7seven
JF-Expert Member
- Mar 27, 2022
- 3,659
- 7,616
Amen! Ubarikiwe sana kwa neno zuri linalomhusu Roho Mtakatifu, watu watapata kitu kutokana na hili Andiko lako,Amen.Namshukuru Mungu amenipa rafiki mpya ambae nikazidi kujifunza jinsi ya kumtumia anaitwa "ROHO MTAKATIFU"
Wengi wetu tumekuwa tukijua tuelekeze maombi kwa Mungu na Yesu Kristo....ila ukisoma biblia vizuri utagundua kuna Ile Roho ambayo inatuunganisha na Mungu na Yesu Kristo nae ndio Roho mtakatifu.
Roho mtakatifu akikaa ndani yetu atatufundisha jinsi ya kumtukuza na, kumsifu na kumuinua Mungu sikuzote.
Ilikuwa kama utani tu nilipewa vitabu viwili vya Benny Hinn "GOOD MORNING HOLLY SPIRIT" na kingine kinaitwa "THE ANOINTING"
Ni vitabu vizuri sana unaweza usiamini siku naanza soma hicho cha "THE ANOINTING" nilishindwa sababu ya upako uliopo moyo wangu ulikuwa unapata kiu ya ajabu isiyo ya kawaida nikashindwa kumaliza page 2...
Unajua tunaomba hatujibiwi hatujui kusali wala kuwasilisha maombi yetu ni Sawa na mwanao aje aseme "Wewe Baba usie na akili naomba daftari maana ni jukumu lako" hautaweza kumpa mtoto hitaji lake lakini mwanao akija kusema
"Pole na kazi Baba, asante kwa zile nauli unazonipa.zinanisaidia sana,pia Baba naomba unisaidie hela ya daftari ili niandike notes nifanye vizuri zaidi"
Utampa huyu mtoto hitaji lake na hiyo ndio kazi ya roho mtakatifu ndani yetu
Mfariji, msaidizi, mshauri, kiongozi, rafiki Yohana 16:7 pia warumi 8:26
kupitia kumjua roho mtakatifu nimekuja kuelewa nyimbo nyingi za dini zinamaana gani kiroho na jinsi Yesu Kristo alivyomtumia roho mtakatifu kuwapa ujumbe waimbaji wake
kuna siku huwa naskiliza wimbo wa HAUFANANISHWI Tu na moyo wangu huwa unajawa na amani ya ajabu sana
Kuna wimbo wa ROSE MUHANDO wa NDIVYO ULIVYO kuna wimbo mwingine wa MAJINA YOTE MAZURI wa Dedo deurnmerci ...pia NENA NAMI wa Marggie Dawn
Hizi nyimbo huwa roho ananifunulia namna ambavyo zinamfurahisha na kumtukuza Mungu Kwa jinsi na namna ya ajabu sana....kuna nyimbo nyingi ila hizi ni zile nilizonazo na kuona nguvu iliyopo.
Roho mtakatifu anafundisha kwa vitendo tu na hkusema Kwa maandiko kwamaana kilakitu kilashida kila ombi basi kinapatikana kwenye biblia yeye ukiomba ujibu Kwa mistari ya biblia.
Pia roho mtakatifu hutumia hatua Saba katika maombi yetu
1: kumkiri Yesu Anza kwa kumkiri Yesu ni nani (wengine huanza Baba wa Mbinguni, mfalme wa wafalme, mwingi wa rehema, utukuzwe wewe ulie kununua vitu vyote) na zingine sifa zote nzuri za Mungu zaburi 98 na 99 zinatoa namna Bora ya kumsifu Mungu.
2: Jambo la pili kufikisha hitaji lako Kwa Mungu
3: kuabudu kumsifu...hapa uoneshe upendo wako kwake... (Ninakupenda Yesu, ninakuinua juu ya vyote, kama sio wewe nisingefika hata sekunde hii, umejawa na rehema Yesu, umejawa na utukufu Messiah)
4: mahusiano binafsi na Mungu.. kumshuhudia ule ukuu wake na Faida za ule uwepo wake maishan mwako.
5: maombezi wa Wengine.....roho mtakatifu atakufunulia wa kumuombea na Jambo la kumuombea.
6: kutoa shukrani mbele za Mungu juu ya mambo yote, mazuri na mabaya kupata na kukosa kwetu.
7: kutoa sifa mbele zake...kumsifu kwa nyimbo au maneno ya sifa kuu
Nilisoma hizi hatua kwenye kitabu cha "Good morning Holly spirit" page 118 ajabu sana roho mtakatifu akijaa na nikianza kunena Kwa lugha huwa napitia stage hizi zote bila kukumbushwa yani najikuta nimegusa steps zote japo sio lazima iwe Kwa mpangilio wote ila nyingi huenda sawa sawa...
Kumkaribisha roho mtakatifu kwenye maombi kuna raha yake na tumtafute awe rafiki yetu kwamaana neno linasema aombae hupewa na atafutae huona na ambishae hufunguliwa