Jihadhali na matapeli hawa maeneo ya kariakoo

Anold

JF-Expert Member
Jul 15, 2010
1,456
614
Wana JF kuna utapeli ambao kwa sasa umeenea maeneo ya kariakoo, najua wapo matapeli miaka yote ila nimeona niwatahadharishe wale ambao wanadhani hawapo. Juzi nilikuwa mtaa ule ambao vifaa vingi vya Ujenzi huuzwa, ni bahati mbaya sana kuwa pamoja na kuishi hapa mjini muda mrefu sifahamu sana mitaa hiyo kwa majina, wakati naendelea na shughuli zangu mara akatokea mtu mmoja ambaye anakila sifa za kuitwa mheshimiwa, alikuwa amevalia suti na vikwelombwezo vyote, tulipokutana alianza kutabasamu na kunichangamkia kana kwamba tunajuana, alinisabahi kwa kuanza hivi,
Tapeli '' aisee mbona kama nakufahamu?
Nikamjibu inawezekana
Tapeli - Hivi hujawahi kuishi mikoa ya Arusha , Tanga au Mbeya? wewe ni mwenyeji wa wapi? aliuliza maswali yote hayo kwa mpigo
Nikamtajia.
Tapeli - Ooooha sawa, akajitambulisha kuwa yeye ni Daktari wa Upasuaji pale Hospital ya wilaya (wilaya ninayotoka). Huna ndugu yako ambaye ameshalazwa pale, MIMI nikamwamnia wapo wengi, akadai kuwa anafahamiana na ndugu yangu mmoja anaitwaaaa .. hakutaja jina mimi nikamtajia mmoja a yeye akadakia ''aah ndiyo mbona tunafahamiana naye sana? akadai wanafahammiana.

baada ya hapo daktari yule akaniambia kuwa yeye ni mwenyeji wa Mkoa ambao mimi nimetoka na kwambwa anafahamiana na Mdogo wangu huyo na kwamba anamsaidia sana anapokwenda kutaka matibabu.

Aliendelea kunieleza kuwa ametokea mnazi mmoja, kuna Daktari mwenzake ambaye amekwemnda kumuomba amsaidie kiasi cha fedha, maana yeye ametoka mtwara kwenya mazishi ya Baba mkwe wake yeye na familia yake na anaelekea wilaya ambayo amenitajia kuwa ndiko anakofanyia kazi( kumbuka hiyo ndiyo wilaya ninayotoka), akaendelea kunieleza kuwa amefika na ndege ya asubuhi kutoka huko mtwara, na kwamba pale Airport alikodi taxi kwenda Ubungo akidhani kuwa ni sh. 10,000 kumbe ni sh. 40,000, ambazo ndizo alizokuwa amebaki nazo kama nauli yake pamoja na famila yake, hivyo alikwenda hapo Mmnazi mmoja kwa Rafiki yake ambaye ni Daktari ili amuongezee lakini kwa bahati mbaya hakumkuta hivyo akaomba nimpatie kiasi hicho cha sh. elfu 40 atanirudishia kwa kumpatia mdogo wangu ili aniletee. kabla ya hapo alikuwa amekwisha niuliza kuwa mimi hapa mjini ninashuguli gani.. pamoja na kwamba mimi sio mtu wa kutaja ofisi ninayofanya kazi niliona nimtajie kwani sikuwa na shaka kuwa mtu niliyekuwa nazungumza naye ni tapeli, hii ilikuwa mapema sana wakati maongezi yetu hayafika mbali hivyo alijua fedha atapata.
kutokana nakudai kuwa yeye ni mwenyeji wa Mkoa ninaotoka, na ukizingatia kuwa wenyeji wa mkoa ule hupenda sana kuzungumza kilugha, ilibidi niingie moja kwa moja..... looooo hapo ndiyo dili lilipoanza kuyeyuka, maana nilimuona akibadilika taswira, nikamhoji inakuwaje yeye ni mwenyeji wa kule tena mtu mzima hajui lugha? akasema unajua mimi sikukulia kule nilirudi ukubwani....

hapo nilishtukia dili na nikajiridhisha fika kuwa hapa kuna kitu, nilichokifanya nilimweleza kuwa pesa niliyokuwa nayo haitoshi kumpatia ila kwa kuwa yeye ni maarufu aende tu akawaambia makondakta wa mabasi yaendayo huko anakokwenda watamwelewa...

Hiyo ndiyo kosakosa ya kutapeliwa niliyokutana nayo Kariakoo, hivyo be careful unapokuwa Kariakoo na maeneomengine hapa jijini.​
 
Asante sana Anold kwa kututahadharisha. jamani tuwe makini na viumbe hawa
 
Dawa yao ni kuwatandika lugha za nyumbani...afu maswali ya udadisi..
Thanx kwa info
 
Mmmhhh pole na ahsante kuna hili limeotoke jana pale posta kweupeeeeeeeeeeeeee

kwa mnaojua pale bakheresa kuna vijana wanafunga mikanda mpaka kwenye kitovu
wakikuona wanakufwata na kujifanya wanataka kupiga dili..mmojaw wao kweupe jamani
mama mmoja karibu na ofisi za bmtl akapaki baada akiwa anapaki akaja kakammoja upande wa pili akiwa anafunga akashikilia kitasa cha pili so mama alipoondoka jamaa nae akaondoka kumbe alipofunga huku upande wa pili uko wazi akarudi kijana akakaa ndani anasechi,,,rooho mtakatifu akamjia mama kaasahau kitu akute kjana ndani ya gari ametulia anahangaika kutafuta mama alipofungua akapiga kelele wale mhanithi wakamwangalia mwenzao akikimbia na yule mama kuanza kuelezea hali halisi kwa kweli ni uhuni wa akili ila ukiwa posta kariakoo akija mtu pembeni wakati unafunga mfukuze then funga tena else kuwa na mazoe ya kucheki milango hasa upande wa pili....
 
kuna moja ana hadithi kama hiyo alitaka kumtapeli ndugu yangu kwa story ya kumtibu baba yake, sasa jama yangu akamwambia kama ni usafiri kwenda airport mimi kesho naenda huko nitakupitia, alipokwenda kumpa lift jamaa hakuonekana
 
Maisha ni magumu sana watu wanatumia kila mbinu ili kuweka ugali wa watoto mezani!!
 
Kibaya zaiidi wansikia serikalini wanaiba ma bilion wanatetewa like gavana na wenzake sembuse wao jamani...kweli inabidi tuwatafutie njia bora zaidi za kuiba
 
Anold, huyo taperi ni wa muda mrefu, nilipambana naye miaka miwili iliyopita maelezo yake yalikuwa hayo hayo uliyoeleza, lakini nilimtolea nje.
 
Mkuu wengine ukiwapa mda wa kuongea nao kama hivyo wanakuwa weshakuliza zamaani ukifika mbele ukijisachi unaanza kujinadia mwizi mwenyewe...so again be careful next time.
 
Ama kweli nchi ya Matapeli huzaa matapeli kila sekunde...
Mumegundua kitu gani ndugu zangu katika simulizi hii...

Mie nimeyaona haya japo nayo nimetumia ujanja wangu (utapeli)

Kwanza simulizi ni ya kitapeli kwani msimulizi haujui hata mtaa alotaka kutapeliwa, pili hata hajatutajia alikuwa akinunua vifaa gani vya ujenzi(utapeli).
Tatu amejuaje yule mtu ni wa heshima na kwanini alikubali kuwa anatoka katika mkoa huo na pia kumjua huyo mdogo wake bandia (tapeli kwa tapeli walikutana)
Hali kadhalika alishindwa kuzungumza hata hiyo lugha ya huko Mtwara bali alimuuliza tu (utapeli)
Inawezekana ukawa mzee ukazaliwa sehemu na usijue vizuri lugha ya nyumbani (kumlazimisha ajue kimtwara ni utapeli pia) we msimulizi hujui lugha ya Taifa ni Kiswahili?

Mwisho, msimulizi(tapeli) alimdanganya tapeli atumie umaarufu kufika Mtwara. Je hiyo ni sawa? Nani Tapeli hapo? ANGEKUOMBA UMPELEKE KWA KONDAKTA UNGEENDA NAE? Lazima Ungekataa! Je huo si uwongo (utapeli)

''SISI WABONGO KWA UTAPELI MMH! TEMA MATE CHINI''
 
Kariakoo noma kweli. Pale ndio shule yenye kelele nyingi(school of hard knocks). Zile shati zenye rangi nzuri nzuri zinazotandikwa chini barabara ya msimbazi na kutangaziwa elfu elfu na elfu na mia tano zote ni blauzi. Na utaona wanaume wingi kweli wakizinunua wakifikiri ni shati. Na viatu vingi vinavyouzwa pale barabarani vimeshikizwa na supper glue baada ya kutatuka, hivyo wadau lazima tuwe makini tuwapo Kariakoo.
 
Back
Top Bottom