HSE Officer
JF-Expert Member
- Apr 10, 2023
- 651
- 844
NowEPISODE 22
“A TRUE STORY BY INSIDER”
Na mimi muda huo niliinuka kuelekea chumbani kwake sikutaka kubisha, niligonga mlango na akasema niingie.
Nilifungua mlango na yeye alikuwa kajilaza kitandani, na muda huo macho yangu yote yalikuwa yakimwangalia Mwanamke mrembo aliyejilaza pale kitandani. Maana alikuwa na kibukta kifupi kinachoishia mapajani katikati, na upande wa juu alikuwa kavaa sport bras.
Sasa ule uzuri wake na vile alivyokuwa nikiona maungo yake vizuri tena live kwa macho nilijikuta nataka kupagawa na mimi sikutaka kuendelea kumtizama maana mnara ulishaanza kusimama wima.
MIMI: “Umeniita nakusikiliza”
IRYN: “Insider nataka unisaidie kutoa vitu humo kwenye makabati, nataka tuvipange vizuri.”
MIMI: “Sawa haina shida.”
IRYN: “Afu Grizmann anakuja mwezi huu, anakusalimia.”
MIMI: “Msalimie pia, mwambie aje na mazaga bhasi.”
Room yake ilikuwa na zile kabati za kutengeneza moja kwa moja. Nilifungua kabati na droo zote moja kwa nyingine.
Sasa kila nikifungua droo nilikuwa nakuta simu na vitu vingine kama chaji, earpods, apple watches na saa. Baada ya kumaliza kukagua drow zote nilihesabu jumla ya idadi za simu na zilikuwa simu 14 ambazo ni Samsung na iphone. Samsung Galaxy S22 ultra (2), Iphone 12 Pro Max (3), Iphone 13 Pro (3) na Iphone 13 Pro Max (6).
Nilishangaa sana asee yaani mtu anakaa na simu nyingi vile ndani na zote zilikuwa ni brand new hakuna hata moja ilofunguliwa. Muda ule nilitamani niibe hata simu moja nifiche lakini ilikuwa ngumu kwa upande wangu. Kuomba simu pia nilikuwa siwezi maana nilipewa simu na Iryn na hakuwai niuliza kuhusu ile simu, nilimpa Mama J na nikachukua simu yake, tulifanya kuexchange na Mama J.
IRYN: “Insider hizo simu zipo ngapi?”
MIMI: “Jumla ziko 14, unakaaje na duka la simu ndani?”
IRYN: “Insidier hizo simu nilipewa kama zawadi tu na watu tofauti, kama hizo iphone 12 Pro Max nilipewa muda mrefu sana toka zinatoka.”
MIMI: “Aisee unabahati sana, unajua uzuri wako unawapagawisha sana wanaume.”
IRYN: “Insider umeanza tena, hizo iphone 12 kuna dada nitawapa saloon, wanani-furahisha sana.”
MIMI: “Na hizo zingine? Si bora hata uuze upate hela maana thamani zinazidi kushuka, na mwaka huu iphone 14 inatoka.”
IRYN: “Sasa naziuzia wapi?”
Nilitamani kumwambia aongee na Muajemi maana anaduka la simu lakini nikaona haitakuwa good idea, Muajemi angejisikia vibaya sana yaani kapeleka zawadi ya simu afu mtu anasimu kibao ndani.”
MIMI: “Niachie hili mimi, nitatafuta mtu wa kumuuzia.”
IRYN: “Okay sawa, nataka now nitumie na Samsung Ultra maana wanaisifia sana.”
Samsung S22 ultra ilikuwa released February lakini Iryn alikuwa nayo tayari tena mbili (2).
MIMI: “Sawa Bossy.”
Alinipiga jicho kali sana maana alikuwaga hapendi kusikia nikimuita hili jina.
MIMI: “Una nipiga jicho na hayo macho yako ya kirembo.”
IRYN: “Insider njoo angalia.”
Na muda huu alikuwa akinionesha picha zake na video mbalimbali alizokuwa Ufaransa.
MIMI: “Ulikuwa unashiriki fashion?”
IRYN: “Niligombea Miss college.”
MIMI: “Ikawaje?”
Na muda huu Iryn alikuwa akitafuta picha ya kunionesha,
IRYN: “Ona nilikuwa wa2, sikushinda. Huyu dada alishinda.”
Huyu dada aliyekuwa akinionesha ambaye ndo alishinda, alikuwa ni mhindi.
MIMI: “Ni kisu hatari.”
IRYN: “Kumbe hata wewe umeona, alishinda huyu alikuwa anasoma Finance.”
MIMI: “Hata hvyo ulijitahidi kuwa wa2 sio kitoto.”
IRYN: “Kupitia haya mashindano ndo nili-miti na Grizmann, kipindi hicho yeye alikua Masters.”
MIMI: “Everything happen for a reason.”
IRYN: “Yeah sure”
MIMI: “Hivi huko Ufaransa Grizz hakucheat kweli?”
Muda huu Iryn aliniangalia akaanza kucheka, ni kama hakutegemea lile swali.
IRYN: “Ana mke na watoto 2.”
MIMI: “Aisee na wewe umeridhika kuwa mchepuko?”
IRYN: “Insider Grizz kuna mambo ananisaidia mengi sana, sometimes we don’t have a choice.”
MIMI: “Ni kweli unachosema ila naona anakupenda sana.”
IRYN: “Yeah he loves me but ni mme wa mtu.”
Sikutaka kuendelea kumwuliza sana kuhusu Grizz na muda huo yeye alitoka kwenda Seblen akiniacha pale chumbani nikiendelea kumpangia vitu vyake.
Wakati amekwenda seblen Mary alikuwa akinipigia simu na Iryn alisikia simu ikiita.
IRYN: “Insider somebody Mary is calling.”
MIMI: “Njoo na simu bhasi.”
Muda huo nilitumia kuongea na Mary, alikuwa akiniuliza kama nipo around ili nikampick ila nikamwambia niko Kijitonyama. Mary pia aliomba kama tutaweza onana muda ule na nikamwambia maybe jumapili nitamcheki.
Na muda huo wakati nikiongea na Mary, kwa upande mwingine Iryn alionekana kuwa makini sana kusikiliza maongezi yetu.
IRYN: “Insider nani huyo?”
MIMI: “Kila nikiongea na mwanamke lazima uulize ni nani.”
Na Iryn kama hakufurahishwa na hili jibu nilimwona kamind flani hivi. Pia kama alijiona ananikosea sana kufuatilia calls zangu.
IRYN: “Ok Insider am sorry”
MIMI: “Usijali najua huna nia mbaya, huyu ni mshikaji wangu.”
IRYN: “Ngoja nikapike chap”
Na mimi nilitoka nikakaa pale seblen na muda huo nilikuwa nikiangalia Tv utafikiri ni Baba mwenye nyumba. Na mimi niliamua kwenda Jikoni kumsaidia kupika muda ule.
“Unanipikia nini Mummy?”
“Nilitaka kupika ndizi na nyama ila nimeona uvivu kumenya ndizi.”
“Si ungesema nikusaidie? Mimi niko kwaajili yako”
“Kesho nitapika usijali.”
“Sasa unapika nini?”
“Tambi za maini.”
Na muda huu mimi niliamua kutengeneza juice ya nanasi na story zikiendelea.
IRYN: “Insider Muajemi anataka twende Zanzibar kutembea”
MIMI: “Aaah mnakwenda lini?”
IRYN: “Ndo najifikiria hapa”
MIMI: “Wewe unapenda?”
IRYN: “Kwenda napenda, ila yule mtu simwamini bado.”
MIMI: “Kwamba unaogopa atakuteka?”
IRYN: “Hamna sio rahisi, anyway nitaangalia.”
MIMI: “Si unakwenda na mimi hapa Bodyguard wako.”
IRYN: “Hahahaah Insider huishiwi vituko”
MIMI: “Nimekwenda jeshini wewe cheka, sikutaka kuwa mjeshi tu.”
Na muda huo nikamwonesha cheti changu cha JKT kile cha Mujibu wa sheria, Iryn haya mambo hajui hivyo alishangaa sana, maana alikuwa haamini kama nilikwenda jeshini.
IRYN: “Insider kumbe umekwenda Jeshi, upo vizuri ndomana mambo yako ni chap sana, na unajali sana muda.”
MIMI: “Nitakulinda kila unakokwenda na hakuna wa kukuzingua.”
Iryn alishiia kufurahi tu muda huu hakuwa na chakusema, pia alisema kesho ambayo ni jumamosi angeenda kuonana na Muajemi. Na mimi niliunga mkono hili jambo kwa asilimia mia kabisa, maana Iryn angekua karibu na Muajemi mimi ningeendelea kufaidi matunda.
MIMI: “Vipi kuhusu kutoka usiku kwenye kazi zako.”
IRYN: “Tutaendelea next week nataka kudeal na wateja wa web tu kwasasa tena ambao wana offa nzuri tu.”
MIMI: “Sawa Bossy Lady.”
Baada ya kumaliza mapishi tulikula chakula na nikamshukuru kwa Dinna, nikamuaga nasepa muda ule, lengo langu ilikuwa kwenda barabarani kuendelea na majukumu ya kusaka pesa.
Wakati nataka kuondoka Iryn aliniita
IRYN: “Insider…. Leo tumeanza mwezi mpya, nikiwa nakulipa naomba upokee hela sijisikii vizuri kuona unakataa hela hata kama tulikuwa kwenye makubaliano.”
MIMI: “Sawa haina shida mummy”
IRYN: “Byee Insider takecare”
Nilitoka pale ilikuwa saa2 usiku tayari na mimi nikaendelea kupiga kazi non-stop, kama mnavyojua kwa Dar weekend ndo watu wanatoka out kutumia hela.
Nilipiga kazi mpaka saa 7 usiku na niliamua kurudi baada ya kupata mteja aliyekuwa anaelekea Mbezi Beach.
*********
Jumamosi niliamka asubuhi sana kama kawaida yangu na nilipiga sana kazi hii siku. Ile Asubuhi kwenye saa5 Msomali alinipigia simu na aliuliza niko wapi nikamwambia niko tabata Baracuda.
Msomali akasema kama nitakwenda mjini nimpigie simu anataka twende Mbweni na alisisitiza sana.
Saa 12 jioni ndo muda ambao nilionana na Msomali na alikuwa pale CBD hotel Gerezani.
Tulitoka hapo kwanza tulianza kupitia Mlimani city kuna mtu alikwenda meet naye na nilisubiri kama 1 hour. Baada ya hapo sasa tukaanza safari ya kwenda Mbweni na tulipitia Barabara ya Mwaikibaki ili kukimbia foleni ya Bagamoyo Road.
MSOMALI: “Insider gari yako ni safi sana na inanukia vizuri.”
MIMI: “Si unajua ofisi lazima iwe safi muda wote, hata hapa umekuta Gari ni chafu.”
MSOMALI: “Kwa hili unajitahid sana hongera.”
MIMI: “Ahsante sana Bossy wangu I really appreciate.”
Saa 3 tulikuwa tumefika Mbweni na tulifika sehemu anayokwenda tukaingia ndani na mimi nilikwenda msubiri kwenye garden
Msomali alitumia kama masaa 2 pale na akatoka akanambia tunakwenda Sea cliff hotel Masaki, ndo nitamwacha pale.
Wakati tuko njiani tulikuwa tunapiga story mbalimbali hasa za Maisha na mademu.
MSOMALI: “Insider kwa kipindi kifupi tulichokutana nimetokea kukubali sana, kuna deal nitakushirikisha by next week, au umeridhika na maisha ya Uber?”
MIMI: “Hapana Bossy sijaridhika maana hii kazi sometimes ni mateso ila ndo hivyo tunapambana kibishi. Kama deal zuri mimi napiga kwasasa nachoangalia pesa tu.”
MSOMALI: “Sawa haina shida Bro!, nitakupigia simu.”
MIMI: “Sawa Bossy nasubiri na nitashukuru sana.”
Tulifika pale Sea cliff na nikamshusha Msomali pale.
MSOMALI: “Bro nikupe kiasi gani? Maana hatukuelewana kabisa.”
MIMI: “Bossy wewe nipe utakayoona haitoniumiza mimi, si unaona wese limepanda bei? Vita ya Ukraine na Russia ndo imeleta majanga.”
MSOMALI: “Ni kweli Bro! vita ya wakubwa hizo sisi wengine ni watizamaji tu, wewe ongea kuwa huru.”
MIMI: “Ok kutoka Posta mpaka Mlimani city 15,000, kutoka Mliman mpaka Mbweni 25,000 na kutoka Mbweni mpaka hapa utanipa 30,000 unipa 70,000 sio mbaya.”
MSOMALI: “Haina shida Bro ngoja nikupe na offa ya bia maana leo weekend”
Msomali alinipa 100,000 na akaondoka pale huku akiahidi kunitafuta kwa ajili ya hilo deal. Na muda huo niliwaza Msomali atakuwa na deal gani?
Na muda huu nilipata request ya mteja alikuwa anakwenda Airpot na alikuwa palepale Sea cliff.
Na huyu mteja alikuwa kauzu sana nakumbuka, maana tulitoka pale Sea cliff mpaka Terminal 3 bila kuongea njiani.
Nilipiga kazi mpaka saa 9 usiku ndo nikarudi kulala, maana nilikuwa na usingizi hatari.
*******
Jumapili saa 4 asubuhi Mama Junior alirudi home na aliletwa na Mamdogo wake home. Niliwapokea na tulishinda na mamdogo pale home mpaka tukala chakula cha mchana na yeye akaaga.
Hii siku nilicheza sana na Junior maana nilim-miss sana, na Junior alikuwa mtundu sana kipindi kile mpaka sasa ni mtundu balaa huyu mtoto.
Mchana Iryn alinipigia simu akasema kama nitapata muda niende kwake ili nipeleke ile mizigo (mashine za saloon) kule Masaki kwa Mama Janeth.
Jioni saa10 nilitoka home na nikamwaga Mama J natoka ila nitawai kurudi tutoke out. Mama J alifurahi sana kusikia hizi taarifa maana ni kama alikuwa amemiss kutoka out na mimi mme wake.
Nilifika kwa Iryn ila sikuingia ndani na niliitoa ile mizigo kibarazani na kuiweka kwa gari. Muda huo nilihisi Iryn atakuwa amelala hivyo sikutaka kumsumbua kabisa. Kwasababu nilikuwa najua ile mizigo inakwenda kwa Mama Janeth nikasema acha niipeleke tu, nikirudi ndo nitamcheki.
Nilipeleka ile mizigo kwa Mama Janeth Masaki, baada ya kufika Mlinzi alinifungulia geti na nilimkuta yuko nje akipanda maua . Nilimsalimia nikamwambia nimeleta mizigo na nikaitoa nikaingiza ndani.
“Mwanangu Ahsante sana.”
Nilimwaga Mama Janeth na mimi nikaondoka kurudi kwa Iryn, na wakati niko njiani Iryn alipiga simu.
“Insider kumbe umepeleka mizigo kwa Mama Janeth.”
“Yeah, wakati nafika hapo ulikuwa umelala, sikutaka kukusumbua.”
“Nilitaka twende wote bhasi lakini.”
“Niko njiani soon nitakuwa hapo.”
Wakati narudi nilitumia njia ya Heilasie Road ambayo inakuja kutokea Bagamoyo Road, kwangu naonaga hii barabara ni rahisi, maana hainaga mambo mengi.
Nilitumia kama dakika 15 kufika Kijitonyama kwa Iryn na nilipark gari nje ya fensi getini, sikutaka kukaa sana pale. Lengo langu lilikuwa nirudi home mapema ili nitoke out na wife.
Niliingia ndani na nilimkuta seblen akichezea laptop yake ya Macbook, nilimsalimia na nikaenda kukaa kwenye kiti.
“Insider…….”
Iryn aliniita na mimi nikamtizama kumsikiliza anataka kusema nini;
“Naam mummy”
“Huyu ni mwanao?
Iryn alikuwa akionesha picha ambayo nilikuwa nimeipost whatsapp status nikiwa na Junior.
TO BE CONTINUED
Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu