Jina la mtoto...

kuna dada mmoja ilitokea hivihivi

baba wa mtoto kapropose jina la mama yake binti akataa, akamwita baby-yanka
mpaka leo huyo mtoto hana nywele!!

wamwite jina jina la bint yangu ''blanca'' hili hatalia sana na nywele zitaota na afya itakuwepo.


Edson umenichekesha cna mbavu...lol
 
Tuwashauri vipi???????

Kama wanashindwa kukubaliana waambie hivi:

Kila mmoja kwa uhuru wake aandike orodha ya majina matano au zaidi (idadi ifanane!) ambayo yupo comfortable kumpa mtoto wao. Halafu baadae wakae pamoja na orodha hizo mbili na watizame kama kuna jina au majina yanayofanana. Kama ni moja tu linafana basi wampe hilo. Kama kuna majina kadhaa yanafanana, basi waandae vikaratasi vyenye majina hayo na wamwombe mtu mwingine achague kimojawapo (kama bahati nasibu vile). vivyo hivyo, kama hakuna yanayofanana basi waandae vikaratasi vyenye majina yote kwenye orodha zao halafu wamwombe mtu mwingine achague kimojawapo.
 
lakini hao nao wanatuumiza tu vichwa vyetu majina yao tayari wanajua kama watamuita gati,bhoke ,manka ,kekue ,mwanamalundi ,kalikenye ,masatu
hilo lao
 
Hahaha! Nilijua tu ntakukamatia hapo. Hahaha! We bingwa wa rivasi? Mkishi = Mshiki? LOL!
umekula senksi bana!nashawishika kuamini kuwa baada ya kumaliza masomo yako ya kidato cha sita ulikamata tempo ya ualimu wa kiswahili makongo
 
.................jina la Mwajabu wala sio jina zuri. Nilikuwa na rafiki yangu anaitwa jina alikuwa na vituko balaa, Mwajabu alikuwa kweli na maajabu ya ajabu.

...Pretty bana, haya basi...wakimwita "Wanda" je? si linaelekeana na 'Wonder' -meaning; Ajabu?

kwani mwajabu maana yake ni nini? labda wale waislamu watuelezee

...Lol, eti waje waislamu... yanapendwa majina ya kizungu, haya ya kina Mwana wa Ajabu, Mwa'Jabu, Mwaju, yanaonekana ya Kiswahili-swahili...:D

Jina lenyewe limekaa kiajabu ajabu, anyway ngoja wenywe waje kutufahamisha.

...Nilipokuwa Primary nilisoma na mtu anaitwa TUMSIFU,... sijalisikia tena jina hilo,...wote wanajiita Glory, Gloria sasa..hivyo hivyo kina Mwangaza kuitwa Lightness, Waridi kuitwa Rose, nk...
 
Wampe jina la Irene sabab ni zuri na wenye nalo wanatabia njema hasa huwa wanabahati, ama charity kama watakubaliana kuchukua jina la kwenye tamthilia sabab lipo wazi na maana yake, hata hope ni zuri kiasi,
Duuu... ila waache utani hao wenye mtoto sabb wanatakiwa wakae chini wao kama wao tena bila kuwahusisha watu wengine na wafikie muafaka kwa upendo sabb utani utani wanaweza fikia kwenye mtafaruku wa kijinga tena mkubwa sana tu.
 
halafu kwa kumbukumbu zangu hii ni 'sapu' sasa nadhani inabidi arudie mwaka au sio mpwa?

Hahaha! Ili akiteleza tena tumpige 'disko'? hahaha! LOL! Mpwa naona umeamua kuweka boundary nzito kwa sisteri.
 
...Lol, eti waje waislamu... yanapendwa majina ya kizungu, haya ya kina Mwana wa Ajabu, Mwa'Jabu, Mwaju, yanaonekana ya Kiswahili-swahili...:D [/FONT]



Mbu bana! kwani waislamu ni waswahili-swahili? mimi nilidhani waarabu arabu?

 
Nani kakwambia majina ya waigizaji ni mazuri??
Kama wewe ni mtu wa dini....tafuta majina mazuri kwenye vitabu vya dini..... UNAKUWA KAMA LIMBUKENI BWANA
 
Kuna rafiki yangu ambaye ameoa hivi karibuni,mkewe
kajifungua mtoto wa kike...
Tatizo sasa ni kuwa yeye baba mtoto alitaka kumpa
mtoto jina la mama yake ambalo ni mwajabu.....
Mama mtoto hataki jina hilo anadai la kishamba...
Yeye anataka mtoto aitwe preta jina la msichana wa
kwenye tamthilia ya wa brazil inayoitwa shades of sin ambayo
inaendelaea sasa hivi.....

Mimi nimemuunga mkono baba mtu......

Nynyi mnaonaje????????????

Tuwashauri vipi???????

inamaana bado tu hawajapata uamuzi wa jina hadi leo????
naomba kujua wanaishi pamoja au bado mama wa mtoto yuko likizo ya uzazi????
basi watupe nafasi wana JF tuwatafutie jina
nlitegemea wangeufanyia kazi ushauri wetu,
kwa sasa wanatumia jina gani kumwita mtoto??
 
Amwite Abigail

n290943.jpg
 
Back
Top Bottom