Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

EPISODE 03

Baada ya siku 3 akanicheki ghost akanambia account yako ipo tayari, akanipa password akanambia download bolt driver app kwa istore then anza kazi. Kweli nikafanya nikaona mambo yako supa nikaona sehem ya kwenda online kama unataka request, nika touch pale nikaona inasearch nikazima data nikalala, nikaplan kuingia mzigoni jioni.

Inaendelea

“Unajua biashara ya Uber ni nzuri sana kwa kijana ambaye anataka kujiajiri, inalipa sana kama utakua makini. Niko kwenye hii biashara toka 2017 nina uzoefu wa kutosha sana, nimepitia mishale mingi sana. Mdogo wangu nakuomba sana zingatia haya, 1. Focus na malengo yako, 2. Acha tamaa, 3. Fanya kazi kwa bidii chukulia kama ni kazi nyingine. Acha tamaa na wanawake, utakutana na mademu wengi sana kuna ambao watataka uwale sababu hana nauli, kuna wamama watu wazima “mashangazi” watakutaka nakuona so HB mdogo wangu wamama wengi watavutiwa sana wewe. Kuwa mkarimu kwa wateja, Ipende ofisi yako “gari yako” hakikisha unafanya usafi muda wote liko safi, kuwa makini sana wakati wa usiku sio kila sehemu ya kwenda. Utakutana na watu wa kila aina chamsingi wewe kuwa humble usipende kugombana na wateja kabisa. Ukizingatia haya utafika mbali na pia gari yako utaiona pesa trust me. “Hayo yalikua maneno ya Dullah akinipa changamoto za biashara hii ya Tax mtandao.”

Niliamka saa 11 jioni nikaingia bafuni nikajiandaa chap nikaweka mazingira mazuri ya gari. Nilianza hii kazi ya Uber mwishoni October 2021, bhasi nikapitia filling station nikajaza mafuta full tank huyo nikaenda kupark gari pale mbezi Beach kwa zena. Hapo nilikua nimeswitch online so dizaini kama App ilikua inasearch requests.

Nimekaa kama nusu saa hollaaa hakuna hata request nikaanza pata wasiwasi au sababu mimi mpya??. Nikampigia simu Dullah kumwambia sipati request, Dullah akanambia vumilia tu zitaita usiwe na wasiwasi.

Baada ya dk 10 hivi nikaskia kitu kinaita “nke nke nkee nkeeke nkeee” uyo chap ni accept, ukweli nilikua bado na kaushamba wa kutumia hii App lakini Dullah alinielekeza namna ya kutumia map na vitu vingine muhimu akanambia vingine utamasta taratibu.

Baada ya kuaccept mteja akapiga simu akanambia fata ramani, nikamjibu sawa, (“kwa mara ya kwanza App lazima itakuchanganya”). Nikaanza kwenda uelekeo wa kawe akapiga simu nakuona unapotea “Oasisi” unakujua?… nikamjibu ndio, mteja akanambia sasa huko unakwenda wapi??. Oasisi nilikua najua kabla hujafika round about ya kwenda whitesand kuna kibarabara cha lami kinakunja kushoto, chap nikageuka nikafika mpaka kwa mteja nikamchukua alikua anakwenda mbweni.

Baada ya kumshusha mteja Mbweni sikukaa sana nikapata request nyingine nika accept mteja alikua anakwenda mbezi beach- shamo tower. Nilipiga kazi mpaka saa 6 usiku nikaingiza 59,000, nikapitia sheli nikajazia mafuta tena yaliyotumika nikabaki na 39,000, nikaona pesa nzuri kwa muda wa masaa 6 tu niliyofanya ikanipa morare sana.

Asubuhi nikaamka 06:00 am nikaanza kazi kama kawaida siku hiyo nilipiga kazi mpaka muda wangu wa kudrive ukaisha. So nilirud home kama 23:00 pm, pesa nilizoingiza sio haba kwenye App ubao ulikua unasoma 153,000/= bado zile pesa nilizokua naingiza nje na App. Ukitoa gharama za wese na cost nyingine faida yangu ilikua kama 80,000 hivi.( “Uber/Bolt kuna driving limit, hutakiwi kudrive zaidi ya masaa 12 kwa siku, ukidrive masaa 12 wanakufungia App ukapumzike kwa masaa 6 then urudi mzigoni tena, kwa mtu anayetafuta pesa hii ni changamoto sana, hapo ndo utaona umuhimu wa kuwa na App zote mbili Uber/Bolt”)

Niseme ukweli kwa muda mfupi ndani ya week nilitengeneza pesa ndefu sana. Mpaka nikaona hakuna haja ya kuajiriwa kama Bolt tu inaniingizia pesa hivi kuna haja gani ya kutafuta kazi??.

Baada ya week 2 kukata “ghost”akanicheki akanambia account yangu ya Uber ipo tayari. Nikaanza kuitumia Uber aisee huku ndo nilianza kupata deals nyingi sana na pesa upande wa nauli zilikua juu tofauti na bolt, huku nikaanza pata connections nyingi na kukutana na foreigners.

*******
Nataka kidogo niwape utofauti wa Uber na Bolt. Uber wako vizuri sana upande wa fares na usalama, kwanza wanaotumia Uber wengi ni foreigners pia ni watu wenye pesa au matajiri. Abiria wa uber akirequest wanajua kwenda na muda itoshe kusema abiria wa Uber ni smart sana. Ukija kwa ndugu zetu wa Bolt abiria wao ni pasua kichwa sana, wateja wa bolt wengi ni wanachuo, wale low income earners ndo unawakuta huku sasa. Abiria wa Bolt ni wanamaneno balaa, ana request usafir anakuweka hata nusu sometimes mpaka one hour afu akija anakupa majibi rahisi nilijua upo mbali. Nauli ikiongezeka kidgo atalalamika balaa, madereva wa Tax mtandao wanakwambia bolt ni kwa maskini na Uber ni kwa matajiri. Pia raha ya Uber hata kama mteja atakuweka baada ya dk 5 inaanza kucharge waiting fee, tofauti na Bolt.

Baada ya kuanza kutumia Uber nikaona nitaendana sana na wateja wa Uber kuliko Bolt hata kimaslahi yapo Uber nikaamua kuachana na Bolt, japo nilikua naitumia kwa nadra sana na baadhi ya mazingira.

“Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya uber na wateja wake kama nilivyosema huko juu. “

Nilivyoanza kutumia Uber nilianza kupata sana hela sio hivyo tu bali niliweza kupata dili nyingi sana. Niliweza kukutana na foreigners wengi sana wa nchi mbalimbali pamoja na matajiri, viongozi wakubwa wa serikali, na celebrities mbalimbali. Niliweza kujuana na watu wengi sana mpaka leo kuna foreigners nachat nao sana hata wakija bongo lazima wanicheki.

Siwezi kusimulia matukio yote maana ni mengi kwakweli nitagusia baadhi. Muda wangu wa kazi ulikua naamka 06:00 am mpaka usiku, kama biashara siku iyo mbaya bhasi mapema niko home kucheza na Junior. Siku za weekend nilikua nakesha siku zingine narudi late night. Nilikua nazingatia sana usafi wa gari, usafi wangu binafsi, yaani siku za kazi nilikua nachomekea kama officer nakwenda kazini kumbe ni Uber tu, hii kitu ilepelekea kupendwa sana na watu na wateja wangu wengi walikua wanawake.

*******

Nikiwa barabarani kama kawaida nilikua Posta nimepaki gari yangu pale, mida ya saa10 jion nikapata request ya kwenda Airport. Nikampeleka yule mteja alikua ni dada, akanambia ameipenda gari yangu atakua ananicheki, baada ya kumdrop pale tukabadilishana namba.

Nilikua pale Terminal 2 nimechili nasubiri request ilikua nishakaa almost dk 45, nikakumbuka Dullah alinambia kwakua unatumia vibao vya njano make sure uko makini sana maana pale Airpot wakijua wewe ni Uber then gari yako haina vibao vyeupe watakupiga fine, hata wale madereva wa tax mle Airpot ni wanaa sana.

Mnajua kwanini madereva wa Tax mle Airpot hawawapendi Uber? Ujio wa Tax mtandao umewaharibia sana biashara afu Tax nyingi mle ndani ni za wafanyakazi wa mle ndani. Mfano kutumia tax ya Airport mpaka Masaki utalipia 50,000-70,000 wakati kwa Uber haizidi 25,000, hapo utaona kama Tax mtandao ikawa msaada sana.

Baada ya 1 hr hivi nikapata request mteja alikua anakwenda Sea cliff hotel, chap aka nitext kupitia App “Are you coming”, nikamjibu ASAP. Yaani “As soon as possible”

Ofcourse nilikua mgeni na Airpot na kwa mara ya kwanza lazima uchanganye kama sio mzoefu wa zile barabara za mle ndani, na pia hakuna barabara ya kutoka Terminal 2 kwenda Terminal 3 ya shortcut “sio kwamba shortcut haipo ila wameiziba tu makusudi”, so pale unavyotoka lazima ulipie then uwe kama unatoka ndo uzunguke ile round about kama unatoka ndo uelekee Terminal 3.

Kama ulikua Terminal 2 unataka kwenda terminal 3 lazima ulipie 2,000 utoke pale terminal 2 then kuingia terminal 3 lazima uchukue card inamaana lazima ulipie tena utakavyotoka terminal 3 (lazima ulipie mara 2). “Hapo jamaa alikua ananielekeza pale terminal 2 maana nilikua sijui na ukichanganya hata barabara tu unalimwa fine, nilisikiliza maelezo vizurii sana nikamasta.”

Message ikaingia kwenye App “I am near the Arrival door” huyu alikuwa mteja.

Nikahisi huyu atakua foreigner tu, nikafika pale wakati nasogea akawa kashasogea barabarani akanipa ishara, nikampakia hao tukasepa. “Wazungu wako chap sana huwa hawapotezi muda kabisa, akirequest labda wewe uzingue, ila wabongo wanaringa sana”. Safari yetu ilikua ni kuelekea Sea cliff hotel kule Masaki, bhasi tukiwa njiani tukaanza story…..

MZUNGU: Bro your Car is very clean

MIMI: Thanks bro! It’s my office, how was the journey??

MZUNGU: Wow was amazing bro and I’m very happy being here in Tanzania .

MIMI: So it’s your first time being here?

MZUNGU: , no bro!, it’s my second time.

MIMI: Welcome bro! so your nationality?

MZUNGU: I’m Swiss bro!

MIMI: Wow nice bro! So What do you do for a living?.

MZUNGU: I am working for WORLD VISION.

Tuliongea mengi sana na Mzungu akanambia kule hotelini ana workmates hivyo atanicheki niwapeleke Morogoro na watakua Tanzania kwa week 2. Tukafika pale Sea cliff hotel nikamdrop tuka exchange contacts.

Jumatano nikiwa mzigoni kama kawaida yangu, alinipigia simu kama nitakua around maeneo ya Sea cliff nimcheki tuongee, jioni nikamcheki akanambia tukutane pale Karambezi cafe.

Tutakutana pale tukaanza story so ishu mezani ilikua ni alikua anatarajia kwenda Morogoro Ijumaa na ndugu zake( jumla watakua 4). Akaniambia tutarudi jumapili hivyo nimpe gharama zangu, nikamwambia badae nitamcheki nikiwa na cost zote. Tuliongea mambo mengi sana ya kimaisha inshort ndani ya muda alikua ametokea kunikubali sana. Bhasi tukaagana pale, katika story zetu nilimwambia na mke na mtoto mmoja hata yeye pia alinambia kaoa ana watoto 2, akanambia Msalimie Junior, before sijaondoka nitakuja kumwona.

Ile night nikamcheki huyu mzungu alikua anaitwa “MANUEL” ni jina lake halisi, nikampa mchanganuo wa gharama zangu nikamwambia hesabu ya jumla kila kitu kitakua chini yangu tukakubaliana $500 kwa zile siku tutakazokua kule Moro. Akanipa kazi nifanye booking ya hotel nzuri kwa ajili ya watu 4 kwa siku 2, that time Morena Hotel ndo ilikua imefunguliwa nika book hotel pale.

Ijumaa asubuhi na mapema nikaenda pale kuwabeba tukaenda Morogoro, nikawadrop pale Morena Hotel, tulifika Morogoro saa5 na dakika kadhaa, siku ileile tukaenda Mzumbe University sijui walikua na Agenda gani pale tukarudi hotelini jion saa11. Manuel akasema “Lets have dinner together” tukaingia hotelini tukaenjoy pale story zilikua nyingi sana, tukapiga na wine za kutosha sana.

Ilikua ishafika saa3 nikawaaga,

“So where are you going to sleep??, hilo lilikua ni swali kutoka kwa Manuel.

Wote wakawa wananitizama wakisubiri jibu. Kuna dada mmoja mzungu akasema , “he doesn’t want to sleep with us here”.

MIMI: No I have my friend here so don’t worry about me guys.

Mimi nilikwenda kwa jamaa yangu anakaa paleple around kihonda stand, nilimpanga mapema. Nilikua nakwepa gharama za hotel,

Asubuhi mapema nikapanda hotelini kuwabeba walikua wanakwenda SUA chuoni sijui walikua na agenda gani, Pale SUA tulitoka mchana ikabidi turudi tena Mzumbe jioni tukarudi hotelin. Kama kawaida have dinner, tukaplan tukirudi dar niwapeleke moja ya viwanja maarufu vya bata.

Jumapili mida ya saa6 mchana tukaanza safari ya kurudi Dar kitu kama kumi kasoro tukawa tumefika. Nikawarudisha pale Sea cliff hotel,

So bro badae tutakwenda wapi? Aliuliza Manuel,

Nikamjibu “Saprise”. Akanambia Ok bro I trust you!!, nikamwambia by 07:00 PM ntakua around kuwachukua, Na mimi nikarudi zangu home. Palepale akanilipa Pesa zangu ambayo tulikubaliana nikapokea, kuja kuhesabu ilikua jumla $550. Nikatabasamu.

Tukiwa parking nilitamani kumwuliza kuhusu wale dada 3 ni nani kwake? lakini nikapotezea nikapanga kumwuliza siku nyingine.” Kweli wale dada walikua ni visu sana kuna mmoja alikua mdogo mdogo hivi nilimwelewa sana.

Nilivyoingia home nikawaza hawa nawapeleka wapi ukicheki leo Jumapili, kwa jumapili sehemu yenye vibe ni Kidimbwi tu ndo watavibe na wale wote pombe wanatumia, so sikupata ukakasi sana.

“Kwa jumapili kidimbwi huwa inajaa sana tuseme ndo kiwanja pekee kwa Jumapili huwa kina vibe hapa mjini”.

Nikapata wazo nifanye booking kabisa “reservation”, maana tukichelewa tutakosa space then niko na hawa wazungu tutaanza hangaika kupata nafasi, sikutaka kupoteza point 3 kwenye vitu vidogo kama hivi.

Nikaingia Instagram nikachukua namba zao nikawapigia simu chap, dada akapokea nikamwambia dhumuni langu akanambia table bado zipo ila I have to make payment before. Nikamwambia dada sikia tuko 5 hawa wengine ni foreigners, sisi tunakuja by 08:00 PM tutakua hapo on time. Dada akawa haelewi hivi akanambia wengi huwa wanapiga simu hawatokei na hii ni biashara huu ndo utaratibu wetu, nikamwambia nakurudia ASAP.

Nika mcall Manuel kumpanga akaniambia good bro! you can proceed. Nikamrudia Dada tena akanambia cost za table kwa VIP inaanzia 500,000 na kuendelea pia akanambia kuna table zingine ili ukae lazima uwe unatumia 200k na kuendelea. Nikaona option 2 ndo nzuri zaidi, akanambia ana reserve ila ikifka muda huo bila taarifa yoyote atawapa watu wengine.

“Bro! tunatoka out, tunakwenda kunywa na kulewa, acha gari tu home kwa usalama zaidi sisi, tunakuja na Uber, nitumie location” ilikua mesage ya Manuel. Nikaona ni jambo jema sana.

By 07:00 PM ontime nikawa nimefika pale Kidimbwi ili kuweka mambo sawa na kuchagua location nzuri. Nikiwa njian nilikua nishampanga dada niko njiani, nilivyofika pale dada Ofcourse akanipeleka moja kwa moja upande wa chini kwa mbele unaona mandhari ya bahari.

Kwenye mbili kasoro Manuel na ndugu zake nao walikua wamefika pale Kidimbwi, ofcourse walikuwa wamependeza sana, niliona jinsi wabongo wakiwatolea macho wale dada waswiss. Walifurahi sana na walipapenda sana pale na yale mazingira walipagawa sana.

Hawa dada 3 wa kizungu ngoja niwape majina yao
“Dada 1, Jina lake Alex, huyu alikua ndo mkubwa age yake ni around 30’s+ hivi”

“Dada 2, jina lake Olivia, huyu alikua around 25-28s”

“Dada 3, jina lake Sophie, huyu alikua mdogo kwa wote age yake 22”. Huyu nilipata muda wa kuzungumza naye vizuri tukiwa Moro,alinitamkia mwenyewe age yake, alikua anasoma bado. Ukweli alikua mzuri sana “kisu”.

*********
Baada ya kuingia ndani wahudumu walikua wanatukimbilia sana, all Eyes on US.

Kila mtu akaagiza anachojua yeye kwa waiter pale, wakati dada anatoka kwenda kufata, Manuel akamnong’eza dada japo alionekana kuelewa alichoongea Manuel.

Baada ya dakika kadhaa dada akaja na Vodka chupa kubwa, mimi niliagiza heineken ila zikaja bucket 2, ikaja backet ya desperados na Corona beer. “Nikajua Manuel alimwambia dada kwa kila order alete backet. Tuka agiza na mishikaki 50 “ yaani kila mtu mishikaki 10”.

*********
Tulianza gambe mapema sana so kadri muda unavyokwenda na watu walizidi kumininika kwa wingi na kufanya mandhari ile izidi kupendeza.

Kuna kitu ambacho nili kinotice kutoka kwa Manuel, nikahisi uwepo wa wale ndugu zake 3 ni kama kuna uhuru anakosa, huko mbele mtakuja kufahamu ni mtu wa namna gani.

Kadri muda unavyozidi kwenda na pombe zilizidi kukolea japo kwa yale mazingira ya upepo wa bahari mwanana wa Kidimbwi ulifanya pombe kuchelewa sana kuchanganya mwilini.

Zikashuka backets zingine tukaendelea kupiga pombe, ukweli wazungu wapo vizuri sana kwenye masuala ya pombe wanakimbiza balaa. Manuel alimaliza ile chupa ya Vodka na alikua ngangari akaagiza nyingine, this time alikua anakunywa na Alex kama wanashare.

Mida ya Saa 9 usiku tukaondoka pale Manuel aka request Uber kurudi Sea cliff na mimi nikarequest kurudi home mbezi beach.

ITAENDELEA KESHO.
Thread inainspire vijana waliokata tamaa wapo juu ya mawe akili haisomi,imestuck.

Tuendelee kuzipigania ndoto,hakuna kukata tamaa.

Kila nitakapokuta notification ya like au reply nitarudi kusoma tena na tena huu uzi!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom