period hapa mwenzako.”

MIMI: “Oohh sawa haina shida have funny mummy.”

Niliona Prisca hana deal tena kaanza kuniletea story za period tena na nikasepa zangu kwenda kwa Maggy Mikocheni.

Baada ya kufika Mikocheni kuna duka niliingia nikanunua wine na soda na mazaga mengine huyo nikaelekea kwake. Nilivyofika pale kwake nilifungua geti na nikaingia ndani na nikapark gari usawa wa apartment yake.

Niligonga mlango haikuchukua muda alitoka kufungua lakini alishangaa baada ya kuniona mimi ni kama hakuamini hivi.

MAGGY: “Yaani Insider sikujua kama unakuja ujue.”

MIMI: “Unipe mwaliko afu nisije? haiwezekani kabisa.” Na muda huu nilikuwa nampa ule mfuko.

MAGGY: “Waow! Umenunua nini?, Jamani thank you, karibu ndani.”

Niliingia ndani akafungua ile wine na akaniletea glass.

MAGGY: “Insider wewe endelea mimi napika huko jikoni. Nimefurahi kukuona maana nilikuwa bored hatari kuna best yangu kanipiga chini.”

MIMI: “Wewe endelea usijali.”

Maggy alionekana kufurahi sana muda huu ni kama nilimsaprize sana kwa upande wake. Na mimi nilikaa seblen nikaona acha niende jikoni tukaendelee na story.

MIMI: “Nakuona upo busy mwenyewe.”

MAGGY: “Nataka nimalizie kupika chap hapa vitu vingine nilikuwa nishapika tayari.”

MIMI: “Leo nitaonja mapishi yako kwa mara ya kwanza.”

MAGGY: “Hahahaa hivi hujawai eeh”

MIMI: “Sijawai zaidi ya mayai ya kukaanga”

MAGGY: “Usijali mimi niko vizuri sana jikoni. Insider nimefurahi sana ujio wako ujue maana niliona siku ishaanz kuwa mbaya.”

MIMI: “Usijali mimi nipo na wewe mpaka majogoo kama utataka, I’m not going anywhere.”

MAGGY: “Badae itabidi tutoke out bhasi au unaonaje.”

MIMI: “Nishasema nipo hapa kwaajili yako wewe utakachosema mimi nitakusikiliza leo.”

MAGGY: “Umetoka kazini?”

MIMI: “Hapana leo sikukuu napumzika, pesa zipo tu.”

MAGGY: “You are right.”

MIMI: “Ukiwa jikoni unaonekana kuwa sexy sana.”

MAGGY: “Mmmh Insider kweli? mimi naona unanizingua tu hapa.”

MIMI: “Kweli you look so sexy”

MAGGY: “Mmhh”

Tulipiga sana story hii siku na Maggy ila kwenye mazungumzo yetu nilikuwaga sithubutu kabisa kuongelea suala la mahusiano yake. Maana ningempa greenlight ya kuuliza mahusiano yangu na mimi sikutakaga wateja zangu wajue maisha yangu.

Saa 11 jioni tulitoka na tulikwenda “Cape Town Fish Market” tulikaa pale mpaka saa 5 usiku. Sikutegemea kuona Maggy kuwa mnywaji mzuri wa pombe kiasi kile na alizipeleka Savannah 8. Kwani nilikuwaga namchukuliaga mwanamke ambaye yuko busy na mambo yake. Maggy alionekana kulewa sana hii siku.

Tulitoka pale Capetown mpaka saa 6 usiku kasoro na nilidrive mpaka Mikocheni anakoishi. Nilifungua geti na nikaingiza gari ndani, na muda huu Maggy alioneka kalewa sana tofauti na wakati tunatoka kule Capetown. Japo alikuwa anajitambua, nilimsaidia kumtoa kwa gari na tukaingia ndani.

TO BE CONTINUED
Nitarud
 
EPISODE 26

“A TRUE STORY BY INSIDER”

Jumatatu ya Pasaka asubuhi nilifanya mawasiliano na yule constructor wa Mzee na nikamwambia baada ya lisaa nitakuwa Mbweni na yeye alisema yuko njiani ndo anaelekea.

Kwa upande mwingine yale materials ya kununua nilimtumia picha Mzee Mollel na alinisaidia kunitajia bei na kunipa connection kwa sehem yanakopatikana, alinitumia namba za baadhi ya masupplier akanambia nikiwapigia simu niwaambie yeye ndo amenikonekti.

Baada ya kufika Mbweni nilikuta kazi zikiendelea na mimi niliwasalimia Mafundi na Jamaa alikuwa amefika tayari.

Sababu alikuwa anajua kinachoendelea pamoja na ujio wangu, hata hakuwa na maswali zaidi alisema nimpe pesa akanunue materials.

“Kwenye kununua materials tutakwenda wote mkuu usiwe na wasiwasi.”

Na muda huu nilifanya kuwasiliana na baadhi ya supplier na tukapata mmoja pale Africana ndo alikuwa na bei nzuri.

Tulikwenda wote na Jamaa mpaka Africana kuna duka kubwa sana pale lipo mataa ya Africana, mkono wa kushoto kama unakwenda Juliana.

Tulifanya manunuzi ya materials mbalimbali na tukarudi Mbweni, vifaa vyote nilisimamimia manunuzi. Jamaa kama alimind hivi kwanza, pia hakuwa akiamini kuona nayajua maduka vile, kumbe nyuma ya Pazia alikuwepo mzee Mollel anayenipa CODE.

Sababu hii siku nilikuwa na miadi na Mama wa2, nilimwaga jamaa na nikaondoka. Nilitoka pale Mbweni kuelekea Mbezi Beach na muda huo ilikuwa saa 6 kasoro za mchana.

Hii siku tulikuwa tunakwenda kumpokea mdogo wake Airport na kuhusu kwenda kuangalia nyumba yake alisema tutakwenda siku nyingine.

Mama wa2 alitumia dakika 30 kutoka ndani na tukaelekea Airport.

“Insider Unaendeleaje.”

“Safi tu, mgeni ataingia sangapi?”

“Saa 8 atakuwa amefika tayari.”

Tuliwasili pale JNIA na tulikwenda moja kwa moja mpaka Terminal 2 ndo tukapark gari. Tuliamua kwenda kukaa kwenye kimgahawa tukimsubiri mgeni.

“Insider leo jioni nataka twende Masaki na wanangu tukatembee.”

“Sawa haina shida mimi nipo free leo.”

“Nilipata taarifa Uber wanasitisha huduma zao vipi kwako utafanyaje?.”

“Kwa wateja wa Card na kampuni bado wanaendelea ila wanaotumia card ni wachache sana, wateja wa cash ndo wengi kwa bongo hapa. Sio mbaya sana lakini maana Bolt bado wapo japo imeniathiri sana.”

“Pole sana ndo changamoto hizo naamini watarudi soon.”

“Ni mambo yanayohusisha serikali acha tuone itakuwaje.”

Suala la Uber kusitisha huduma zao kwa upande wa magari ni kutokana na LATRA kuwataka kupunguza kamisheni zao kutoka 25% mpaka 15%. Madereva wa Tax mtandao wolilamika kwa mamlaka husika kuwa hizi kampuni zinatoza kamisheni kubwa sana. Uber hawakuwa tayari kupunguza kamisheni zao kwani walisema wanatozwa kodi na tozo kibao hivyo wangeendesha biashara kwa hasara.

Tuliendelea kukaa pale na Mama wa2 huku story zikiendelea maana ndege ilichelewa kutoka KIA kwa taarifa ambazo Mama wa2 alizipata.

Saa 9 kasoro ndege iliwasili na na baada ya dakika 15 mamdogo alitoka na wakakumbatiana na dada yake pale. Walionekana kumisiana sana.

Nilimsaidia kubeba bag lake na tulikwenda parking tulikokuwa tumepark gari na tukaanza safari ya kurudi Mbezi Beach.

MAMA WA2: “Insider huyu ndo mdogo wangu wa mwisho anaitwa Joana.

MIMI: “Nimeona pia mmefanana sana, Joana karibu sana Dar es Salaam.”

“Ahsante.”

MAMA WA2: “Huyu anaitwa Insider ni mtu wangu wa karibu sana.”

MIMI: “Mama mkwe hujawai kunambia kuwa una mdogo mzuri hivi.”

Na wote waliishia kucheka muda huu na walikuwa wamekaa siti za nyuma.

Njiani walikiwa busy sana wakiongea mambo yao na tulitumia kama dk40 kufika nyumbani maana hakukuwa na foleni kabisa.

Tuliingia ndani muda ule na mimi nikatoa bag la mgeni nikaingiza ndani.

Baada ya kuingia ndani mamdogo alisalimiana na kina Rachel na Pili na mimi muda huu nilikuwa nawaza msosi maana njaa ilikuwa inanigonga balaa, toka asubuhi nilikuwa sijaingiza chochote tumboni.

Mama wa2 alitukaribisha dining kwaajili ya lunch na mimi ndo nilikuwa wakwanza kufika pale. Nilikuwa nimeshapazoea kwa Mama wa2 ilikuwa kama niko nyumbani tu.

Na wakati tuko dining Mama wa2 aliwaambia bint zake wajiandae kwaajili ya kutoka out. Mama wa2 alikuwa busy sana na mdogo wake hii siku hata nilipomaliza kula nilimshukuru kwa chakula na mimi nikaenda kukaa seblen.

Joana pia alikwenda kujiandaa na wakati huo bint zake walikuwa wako tayari wamejiandaa.

MAMA WA2: “Insider tunakwenda wapi eti?”

PILI: “Mama twende Slip way.”

MIMI: “Kama watoto wanataka kwenda huko tuwapeleke haina shida.”

MAMA WA2: “Bhasi tutakwenda huko.”

Na muda huu akina Pili na Rachel walionekana kufurahia sana kwenda huko.

Baada ya dakika 20 mamdogo alikuwa naye kajiandaa na ametoka hao tukaanza safari na muda huo ilikuwa saa 11 jioni.

Tulitumia dakika 25 kufika eneo lile na hii siku palionekana kuwa busy sana na tulikwenda upande wa chini wa Restaurant.

Tulitafuta sehemu nzuri ya kutosha watu sita na tukakaa, kwenye hii meza mimi pekee ndo nilikuwa mwanaume pale na hii ilikuwa ikinipa ufahari flani hivi.

Kila mtu aliagiza anachotaka kwa upande wangu sikutaka kuagiza chakula maana nilikuwa nimeshiba, niliagiza heineken 3 tu maana sikutaka kulewa hii siku. Kwa upande mwingine mama wawili aliagiza bucket ya Savanna kwaajili yake na mdogo wake.

Story zilikuwa zimetawala meza yetu tukicheka na mimi nilikuwa nimekaa karibu na Pili nampigisha story sana,

Sasa wakati dada analeta vinywaji Pili alishangaa sana kuona dada kaniwekea heineken pale mezani.

PILI: “Uncle Insider na wewe unakunywa kumbe?”

MIMI: “Nakunywa kwaajili yako hapa.”

PILI: “Toka hapa! mimi situmii pombe”

MIMI: “Wewe ni mchaga soon utaanza kutumia, muulize mama yako alianzaje kutumia. Unataka sikuonjeshe kidogo?”

PILI: “Aku sitaki mimi. Kwanza Baba yangu sio Mchagga”

Pili alikuwa kashanizoea kwa muda mfupi hata Mama wa2 alishangaa sana kuona Pili kanizoea haraka vile.

Mida ya saa moja usiku wakati tukiendelea kunywa na kupiga story, Prisca alinipigia simu, nikaamua kutoka eneo lile ili nikaongee naye mbali na pale.

PRISCA: “Hello baby how you doing?”

MIMI: “Niko poa za toka jana.”

PRISCA: “Safi tu, nimekumiss”

MIMI: “Jana ulinambia mnatoka as family nipe ripoti.”

PRISCA: “Insider ungekuwa unanijali ungekuwa ulinipigia simu na ukajua kinachoendelea.”

MIMI: “Aisee, nijue kinachoendelea kwenye mambo ya familia yenu?, naona kama unanikosea.”

PRISCA: “Sasa unataka ripoti ya nini?”

MIMI: “Ripoti niliyotaka mimi nijue ulirudi sangapi, Jana sikutaka kukutafuta maana nilijua utakuwa busy na Familia.”

PRISCA: “Okay we had funny yesterday, inshort we enjoyed.”

MIMI: “Nice na uko wapi kwa sasa?”

PRISCA: “Niko home nimelala on bed. Nimekumiss nataka nikuone.”

MIMI: “Acha uongo unanimisije na upo period?”

PRISCA: “Insider unataka kumaanisha kwasababu niko period siwezi onana na wewe? You only want sex from me that's all you care about.”

MIMI: “Prisca mimi naona hayo ni mawazo yako, ila naomba utambue kitu kimoja. Usifikiri mimi kama napenda sana kumchepuka Mama Junior na ninampenda sana. Unapaswa kunipa vile navyokosa kwa Mama Junior na sio kulalamika, kumbuka ulichagua mwenyewe na hukulazimishwa na kama unaona nakuumiza unaweza kuniacha na maisha yangu.”

PRISCA: “Leo ndo nimeprove upo na mimi kwasababu ya shida zako na huna hata tone la upendo kwangu, Ahsante nashukuru.” Akakata na simu.

Mimi sikutaka kumpigia tena simu niliamua kumpotezea na nikasema hasira zake zitakuwa sababu ya Period.

Wakati nimerudi pale mezani Mama wa2 aliniangalia afu akatabasamu

“Insider naona ulikuwa kujenga matofali”

Na mimi niliishia kucheka tu muda huu.

Tulikaa mpaka saa4 usiku ndo tukatoka pale na muda huu Mama J alikuwa akisumbua sana kwa kupiga simu.

Baada ya kuwashusha akina Mama wa2 alinipa malipo yangu na mimi nikaelekea nyumbani.

Nilimkuta wife yuko seblen anaangalia movie na mimi niliwasalimia na nikaunganisha bafuni kuoga.

Wakati nimetoka bafuni nilimkuta wife yuko kitandani amejilaza kizembe.

MIMI: “Nambie swahiba toka jana hatujaongea kabisa, hujanambia sikukuu ilikwendaje.”

WIFE: “Ilikuwa poa tu, Mama anakusalimia pia amesema uache tabia mbaya. Kwanini hupendi kujumuika na sisi?”

MIMI: “Usijali mwambie nitakwenda msalimia, na vipi kuhusu Mzee ulifanikiwa kuongea naye?”

WIFE: “Ndio alisema mwisho wa mwezi huu atanipa hizo hela.”

MIMI: “Wow nice umetisha sana swahiba, nafanya haya mambo kwaajili yako na hii bajaji tutatumia jina lako.”

WIFE: “Sawa haina shida, twende ukale maana leo nimekupikia vitamu.”

MIMI: “Sawa tangulia nakuja.”

Muda huu nilikaa kitandani maana nilikuwa nafuraha sana kuona jambo limefanikiwa tayari.

**********

Hii week baada ya Pasaka nilikuwa nashinda tu kule kwa Mzee Pama Mbweni. Asubuhi nikishawapeleka wateja wangu Posta naunganisha moja kwa moja mpaka Mbweni. Sikutakaa kaa mbali kabisa na eneo la tukio nilitaka kusimamia kila hatua kwenye ile nyumba.

Kazi ilikuwa inakimbia balaa na kwa upande mwingine mtu wa bustani alikuwa amekuja tukakubaliana bei na nikamwambia miti na maua tutakwenda nunua wote.

Mpaka kufikia jumapili nyumba ilikuwa imekamilika kila kitu kwa ndani na ilibaki vitu vidogo nje vya kumalizia kama kuweka tank na kumalizia pavings. Jumatatu ndo tulimalizia kila kitu na nikatafuta mtu wa kufanya usafi mle ndani, nje na kutengeneza barabara inayokwenda kwenye ile nyumba maana ilikuwa mbovu sana.

Kufikia jumatatu kila kitu kilikuwa kimekamilika vilibaki vitu vichache sana ambavyo sio vya lazima, lakini nyumba ilikuwa tayari kwaajili ya kuhamia.

Katika zile Pesa ambazo alinikabidhi mzee nilibakiwa na kama 3,200,000/= na hapo ndo nikajua jamaa alimpiga mzee japo pia nilipata discount kwenye mizigo ila kulikuwa na balance kubwa sana.

Niliitamani sana hii pesa lakini niliogopa jamaa anaweza kunisnitch kwa Mzee akampa hesabu za vitu na gharama zote afu nikapoteza trust kwa Mzee. Palepale nikachomoa million moja nikasema hii nitaitolea maelezo kwa Mzee ila hii amount inayobaki nitamrudishia.

***********

Kwa upande mwingine Jumapili ndo siku ambayo Pili alikuwa ana rudi shule hivyo Mama wa2 aliomba kampani yangu.

Nilitoka Mbweni kuelekea Mbezi Beach kwa Mama wa2 na saa 7 mchana nilikuwa pale.

Saa 8 mchana ndo tulitoka kuelekea Bagamoyo shuleni. Tulitumia saa moja na nusu kufika Bagamoyo shuleni na Mama wa2 alikwenda kumkabidhi.

Na hii siku walionekana Wazazi wengi wakiwarudisha watoto wao shule.

Baada ya kumuandikisha kuna sehemu tulikaa tukiwa tunaongea na mimi nilimshauri sana Pili asome kwa bidii na akae mbali na wanaume. Ilibidi nimchane ukweli ajitunze Mafisi “wazee wa kula kimasihara” sio watu wazuri Kabisa awe makini.

Pili alionekana kuwa makini sana akisikiliza ushauri wangu na nilitoa laki moja nikampa itamsaidia kama pocket money.

Niliona aibu kumwacha bila kitu afu mama yake alikuwa kanisaidia mkopo wa Pesa nyingi, niliamua kurudisha shukrani kwa njia hiyo.

Pili alishukuru na alifurahi sana, akasema next time nikamchukue na Mama yake pia alimpa Matron namba yangu incase kama kuna lolote wanaweza kunipigia na mimi. Na mama wa2 alininiandikisha mimi kama Uncle wa Pili.

Tuliondoka pale shuleni na kuanza safari ya kurudi Dar na njiani tulikuwa tukiongea mambo mengi sana na Mama wa2.

MAMA WA2: “Insider mwanangu Pili amekuzoea haraka sana, the way ambavyo unaongea naye nilikuwa najiskia faraja sana. Baba yake hajawai hata siku moja kumpa ushauri binti yake nashukuru sana kwa leo.”

MIMI: “Pili ni kama mdogo wangu lazima nihakikishe anafikia malengo yake na kama unajambo lolote usisite kunambia.”

MAMA WA2: “Next time utamfata wakifunga shule.”

Tulitumia lisaa kufika Mbezi Beach nikamwacha kwake na mimi nikarudi zangu home mapema sana.

Usiku mzee alinicheki akanambia kesho nikamchukue Airport ndo anarudi na anatarijia kuingia saa 7 mchana na alinisisitiza sana kuwa ontime, maana tungeenda na kukagua nyumba kule Mbweni.

Asubuhi nilimka mapema na nikafanya usafi wa gari mwenyewe na baada ya kumaliza nilirudi ndani ili nipate kifungua kinywa.

*********

Tarehe 26 ndo siku ambayo mzee alirudi kutoka safari na ilikuwa ni siku ya Muungano. Na mimi mapema sana nilikuwa pale Terminal 3 nikimsubiri.

Nilimcheki dada Tyna akanambia yuko busy atanichek mida kidogo, na muda huu nilikuwa nikipiga story na yule jamaa yangu mlinzi.

Saa 8 kasoro ndo muda ambao mzee Pama aliwasili pale JNIA na nilimpokea na baada ya dakika chache tuliondoka maeneo yale.

Safari yetu ilikuwa ni kwenda moja kwa moja mpaka Mbweni ili afanye ukaguzi wa nyumba. Na tulitumia saa moja na nusu kufika pale

Mzee alifanya ukaguzi wa nyumba na aliridhika kuona jinsi ujenzi ulivyokuwa umekamilika vizuri tena kwa viwango vya hali ya juu. Pia alishangaa kuona nimetengeneza ile Barabara na imekaa vizuri, alishangaa kuona nimetengeneza bustani mpaka nje ya geti na palikuwa pamejengwa vizuri. Mzee pia alinisifu kwa kufanya usafi wa nyumba nje na ndani.

Mzee alimjengea mchepuko wake mjengo mkali sana tena wa kisasa, nyumba ilikuwa kubwa ya vyumba vinne.

MIMI: “Mzee naona unataka kuwa na Familia kubwa vyumba ni vingi sana.”

MZEE: “Nataka anizalie watoto wa3 hata pale tayari ni mjamzito.”

MIMI: “Hongera sana Mzee ni jambo la neema hilo.”

MZEE: “Kabisa, Kijana niseme Ahsante kwa kazi nzuri uliyofanya umenifurahisha sana, materials ni zenyewe hakuna ulichokosea.”

MIMI: “Mzee nilikuwa namsimamia Fundi mwanzo mwisho nilikuwa nakuja asubuhi nashinda na Mafundi jioni narudi nyumbani. Ndomana unaona kila kitu kimeenda vizuri na kwa wakati sahihi.”

MZEE: “Hii nyumba nimejenga kwa siri sana hakuna anayejua kabisa hili suala.”

MIMI: “Sasa suala la watoto vipi hutaki wajuane?”

MZEE: “Hao hakuna shida watajuana tu ila sitaki ifahamike kama mke mdogo anakaa huku italeta shida.”

MIMI: “Sawa mzee hapo nimekuelewa”

Mzee Pama alikuwa ni mzee wa umri wa miaka 60-65 alikuwa anacheza humu ila alikuwa ni dizaini ya wale wazee wajanja au wahuni.

Tulitoka pale Mbweni saa 11 jioni na Mzee alinambia nimpeleke kwake Ununio.

Wakati tumeingia kwenye gari nilifungua drow na nikatoa invoices za manunuzi na nikamkabidhi, na alianza kuzitizama muda ule.

MIMI: “Mzee na hii Pesa ndo ilibakia kwenye manunuzi.”

MZEE: “Kijana kama pesa imebaki ni yako, umefanya kazi kubwa sana. Bila kumsimamia Fundi vizuri angenipiga yule mshenzi.”

Nilimshukuru Mzee na nikawasha gari ili tuondoke eneo lile. Nilimpeleka Mzee kwake ununio na akaniahidi kunitafuta kwani kuna vitu vya kununua vingi anataka nimsaidie kusimamia.

Muda huu nilijikuta nam-miss sana Iryn kwakweli, kwani ndo ilikuwaga mida ya kwenda kwa Iryn kumchukua. Licha ya yote Iryn alikuwa ni moja ya watu wangu wa karibu sana na ilitokea kuelewana sana.

Tulikuwa tunakwenda karibu mwezi bila mawasiliano yoyote na nilikuwa sijui maendeleo yake, kipindi hiki.

Kwasababu mwisho wa mwezi ulikuwa umekaribia nikawaza muda ule niende kwake Kijitonyama. Na lengo langu ilikuwa nijishushe nimwombe msamaha kama kuna sehemu nilimkwaza.

Niliona sometimes ni bora kuwa mjinga ili mambo yako yaende ila kwa upande mwingine niliwaza hivi nikijishusha sana si ataniona mimi bwege? Yaani bila yeye maisha yangu hayaendi? Niliwaza pale ataweza kunisumbua sana huko mbeleni. Pia nilikuwa nawaza ni jambo gani ambalo limemkera mpaka kuchukua maamuzi yale?. Iryn ni mwanamke ambaye ni hatabiriki “UNPREDICTABLE”.

Saa 12 jion nilikuwa pale kwa Iryn Kijitonyama na hata sikumpigia simu niliamua kwenda bila kutoa taarifa, nilitaka iwe saprize.

Nilipark gari nje ya geti na nikafungua geti maana nilikuwa tayari mwenyeji kwenye zile apartments. Niligonga mlango wake na baada ya dakika kadhaa alitoka kufungua.

IRYN: “Ooh Insider karibu na nilikuwa nawaza nikupigie simu toka jana ili uje tumalizane maana namzigo wako.”

MIMI: “Ooh sawa ila mimi sijaja kwaajili ya hilo, nimekuja kukuona na kukujulia hali maana ni muda kidogo toka unitumie ile text ya kuterminate mkataba, pia nilitaka kujua sababu ni nini mpaka ukaamua vile.”

IRYN: “Insider hakuna sababu yoyote na hakuna jambo lolote baya ambalo umefanya, ila nataka kufocus na masuala ya mama kwa sasa.”

MIMI: “Kama hakuna jambo nililokukosea ungenipigia simu na tungekaa chini tukaongea. Iryn mimi ni binadamu sijakamilika kwa asilimia mia, kama kuna sehemu nilikukosea nisamehe. Iryn naomba utambue mimi ni Mwanaume ambaye nakuheshimu sana na bado utaendelea kuwa mtu muhimu sana kwenye moyo wangu.”

IRYN: “Insider hakuna shida mimi naona wewe ndo una wasiwasi.”

MIMI: “Hapana mimi nimekuja kukuomba msamaha pale ambapo sikuwa sawa na nimekukosea. Sijaja hapa kuomba unirudishe kazini, masuala ya kazi ni yako na ni maamuzi yako wewe.”

Na muda huu Iryn hakuongea kitu bali alifunga laptop yake na kuingia chumbani na mimi nilikaa pembeni ya coach. Na baada ya dakika 3 Iryn alitoka akiwa ameshika bahasha ndogo ya kaki

IRYN: “Insider pesa zako hizi nimeweka na fine ya kuvunja mkataba na wewe.”

Na muda huu alinikabidhi ile bahasha na mimi nikasimama nikaipokea ile bahasha pale na nikaiweka mfuko wa nyuma.

MIMI: “Ahsante but nishaelewa tatizo ni nini.”

IRYN: “What do you mean?”

Na muda uleule nikamshika mikono yake miwili na nikapandisha mikono yangu kuzunguka kiuno chake na nikamvuta upande wangu kwa nguvu, kilikuwa kitendo cha ghafla sana. Nikampa ulimi wangu na yeye akanipa wake haraka bila kizuizi na tulichezeshana pale kwa sekunde kadhaa na palepale tulishtuka tukaacha ule mchezo.

MIMI: “I mean hiki ndo ulichokuwa unakitaka, Iryn thank you for everything, I have missed you so much. Mimi naondoka nikutakie maisha mema ila kama utahitaji msaada wangu never hesitate to call me. Byee.!

Nilimwacha pale Iryn katika sintofahamu kwani hakuweza kuongea neno lolote muda ule na alikuwa akiniona nikipotea machoni mwake live.

Na wakati niko kwa gari nilikuwa mtu mwenye furaha sana na kama nilikuwa nimepata Nguvu mpya na nikajisemea pale “When one door closes another opens.”

EPISODE 27

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
Here we go
 
Unatembea nazo hawa watu sijui wanabisha nini wakati utaratibu ni kudeclare ila sasa wewe mtanzania kubeba million 50 ni mzigo kwanza na hizo pesa unazipeleka wapi?

Kwa dollar ni simple sana hata kuzicarry unaweza weka dollar $50k kwenye surual freshy kabisa.
Extra ya USD 10 000 ni lazima ku declare. Watu wanabeba sana kwa magendo.
 
Kuna sehemu BROKE BOYS kaeleza vizuri. Na ndio utaratibu ulivyo. Kuna kiwango cha pesa huulizwi kusafiri nacho ila kiwango kinachozidi lazima kiwe na maelezo kuzuia utakatishaji wa fedha. Hii ni kutia ndani kiwango cha pesa kichotumwa au kuingia kupitia Bank toka nje ya nchi.
Na hii sheria imewekwa ili kukabiliana na illicit financial flows.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom